Swali kwa Wana UKAWA: Is UKAWA for Real or Just A Marriage of Convenience?.-Ni Swali Tuu!.

Pasco, hii haitasambaratisha UKAWA?
Mag3, Mkandara, JokaKuu, MchunguZI

Vyama vyote vya siasa ukianza na CCM, sehemu kubwa ya mazungumzo yao siyo ya kweli, not really. Vyama vya upinzani ni rahisi kulinda maneno yao kwa kusema ni wakweli, lakini kwa CCM hawawezi maana wameshaonyesha kwa vitendo wakiwa madarakani kwamba ni waongo. CCM ni waongo.

UKAWA haiwezi kusambaratika kwa kuwa lengo siyo kuwa m/kiti wa chama chochote kile! Habari hizi kama ni za kweli zitakuwa na lengo la kuwakomoa CCM ambacho ndicho UKAWA wanachokitafuta. Anaweza kupewa nafasi ya kugombea Urais na ikapita kwa sababu sioni kama urais ni dili yoyote kwa UKAWA. Sheria iliyopo inampa ushindi aliyetangazwa, siyo aliyeshinda. CCM kwa tabia zao za siku zote, watalazimisha yoyote atangazwe.

Kwa Lowasa sioni faida kwake zaidi ya kuwakomoa CCM kwa maamuzi yaliyofanywa. Inagwa lengo lake kwa nguvu ilikuwa ni urais, siamini kwamba ana imani kwamba akiwa UKAWA anaweza kuwa rais.

Nchi ni ngumu, haifuati sheria. Sasa hivi mawaziri wote wanatumia magari ya serikali na madereva wa serikali kutafuta kura majimboni, kinyume na sheria. wanachokifanya ni kuweka namba za bandia.
 
Wanabodi,
Swali hili linafuatia washirika wawili wakuu wa UKAWA, CHADEMA na CUF, kila mmoja kukumbwa na tatizo la 'superiority complex' kwa kujiona yeye ni bora zaidi, hivyo kutaka kujimegea pande kubwa!. Conveniences hizi zitafikia peak wakati wa uteuzi wa mgombea urais, CUF tayari wakiwa na mgombea wao wa kudumu!, jee atakubali kujishusha na kuruhusu mgombea wa ushindi ndie aibebe UKAWA?!. Chadema nao wanaye mgombea wao ambao wanaamini aliisha shinda ila akapokwa, kwao huu ni muda wa kumalizia alipo ishia!.

UKAWA wakiweza kulimaliza hili la uteuzi wa mgombea urais salama, then angalau kutakuwa na matumaini ya mabadiliko!, lakini kwa ubinafsi wa viongozi wa UKAWA, nina mashaka kama hili litapita salama, hivyo wale wote wenye matumaini na upinzani kuingia ikulu October, keep high hopes for best, but get prepared for the worst, iwapo watashindwa kumpata mgombea muafaka wa kuwaletea ushindi, 2015 ni CCM tena!.

Pasco.
Kujiuzulu kwa Prof. Lipumba, kunatokana na yeye kuwa ni mgombea wa kudumu wa CUF kwenye urais wa Muungano, kitendo cha kupokelewa Lowassa, kumemrender Lipumba jobless!. Ila alichofanya Lipumba, Huo Ndio Uanaume!, Kususa ni Tabia za Kike!.

Yule msusaji nae vivyo hivyo, japo anajijua hana uwezo kushindana na CCM, alitegemea angekuwa yeye, kugombea ili kugombea tuu, na sio kugombea ili kushinda!. Amepatikana mgombea mwenye sifa ambae akigombea ni kushinda kwa ushindi wa kishindo mapema tuu asubuhi!, sasa ndio na yeye amesusa!.

Ukilisoma bandiko langu nimezungunzia matatizo matatu ya viongozi wa UKAWA, superiority complex, conveniences na ubinafsi wa viongozi, na haya sasa ndio matokeo!.

Pasco
 

Nilitolea mfano wapinzani siku zote wanaelewa the playing ground or the playing field ya the game of politics in Tanzania, is not level!, licha ya wapinzani kulijua hili, lakini kila uchaguzi huwa wana sign kukubaliana the rules of the game, na mwisho wa siku wanapigwa wanaishia kulia lia!.

Uchaguzi wa 2010, waliosaini rules of the game za NEC kwa Chadema ni Mbowe na Dr. Slaa, walipopigwa Dr akasusa kuyatambua matokeo, nikasema kama hapo mwanzo ulikubali, ukapeleka tumu uwanjani, ukipigwa, huwezi kukataa kuyatumbua matokeo!. Baada yakugundua the playing field is not level, dawa ilikuwa ni kutopeleka timu uwanjani ili game lisichezwe hadi uwanja usawazishwe!. Tunaingia tena kwenye uchaguzi mwingine, timu ni zile zile, uwanja ule ule, wachezaji wale wale, refa yule yule na rules of the game zile zile, hivyo mtu anayeyajua haya bado akapeleka timu kwa kutegemea matokeo tofauti, huyo atakuwa ni kichaa!.

Niliwapongeza sana wapinzani walipopata fursa kwenda ikulu nikidhani sasa watapigania kusawazishwa kwa uwanja, kumbe wenzetu walikwenda kufakamia tuu juisi, chai na vitafunwa, as if all is well!. Adui mkubwa wa hiki kiini macho cha UKAWA ni sheria zetu kandamizi, ambazo CUF, NCCR na Chadema wanazikumbatia to their advantage, pale wanapopata fursa kuzitumia kwa kuchinjia!, ila unapofikia wakati wa wao kuchinjwa, kazi yao ni kulia lia tuu!. Huu mimi nauita ujinga!.

Pasco.
Najikumbusha tuu!.
 
Kujiuzulu kwa Prof. Lipumba, kunatokana na yeye kuwa ni mgombea wa kudumu wa CUF kwenye urais wa Muungano, kitendo cha kupokelewa Lowassa, kumemrender Lipumba jobless!. Ila alichofanya Lipumba, Huo Ndio Uanaume!, Kususa ni Tabia za Kike!.

Yule msusaji nae vivyo hivyo, japo anajijua hana uwezo kushindana na CCM, alitegemea angekuwa yeye, kugombea ili kugombea tuu, na sio kugombea ili kushinda!. Amepatikana mgombea mwenye sifa ambae akigombea ni kushinda kwa ushindi wa kishindo mapema tuu asubuhi!, sasa ndio na yeye amesusa!.

Ukilisoma bandiko langu nimezungunzia matatizo matatu ya viongozi wa UKAWA, superiority complex, conveniences na ubinafsi wa viongozi, na haya sasa ndio matokeo!.

Pasco
 
Wanabodi,

Huu ndio mwaka wa uchaguzi, matumaini yote ya upinzani nchi Tanzania kuweza kushinda uchaguzi na kuingia Ikulu yetu ya Magogoni ni kupitia ushirikiano wa vyama kuunda umoja wenye nguvu kwa kusimamisha mgombea mmoja wa upinzani kukabiliana na mgombea wa CCM,

Kwa ubinafsi wa viongozi wa Upinzani, nina mashaka kama hili litapita salama, hivyo wale wote wenye matumaini na upinzani kuingia ikulu October, keep high hopes for best, but get prepared for the worst, iwapo watashindwa kumpata mgombea muafaka wa kuwaletea ushindi, 2015 ni CCM tena!.

Pasco.
Wanabodi japo sasa mimi ni kada wa Chama cha Mapinduzi, ndani ya CCM kuna makada Wazalendo ambao kwao ni Tanzania kwanza.

Hivyo nawaomba msome hoja zangu with an open mind, kwa kuzingatia nguvu za hoja na sio hoja za nguvu!.

Sasa tunaelekea uchaguzi mwingine wa vyama vingi hapo October 25. Uchaguzi wa 2015 tuliingia tukiwa na CCM taaban, na CCM ikashinda, sasa uchaguzi huu, tunaingia na CCM imara, what are the chances of opposition to win?.

Upinzani Tanzania unakabiliwa na ugonjwa ule ule wa ubinafsi, wa kushindwa kumsimamisha mgombea mmoja, utakao pelekea Wapinzani kugawana kura huku chama changu CCM kikipeta kwa ulaini.

Haku bara, hakuna ubishi kuhusu JPM na CCM kutwaa ushindi wa kishindo.
Zanzibar ndio kuna kazi kidogo, Maalim Seif atapapata kura kadhaa ila hazitatosha.

Huku bara nilidhani Wapinzani wataendeleza kama UKAWA but very unfortunately, wanakwenda kugawana kura na CCM kidedea.

Umuhimu wa hoja kama hizi ni kuwaanda kisaikolojia kukubali matokeo!.

Ukiwa na too great expectations utashinda uchaguzi, ukishindwa utaumia sana!.
Lakini ukiwa na too great expectations za kushinda uchaguzi, akatokea mtu akakuambia utashwa, hata kama uta mu ignore na kumpuuza, kwasababu unaamini utashinda, ukweli ukiishajitokeza umeshindwa, amini usiamini, yes utaumia kushindwa, lakini haitaumia sana na kushindwa huko, hakutakuwa na impact mbaya kama ya kuanguka na kuzimia, kwasababu you knew, hata kama uli ignore na kupuuzia, but you knew, the impact is not the same
Hivyo kwa wapinzani wote mlinisoma hapa, kwa sasa just ignore, puuzia, lakini kitakacho tokea October 25, utanikumbuka, utanishukuru nimekusaidia kukupunguzia impact ya maumivu ya kupigwa!.
Pole.
P
 
Mayalla mimi ni CCM pia lakini uchambuzi wako ni wa kijinga sana
1. Kwanza uchaguzi umeshaporwa na chama Chang ukiwa kukata wagombea wa upinzani tu.
2. Matumizi ya vyombo vya habari ni biased na kifisadi.
3. Hoja na Sera zipo upande mmoja na CCM hatujibu hoja kukidhi kiu ya wananchi kwenye maswali mbalimbali wanayohitaji.
4. Hakuna faida ya kufanya siasa sisi wenyewe kwa miaka mitano
5. Mgombea wetu hana mvuto narudia hana mvuto hata kwenye namna yake ya kuhutubia
6. Ushindi ni wa CCM kwa nguvu yoyote ila sio kwa uchaguzi. Wenye akili tunajipanga kwa CCM mpya 2025 ambapo hali itakua mbaya zaidi.
 
Back
Top Bottom