Swali kwa mheshimiwa Zitto !!!!

KadaMpinzani

JF-Expert Member
Jan 31, 2007
3,715
86
Za saa hivi mheshimiwa !

Pole sana kwa kazi, na hongera kwa kulitumikia taifa letu.
Mimi binafsi nina maswali machache ambayo ningependa uyaclear wewe binafsi na sio kama chama. Tokea kifo cha mama Mbatia (Mungu amrehemu) kumetokea, maneno meeeengi sana ya kisiasa hasa tena hapa yakiongozwa na wafuasi wa Chadema tawi la JamboForums. Sasa mheshimiwa, wewe kama Zitto (sahau siasa kwa dakika moja) unachukuliaje hili suala zima la watu kuhusisha kifo cha mama Mbatia na siasa, wengi wakisema kwamba wewe zitto ulitaka kuuliwa. Kwa kweli hata kama tunataka maendeleo ndani ya vyama vyetu, nafahamu fika kwamba kuna dirty taactics ambazo hutumiwa, lakini hii ni MBAYA SANA TENA SANA kwa taifa letu.

Naamini wengi watasema mie chizi kwa kuwa napingana nao, lakini vile vile naamini chizi huyo huyo katika maneno kumi atakayoongea basi angalau hata moja linaweza likawa na maana. Mheshimiwa tukumbuke kwamba maendeleo ya nchi yetu, mapenzi ya nchi yetu, na maendeleo ya kisiasa ni mambo ya kidunia tu hivyo jiangalie wewe mwenyewe katika kutetea ule ukweli unaoufahamu na kupinga yale yasiyo ya kweli ( Kama na hili pia litakuwemo ndani).

Kwa kweli, Zitto sitokuficha umefika katika hatua nzuri sana, na katika hatua hiyo sidhani kama wengi walio wapinzani wako, na hata wale walio karibu yako watapenda ufanikiwe zaidi yao, KUMBUKA NIMESEMA WALE WAPINZANI WAKO NA HATA WALE ULIO NAO KARIBU hivyo jiangalie sana na watu wanaosema wako karibu na wewe maana watu hao hao (hapa JF) washasema ulitaka kuuliwa (huku wakiwa hawana proove ukiangalia hawakuwa katika eneo la tukio )

Sasa najua unaweza ukawa busy, hivyo ukachukua muda mrefu kujibu lakini natumaini hata kama itachukua muda mwingi angalau upitie hapa na udondoshe walau maneno machache !

Shukrani !
KadaMpinzani for JF !
 
Back
Top Bottom