Swali kwa mh.waziri mkuu kupitia mh. Ole medee (mb) arumeru magharibu

Ndachuwa

JF-Expert Member
Mar 8, 2006
6,269
4,569
Mh. Ole Medee wengi wa wapiga kura wako hawatakuelewa kama hutamuuliza waziri katika kipindi cha maswali ya hapo kwa hapo swali lifuatalo.

Mh. Waziri Mkuu, mwaka huu Halmashauri ya Arusha vijijini imekuwa ikifanya jitahada za kuwapatia wananchi viwanja vilivyopimwa na tayari viwanja vimetolewa katika maeneo ya Gomba Estates na Burka, naipongeza serikali kwa jitihada hizo; swali

1. Hivyo viwanja ni kwa ajili ya Watanzania wote au ni kwa ajili ya kundi dogo lenye uwezo wa kifedha kwani bei za kiwanja inaanzia TShs. 4,000,000 hadi 32,000,000 pesa ambayo hata mfanyakazi wa serikali hawezi kumudu.

2. Pale ambapo waombaji ni wengi kuliko viwanja vilivyopo (mfano Burka) ni utaratibu gani unatumika ili kutoa haki/nafasi kwa kila mwombaji pasipo kubagua? Na Jee wote waliolipia viwanja wametumia majina yao halisi?
 
EL anamiliki 60% ya viwanja hivyo pia JK ana viwanja pia sidhani kama ilikuwa kwa ajili ya watanzania wa kawaida, nadhani ilikuwa ni jinsi ya kuvichakachua ndo maana wakatumia zuga ya kuwahadaa wananchi wameliwa buku kumi kumi zao za kuchukua form na form halali zikaisha zikachakachuliwa so wananchi wameumizwa zaidi
 
EL anamiliki 60% ya viwanja hivyo pia JK ana viwanja pia sidhani kama ilikuwa kwa ajili ya watanzania wa kawaida, nadhani ilikuwa ni jinsi ya kuvichakachua ndo maana wakatumia zuga ya kuwahadaa wananchi wameliwa buku kumi kumi zao za kuchukua form na form halali zikaisha zikachakachuliwa so wananchi wameumizwa zaidi

Kwenye ugawaji wa viwanja baraza la madiwani linahusikaje? Nauliza kwa sababu tangazo la viwanja lilitoka bazara la madiwani likiwa limevunjwa na offer zikatoka kabla ya baraza jipya la madiwani kuingia kazini.
 
kwani hao uliowataja sio watanzania ?? wao hawana haki ya kuvipata??? mbona vile vya gomba viligawiwa kwa watu alafu wakaviuza badala ya kuviendeleza ? acha hizo wewe . mimi ni mmoja wapo wa waliopata na ni mtu mdogo sana kwenye hii nchii.
 
kwani hao uliowataja sio watanzania ?? wao hawana haki ya kuvipata??? mbona vile vya gomba viligawiwa kwa watu alafu wakaviuza badala ya kuviendeleza ? acha hizo wewe . mimi ni mmoja wapo wa waliopata na ni mtu mdogo sana kwenye hii nchii.

Swali ni hiyo formula iliyotumika hadi wewe ukapata iliwatendea waombaji wote haki, yaani kila mtu alikuwa na uwezekano wa kupata kwa kutumia "selection method" inayoeleweka?
 
kwani hao uliowataja sio watanzania ?? wao hawana haki ya kuvipata??? mbona vile vya gomba viligawiwa kwa watu alafu wakaviuza badala ya kuviendeleza ? acha hizo wewe . mimi ni mmoja wapo wa waliopata na ni mtu mdogo sana kwenye hii nchii.
Watu wadogo kwenye nchi hii wanakaa mbele ya computer zao waki surf internet? Unanitia shaka. Naomba mwongozo wa Spika!
 
Watu adogo kwenye nchi hii wanakaa mbele ya computer zao waki surf internet? Unanitia shaka. Naomba mwongozo wa Spika!



teh teh teh huwezi amini watu wanafanyia biashara maeneo waliyopewa kama hawana akili nzuri badala ya kuyaendeleza , mimi nimechukua mkopo ndio maana nimeweza kulipia . kweli pale burka ni sehemu tamu sana kuliko sehemu yoyote .
 
Watu adogo kwenye nchi hii wanakaa mbele ya computer zao waki surf internet? Unanitia shaka. Naomba mwongozo wa Spika!

Nusu saa 1000 bado maskini wa Tanzania kama anaweza kumeza Serengeti tatu atashindwaje kulipia Internet Shs. 1000? Vile vile wengine tuna access sehemu tulizoajiriwa
 
Naomba mwongozo! Ni kanuni ya ngapi ya bunge inaruhusu maswali kwa waziri mkuu kujadiliwa nje ya bunge?
 
Unajua Mizengo Kayanza Peter Pinda atajibu nini?Atajibu hivi:

''...Kwanza nimshukuru ndugu yangu Mhe. Ole Medee(MB) wa jimbo la Arumeru Magh. kwa swali lake zuri. Baada ya kusema hayo naomba ni mjibu kama ifuatavyo...(anakohoa kidogo). Sina taarifa sahihi za uuzwaji wa viwanja vya maeneo hayo ya Burka na Gomba Estates huko Arusha ila napenda nimhakikishie ndugu yangu Ole Medee kwamba baada ya kuahirishwa kwa Bunge lako tukufu nitashirikiana na Mhe. MB kwa karibu kujua ukweli wa jambo hilo. Iwapo itabainika kuwa taratibu za ugawaji wa maeneo hayo zilikiukwa,hatua kali zitachukuliwa kwa wahusika. Asante''.Makofi kwa wingi toka upande wa Wabunge wa CCM.

Ndiyo itakuwa imetoka!
 
Naomba mwongozo! Ni kanuni ya ngapi ya bunge inaruhusu maswali kwa waziri mkuu kujadiliwa nje ya bunge?
Kwa sababu ya bora utawala wananji wanaruhusa kabisaaaaa kuchadili fitu finavyohusu mstakabari wa nji yao wasee.
 
Unajua Mizengo Kayanza Peter Pinda atajibu nini?Atajibu hivi:

''...Kwanza nimshukuru ndugu yangu Mhe. Ole Medee(MB) wa jimbo la Arumeru Magh. kwa swali lake zuri. Baada ya kusema hayo naomba ni mjibu kama ifuatavyo...(anakohoa kidogo). Sina taarifa sahihi za uuzwaji wa viwanja vya maeneo hayo ya Burka na Gomba Estates huko Arusha ila napenda nimhakikishie ndugu yangu Ole Medee kwamba baada ya kuahirishwa kwa Bunge lako tukufu nitashirikiana na Mhe. MB kwa karibu kujua ukweli wa jambo hilo. Iwapo itabainika kuwa taratibu za ugawaji wa maeneo hayo zilikiukwa,hatua kali zitachukuliwa kwa wahusika. Asante''.Makofi kwa wingi toka upande wa Wabunge wa CCM.

Ndiyo itakuwa imetoka!
Teh teh teh teh teh teh ulishawahi kuwa kwenye system? naona kama vile unajibu kitu kinachofanyika kila siku katika life cycle yetu. Bwahahahahahaha
 
Bei nitatizo si kama mchangiaji mmoja alivyosema si tatizo......sehemu kubwa ya watanzania waliopiga kura na hasa waliojitokeza kudai matokeo pale yalipocheleweshwa ni watu waliokua wanaulilia ukombozi ili ikiwezekana wapate wenzao wakuwatetea ktk mambo ya msigi likiwapo hili la bei za viwanja vinavyoanzia 4m, 8m.Kwa mtazamo wakawaida hilo ni pato la mtu wa juu sana hivyo watu wana haki yakudai bei ishuke
Pili sina hakika hao vigogo kama bado hawajapata sehemu za kuishi(kwa maana ya kujenga) zaidi yakutaka wajiongezee maeneo (kulimbikiza) wakati wengine bado hata kiwanja hawana.
 
Ubinafsi huo ndo umewafanya kufikia uko ngoja tuje pata kiongozi muadilifu yote hayo yatakuwa historia
 
Back
Top Bottom