Swali kwa Ayubu Rioba: Siku hizi sera ya Taifa inaruhusu taasisi za kidini kunufaika na fedha za walipa kodi kupitia TBC?

maelezo meengi kisa inakuuma kwa maudhui ya kiislam kutumia siku ya ijumaa.mbona hupingi wakristo kutumia siku ya jumaa pili? acha chuki za hovyo hizo.
vile vile mbona huja hoji kwani ccm wanatumia TBC katika mambo yao? chukulia mfano kipindi cha kampeni kila sehemu mwenda zake alipokuwa ccm walirusha live, na hata sehemu akihutubia njiani nao walikuwa wanarusha live hizo ni kampeni za chama kimoja mbona hukuhoji hilo?
Hata jana tu katibu wa ccm na sekretariet yake walivyopokelewa hapo Lumumba TBC walirusha live.mbona husemi kwamba ccm inabidi watumie tv yao ya channel ten.Acha chuki ndugu kazi iendelee
Hoja inayojadiliwa hapa inahusu uvunjaji wa Katiba ibara ya 4(1) na 19(2).
Hayo unayoyaibua ni hoja tofauti.
Anzisha bandiko jingine kwa ajili yake.
 
Mkuu, kule Bungeni huwa wanafanya sala kila waanzapo session, na hata kwenye matukio makubwa ya kitaifa kama sherehe za maadhimisho mbalimbali huwa wanaalikwa viongozi wa dini zote kufanya sala, je ina maana kumtaja Mungu katika sehemu kama hizo ni matumizi mabaya ya nafasi/muda wa umma?

1. Kule Bungeni huwa wanafanya sala kila waanzapo session, wanamtaja "Mungu" bila kutwambia Mungu yupi, anayesoma dua sio padre, sio shehe, sio mchungaji. Wakati huo huo Katiba ya nchi haina neno Mungu. Ibara ya 4(1) na 19(2) zinataka Bunge kutenganisha shughuli zake na shughuli za kidini. Bado huoni tatizo hapo? Kuna mapokeo yanayovunja Katiba na yanaendelezwa kiajabu tu.

2. Kwenye matukio makubwa ya kitaifa kama sherehe za maadhimisho mbalimbali huwa wanaalikwa viongozi wa dini zote kufanya sala. Kumtaja Mungu katika sehemu kama hizo bila kueleza ni Mungu yupi anatajwa ni ukasuku. Ni Mungu anayekula kitimoto au Mungu asiyekula kitimoto? Mungu mwenye nafsi tatu au MUngu mwenye nafsi moja? Mungu mwenye mwili au Mungu ambaye ni roho tupu? Mungu anayetumia kondomu au Mungu asiyetumia kondomu? Msawali haya machache yanakuonyesha ukubwa wa ukasuku wetu.

3. Kumtaja Mungu katika sehemu za umma ambako kuna watu wanashilia mtazamo tofauto kuhusu hulka ya MUngu, na bila kueleza ni Mungu yupi anatajwa ni uchokozi wa kidini. Kwa mfano najiuliza:

-- Ni Mungu anayekula kitimoto (Mungu Mkristo) au Mungu asiyekula kitimoto (Mungu Muislamu)?

-- Mungu mwenye nafsi tatu (Mungu Mkristo) au MUngu mwenye nafsi moja (Mungu Muislamu)?

--Mungu mwenye mwili (Mungu Mkristo) au Mungu ambaye ni roho tupu (Mungu Muislamu)?

-- Mungu anayetumia kondomu (Mungu Mlutheri) au Mungu asiyetumia kondomu (Mungu Mkatoliki)? Msawali haya machache yanakuonyesha ukubwa wa ukasuku wetu.

4. Kutokana na matatu hapo juu, ni wazi kuwa dua za Bungeni na sala za kufungua matukio ya kiserikali ni uchokozi wa kidini na zinamaanisha uvunjaji wa Ktiba ya nchi ibara ya 4(1) kama ikisomwa pamoja na ibara ya 19(2).
 
Samahani... we mwenzetu ni mgeni nchi hii? Au unataka kutuambia umeanza kutazama tiibiisii wakati huu wa SSH? wakati wa Mwendazake, JK, BM havikuwepo hivyo vipindi au enzi za AHM na JKN hukuwahi kusikiliza RTD vitu kama "inueni mioyo... Quran tukufu?"
JE WADHANI KWANINI RAIS SSH KAJA NA SALAAM MPYA YA KITAIFA? JE WADHANI KWANINI HIYO SALAAM YAKE BAADHI WANAIPINGA? Je kwanini wapo viongozi bado wanatoa salaam za kidini kwenye mikutano au vikao vya serikali ilhali serikali haina dini?
Salamu Mpya ya Rais Samia ndio Mwarobaini wa tatizo la salamu za kidini kwenye matukio ya kiserikali.

Vipindi vya "inueni mioyo" na "Quran tukufu" kupitia TBC na RTD vimekuwapo muda mrefu, na vimeongezeka siku hizi.

Kwa hiyo hoja yangu inazo sababu za muda mrefu na sababu za karibuni.

Sasa nasema: Kwa kuwa Vipindi hivi vinavunja ibara ya 4(1) na 19(2) za Katiba ya Tanzania, basi ni batili.

Nataka tujisahihishe.
 
Kuna madaktari wanafanya kazi kwenye hospitali za mashirika ya dini je nao waondolewe?
Kazi ya udaktari sio tendo la kidini. Hivyo, madaktari wa serikali walioko katika hospitali zinazomilikiwa na madhehebu ya dini hawavunji ibara ya 4(1( na 19(2) ya Katiba ya nchi.

Kazi ya uhasibu sio tendo la kidini.Hivyo, mapadre/masista wanaofanya kazi serikalini, kama ilivyo pale ofisi ya RC Dar, hawavunji ibara ya 4(1( na 19(2) ya Katiba ya nchi.
 
Sasa kama TV za kisekta hazifiki ndio tutumie kodi ya umma kueneza dini katika maeneo hayo? Hapana!
Kumbuka wanaotazama hizo TV programs ni walewale wanaokwenda makanisani na misikitini, pia hivyo vipindi vinaonyeshwa siku za ibada zao tu na siyo siku zingine
 
Kazi ya udaktari sio tendo la kidini. Hivyo, madaktari wa serikali walioko katika hospitali zinazomilikiwa na madhehebu ya dini hawavunji ibara ya 4(1( na 19(2) ya Katiba ya nchi.

Kazi ya uhasibu sio tendo la kidini.Hivyo, mapadre/masista wanaofanya kazi serikalini, kama ilivyo pale ofisi ya RC Dar, hawavunji ibara ya 4(1( na 19(2) ya Katiba ya nchi.
Hizo ibara zinasemaje Mama Amon
 
Kumbuka wanaotazama hizo TV programs ni walewale wanaokwenda makanisani na misikitini, pia hivyo vipindi vinaonyeshwa siku za ibada zao tu na siyo siku zingine
Naona unajali sana matokeo bila kuzingatia mbinu inayotumika kufikia matokeo hayo.
Mwanafunzi akitazamia na kushinda mtihani sawa, hata kama ni Mr. Zero!
Hapana.
Hoja yangu inaanzia kwenye uvunjaji wa Katiba ibara ya 4(1) na 19(2).
Jielekeze kwenye hoja.
 
MPUMBAF MJINGA MDINI
Kawaida yenu tunaijua mkisha ona Nchi inaongozwa na WAISLAM mtaanza kuhoji kila aina ya ujinga Madhebu za Kikristo kila siku zitatoa MATAMKO mkitawa na Wagalatia wenzenu hata wakivuruga Nchi namna gani mnaufyata kimyaaa
Tumesha wazioe Waatoliki mnataka Nchi iwe ktk mikono yenu tu pumbaf zenu!
Inaonekana we punda hujasoma hata ameandika nini.. unawaza ujinga tu muda wote. Ndo maana amesema ni vyema kila dini utumie vyombo vyake vya habari.
 
View attachment 1792731
Dk. Ayub Chacha Rioba, Mkrugenzi Mtendaji wa TBC

Kwa kuzingatia matakwa ya katiba ya Tanzania, swali hapo juu linatokana na bonde la ufa lililopo kati ya yale ninayoyaona, na yale ninayoyatarajia kuhusiana na uendeshaji wa TBC.

Niliyoyaona TBC1

Tangu 15 Novemba 2020
nilipoikosoa TBC katika namna inavyotekeleza dhima yake ya kuelimisha umma juu ya COVID19 kwa kuzingatia misingi ya ukweli, ukweli wote na ukweli pekee, leo tena, tarehe 21 Mei 2021, nimeona matukio mawili yasiyo ya kawaida.
  1. Asubuhi kabla ya kipindi cha Bunge cha mswali na majibu TBC1 walirusha kipindi cha "Madrasa" kilichokuwa na ujumbe unaotembea kwa upande wa chini ukisomeka "Mashindano ya Kuhifadhi Kurani Tukufu kwa Waislamu Wanawake Yameandaliwa na Taasisi ya Kiislam ya African Relief Foundation." Kurani zilizokuwa zinasomwa zimeandikwa kwa Kiarabu.
  2. Mchana, mara tu baada ya matangazo ya Maadhimisho ya miaka 40 ya kuanzishwa kwa SADC, ambako Ayub Rioba alikuwa mwongozaji, kilifuata kipindi ncha swala ya Kiislamu. Swala ilianza kwa maelezo ya Kiarabu kwa dakika zipatazo tano.
Nafahamu pia kwamba, TBC1 imekuwa na kawaida ifuatayo:
  1. Kila alfajiri madhehebu ya dini tofauti hupewa muda wa kusoma sala ya asubuhi.
  2. Kila usiku wa kati, kabla ya saa sita, madhehebu ya dini tofauti hupewa muda wa kusoma sala ya kufunga siku.
  3. Kila Jumapili pia, madhehebu ya dini tofauti hupewa muda wa kusoma ibada za Jumapili.
Matarajio kwa mujibu wa Katiba

Katiba ya Tanzania, ibara ya 19(2) inasema kuwa, "shughuli na uendeshaji wa jumuiya za dini zitakuwa nje ya shughuli za mamlaka ya nchi."

Na ibara ya 4(1) inasema kuwa shughuli zote za Mamlaka ya Nchi katika Jamhuri ya Muungano zitatekelezwa na kudhibitiwa na vyombo vyenye mamlaka ya utendaji, mamlaka ya kutekeleza utoaji haki, na mamlaka ya kutunga sheria. Yaani, Serikali, Bunge, na Mahakama.

Hivyo, matarajio yangu ni kwamba, kwa kuwa TBC ni mali inayoendeshwa kwa kodi ya umma chini ya usimamizi wa serikali isiyofungamana na dini yoyote, basi yafuatayo yanapaswa kuonekana:

  1. Programu zenye sura ya kitaifa katika ngazi ya maudhui
  2. Programu zenye sura ya kitaifa katika ngazi ya lugha
Hii maana yake ni kwamba, yafuatayo hayapaswi kuonekana:
  1. Programu zenye sura ya kisekta katika ngazi ya maudhui
  2. Programu zenye sura ya kisekta katika ngazi ya lugha

Pia, nafahamu kuwa, dini nyingi tayari zinavyo vyombo vyake vya habari kwa ajili ya kuendesha shughuli zake. Kanisa Katoliki wana Tumaini TV, KKKT wana Upendo TV, Waislam wana Iman TV, Wapagani wa "Ramli TV," nk

Nakumbuka kuwa, kwa sehemu kubwa, sala nyingi za madhehebu ya KiIslamu zinatumia lugha ya Kiarabu, jambo ambalo linakiuka sera ya kujenga umoja wa kitaifa kwa kutumia lugha ya Taifa la Tanzania.

Hata ibada kadhaa na litania nyingi za Kikristo zinasomwa kwa lugha ya Kilatini ambayo sio lugha ya Taifa la Tanzania.

Nakumbuka kuna wakati Kardinali pengo alikuwa anaitwa na wazee wetu wa kule Mwenge Parokiani, Dar es Salaam, ili akawaendeshee ibada kwa lugha ya Kilatini, kama walivyokuwa wamezoea zamani, kabla Kanisa Katoliki halijatunga sera ya kuendesha ibada kwa Kiswahili na kimila.

Kwa hiyo, katika mazingira ya sasa, yafuatayo ni matarajio yangu:

  1. Kanisa Katoliki waendeshe programu zao za kisekta kupitia Tumaini TV,
  2. KKKT waendeshe programu zao za kisekta kupitia Upendo TV,
  3. Waislam waendeshe programu zao za kisekta kupitia Iman TV,
  4. Wapagani waendesha programu zao za kisekta kupitia "Ramli TV," nk
Uhalisia wa mambo

Pamoja na matarajio haya, uhalisia wa mambo ni kwamba, matakwa ya Katiba ya Tanzania kuhusu umuhimu na ulazima wa kutenganisha dini na dola hayajatimia kama ifyatavyo:

  1. Kanisa Katoliki wanaendesha programu zao za kisekta kupitia TBC1,
  2. KKKT wanaendesha programu zao za kisekta kupitia TBC1,
  3. Waislam wanaendesha programu zao za kisekta kupitia TBC1,
  4. Shughuli za Bunge zinaanza kwa kusoma dua kwa "Mola",
  5. Viapo vya watumishi wa umma vinamaliziwa kwa maneno "Ewe Mwenyezi Mungu Nisaidie," wakati Katiba ya nchi haitambui neno "Mungu."
Kama Katiba ya nchi inayakataza mambo haya, kwa nini tunayatenda, kama ambavyo mfano wa TBC1 leo umeonyesha?

Ni muhimu swali hili lijibiwe ili tujichunguze kama vyombo vya dola vinakweza maslahi ya vikundi na kutweza maslahi ya pamoja kitaifa, au vinginevyo.

Napendekeza kwamba ni kosa la kikatiba kutumia kodi ya raia asiye na dini kuhudumia taasisi za kidini. Ni kama ambavyo ni kosa kutumia kodi ya mtu asiye na chama cha siasa kutoa ruzuku kwa chama cha siasa. Kuna tatizo hapo.

Mapendekezo kuhusu mtazamo wa kisera

Nakumbusha kwamba, kote duniani, sera za kutenganisha dini na dola hugawanyika katika sehemu mbili:

  1. Sera zinazofuata mtindo wa Kimarekani.
  2. Sera zinazofuata mtindo wa Kijerumani.
Sera zinazofuata mtindo wa Kimarekani. Hapa, serikali huyapiga kisogo masuala yote ya dini, kiasi kwamba hakuna senti ya mlipa kodi inatumika kufadhili taasisi za kidini. Habari ya sijuo airtime kwa programu za kidini, sijui kufungua bunge kwa dua, hakuna.

Sera zinazofuata mtindo wa KIjerumani. Hapa, serikali haiyapigi kisogo masuala yote ya dini, kwani kuna senti fulani ya mlipa kodi inatumika kufadhili taasisi za kidini. Kwa mfano, huko Ujerumani, mfumo wa "TRA" yao unatumika kukusanya sadaka kutoka kwa waumini ambao ni waajiriwa, halafu sadaka hiyo inakabidhiwa kwa makanisa yaliyosajili waumini wao. Lakini, mfumo huu unabagua baadhi ya madhehebu ya kidini.

Hivyo basi, kwa kuwa Sera zinazotenganisha dini na dola kwa kufuata mtindo wa Kijerumani zina ubaguzi; na kwa kuwa sera zinazotenganisha dini na dola kwa kufuata mtindo wa Kimarekani hazina ubaguzi, napendekeza yafuatayo:

  1. Kwamba, programu zote za kidini, ambazo kwa sababu hiyo ni programu za kisekta ziondolewe katika TBC;
  2. Kwamba, programu zote za kidini, ambazo kwa sababu hiyo ni programu za kisekta ziendeshwe kupitia vituo binafsi vya madhehebu ya kidini;
  3. Kwamba, TBC ijielekeze katika programu zenye kujenga umoja wa kitaifa kwa kueneza lugha ya Taifa, na sio lugha nyinginezo;
  4. Kwamba, utaratibu wa kusoma dua mwanzoni mwa shughuli za Bunge ufutwe.
  5. Kwamba, Bunge litunge sheria inayotoa mwongozo rasmi kuhusu sera ya kutenganisha dini na dola hapa nchini Tanzania. Yaweza kuitwa "The Separation of Religion and State Act of 2021."
Pingamizi tarajiwa na majibu yake

Kuna pingamizi moja naona laweza kuibuka dhidi ya hoja yangu hapo juu. Linahusu tafsiri potofu ya tunu ya uvumilivu. Kwa hiyo nalijibu mapema kabla halijaibuka.

Kuna watu watasema kuwa kwa sababu ya tunu ya uvumilivu tunayoikubali wote, basi inabidi haya yafanyike:

  1. Kwamba, madhehebu tofauti yapeane zamu ya kuhubiri katika vyombo vya habari vya Taifa;
  2. Kwamba, madhehebu tofauti yapeane zamu ya kuhubiri katika vituo vya mabasi barabarani;
  3. Kwamba, madhehebu tofauti yapeane zamu ya kuhubiri katika mabasi ya wasafiri;
  4. Kwamba, madhehebu tofauti yapeane zamu ya kuhubiri katika darasa lenye wanafunzi wale wale ndani ya shule moja;
  5. Kwamba, madhehebu tofauti yapeane zamu ya kufungua mkutano ule ule wa kiserikali;
  6. Kwamba, madhehebu tofauti yapeane zamu ya kusoma dua ya kufungua vikao vya Bunge;
  7. Na mifano mingine kama hiyo;

Napinga tafsiri hii ya neno "uvumilivu" kwa sababu ya maelezo yafuatayo, na ambayo yanakubaliana na kile ambacho tumekuwa tunafanya katika baadhi ya sehemu za maisha yetu ya kila siku.

Fikiria kwamba, kuna mtu A anayeamini kuwa kitendo X ni haramu kidini, na hivyo kuamini kuwa kitendo hiki kinapaswa kupingwa.

Lakini, kwa mujibu wa tunu ya uvumilivu, mtu A anatakiwa kuamini kwamba ni sahihi kujizuia kupinga kitendo X, endapo kitafanywa na mtu baki B, kwa sababu kitendo hicho ni miongoni mwa matendo yanayopaswa kuvumiliwa na wanajamii.

Kwa hiyo, uamuzi wa mtu A kuvumilia kitendo cha mtu B unaonekana kumaanisha kwamba, mtu A anakubali imani kwamba “X ni kitendo kinachopaswa kupingwa” na anakubali imani kwamba “X ni kitendo kisichopaswa kupingwa,” ambazo ni imani mbili zinazopingana kimantiki.

Hata hivyo, kama tunu ya uvumilivu ikitafsiriwa vizuri haitaonekana kuwa na mkanganyiko huu wa kimantiki. Kwa mujibu wa tafsiri sahihi ya tunu ya uvumilivu, kukubalika na kukataliwa kwa kitendo X kunategemea mazingira ya kitendo hicho.

Yaani, uvumilivu wa mtu A kuhusu imani X, katika mazingira M, haumaanishi kwamba mtu A anapaswa kuonyesha uvumilivu kuhusu imani X, katika kila mazingira mbali na mazingira M.

Ndio kusema kwamba, kitendo X sio haramu kila wakati, kila mahali na kwa kila mtendaji. Yaani, wema wa kitendo X, au ubaya wake, unategenea mazingira ambako kitendi hicho kitafanyika.

Kwa hiyo, tafsiri sahihi ya tunu ya uvumilivu iko hivi: fikiria kwamba kuna mtu A anayemaini kuwa kitendo X ni haramu kidini, na hivyo kuamini kuwa kitendo hiki kinapaswa kupingwa katika mazingira M.

Lakini, kwa mujibu wa tunu ya uvumilivu, mtu A anatakiwa kuamini kwamba ni sahihi kujizuia kupinga kitendo X, endapo kitafanywa na mtu baki B, kwa sababu kitendi hicho ni miongoni mwa matendo yanayopaswa kuvumiliwa katika mazingira N.

Kwa hiyo, uamuzi wa mtu A kuvumilia kitendo cha mtu B unamaanisha kwamba, mtu A anakubali imani kwamba “X ni kitendo kinachopaswa kupingwa” katika mazingira M na anakubali imani kwamba “X ni kitendo kisichopaswa kupingwa,” katika mazingira N.

Ukitumia somo hili katika mjadala wa sasa, maana yake ni hii: “X ni kitendo kinachopaswa kupingwa” katika mazingira M na anakubali imani kwamba “X ni kitendo kisichopaswa kupingwa,” katika mazingira N, ambapo:

  • X ni kitendo cha kuendesha programu za kisekta katika TV
  • M ni mazingira yanayohusisha TV ya Taifa TBC
  • N ni mazingira yanayohusisha TV ya taasisi ya kidini kama vile Tumaini TV, Iman TV, Upendo TV, nk.
  • Ambapo, mazingira M na mazingira N yote yanapatikana ndani ya nchi moja ya Tanzania.
Huu ndio uvumilivu tuliofundishwa tangu shule ya chekechea mpaka chuo kikuu, na sio vinginevyo.

Katika Taifa moja, lenye mseto wa kidini, lazima kuwepo na sehemu za umma mpana ambako programu za kisekta hazikanyagi. Maeneo hayo ni pamoja na:

  • Vyombo vya habari vya Taifa (Hapa, lugha ya Taifa ni alama na nyenzio ya kujenga Utaifa)
  • Shule za Taifa (Hapa sare ni alama na nyenzio ya kujenga Utaifa)
  • Vyuo vya Taifa (Hapa mtaala mmoja ni alama na nyenzio ya kujenga Utaifa)
  • Vituo vya usafiri wa umma (Hapa vituo vya mabasi ni mfano wa uwepo wa maslahi ya pamoja Kitaifa)
  • Maktaba za Taifa Hapa vitabu mmoja ni mfano wa uwepo wa maslahi ya pamoja Kitaifa)
  • Barabara za Taifa (Hapa barabara ni mfano wa uwepo wa maslahi ya pamoja Kitaifa)
  • Na kadhalika
Katika maeneo haya ni marufu kuendesha mihadhara ya kidini kama ambavyo tumekuwa tunashuhudia tangu DG wa TISS aliyepita na aliyekuwa na mrengo wa kilokole, alipopewa mamlaka ya kuongoza TISS. Tujisahihishe kuanzia leo.
Mwanasheria anapokosa wateja mda mrefu
 
View attachment 1792731
Dk. Ayub Chacha Rioba, Mkrugenzi Mtendaji wa TBC

Kwa kuzingatia matakwa ya katiba ya Tanzania, swali hapo juu linatokana na bonde la ufa lililopo kati ya yale ninayoyaona, na yale ninayoyatarajia kuhusiana na uendeshaji wa TBC.

Niliyoyaona TBC1

Tangu 15 Novemba 2020
nilipoikosoa TBC katika namna inavyotekeleza dhima yake ya kuelimisha umma juu ya COVID19 kwa kuzingatia misingi ya ukweli, ukweli wote na ukweli pekee, leo tena, tarehe 21 Mei 2021, nimeona matukio mawili yasiyo ya kawaida.
  1. Asubuhi kabla ya kipindi cha Bunge cha mswali na majibu TBC1 walirusha kipindi cha "Madrasa" kilichokuwa na ujumbe unaotembea kwa upande wa chini ukisomeka "Mashindano ya Kuhifadhi Kurani Tukufu kwa Waislamu Wanawake Yameandaliwa na Taasisi ya Kiislam ya African Relief Foundation." Kurani zilizokuwa zinasomwa zimeandikwa kwa Kiarabu.
  2. Mchana, mara tu baada ya matangazo ya Maadhimisho ya miaka 40 ya kuanzishwa kwa SADC, ambako Ayub Rioba alikuwa mwongozaji, kilifuata kipindi ncha swala ya Kiislamu. Swala ilianza kwa maelezo ya Kiarabu kwa dakika zipatazo tano.
Nafahamu pia kwamba, TBC1 imekuwa na kawaida ifuatayo:
  1. Kila alfajiri madhehebu ya dini tofauti hupewa muda wa kusoma sala ya asubuhi.
  2. Kila usiku wa kati, kabla ya saa sita, madhehebu ya dini tofauti hupewa muda wa kusoma sala ya kufunga siku.
  3. Kila Jumapili pia, madhehebu ya dini tofauti hupewa muda wa kusoma ibada za Jumapili.
Matarajio kwa mujibu wa Katiba

Katiba ya Tanzania, ibara ya 19(2) inasema kuwa, "shughuli na uendeshaji wa jumuiya za dini zitakuwa nje ya shughuli za mamlaka ya nchi."

Na ibara ya 4(1) inasema kuwa shughuli zote za Mamlaka ya Nchi katika Jamhuri ya Muungano zitatekelezwa na kudhibitiwa na vyombo vyenye mamlaka ya utendaji, mamlaka ya kutekeleza utoaji haki, na mamlaka ya kutunga sheria. Yaani, Serikali, Bunge, na Mahakama.

Hivyo, matarajio yangu ni kwamba, kwa kuwa TBC ni mali inayoendeshwa kwa kodi ya umma chini ya usimamizi wa serikali isiyofungamana na dini yoyote, basi yafuatayo yanapaswa kuonekana:

  1. Programu zenye sura ya kitaifa katika ngazi ya maudhui
  2. Programu zenye sura ya kitaifa katika ngazi ya lugha
Hii maana yake ni kwamba, yafuatayo hayapaswi kuonekana:
  1. Programu zenye sura ya kisekta katika ngazi ya maudhui
  2. Programu zenye sura ya kisekta katika ngazi ya lugha

Pia, nafahamu kuwa, dini nyingi tayari zinavyo vyombo vyake vya habari kwa ajili ya kuendesha shughuli zake. Kanisa Katoliki wana Tumaini TV, KKKT wana Upendo TV, Waislam wana Iman TV, Wapagani wa "Ramli TV," nk

Nakumbuka kuwa, kwa sehemu kubwa, sala nyingi za madhehebu ya KiIslamu zinatumia lugha ya Kiarabu, jambo ambalo linakiuka sera ya kujenga umoja wa kitaifa kwa kutumia lugha ya Taifa la Tanzania.

Hata ibada kadhaa na litania nyingi za Kikristo zinasomwa kwa lugha ya Kilatini ambayo sio lugha ya Taifa la Tanzania.

Nakumbuka kuna wakati Kardinali pengo alikuwa anaitwa na wazee wetu wa kule Mwenge Parokiani, Dar es Salaam, ili akawaendeshee ibada kwa lugha ya Kilatini, kama walivyokuwa wamezoea zamani, kabla Kanisa Katoliki halijatunga sera ya kuendesha ibada kwa Kiswahili na kimila.

Kwa hiyo, katika mazingira ya sasa, yafuatayo ni matarajio yangu:

  1. Kanisa Katoliki waendeshe programu zao za kisekta kupitia Tumaini TV,
  2. KKKT waendeshe programu zao za kisekta kupitia Upendo TV,
  3. Waislam waendeshe programu zao za kisekta kupitia Iman TV,
  4. Wapagani waendesha programu zao za kisekta kupitia "Ramli TV," nk
Uhalisia wa mambo

Pamoja na matarajio haya, uhalisia wa mambo ni kwamba, matakwa ya Katiba ya Tanzania kuhusu umuhimu na ulazima wa kutenganisha dini na dola hayajatimia kama ifyatavyo:

  1. Kanisa Katoliki wanaendesha programu zao za kisekta kupitia TBC1,
  2. KKKT wanaendesha programu zao za kisekta kupitia TBC1,
  3. Waislam wanaendesha programu zao za kisekta kupitia TBC1,
  4. Shughuli za Bunge zinaanza kwa kusoma dua kwa "Mola",
  5. Viapo vya watumishi wa umma vinamaliziwa kwa maneno "Ewe Mwenyezi Mungu Nisaidie," wakati Katiba ya nchi haitambui neno "Mungu."
Kama Katiba ya nchi inayakataza mambo haya, kwa nini tunayatenda, kama ambavyo mfano wa TBC1 leo umeonyesha?

Ni muhimu swali hili lijibiwe ili tujichunguze kama vyombo vya dola vinakweza maslahi ya vikundi na kutweza maslahi ya pamoja kitaifa, au vinginevyo.

Napendekeza kwamba ni kosa la kikatiba kutumia kodi ya raia asiye na dini kuhudumia taasisi za kidini. Ni kama ambavyo ni kosa kutumia kodi ya mtu asiye na chama cha siasa kutoa ruzuku kwa chama cha siasa. Kuna tatizo hapo.

Mapendekezo kuhusu mtazamo wa kisera

Nakumbusha kwamba, kote duniani, sera za kutenganisha dini na dola hugawanyika katika sehemu mbili:

  1. Sera zinazofuata mtindo wa Kimarekani.
  2. Sera zinazofuata mtindo wa Kijerumani.
Sera zinazofuata mtindo wa Kimarekani. Hapa, serikali huyapiga kisogo masuala yote ya dini, kiasi kwamba hakuna senti ya mlipa kodi inatumika kufadhili taasisi za kidini. Habari ya sijuo airtime kwa programu za kidini, sijui kufungua bunge kwa dua, hakuna.

Sera zinazofuata mtindo wa KIjerumani. Hapa, serikali haiyapigi kisogo masuala yote ya dini, kwani kuna senti fulani ya mlipa kodi inatumika kufadhili taasisi za kidini. Kwa mfano, huko Ujerumani, mfumo wa "TRA" yao unatumika kukusanya sadaka kutoka kwa waumini ambao ni waajiriwa, halafu sadaka hiyo inakabidhiwa kwa makanisa yaliyosajili waumini wao. Lakini, mfumo huu unabagua baadhi ya madhehebu ya kidini.

Hivyo basi, kwa kuwa Sera zinazotenganisha dini na dola kwa kufuata mtindo wa Kijerumani zina ubaguzi; na kwa kuwa sera zinazotenganisha dini na dola kwa kufuata mtindo wa Kimarekani hazina ubaguzi, napendekeza yafuatayo:

  1. Kwamba, programu zote za kidini, ambazo kwa sababu hiyo ni programu za kisekta ziondolewe katika TBC;
  2. Kwamba, programu zote za kidini, ambazo kwa sababu hiyo ni programu za kisekta ziendeshwe kupitia vituo binafsi vya madhehebu ya kidini;
  3. Kwamba, TBC ijielekeze katika programu zenye kujenga umoja wa kitaifa kwa kueneza lugha ya Taifa, na sio lugha nyinginezo;
  4. Kwamba, utaratibu wa kusoma dua mwanzoni mwa shughuli za Bunge ufutwe.
  5. Kwamba, Bunge litunge sheria inayotoa mwongozo rasmi kuhusu sera ya kutenganisha dini na dola hapa nchini Tanzania. Yaweza kuitwa "The Separation of Religion and State Act of 2021."
Pingamizi tarajiwa na majibu yake

Kuna pingamizi moja naona laweza kuibuka dhidi ya hoja yangu hapo juu. Linahusu tafsiri potofu ya tunu ya uvumilivu. Kwa hiyo nalijibu mapema kabla halijaibuka.

Kuna watu watasema kuwa kwa sababu ya tunu ya uvumilivu tunayoikubali wote, basi inabidi haya yafanyike:

  1. Kwamba, madhehebu tofauti yapeane zamu ya kuhubiri katika vyombo vya habari vya Taifa;
  2. Kwamba, madhehebu tofauti yapeane zamu ya kuhubiri katika vituo vya mabasi barabarani;
  3. Kwamba, madhehebu tofauti yapeane zamu ya kuhubiri katika mabasi ya wasafiri;
  4. Kwamba, madhehebu tofauti yapeane zamu ya kuhubiri katika darasa lenye wanafunzi wale wale ndani ya shule moja;
  5. Kwamba, madhehebu tofauti yapeane zamu ya kufungua mkutano ule ule wa kiserikali;
  6. Kwamba, madhehebu tofauti yapeane zamu ya kusoma dua ya kufungua vikao vya Bunge;
  7. Na mifano mingine kama hiyo;

Napinga tafsiri hii ya neno "uvumilivu" kwa sababu ya maelezo yafuatayo, na ambayo yanakubaliana na kile ambacho tumekuwa tunafanya katika baadhi ya sehemu za maisha yetu ya kila siku.

Fikiria kwamba, kuna mtu A anayeamini kuwa kitendo X ni haramu kidini, na hivyo kuamini kuwa kitendo hiki kinapaswa kupingwa.

Lakini, kwa mujibu wa tunu ya uvumilivu, mtu A anatakiwa kuamini kwamba ni sahihi kujizuia kupinga kitendo X, endapo kitafanywa na mtu baki B, kwa sababu kitendo hicho ni miongoni mwa matendo yanayopaswa kuvumiliwa na wanajamii.

Kwa hiyo, uamuzi wa mtu A kuvumilia kitendo cha mtu B unaonekana kumaanisha kwamba, mtu A anakubali imani kwamba “X ni kitendo kinachopaswa kupingwa” na anakubali imani kwamba “X ni kitendo kisichopaswa kupingwa,” ambazo ni imani mbili zinazopingana kimantiki.

Hata hivyo, kama tunu ya uvumilivu ikitafsiriwa vizuri haitaonekana kuwa na mkanganyiko huu wa kimantiki. Kwa mujibu wa tafsiri sahihi ya tunu ya uvumilivu, kukubalika na kukataliwa kwa kitendo X kunategemea mazingira ya kitendo hicho.

Yaani, uvumilivu wa mtu A kuhusu imani X, katika mazingira M, haumaanishi kwamba mtu A anapaswa kuonyesha uvumilivu kuhusu imani X, katika kila mazingira mbali na mazingira M.

Ndio kusema kwamba, kitendo X sio haramu kila wakati, kila mahali na kwa kila mtendaji. Yaani, wema wa kitendo X, au ubaya wake, unategenea mazingira ambako kitendi hicho kitafanyika.

Kwa hiyo, tafsiri sahihi ya tunu ya uvumilivu iko hivi: fikiria kwamba kuna mtu A anayemaini kuwa kitendo X ni haramu kidini, na hivyo kuamini kuwa kitendo hiki kinapaswa kupingwa katika mazingira M.

Lakini, kwa mujibu wa tunu ya uvumilivu, mtu A anatakiwa kuamini kwamba ni sahihi kujizuia kupinga kitendo X, endapo kitafanywa na mtu baki B, kwa sababu kitendi hicho ni miongoni mwa matendo yanayopaswa kuvumiliwa katika mazingira N.

Kwa hiyo, uamuzi wa mtu A kuvumilia kitendo cha mtu B unamaanisha kwamba, mtu A anakubali imani kwamba “X ni kitendo kinachopaswa kupingwa” katika mazingira M na anakubali imani kwamba “X ni kitendo kisichopaswa kupingwa,” katika mazingira N.

Ukitumia somo hili katika mjadala wa sasa, maana yake ni hii: “X ni kitendo kinachopaswa kupingwa” katika mazingira M na anakubali imani kwamba “X ni kitendo kisichopaswa kupingwa,” katika mazingira N, ambapo:

  • X ni kitendo cha kuendesha programu za kisekta katika TV
  • M ni mazingira yanayohusisha TV ya Taifa TBC
  • N ni mazingira yanayohusisha TV ya taasisi ya kidini kama vile Tumaini TV, Iman TV, Upendo TV, nk.
  • Ambapo, mazingira M na mazingira N yote yanapatikana ndani ya nchi moja ya Tanzania.
Huu ndio uvumilivu tuliofundishwa tangu shule ya chekechea mpaka chuo kikuu, na sio vinginevyo.

Katika Taifa moja, lenye mseto wa kidini, lazima kuwepo na sehemu za umma mpana ambako programu za kisekta hazikanyagi. Maeneo hayo ni pamoja na:

  • Vyombo vya habari vya Taifa (Hapa, lugha ya Taifa ni alama na nyenzio ya kujenga Utaifa)
  • Shule za Taifa (Hapa sare ni alama na nyenzio ya kujenga Utaifa)
  • Vyuo vya Taifa (Hapa mtaala mmoja ni alama na nyenzio ya kujenga Utaifa)
  • Vituo vya usafiri wa umma (Hapa vituo vya mabasi ni mfano wa uwepo wa maslahi ya pamoja Kitaifa)
  • Maktaba za Taifa Hapa vitabu mmoja ni mfano wa uwepo wa maslahi ya pamoja Kitaifa)
  • Barabara za Taifa (Hapa barabara ni mfano wa uwepo wa maslahi ya pamoja Kitaifa)
  • Na kadhalika
Katika maeneo haya ni marufu kuendesha mihadhara ya kidini kama ambavyo tumekuwa tunashuhudia tangu DG wa TISS aliyepita na aliyekuwa na mrengo wa kilokole, alipopewa mamlaka ya kuongoza TISS. Tujisahihishe kuanzia leo.
Kimingi hakuna swali

Mimi hi mkristu, na nimestruggle Sana kuona swali liko wapi

Huwezi kuandika maelezo page tatu justifying what you want people to believe and expect it to be a question

You bias took you far down the road exposing your hatred and intolerance over other religions
 
Haya maswali yako hayana mantiki
Samahani... we mwenzetu ni mgeni nchi hii? Au unataka kutuambia umeanza kutazama tiibiisii wakati huu wa SSH? wakati wa Mwendazake, JK, BM havikuwepo hivyo vipindi au enzi za AHM na JKN hukuwahi kusikiliza RTD vitu kama "inueni mioyo... Quran tukufu?"
JE WADHANI KWANINI RAIS SSH KAJA NA SALAAM MPYA YA KITAIFA? JE WADHANI KWANINI HIYO SALAAM YAKE BAADHI WANAIPINGA? Je kwanini wapo viongozi bado wanatoa salaam za kidini kwenye mikutano au vikao vya serikali ilhali serikali haina dini?
 
Umeenda mbali sana, inawezekana wakawa wanatumika bila wao kujua kama wanatumika.

Japo I highly doubt that kwani TBC ipo kwa ajili ya umma wa watanzania na Waislamu na Wakristu ni moja ya makundi makubwa yaliyopo.

Mfano. Siku kama ya leo Ijumaa Waislamu (kundi mojawapo) ndio huswali na lugha kuu inayotumika kwenye dini yao ni kiarabu, this is the reality we should face it is worldwide otherwise walazimishwe kubadili lugha which is not possible, coz watakuwa tofauti na wenzao duniani.

Same kwa wakristu siku ya jumapili nao hurushwa hewani bahati nzuri kwao lugha inayotumika ni kiswahili, I think this to you is not a problem.

Hicho kimekuwa intended kuwafikia walengwa pekee, ni kweli usemavyo Tanzania/serikali haina dini, lakini pia ukumbuke watu wake wana dini zao.

Hili naona tulikubali tu halikwepeki, au kama wataka kuondolewa vipindi vya dini TBC basi viondolewe vyote bila kujali lugha inayotumika.
Katika hoja ya imani si kweli wakristu na waislamu ndio makundi makubwa katika jamii ya watanzania. Wasio na imani hizo ndio kundi kubwa, japo hawapewi nafasi kwa sababu wenye uwezo wa kutoa nafasi wapo kati ya makundi hayo mawili. Ni dhuluma kutumia hela ya walipa kodi wasioa amini kuendesha mambo yasiyo wahusu.
 
Wahindu wanaokwenda kwenye mahekalu kumuabudu Krishna kipindi chao kipo lini?
Kumbuka wanaotazama hizo TV programs ni walewale wanaokwenda makanisani na misikitini, pia hivyo vipindi vinaonyeshwa siku za ibada zao tu na siyo siku zingine
 
Utaratibu wa sasa ni mzuri kuliko unavyotaka iwe.
Ni kweli kuna kupishana kwenye dini zetu, waislamu wataamini kile ambacho wakristo hawakiamini, hivyo pia wakristo watasema Yesu ni Mungu, ingawa waislam hawaamini hilo, lakini wanalazimika kuvumiliana.
Haya yasemwe kwenye vyombo kama hivi ili kuzidi kuimarisha tunu ya uvumilivu kwa kuwa hata mitaani tumechanganyika sana.
Kufanya ibada hizi kwenye vyombo kama TBC kunawalazimisha watu kama wewe kuzoea maisha ya kuvumilia, hasa pale unaposikia mafundisho yanayoenda kinyume na imani yako.
Kuhusu matumizi ya Lugha ya kiarabu kwenye kuendesha ibada za kiislam, hilo halikwepeki.
Moja wapo ya msingi muhimu wa ibada za waislam ni lugha.
Hakuna ibada kama haitumiki lugha ya kiarabu.
Madai ya kung'ang'ania Kiswahili pekee kwa sababu za kuimarisha umoja wetu hazina msingi.
Ndiyo maana kuna wakati hata viongozi wanatumia lugha nyingine za kigeni au za makabila yao ili kufikisha ujumbe fasaha kwa wasilkilizaji.
Vinginevyo TBC ni chombo cha walipa kodi wa Tanzania, ni haki yao kutumia chombo hicho bila kujali vyombo vingine ulivyotaja hata kama vitapewa masafa marefu zaidi.
Utaratibu huu umetumika miaka mingi, umekubalika na pande zote.
Ubaki kama ulivyo kwa afya ya umoja wetu.
 
..Mbona huku hoji haya hapo kabla..kwanini baada ya tangazo la mashindano ya kusoma qur'an tukufu? kwanini leo?
Actually hii post awali kabisa haikuwa detailed namna hii, nadhani imekuja kuwekwa nyama baadaye baada ya mjadala kuwa mzito.
 
Back
Top Bottom