Synthesizer
JF-Expert Member
- Feb 15, 2010
- 11,143
- 18,774
Ubaguzi wa rangi ni jambo linalochukiwa na wengi wa watu walio na akili timamu. Hata hivyo, katika nyanja nyingi linahalalishwa bila wengi wetu kuelewa. Kwa mfano, kwa nini Obama anasemwa kuwa raisi wa kwanza "black" wa Marekani wakati mama yake ni mzungu na baba yake mbantu? Kama ni halali Obama kujiita "black" kwa nini si halali yeye kujiita "white" wakati uzaliwa wake ni kwa ratio ya 50:50 black and white?
Nimeshashuhudia watu wakibeza pale mtu mchanganyiko wa mzungu na mbantu anaposema yeye ni mzungu. Kwa nini sio mzungu na bali ni "black"?
Kwa maoni yangu bado Marekani haijawa na raisi "black". Obama ni raisi "coloured" wa kwanza Marekani. Kumuita Obama "black" ni kuaendeleza kanuni ya Amerika ya Kusini iliyokuwa imezama katika kutumia watu weusi kama watumwa, ambapo ili uwe white lazima usiwe na hata chembe ya ubantu katika ukoo wako.
Nimeshashuhudia watu wakibeza pale mtu mchanganyiko wa mzungu na mbantu anaposema yeye ni mzungu. Kwa nini sio mzungu na bali ni "black"?
Kwa maoni yangu bado Marekani haijawa na raisi "black". Obama ni raisi "coloured" wa kwanza Marekani. Kumuita Obama "black" ni kuaendeleza kanuni ya Amerika ya Kusini iliyokuwa imezama katika kutumia watu weusi kama watumwa, ambapo ili uwe white lazima usiwe na hata chembe ya ubantu katika ukoo wako.