darubin ya mbao
JF-Expert Member
- Aug 3, 2016
- 1,893
- 4,023
Itifaki imezingatiwa,
Niende moja kwa moja kwenye mada, nimekua nikijiuliza hili swali kwanini tusitumie simu zetu za mkononi kupiga kura, hii itaokoa muda , gharama na ile adha ya kuwataka watu wakapige kura kwenye vituo walivyojiandikishia.
Nimepata wazo hili baada ya kuona mfumo fulani wa ugawaji wa mbolea kwa wakulima ambapo mkulima anaingiza taarifa zake kwa maana ya jina, mahali anapoishi, na namba ya kitambulisho cha mpiga kura kisha mwishoni anaweka idadi ya hekari anazolima , sasa huu mfumo ukiingiza namba ya mpiga kura mara mbili itakwambia kitambulisho hichi kimeshatumika kufanya usajili
Na baada ya usajili huo taarifa za mkulima huonekana kwenye App ya YARA connect ambapo kila kitu alichoingiza kitaonekana pale, ukitaka kuona ninachokisema bonyeza *149*46*16# kisha fuata maelekezo ni rahisa na ipo user friendly
Pia kuna hii mifumo ya kununua vifurushi vya mitandao ya simu za mkononi inaweza kuwa modified kidogo tu na kuwezesha upigaji wa kura, kama ambavyo tunachagua aina ya kifurushi basi kwenye kura tunachagua wagombea tunaowataka
Hapo juu nimetolea kama mifano tu ili mada ieleweke kwa wepesi lakini najua wataalamu wa IT wanaweza kutengeneza mfumo wa USSD tofauti na hiyo niliyoielezea hapo , na hivyo kufanya zoezi la kupiga kura liende kidigitali.
Niende moja kwa moja kwenye mada, nimekua nikijiuliza hili swali kwanini tusitumie simu zetu za mkononi kupiga kura, hii itaokoa muda , gharama na ile adha ya kuwataka watu wakapige kura kwenye vituo walivyojiandikishia.
Nimepata wazo hili baada ya kuona mfumo fulani wa ugawaji wa mbolea kwa wakulima ambapo mkulima anaingiza taarifa zake kwa maana ya jina, mahali anapoishi, na namba ya kitambulisho cha mpiga kura kisha mwishoni anaweka idadi ya hekari anazolima , sasa huu mfumo ukiingiza namba ya mpiga kura mara mbili itakwambia kitambulisho hichi kimeshatumika kufanya usajili
Na baada ya usajili huo taarifa za mkulima huonekana kwenye App ya YARA connect ambapo kila kitu alichoingiza kitaonekana pale, ukitaka kuona ninachokisema bonyeza *149*46*16# kisha fuata maelekezo ni rahisa na ipo user friendly
Pia kuna hii mifumo ya kununua vifurushi vya mitandao ya simu za mkononi inaweza kuwa modified kidogo tu na kuwezesha upigaji wa kura, kama ambavyo tunachagua aina ya kifurushi basi kwenye kura tunachagua wagombea tunaowataka
Hapo juu nimetolea kama mifano tu ili mada ieleweke kwa wepesi lakini najua wataalamu wa IT wanaweza kutengeneza mfumo wa USSD tofauti na hiyo niliyoielezea hapo , na hivyo kufanya zoezi la kupiga kura liende kidigitali.