Swali Gomvi: Korona 2.0 kwani Rais Magufuli ni mbia wa maisha yenu?

Go Corona Goooo.....
20210128_225622.jpg
 
Rais Magufuli anajua anachokifanya, pia anajua kuna Covid19 phase II. Ila ameona athari za kuruhusu lockdown ya Nchi nzima kama wengine wanavyofanya itaathiri Sana Raia wake kuliko kutoweka lockdown.

Watanzania ni maskini wa kutupwa, tusije kufa kwa njaa kabla ya Corona.

Muhimu alichosema ni kuchukua tahadhali za kujikinga. Tahadhari ulizosema hapo juu ni muhimu zikachukuliwa na kila mwananchi,

Ila kulikuwa na haja yeye Kama Amiri jeshi Mkuu aseme kwa kusisitiza kuhusu hilo.

Hatujitaji lockdown. Tunahitaji kukiri kuwa tuna tatizo na kisha kuchukua hatua (hasa za kitabibu). Kunawa mikono, kuvaa barakoa kufanya social distacing na kujifukiza ni mambo yaliyo mikononi mwa mtu mmoja mmoja! Huwezi kusema hakuna corona halafu ukasisitiza hatua hizo.

Kabla ya kutubu, kukiri ni mkosaji ni jambo la kwanza!!
 
Wizara ya afya ilishatoa muongozo jinsi ya kujikinga na korona, pia serikali ilitoa njia mbadala ikiwepo kujifukiza na kupiga nyungu. Si hivyo tu bali mashirika yasio ya kiserikali ikiwepo msalaba mwekundu, HPSS nk waliungana na wadau wengine wakiwepo akina mrisho mpoto kuzunguka nchi nzima na kutoa elimu ya korona ..

Katika hali isiyo ya kawaida watu wameziba masikio na kushinikiza Rais aseme, rais aseme... Watu wanaleta politics kwenye afya, ndio maana nikasema wanadeka.. mbona wanavaa kondomu wakienda kuzini? Nani anawafundisha? Ifike wakati siasa zikae pembeni na watu wajifunze kuwajibika. Lawama hazisaidii

Sent from my Android using JamiiForums mobile app
Wewe uko nchi gani?
Huu ni mlipuko mpya wa waka 2021, siyo ule wa mwaka 2020.

Usipowatangazia wananchi kuwa kuna tatizo limejitokeza tena na hivyo watu wajihadhari wengi wataenfelea kuamini kuwa tulishaishinda orona mwaka 2020 na hivyo hakuna tatizo tena kumbe lipo
 
Korona 2.0 Kwani Rais ana Ubia na Maisha Yenu?

Na. M. M. Mwanakijiji
Naandika kama shabiki wa Magufuli; naandika kama mtu ambaye nimeelewa malengo yake na mitazamo yake, na ninaandika kama mtu ambaye sijaegesha akili yangu mahali mwenyewe nikaondoka. Nimesoma na kufuatilia mijadala ya kile kinachodaiwa kuwa ni wimbi la pili (2.0) la maambukizi ya ugonjwa wa virusi vya corona (COVID-19) ambayo yanasemekana yanaendelea nchini mwetu. Wapo wengi ambao wanamuangalia Rais awape mwongozo wa nini cha kufanya na kwa kiasi kikubwa wanafanya hivyo kwa sababu Rais ndio kiongozi mkuu wa serikali na nchi.

Neno la Rais lina uzito wake, hofu za Rais zina uzito wake na ikumbukwe kuwa wengi wanachukulia kuwa kwa vile Rais ana watu wengi wanaomzunguka basi ana taarifa za mambo mengi ambayo labda watu nje ya serikali hawana. Aliposema watu wajifukize, mamilioni walijifukiza, aliposema watu wafunge na kuomba, watu walifunga na kuomba, aliposema watu waiage korona watu walifanya na send off! Na alipotangaza kuwa korona hakuna Tanzania na kuwa imekwisha watu waliamini hivyo.

Sasa hili wimbi la pili ni kweli? Kama ni kweli je Watanzania wafanye nini? Je, watu wanaokufa ni kweli wote wanakufa kwa korona au magonjwa mengine? Na kama wimbi hili kweli lipo kama nchi tufanye nini na kama mtu mmoja mmoja tufanye nini? Ni wazi msimamo wa serikali umetolewa na Rais jana huko Chato na kuwa hakuna mtendaji wa serikali atakayepingana na Rais kwenye hili isipokuwa kama yuko tayari kujiuzulu akipinga (resigning in protest). Kwa vile msimamo wa serikali unajulikana na kuwa serikali haitaleta lock down, na kuwa hata chanjo watu wafikirie mara mbilimbili basi sehemu ya nini kila mtu afanye ndio swali linalohitaji kujibiwa.

Ndugu zangu naandika kama shabiki; Watanzania msijitoe ufahamu na mkajifanya nyie fyatu! Rais si mbia wa maisha yenu, ya mababa na mama zenu, na wala si mbia wa maisha ya watoto wenu! Mnapougua, kuuguza na kuuguliwa yote hayo ni yenu; mauti yakiwafikia vilio ni kwenye nyumba zenu, jamaa, ndugu na marafiki zenu. Sasa kama hili ni kweli, kwanini watu wengine wafikiri wanaweza kuifanyia ibada imani ya mtu mwingine? Hivi, mnajua kwanini mitume wengine hawakuungana na Petro kujaribu kutembea juu ya maji japo wote walimuona Yesu akitembea juu ya maji na walimsikia Yesu akimwambia Petro atembee? (Mathayo 14:22-33).
View attachment 1687880

Rais Magufuli anaweza kuwa na imani kubwa kabisa hata ya kutembea juu ya maji na akatembea; lakini wangapi wanaamini kama yeye? Kama imani yako haijafikia ile ya Magufuli sasa unakanyaga maji ya nini?

Ndugu zangu kuna njia tatu/nne kubwa na za haraka za kupunguza maambukizi ya corona:

1. Vaa barakoa iliyotengenezwa na kitambaa cha pamba (siyo hariri). Kuvaa barakoa kuna kulinda wewe na kinamlinda mwingine. Ukivaa barakoa funika pua na mdomo (korona inaingia zaidi kupitia puani!)

2. Osha mikono kwa sabuni mara kwa mara; epuka kusalimiana na watu kwa kushikana mikono. Ikitokea hivyo hakikisha huingiza vidole midomoni au puani (jitahidi kuosha kabla ya kufanya hivyo na baada).

3. Jiweke umbali wa karibu mita moja kutoka kwa mtu mwingine ambaye si wa nyumbani mwako. Na hii inaendana na kuepuka misongamano isiyo ya lazima hasa mahali ambapo watu hawavai barakoa. Na wale wenye ndugu (wazazi, mababu wazee) waambieni wasiende makanisani au misikitini kwa wakati huu au makanisa na misikiti iweke taratibu za kuhakikisha watu wanakaa mbalimbali na wanavaa barakoa!

4. Jifukize nyungu; sijui ni kwa namna gani hii ilisaidie kuzuia wimbi la kwanza lakini kama watu watafanya tena na kwa wingi wao mnaweza kujikuta mnazuia tena wimbi hili la pili maana kama ni chanjo msijipe matumaini saini.

Njia hizo tatu ndio njia zitakazokinga maisha yako na maisha ya wale uwapendeo. Lakini kama unafikiria Rais ana ubia na maisha yako haya we. Kwa sababu lile swali la bahati nasibu ya Magufuli kama italipa bado linasimama.
Kwahiyo maneno mengi kumbe umeukana leo msimamo wa rolimodo wako .
 
Rais Magufuli anajua anachokifanya, pia anajua kuna Covid19 phase II. Ila ameona athari za kuruhusu lockdown ya Nchi nzima kama wengine wanavyofanya itaathiri Sana Raia wake kuliko kutoweka lockdown.

Watanzania ni maskini wa kutupwa, tusije kufa kwa njaa kabla ya Corona.

Muhimu alichosema ni kuchukua tahadhali za kujikinga. Tahadhari ulizosema hapo juu ni muhimu zikachukuliwa na kila mwananchi,

Ila kulikuwa na haja yeye Kama Amiri jeshi Mkuu aseme kwa kusisitiza kuhusu hilo.
Lockdown siyo suluhisho zuri kwa aina ya maisha ya wengi wetu kwenye jamii yetu.
Kuongelea hadharani uwepo wa ugonjwa, kukumbushana njia zinazo sadikika kupunguza kasi ya maambukizi ndiyo suluhisho zuri kwa muda uu, na ndiyo zilitusaidia wakati wa wimbi la kwanza la COVID-19.

Hakuna ushahidi mzuri wa kisayansi na unao onesha sala zilitusaidia
 
Huku hakukuwa na utafiti lakini alipanga foleni ili apate kikombe cha Babu, lakini chanjo ya MABEBERU iliyofanyiwa utafiti anaikana! WANAFIKI bana!
1611879414145.jpeg

Korona 2.0 Kwani Rais ana Ubia na Maisha Yenu?


Na. M. M. Mwanakijiji
Naandika kama shabiki wa Magufuli; naandika kama mtu ambaye nimeelewa malengo yake na mitazamo yake, na ninaandika kama mtu ambaye sijaegesha akili yangu mahali mwenyewe nikaondoka. Nimesoma na kufuatilia mijadala ya kile kinachodaiwa kuwa ni wimbi la pili (2.0) la maambukizi ya ugonjwa wa virusi vya corona (COVID-19) ambayo yanasemekana yanaendelea nchini mwetu. Wapo wengi ambao wanamuangalia Rais awape mwongozo wa nini cha kufanya na kwa kiasi kikubwa wanafanya hivyo kwa sababu Rais ndio kiongozi mkuu wa serikali na nchi.

Neno la Rais lina uzito wake, hofu za Rais zina uzito wake na ikumbukwe kuwa wengi wanachukulia kuwa kwa vile Rais ana watu wengi wanaomzunguka basi ana taarifa za mambo mengi ambayo labda watu nje ya serikali hawana. Aliposema watu wajifukize, mamilioni walijifukiza, aliposema watu wafunge na kuomba, watu walifunga na kuomba, aliposema watu waiage korona watu walifanya na send off! Na alipotangaza kuwa korona hakuna Tanzania na kuwa imekwisha watu waliamini hivyo.

Sasa hili wimbi la pili ni kweli? Kama ni kweli je Watanzania wafanye nini? Je, watu wanaokufa ni kweli wote wanakufa kwa korona au magonjwa mengine? Na kama wimbi hili kweli lipo kama nchi tufanye nini na kama mtu mmoja mmoja tufanye nini? Ni wazi msimamo wa serikali umetolewa na Rais jana huko Chato na kuwa hakuna mtendaji wa serikali atakayepingana na Rais kwenye hili isipokuwa kama yuko tayari kujiuzulu akipinga (resigning in protest). Kwa vile msimamo wa serikali unajulikana na kuwa serikali haitaleta lock down, na kuwa hata chanjo watu wafikirie mara mbilimbili basi sehemu ya nini kila mtu afanye ndio swali linalohitaji kujibiwa.

Ndugu zangu naandika kama shabiki; Watanzania msijitoe ufahamu na mkajifanya nyie fyatu! Rais si mbia wa maisha yenu, ya mababa na mama zenu, na wala si mbia wa maisha ya watoto wenu! Mnapougua, kuuguza na kuuguliwa yote hayo ni yenu; mauti yakiwafikia vilio ni kwenye nyumba zenu, jamaa, ndugu na marafiki zenu. Sasa kama hili ni kweli, kwanini watu wengine wafikiri wanaweza kuifanyia ibada imani ya mtu mwingine? Hivi, mnajua kwanini mitume wengine hawakuungana na Petro kujaribu kutembea juu ya maji japo wote walimuona Yesu akitembea juu ya maji na walimsikia Yesu akimwambia Petro atembee? (Mathayo 14:22-33).
View attachment 1687880

Rais Magufuli anaweza kuwa na imani kubwa kabisa hata ya kutembea juu ya maji na akatembea; lakini wangapi wanaamini kama yeye? Kama imani yako haijafikia ile ya Magufuli sasa unakanyaga maji ya nini?

Ndugu zangu kuna njia tatu/nne kubwa na za haraka za kupunguza maambukizi ya corona:

1. Vaa barakoa iliyotengenezwa na kitambaa cha pamba (siyo hariri). Kuvaa barakoa kuna kulinda wewe na kinamlinda mwingine. Ukivaa barakoa funika pua na mdomo (korona inaingia zaidi kupitia puani!)

2. Osha mikono kwa sabuni mara kwa mara; epuka kusalimiana na watu kwa kushikana mikono. Ikitokea hivyo hakikisha huingiza vidole midomoni au puani (jitahidi kuosha kabla ya kufanya hivyo na baada).

3. Jiweke umbali wa karibu mita moja kutoka kwa mtu mwingine ambaye si wa nyumbani mwako. Na hii inaendana na kuepuka misongamano isiyo ya lazima hasa mahali ambapo watu hawavai barakoa. Na wale wenye ndugu (wazazi, mababu wazee) waambieni wasiende makanisani au misikitini kwa wakati huu au makanisa na misikiti iweke taratibu za kuhakikisha watu wanakaa mbalimbali na wanavaa barakoa!

4. Jifukize nyungu; sijui ni kwa namna gani hii ilisaidie kuzuia wimbi la kwanza lakini kama watu watafanya tena na kwa wingi wao mnaweza kujikuta mnazuia tena wimbi hili la pili maana kama ni chanjo msijipe matumaini saini.

Njia hizo tatu ndio njia zitakazokinga maisha yako na maisha ya wale uwapendeo. Lakini kama unafikiria Rais ana ubia na maisha yako haya we. Kwa sababu lile swali la bahati nasibu ya Magufuli kama italipa bado linasimama.
 
Lockdown siyo suluhisho zuri kwa aina ya maisha ya wengi wetu kwenye jamii yetu.
Kuongelea hadharani uwepo wa ugonjwa, kukumbushana njia zinazo sadikika kupunguza kasi ya maambukizi ndiyo suluhisho zuri kwa muda uu, na ndiyo zilitusaidia wakati wa wimbi la kwanza la COVID-19.

Hakuna ushahidi mzuri wa kisayansi na unao onesha sala zilitusaidia
Umemaliza kila kitu Mkuu

Cc
Washauri wa Mkuu
 
Wewe uko nchi gani?
Huu ni mlipuko mpya wa waka 2021, siyo ule wa mwaka 2020.

Usipowatangazia wananchi kuwa kuna tatizo limejitokeza tena na hivyo watu wajihadhari wengi wataenfelea kuamini kuwa tulishaishinda orona mwaka 2020 na hivyo hakuna tatizo tena kumbe lipo
Corona ya 2020 na hii ya 2021 ni ileile, njia za kujikinga ni zile zile, social distancing, barakoa nk... Sasa watangaze nini cha ziada?? Nini kimeongezeka kwenye korona hii?

Sent from my Android using JamiiForums mobile app
 
Kuna watu wanadhania au wanaombea Magufuli abadilike.....JPM Yuko alivyo hawezi kuwa tofauti na alivyo...la maana ni watu kufanya maamuzi wakizingatia ukweli huu. Kawaambia hakuna lockdown, anabeza chanjo, hajakubali uwepo na ukali wa korona..Sasa leo mnataka aamke ale matapishi yake, Mara ya mwisho kukiri amekosea ilikuwa lini!? Amkeni msijitoe ufahamu...Linda maisha Yako, ya ndugu zako....we endekeza kumngojea Magufuli...
Hapa nimekuelewa na sitakuandikia gazeti refu kukujibu.

Ni kwamba, anayewaongoza waTanzania yupo kwenye madaraka hayo kwa njia batili kwa sababu kalazimisha kuwepo kwenye uongozi na waTanzania hawana lolote wanaloweza kufanya kumwondoa hapo hata kama wanaona anafanya makosa na anatabia zake mbaya asizoweza kuzibadili.

Njia unayopendekeza ni kwa waTanzania wampuuze, wasimsikilize, wafanye wanayoona yanawafaa wao, kila mtu kwa njia zake mwenyewe, kwani hakuna kiongozi mwingine wa kuwaunganisha wafanye mambo wanayoona kuwa ni kwa manufaa yao na taifa lao.

Usilopendekeza hapa kwa maksudi ni kuwasihi waTanzania waungane kwa umoja wao kukataa makosa anayofanya, bali unaona ni bora waendelee kuvumilia makosa anayofanya kwa wao kujifanyia ya kwao kila mmoja kwa njia zake mwenyewe azijuazo. Hupendekezi kwa umoja wao waungane na watafute njia za pamoja za kuondoa tatizo.
 
Nyie mashabiki mtapoteza wengi maana kila jambo mnaingiza ushabiki.
 
Basi kifuatacho nadhani kusiwe na Rais kabisa nchi hii.

Kwasababu mnakwepa majukumu ya dhahiri kwa vijisababu vya kijinga tu wakati mnatumbua kodi za walalahoi kwa kazi hiyo.

Yaani pesa na treatment za kifahari zinazotokana na kodi za walalahoi mnataka ila majukumu yake HAMTAKI.

Mtanzania akipigwa marufuku kwenda nchi za ng'ambo anaweza kutatua vipi hali hiyo peke yake ?

( Je, Raia wa kawaida anaweza kurejesha confidence ya nchi kwa watu wa mataifa mengine )
Tunawalaumu China kwa kutodhibiti ugonjwa mpaka unausumbua dunia, leo tena wengine wanapambana, halafu sisi tupo tupo tu tumekaa, tunasubiri wakimaliza, tuwapelekee.

Je, mikusanyiko mikubwa kama shule raia wa kawaida ana nafasi gani hapo bila Mwongozo ??

Je, ukubwa wa Tatizo ukoje hizi taarifa mwananchi wa kawaida anazipataje ili ajilinde. Knowledge is power.

Wewe Jamaa ni mwehu. Magu huyo anaetandika watu risasi 36 na kutaka wakazikwe haraka haraka ndio mwenye imani ya Petro. Yuko wapi Azory Gwanda, Kanguye, Ben Saanane, enyi wacha mungu ??

Sasa kama imani ndio imekuwa kimbilio la Magufuli, hao maaskari wenye mabunduki na helkopter za ulinzi anatembeatembea nazo za nini ??

Anyway, sasa tuanze kutibu MARALIA, TYPHOID, KIPINDU PINDU, UKIMWI, kwa imani ya Petro.

Kila kitu cha wazungu ni kibaya na hakifai isipokuwa pesa zao, mabomu ya machozi, vifaru vya kijeshi, mabunduki, magari ya washa washa, , vx-v8
😂😂😂 Facts za wenye chuki na kinyongo😂😂, anyway v8 hazichukuliw zinanunuliwa, mm mwenyew nimejinunulia binafs ya kutembelea, fanya Kaz chuki ipungue
 
Back
Top Bottom