Swali Gomvi: Korona 2.0 kwani Rais Magufuli ni mbia wa maisha yenu?

Kwanza hakuna anaetaka Lock down pia usisahau umaskini huo wao ndio wamewatengenezea watanganyika!

Sent from my Nokia 8.1 using JamiiForums mobile app
Mkuu usitake kufukua makabuli kuhusu umaskini wetu, muhimu tumshinde adui wetu Corona.

Unajua viongozi wengine wamelala usingizi wa milele, you can do nothing to them
 
Kwa hiyo tuseme katika vita hii hatuna nahodha? Kuwa kila mtu awe na lwake?
Na je kazi za Rais wa nchi kipindi cha majanga ni zipi? Je mataifa mengine viongozi wao wanachukua hatua gani?.
Watu wanadeka sana... Wanasubiri Rais aseme ndio wachukue hatua, sasa ni kuwaacha waendelee kulalama. Na pia chanjo kama wanaitaka wasafiri huko nje hata malawi wakaipate.

Suala la afya linaanza na mtu binafsi, kama huwezi kulinda familia yako basi mtaangamia na kulalamika ambapo pia itakua ni dua la kuku kwa mwewe.
 
Korona 2.0 Kwani Rais ana Ubia na Maisha Yenu?

Na. M. M. Mwanakijiji
Naandika kama shabiki wa Magufuli; naandika kama mtu ambaye nimeelewa malengo yake na mitazamo yake, na ninaandika kama mtu ambaye sijaegesha akili yangu mahali mwenyewe nikaondoka. Nimesoma na kufuatilia mijadala ya kile kinachodaiwa kuwa ni wimbi la pili (2.0) la maambukizi ya ugonjwa wa virusi vya corona (COVID-19) ambayo yanasemekana yanaendelea nchini mwetu. Wapo wengi ambao wanamuangalia Rais awape mwongozo wa nini cha kufanya na kwa kiasi kikubwa wanafanya hivyo kwa sababu Rais ndio kiongozi mkuu wa serikali na nchi.

Neno la Rais lina uzito wake, hofu za Rais zina uzito wake na ikumbukwe kuwa wengi wanachukulia kuwa kwa vile Rais ana watu wengi wanaomzunguka basi ana taarifa za mambo mengi ambayo labda watu nje ya serikali hawana. Aliposema watu wajifukize, mamilioni walijifukiza, aliposema watu wafunge na kuomba, watu walifunga na kuomba, aliposema watu waiage korona watu walifanya na send off! Na alipotangaza kuwa korona hakuna Tanzania na kuwa imekwisha watu waliamini hivyo.

Sasa hili wimbi la pili ni kweli? Kama ni kweli je Watanzania wafanye nini? Je, watu wanaokufa ni kweli wote wanakufa kwa korona au magonjwa mengine? Na kama wimbi hili kweli lipo kama nchi tufanye nini na kama mtu mmoja mmoja tufanye nini? Ni wazi msimamo wa serikali umetolewa na Rais jana huko Chato na kuwa hakuna mtendaji wa serikali atakayepingana na Rais kwenye hili isipokuwa kama yuko tayari kujiuzulu akipinga (resigning in protest). Kwa vile msimamo wa serikali unajulikana na kuwa serikali haitaleta lock down, na kuwa hata chanjo watu wafikirie mara mbilimbili basi sehemu ya nini kila mtu afanye ndio swali linalohitaji kujibiwa.

Ndugu zangu naandika kama shabiki; Watanzania msijitoe ufahamu na mkajifanya nyie fyatu! Rais si mbia wa maisha yenu, ya mababa na mama zenu, na wala si mbia wa maisha ya watoto wenu! Mnapougua, kuuguza na kuuguliwa yote hayo ni yenu; mauti yakiwafikia vilio ni kwenye nyumba zenu, jamaa, ndugu na marafiki zenu. Sasa kama hili ni kweli, kwanini watu wengine wafikiri wanaweza kuifanyia ibada imani ya mtu mwingine? Hivi, mnajua kwanini mitume wengine hawakuungana na Petro kujaribu kutembea juu ya maji japo wote walimuona Yesu akitembea juu ya maji na walimsikia Yesu akimwambia Petro atembee? (Mathayo 14:22-33).
View attachment 1687880

Rais Magufuli anaweza kuwa na imani kubwa kabisa hata ya kutembea juu ya maji na akatembea; lakini wangapi wanaamini kama yeye? Kama imani yako haijafikia ile ya Magufuli sasa unakanyaga maji ya nini?

Ndugu zangu kuna njia tatu/nne kubwa na za haraka za kupunguza maambukizi ya corona:

1. Vaa barakoa iliyotengenezwa na kitambaa cha pamba (siyo hariri). Kuvaa barakoa kuna kulinda wewe na kinamlinda mwingine. Ukivaa barakoa funika pua na mdomo (korona inaingia zaidi kupitia puani!)

2. Osha mikono kwa sabuni mara kwa mara; epuka kusalimiana na watu kwa kushikana mikono. Ikitokea hivyo hakikisha huingiza vidole midomoni au puani (jitahidi kuosha kabla ya kufanya hivyo na baada).

3. Jiweke umbali wa karibu mita moja kutoka kwa mtu mwingine ambaye si wa nyumbani mwako. Na hii inaendana na kuepuka misongamano isiyo ya lazima hasa mahali ambapo watu hawavai barakoa. Na wale wenye ndugu (wazazi, mababu wazee) waambieni wasiende makanisani au misikitini kwa wakati huu au makanisa na misikiti iweke taratibu za kuhakikisha watu wanakaa mbalimbali na wanavaa barakoa!

4. Jifukize nyungu; sijui ni kwa namna gani hii ilisaidie kuzuia wimbi la kwanza lakini kama watu watafanya tena na kwa wingi wao mnaweza kujikuta mnazuia tena wimbi hili la pili maana kama ni chanjo msijipe matumaini saini.

Njia hizo tatu ndio njia zitakazokinga maisha yako na maisha ya wale uwapendeo. Lakini kama unafikiria Rais ana ubia na maisha yako haya we. Kwa sababu lile swali la bahati nasibu ya Magufuli kama italipa bado linasimama.

hakuna nchi tam kama tanzania, yaaani tunajiamulia mambo yetu! kuna wale wanawake wa ufipa wao mpaka amsterdam awape mwongozo
 
Kuna watu wanadhania au wanaombea Magufuli abadilike.....JPM Yuko alivyo hawezi kuwa tofauti na alivyo...la maana ni watu kufanya maamuzi wakizingatia ukweli huu. Kawaambia hakuna lockdown, anabeza chanjo, hajakubali uwepo na ukali wa korona..Sasa leo mnataka aamke ale matapishi yake, Mara ya mwisho kukiri amekosea ilikuwa lini!? Amkeni msijitoe ufahamu...Linda maisha Yako, ya ndugu zako....we endekeza kumngojea Magufuli...
 
Wewe mleta mada hujui wajibu wa raisi kwenye issue ya collective effort ya kupambana na pandemic?

Kwamba raisi
1. Aendelee kuachia watalii wanaotoka nchi zenye korona waingie ndani ya nchi Lakini sisi tuendelee kujikinga tu na korona hiyo maana ni issue binafsi?

2. Aendelee kukandia na kudiscourage uvaaji wa barakoa kila apatapo nafasi ya kukutana na hadhara?
 
Kuna watu wanadhania au wanaombea Magufuli abadilike.....JPM Yuko alivyo hawezi kuwa tofauti na alivyo...la maana ni watu kufanya maamuzi wakizingatia ukweli huu. Kawaambia hakuna lockdown, anabeza chanjo, hajakubali uwepo na ukali wa korona..Sasa leo mnataka aamke ale matapishi yake, Mara ya mwisho kukiri amekosea ilikuwa lini!? Amkeni msijitoe ufahamu...Linda maisha Yako, ya ndugu zako....we endekeza kumngojea Magufuli...
Tusaidie kumueleza ukweli.

Ushabiki wenu ambao ni unconditional ndiyo unampa nguvu kuendelea kuhatarisha maisha ya wananchi

Sisi wenye access ya mitandao tuna nafuu kujua hali ya korona inaendaje, bali mamilioni ya wananchi wanaotegemea channel za serikali na mainstream media kuelimika na janga hili wapo hatarini maana hawapati taarifa sahihi kutokana serikali kutotaka kutoa elimu sahihi na endelevu ya hili janga.

Raisi anaponda barakoa kila akipata nafasi na anareward tabia ya kutovaa barakoa kwa kuwapongeza wasiozivaa, hapo unaona hakuna shida?
 
Korona 2.0 Kwani Rais ana Ubia na Maisha Yenu?

Na. M. M. Mwanakijiji
Naandika kama shabiki wa Magufuli; naandika kama mtu ambaye nimeelewa malengo yake na mitazamo yake, na ninaandika kama mtu ambaye sijaegesha akili yangu mahali mwenyewe nikaondoka. Nimesoma na kufuatilia mijadala ya kile kinachodaiwa kuwa ni wimbi la pili (2.0) la maambukizi ya ugonjwa wa virusi vya corona (COVID-19) ambayo yanasemekana yanaendelea nchini mwetu. Wapo wengi ambao wanamuangalia Rais awape mwongozo wa nini cha kufanya na kwa kiasi kikubwa wanafanya hivyo kwa sababu Rais ndio kiongozi mkuu wa serikali na nchi.

Neno la Rais lina uzito wake, hofu za Rais zina uzito wake na ikumbukwe kuwa wengi wanachukulia kuwa kwa vile Rais ana watu wengi wanaomzunguka basi ana taarifa za mambo mengi ambayo labda watu nje ya serikali hawana. Aliposema watu wajifukize, mamilioni walijifukiza, aliposema watu wafunge na kuomba, watu walifunga na kuomba, aliposema watu waiage korona watu walifanya na send off! Na alipotangaza kuwa korona hakuna Tanzania na kuwa imekwisha watu waliamini hivyo.

Sasa hili wimbi la pili ni kweli? Kama ni kweli je Watanzania wafanye nini? Je, watu wanaokufa ni kweli wote wanakufa kwa korona au magonjwa mengine? Na kama wimbi hili kweli lipo kama nchi tufanye nini na kama mtu mmoja mmoja tufanye nini? Ni wazi msimamo wa serikali umetolewa na Rais jana huko Chato na kuwa hakuna mtendaji wa serikali atakayepingana na Rais kwenye hili isipokuwa kama yuko tayari kujiuzulu akipinga (resigning in protest). Kwa vile msimamo wa serikali unajulikana na kuwa serikali haitaleta lock down, na kuwa hata chanjo watu wafikirie mara mbilimbili basi sehemu ya nini kila mtu afanye ndio swali linalohitaji kujibiwa.

Ndugu zangu naandika kama shabiki; Watanzania msijitoe ufahamu na mkajifanya nyie fyatu! Rais si mbia wa maisha yenu, ya mababa na mama zenu, na wala si mbia wa maisha ya watoto wenu! Mnapougua, kuuguza na kuuguliwa yote hayo ni yenu; mauti yakiwafikia vilio ni kwenye nyumba zenu, jamaa, ndugu na marafiki zenu. Sasa kama hili ni kweli, kwanini watu wengine wafikiri wanaweza kuifanyia ibada imani ya mtu mwingine? Hivi, mnajua kwanini mitume wengine hawakuungana na Petro kujaribu kutembea juu ya maji japo wote walimuona Yesu akitembea juu ya maji na walimsikia Yesu akimwambia Petro atembee? (Mathayo 14:22-33).
View attachment 1687880

Rais Magufuli anaweza kuwa na imani kubwa kabisa hata ya kutembea juu ya maji na akatembea; lakini wangapi wanaamini kama yeye? Kama imani yako haijafikia ile ya Magufuli sasa unakanyaga maji ya nini?

Ndugu zangu kuna njia tatu/nne kubwa na za haraka za kupunguza maambukizi ya corona:

1. Vaa barakoa iliyotengenezwa na kitambaa cha pamba (siyo hariri). Kuvaa barakoa kuna kulinda wewe na kinamlinda mwingine. Ukivaa barakoa funika pua na mdomo (korona inaingia zaidi kupitia puani!)

2. Osha mikono kwa sabuni mara kwa mara; epuka kusalimiana na watu kwa kushikana mikono. Ikitokea hivyo hakikisha huingiza vidole midomoni au puani (jitahidi kuosha kabla ya kufanya hivyo na baada).

3. Jiweke umbali wa karibu mita moja kutoka kwa mtu mwingine ambaye si wa nyumbani mwako. Na hii inaendana na kuepuka misongamano isiyo ya lazima hasa mahali ambapo watu hawavai barakoa. Na wale wenye ndugu (wazazi, mababu wazee) waambieni wasiende makanisani au misikitini kwa wakati huu au makanisa na misikiti iweke taratibu za kuhakikisha watu wanakaa mbalimbali na wanavaa barakoa!

4. Jifukize nyungu; sijui ni kwa namna gani hii ilisaidie kuzuia wimbi la kwanza lakini kama watu watafanya tena na kwa wingi wao mnaweza kujikuta mnazuia tena wimbi hili la pili maana kama ni chanjo msijipe matumaini saini.

Njia hizo tatu ndio njia zitakazokinga maisha yako na maisha ya wale uwapendeo. Lakini kama unafikiria Rais ana ubia na maisha yako haya we. Kwa sababu lile swali la bahati nasibu ya Magufuli kama italipa bado linasimama.

Mwanakijiji naona mwaka huu wamekuombea na utaacha ushabiki urudi kama yule Mwanakijiji wa 2007 tunaye mjua
 
Korona 2.0 Kwani Rais ana Ubia na Maisha Yenu?

Na. M. M. Mwanakijiji
Naandika kama shabiki wa Magufuli; naandika kama mtu ambaye nimeelewa malengo yake na mitazamo yake, na ninaandika kama mtu ambaye sijaegesha akili yangu mahali mwenyewe nikaondoka. Nimesoma na kufuatilia mijadala ya kile kinachodaiwa kuwa ni wimbi la pili (2.0) la maambukizi ya ugonjwa wa virusi vya corona (COVID-19) ambayo yanasemekana yanaendelea nchini mwetu. Wapo wengi ambao wanamuangalia Rais awape mwongozo wa nini cha kufanya na kwa kiasi kikubwa wanafanya hivyo kwa sababu Rais ndio kiongozi mkuu wa serikali na nchi.

Neno la Rais lina uzito wake, hofu za Rais zina uzito wake na ikumbukwe kuwa wengi wanachukulia kuwa kwa vile Rais ana watu wengi wanaomzunguka basi ana taarifa za mambo mengi ambayo labda watu nje ya serikali hawana. Aliposema watu wajifukize, mamilioni walijifukiza, aliposema watu wafunge na kuomba, watu walifunga na kuomba, aliposema watu waiage korona watu walifanya na send off! Na alipotangaza kuwa korona hakuna Tanzania na kuwa imekwisha watu waliamini hivyo.

Sasa hili wimbi la pili ni kweli? Kama ni kweli je Watanzania wafanye nini? Je, watu wanaokufa ni kweli wote wanakufa kwa korona au magonjwa mengine? Na kama wimbi hili kweli lipo kama nchi tufanye nini na kama mtu mmoja mmoja tufanye nini? Ni wazi msimamo wa serikali umetolewa na Rais jana huko Chato na kuwa hakuna mtendaji wa serikali atakayepingana na Rais kwenye hili isipokuwa kama yuko tayari kujiuzulu akipinga (resigning in protest). Kwa vile msimamo wa serikali unajulikana na kuwa serikali haitaleta lock down, na kuwa hata chanjo watu wafikirie mara mbilimbili basi sehemu ya nini kila mtu afanye ndio swali linalohitaji kujibiwa.

Ndugu zangu naandika kama shabiki; Watanzania msijitoe ufahamu na mkajifanya nyie fyatu! Rais si mbia wa maisha yenu, ya mababa na mama zenu, na wala si mbia wa maisha ya watoto wenu! Mnapougua, kuuguza na kuuguliwa yote hayo ni yenu; mauti yakiwafikia vilio ni kwenye nyumba zenu, jamaa, ndugu na marafiki zenu. Sasa kama hili ni kweli, kwanini watu wengine wafikiri wanaweza kuifanyia ibada imani ya mtu mwingine? Hivi, mnajua kwanini mitume wengine hawakuungana na Petro kujaribu kutembea juu ya maji japo wote walimuona Yesu akitembea juu ya maji na walimsikia Yesu akimwambia Petro atembee? (Mathayo 14:22-33).
View attachment 1687880

Rais Magufuli anaweza kuwa na imani kubwa kabisa hata ya kutembea juu ya maji na akatembea; lakini wangapi wanaamini kama yeye? Kama imani yako haijafikia ile ya Magufuli sasa unakanyaga maji ya nini?

Ndugu zangu kuna njia tatu/nne kubwa na za haraka za kupunguza maambukizi ya corona:

1. Vaa barakoa iliyotengenezwa na kitambaa cha pamba (siyo hariri). Kuvaa barakoa kuna kulinda wewe na kinamlinda mwingine. Ukivaa barakoa funika pua na mdomo (korona inaingia zaidi kupitia puani!)

2. Osha mikono kwa sabuni mara kwa mara; epuka kusalimiana na watu kwa kushikana mikono. Ikitokea hivyo hakikisha huingiza vidole midomoni au puani (jitahidi kuosha kabla ya kufanya hivyo na baada).

3. Jiweke umbali wa karibu mita moja kutoka kwa mtu mwingine ambaye si wa nyumbani mwako. Na hii inaendana na kuepuka misongamano isiyo ya lazima hasa mahali ambapo watu hawavai barakoa. Na wale wenye ndugu (wazazi, mababu wazee) waambieni wasiende makanisani au misikitini kwa wakati huu au makanisa na misikiti iweke taratibu za kuhakikisha watu wanakaa mbalimbali na wanavaa barakoa!

4. Jifukize nyungu; sijui ni kwa namna gani hii ilisaidie kuzuia wimbi la kwanza lakini kama watu watafanya tena na kwa wingi wao mnaweza kujikuta mnazuia tena wimbi hili la pili maana kama ni chanjo msijipe matumaini saini.

Njia hizo tatu ndio njia zitakazokinga maisha yako na maisha ya wale uwapendeo. Lakini kama unafikiria Rais ana ubia na maisha yako haya we. Kwa sababu lile swali la bahati nasibu ya Magufuli kama italipa bado linasimama.

Maskini Mzee Mwanakijiji... amepoteza kabisa uwezo wa kufikiri.

Unamtenganishaje JPM Na Urais na majukumu yake .

Kauli ya Rais ni kauli ya kufanyiwa kazi na haiwezi kubezwa hata kidogo . Sasa Mh Rais anapobeza mambo muhimu muhimu kama ya kutoa data za Corona , Matibabu Na hata kubeza Vaccine ni kauli nzito ya kuangamiza jamii.

1. Kauli ya Rais ni Kauli ya Tanzania Na inapelekea watu kutengwa Na wengine duniani , unawezaje kuibeza kwamba iachwe tu .
2. Kauli ya Rais ni msimamo wa nchi unayopelekea watu Kuendelea kukusanyika Na maeneo kama Mashule , masoko Na viwanja vya mipira .. kunaleta maambukizi Na Vifo ambavyo vingeweza kuzuiwa , Tunaweza ku ignore tu eti kisa Mwanakijiji ni shabiki wa JPM .

3. Kauli ya kubeza Vaccine inatufanya tuonekane vituko na kunaweza kuathiri shughuli binafsi za wananchi eti tui ignore tu kisa Mwanakijiji ni shabiki wa JPM..

Sometime you need to be serious .. usije Na utopolo hapa jamvini
 
Kuna watu wanadhania au wanaombea Magufuli abadilike.....JPM Yuko alivyo hawezi kuwa tofauti na alivyo...la maana ni watu kufanya maamuzi wakizingatia ukweli huu. Kawaambia hakuna lockdown, anabeza chanjo, hajakubali uwepo na ukali wa korona..Sasa leo mnataka aamke ale matapishi yake, Mara ya mwisho kukiri amekosea ilikuwa lini!? Amkeni msijitoe ufahamu...Linda maisha Yako, ya ndugu zako....we endekeza kumngojea Magufuli...
Magufuli ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Katika nchi ambayo kauli ya Rais ina nguvu kama Amri ya Mungu, kila litokalo mdomoni mwa Rais lina impact kubwa sana.

Suala hapa sio kuwa "Magufuli habadiliki" bali ninyi wapambe wake mchangie kuleta mabadiliko hayo. Akipita hapa JF na kuona mshauri wake mkuu unawalaumu wananchi kwa "kosa" la kutegemea Magufuli, badala ya kumkosoa yeye anayejaribu kuwaghilibu Watanzania kuwa Korona ni ugonjwa kama malaria tu, ni ngumu kwake kuona haja ya kubadilika.

Kama mnampenda kwa dhati basi msiwe waimba mapambio tu. Ifike mahala mumwambie "hapana, hii sio sawia."

By the way, sidhani kama kuna watu wanaosubiri Magufuli abadilike. "Jiwe halibadiliki" anyway. Kinachotarajiwa na wengine ni angalau kukaa kimya badala ya kuongea utopolo unaogharimu maisha ya watu.
 
Kwa hiyo tuseme katika vita hii hatuna nahodha? Kuwa kila mtu awe na lwake?
Na je kazi za Rais wa nchi kipindi cha majanga ni zipi? Je mataifa mengine viongozi wao wanachukua hatua gani?.
Kwenye Nchi yetu korona haijatangazwa kua ni janga la kitaifa, hata hivyo serikali kupitia wizara ya afya na wadau wengine wakiwepo HPSS walizunguka Tanzania nzima kutoa elimu ya korona, sasa nashangaa watu wanakazana Magufuli, Magufuli... Ndio maana nauliza hamuwezi kuchukua hatua mpaka nahodha aseme? Yaani Magufuli atoe muongozo wa korona ndio uchukue hatua?



Sent from my Android using JamiiForums mobile app
 
Hakuna anayedeka! Ni jukumu la serikali kupitia kwa waziri wa afya kuwaambia umma juu ya hali halisi na nn kifanyike. Siyo lazima lock down km Rais anavyojitetea kuwa watu baadhi wanalazimisha lockdown.
Itoshe kukiri kuwa kuna tatizo lenye ukubwa kidogo na mbinu za kushinda ni 1,2,3 nk. Kusema “Siyo kubwa, haipo ni chache sana” nikukanganya umma
Wizara ya afya ilishatoa muongozo jinsi ya kujikinga na korona, pia serikali ilitoa njia mbadala ikiwepo kujifukiza na kupiga nyungu. Si hivyo tu bali mashirika yasio ya kiserikali ikiwepo msalaba mwekundu, HPSS nk waliungana na wadau wengine wakiwepo akina mrisho mpoto kuzunguka nchi nzima na kutoa elimu ya korona ..

Katika hali isiyo ya kawaida watu wameziba masikio na kushinikiza Rais aseme, rais aseme... Watu wanaleta politics kwenye afya, ndio maana nikasema wanadeka.. mbona wanavaa kondomu wakienda kuzini? Nani anawafundisha? Ifike wakati siasa zikae pembeni na watu wajifunze kuwajibika. Lawama hazisaidii

Sent from my Android using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom