Swali Gomvi: Korona 2.0 kwani Rais Magufuli ni mbia wa maisha yenu?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,474
39,987
Korona 2.0 Kwani Rais ana Ubia na Maisha Yenu?

Na. M. M. Mwanakijiji
Naandika kama shabiki wa Magufuli; naandika kama mtu ambaye nimeelewa malengo yake na mitazamo yake, na ninaandika kama mtu ambaye sijaegesha akili yangu mahali mwenyewe nikaondoka. Nimesoma na kufuatilia mijadala ya kile kinachodaiwa kuwa ni wimbi la pili (2.0) la maambukizi ya ugonjwa wa virusi vya corona (COVID-19) ambayo yanasemekana yanaendelea nchini mwetu. Wapo wengi ambao wanamuangalia Rais awape mwongozo wa nini cha kufanya na kwa kiasi kikubwa wanafanya hivyo kwa sababu Rais ndio kiongozi mkuu wa serikali na nchi.

Neno la Rais lina uzito wake, hofu za Rais zina uzito wake na ikumbukwe kuwa wengi wanachukulia kuwa kwa vile Rais ana watu wengi wanaomzunguka basi ana taarifa za mambo mengi ambayo labda watu nje ya serikali hawana. Aliposema watu wajifukize, mamilioni walijifukiza, aliposema watu wafunge na kuomba, watu walifunga na kuomba, aliposema watu waiage korona watu walifanya na send off! Na alipotangaza kuwa korona hakuna Tanzania na kuwa imekwisha watu waliamini hivyo.

Sasa hili wimbi la pili ni kweli? Kama ni kweli je Watanzania wafanye nini? Je, watu wanaokufa ni kweli wote wanakufa kwa korona au magonjwa mengine? Na kama wimbi hili kweli lipo kama nchi tufanye nini na kama mtu mmoja mmoja tufanye nini? Ni wazi msimamo wa serikali umetolewa na Rais jana huko Chato na kuwa hakuna mtendaji wa serikali atakayepingana na Rais kwenye hili isipokuwa kama yuko tayari kujiuzulu akipinga (resigning in protest). Kwa vile msimamo wa serikali unajulikana na kuwa serikali haitaleta lock down, na kuwa hata chanjo watu wafikirie mara mbilimbili basi sehemu ya nini kila mtu afanye ndio swali linalohitaji kujibiwa.

Ndugu zangu naandika kama shabiki; Watanzania msijitoe ufahamu na mkajifanya nyie fyatu! Rais si mbia wa maisha yenu, ya mababa na mama zenu, na wala si mbia wa maisha ya watoto wenu! Mnapougua, kuuguza na kuuguliwa yote hayo ni yenu; mauti yakiwafikia vilio ni kwenye nyumba zenu, jamaa, ndugu na marafiki zenu. Sasa kama hili ni kweli, kwanini watu wengine wafikiri wanaweza kuifanyia ibada imani ya mtu mwingine? Hivi, mnajua kwanini mitume wengine hawakuungana na Petro kujaribu kutembea juu ya maji japo wote walimuona Yesu akitembea juu ya maji na walimsikia Yesu akimwambia Petro atembee? (Mathayo 14:22-33).
1611807660221.png


Rais Magufuli anaweza kuwa na imani kubwa kabisa hata ya kutembea juu ya maji na akatembea; lakini wangapi wanaamini kama yeye? Kama imani yako haijafikia ile ya Magufuli sasa unakanyaga maji ya nini?

Ndugu zangu kuna njia tatu/nne kubwa na za haraka za kupunguza maambukizi ya corona:

1. Vaa barakoa iliyotengenezwa na kitambaa cha pamba (siyo hariri). Kuvaa barakoa kuna kulinda wewe na kinamlinda mwingine. Ukivaa barakoa funika pua na mdomo (korona inaingia zaidi kupitia puani!)

2. Osha mikono kwa sabuni mara kwa mara; epuka kusalimiana na watu kwa kushikana mikono. Ikitokea hivyo hakikisha huingiza vidole midomoni au puani (jitahidi kuosha kabla ya kufanya hivyo na baada).

3. Jiweke umbali wa karibu mita moja kutoka kwa mtu mwingine ambaye si wa nyumbani mwako. Na hii inaendana na kuepuka misongamano isiyo ya lazima hasa mahali ambapo watu hawavai barakoa. Na wale wenye ndugu (wazazi, mababu wazee) waambieni wasiende makanisani au misikitini kwa wakati huu au makanisa na misikiti iweke taratibu za kuhakikisha watu wanakaa mbalimbali na wanavaa barakoa!

4. Jifukize nyungu; sijui ni kwa namna gani hii ilisaidie kuzuia wimbi la kwanza lakini kama watu watafanya tena na kwa wingi wao mnaweza kujikuta mnazuia tena wimbi hili la pili maana kama ni chanjo msijipe matumaini saini.

Njia hizo tatu ndio njia zitakazokinga maisha yako na maisha ya wale uwapendeo. Lakini kama unafikiria Rais ana ubia na maisha yako haya we. Kwa sababu lile swali la bahati nasibu ya Magufuli kama italipa bado linasimama.
 
Rais Magufuli anajua anachokifanya, pia anajua kuna Covid19 phase II. Ila ameona athari za kuruhusu lockdown ya Nchi nzima kama wengine wanavyofanya itaathiri Sana Raia wake kuliko kutoweka lockdown.

Watanzania ni maskini wa kutupwa, tusije kufa kwa njaa kabla ya Corona.

Muhimu alichosema ni kuchukua tahadhali za kujikinga. Tahadhari ulizosema hapo juu ni muhimu zikachukuliwa na kila mwananchi,

Ila kulikuwa na haja yeye Kama Amiri jeshi Mkuu aseme kwa kusisitiza kuhusu hilo.
 
Basi kifuatacho nadhani kusiwe na Rais kabisa nchi hii.

Kwasababu mnakwepa majukumu ya dhahiri kwa vijisababu vya kijinga tu wakati mnatumbua kodi za walalahoi kwa kazi hiyo.

Yaani pesa na treatment za kifahari zinazotokana na kodi za walalahoi mnataka ila majukumu yake HAMTAKI.

Mtanzania akipigwa marufuku kwenda nchi za ng'ambo anaweza kutatua vipi hali hiyo peke yake ?

( Je, Raia wa kawaida anaweza kurejesha confidence ya nchi kwa watu wa mataifa mengine )
Tunawalaumu China kwa kutodhibiti ugonjwa mpaka unausumbua dunia, leo tena wengine wanapambana, halafu sisi tupo tupo tu tumekaa, tunasubiri wakimaliza, tuwapelekee.

Je, mikusanyiko mikubwa kama shule raia wa kawaida ana nafasi gani hapo bila Mwongozo ??

Je, ukubwa wa Tatizo ukoje hizi taarifa mwananchi wa kawaida anazipataje ili ajilinde. Knowledge is power.

Wewe Jamaa ni mwehu. Magu huyo anaetandika watu risasi 36 na kutaka wakazikwe haraka haraka ndio mwenye imani ya Petro. Yuko wapi Azory Gwanda, Kanguye, Ben Saanane, enyi wacha mungu ??

Sasa kama imani ndio imekuwa kimbilio la Magufuli, hao maaskari wenye mabunduki na helkopter za ulinzi anatembeatembea nazo za nini ??

Anyway, sasa tuanze kutibu MARALIA, TYPHOID, KIPINDU PINDU, UKIMWI, kwa imani ya Petro.

Kila kitu cha wazungu ni kibaya na hakifai isipokuwa pesa zao, mabomu ya machozi, vifaru vya kijeshi, mabunduki, magari ya washa washa, , vx-v8
 
Na. M. M. Mwanakijiji
Naandika kama shabiki wa Magufuli; naandika kama mtu ambaye nimeelewa malengo yake na mitazamo yake, na ninaandika kama mtu ambaye sijaegesha akili yangu mahali mwenyewe nikaondoka. Nimesoma na kufuatilia mijadala ya kile kinachodaiwa kuwa ni wimbi la pili (2.0) la maambukizi ya ugonjwa wa virusi vya corona (COVID-19) ambayo yanasemekana yanaendelea nchini mwetu. Wapo wengi ambao wanamuangalia Rais awape mwongozo wa nini cha kufanya na kwa kiasi kikubwa wanafanya hivyo kwa sababu Rais ndio kiongozi mkuu wa serikali na nchi.
Sijasoma hadi huko mwisho wa bandiko refu.

Hii hapa inatosha kabisa kujua umeandika nini huko.

1. Mstari wa kwanza unajitambulisha kuwa wewe ni "shabiki", hii ina maana unawapotezea muda wasomaji wako wasiokuwa "mashabiki" kama wewe kuendelea kupoteza muda wao kwa kusoma mambo ya 'kishabiki'.

2. Una hakika "unaelewa malengo yake na mitizamo yake"? Huwezi kuwa umepofushwa na "ushabiki" tu ulioutangaza hapa?

3. Unajuaje kwamba hili ni "wimbi la pili la corona" na sio wimbi lile lile la kwanza kutokana na kusitisha juhudi zote za kupambana na corona huko nyuma kwa madai kwamba haipo nchini bila ya ushahidi wowote wa madai hayo.

4. Unaandika kuwa "...kile kinachodaiwa kuwa ni wimbi la pili la maambukizi..., ambayo 'yanasemekana'; kwa nini watu wajadili mambo ambayo huna uhakika nayo wewe mwenyewe. Hii ni sehemu ya kuwavuruga na kuwachanganya akili waTanzania kama anavyofanya huyo unayemshabikia?

5. Mwisho unaandika, kama mtu aliyezinduka toka kwenye ndoto mbaya: "Wapo wengi ambao wanamuangalia Rais awape mwongozo wa nini cha kufanya..." Kwani wewe ungependa wamwangalie kiongozi wao kama "mpotoshaji" kama anavyojipambanua sasa hivi kuwa ndiyo lengo lake hasa kwa haya anayoyasemea juu ya ugonjwa huu na kutaka waTanzania waamini kuwa 'wazungu' kwa ujumla wao lengo lao ni kuwaangamiza watu weusi?

Naona hii itakuwa ni 'awamu ya pili' ya mkataba ulioingia na huyo mtu wako kwa kzai hii chafu ya kuwavuruga akili waTanzania.

Nchi inaingia vitani, nyinyi mnasema watu wafanye ya kwao wasimsikilize Jemadari mkuu; hiyo itakuwa vita ya namna gani.
 
Baada ya kuona umeanza kwa kuandika kuwa wewe Ni SHABIKI wake Basi nimeamua kukupuuza.
Wewe uko kishabiki kwa hiyo huna lolote la maana la kutuambia.

Kwa sababu huyo unaemshabikia hata akikosea utamsifia kwa kupindissha makosa yake Kama hivi Sasa.

Na nchi inaingia kwenye aibu kwa sababu ya watu kama wewe.
Nyinyi kila kitu Ni ushabiki tu.

Zamani nilidhani kila Mzee Ana busara,nikaja kugundua kua sio kweli kwa sababu Hawa vijana wajinga,wapumbavu,vibaka na walio hovyo wote leo hii watakuja kuwa wazee baadae.

Kwa maana hiyo watazeeka ama wanazeeka na ujingaujinga wao.
Tumekua hasara, pamba upambavyo.
 
Binafsi sikubaliani sana na hilo japo katika mambo flani flani kweli hana ubia na maisha yetu. Linapokuja janga kwa Taifa ni kweli Rais hana ubia na maisha Yetu? Rais wa nchi ni nani?

Tuangalie wimbi la kwanza la Covid 19
Katika wimbi hili Serikali ilichukua hatua kwa kufuata miongozo ya WHO ili kumlinda Rais wa nchi hivyo idara za usalama zilimpeleka Rais Chato kwa lock down isiyo rasmi kwa miezi mitatu, huku msisitizo ukitolewa wa tahadhari kubwa na njia mbadala yakupambana na Covid 19.

Wimbi la pili; Covid 19
Hatua zakumlinda Rais zimeendelea kuchukuliwa na sasa miezi miwili shughuli za serikali zimehamia Chato. Wananchi wanachoomba ni uwazi kwamba covid 19 wimbi la pili ipo nchini na wananchi wachukue hatua ambazo ndg Mzee Mwanakijiji umeziainisha, serikali imepata taarifa imejiridhisha inamkimbiza JPM Chato alafu isiwaambie Wananchi chakufanya, kwangu mm siyo sahihi.

Rais wa nchi kwa mujibu wa katiba na kiapo chake ana Ubia na maisha yetu.

“Kama JPM ana hiyo imani unayosema yakutembea juu ya bahari, sasa bahari ni Covid 19 na kutembea juu yake ni yeye kuendelea na shughuli za serikali katika mikoa yote pasipo na hofu”
 
Sijasoma hadi huko mwisho wa bandiko refu.

Hii hapa inatosha kabisa kujua umeandika nini huko.

1. Mstari wa kwanza unajitambulisha kuwa wewe ni "shabiki", hii ina maana unawapotezea muda wasomaji wako wasiokuwa "mashabiki" kama wewe kuendelea kupoteza muda wao kwa kusoma mambo ya 'kishabiki'.

2. Una hakika "unaelewa malengo yake na mitizamo yake"? Huwezi kuwa umepofushwa na "ushabiki" tu ulioutangaza hapa?

3. Unajuaje kwamba hili ni "wimbi la pili la corona" na sio wimbi lile lile la kwanza kutokana na kusitisha juhudi zote za kupambana na corona huko nyuma kwa madai kwamba haipo nchini bila ya ushahidi wowote wa madai hayo.

4. Unaandika kuwa "...kile kinachodaiwa kuwa ni wimbi la pili la maambukizi..., ambayo 'yanasemekana'; kwa nini watu wajadili mambo ambayo huna uhakika nayo wewe mwenyewe. Hii ni sehemu ya kuwavuruga na kuwachanganya akili waTanzania kama anavyofanya huyo unayemshabikia?

5. Mwisho unaandika, kama mtu aliyezinduka toka kwenye ndoto mbaya: "Wapo wengi ambao wanamuangalia Rais awape mwongozo wa nini cha kufanya..." Kwani wewe ungependa wamwangalie kiongozi wao kama "mpotoshaji" kama anavyojipambanua sasa hivi kuwa ndiyo lengo lake hasa kwa haya anayoyasemea juu ya ugonjwa huu na kutaka waTanzania waamini kuwa 'wazungu' kwa ujumla wao lengo lao ni kuwaangamiza watu weusi?

Naona hii itakuwa ni 'awamu ya pili' ya mkataba ulioingia na huyo mtu wako kwa kzai hii chafu ya kuwavuruga akili waTanzania.
Kalamu.
Amini nakuambia sio kila mtu ajiitae Mzee Ana hekima,busara na akili,amini.
Jiulize hivi,
Waliokua vijana woote wahuni,vibaka,majambazi,wezi,wazinzi,watumia mihadharati na kila Aina ya uovu.
Hawa huwa hawazeeki?
,je huwa wanakwenda wapi?
Basi hao ndo mmojawapo huyu Mzee Anayejiita Mwanakijiji.
 
Mzee mwanakijiji jana nilikutag ili nione msimamo wako kwenye hili gonjwa linalohitaji mapambano ya kisayansi, na kwakuwa rais wetu ni mwanasayansi nilitaka nione msimamo wako kwa rais mwanasayansi dhidi ya gonjwa la kisayansi. Ila nimegundua umekuwa mtumwa wa mahaba niue, jambo ambalo huko nyuma ulituaminisha kuwa huna. Hongera shabiki wa Magufuli kama ulivyojinasibu.
 
Kalamu.
Amini nakuambia sio kila mtu ajiitae Mzee Ana hekima,busara na akili,amini.
Jiulize hivi,
Waliokua vijana woote wahuni,vibaka,majambazi,wezi,wazinzi,watumia mihadharati na kila Aina ya uovu.
Hawa huwa hawazeeki?
,je huwa wanakwenda wapi?
Basi hao ndo mmojawapo huyu Mzee Anayejiita Mwanakijiji.
Hapana.

Huyu mtu alikuwa na akili zake nzuri tu hadi alipoingia kwenye mkataba na shetani ili kukidhi mahitaji ya tumbo lake. Inahudhunisha sana kwa kuuza utu wake.
 
Ndugu zangu kuna njia tatu/nne kubwa na za haraka za kupunguza maambukizi ya corona:

1. Vaa barakoa iliyotengenezwa na kitambaa cha pamba (siyo hariri). Kuvaa barakoa kuna kulinda wewe na kinamlinda mwingine. Ukivaa barakoa funika pua na mdomo (korona inaingia zaidi kupitia puani!)

2. Osha mikono kwa sabuni mara kwa mara; epuka kusalimiana na watu kwa kushikana mikono. Ikitokea hivyo hakikisha huingiza vidole midomoni au puani (jitahidi kuosha kabla ya kufanya hivyo na baada).

3. Jiweke umbali wa karibu mita moja kutoka kwa mtu mwingine ambaye si wa nyumbani mwako. Na hii inaendana na kuepuka misongamano isiyo ya lazima hasa mahali ambapo watu hawavai barakoa. Na wale wenye ndugu (wazazi, mababu wazee) waambieni wasiende makanisani au misikitini kwa wakati huu au makanisa na misikiti iweke taratibu za kuhakikisha watu wanakaa mbalimbali na wanavaa barakoa!

4. Jifukize nyungu; sijui ni kwa namna gani hii ilisaidie kuzuia wimbi la kwanza lakini kama watu watafanya tena na kwa wingi wao mnaweza kujikuta mnazuia tena wimbi hili la pili maana kama ni chanjo msijipe matumaini saini.

Njia hizo tatu ndio njia zitakazokinga maisha yako na maisha ya wale uwapendeo. Lakini kama unafikiria Rais ana ubia na maisha yako haya we. Kwa sababu lile swali la bahati nasibu ya Magufuli kama italipa bado linasimama.
Maoni aina hii nimeyasikia sehemu nyingi sana kutoka kwa watetezi wa mfumo! Mnachoshau ni kwamba, maoni yenu ni applicable kwa watu wa mitandaoni hususani JF na Twitter ndio ambao wana access to mass information ya kile kinachoendelea duniani kote.

Wale wenzangu mimi hata huo muda wa kusikiliza redio hawana! Halaiki hii hawana taaqrifa za kitaalamu kwa sabbabu wataalamu wetu hawawezi kwenda kinyume na matamko ya Rais.

Matokeo yake, kauli kama chanjo zawazungu ni uongo mtupu ndizo zinazowafikia wananchi wengi kwa sababu ndizo taarifa zinazosambazwa na traditional media! Taarifa kutoka kwa wana mamlaka kwamba hakuna korona ndizo zinawafikia wananchi walio wengi.

Sasa hao huwezi kuwaambia eti watumie hizo suggestions zako wakati taarifa wanazopata wao ni kwamba mambo ni shwari, na hao mabeberu ni wivu wao tu wa kutaka kupigana nasi kiuchumi ndo maana wanasema kuna korona ukweli lakini ukweli ni kwamba WANAWATISHA TU, korona HAKUNA.

Last week nilienda Dar es salaam. Nikilinganisha Dar es salaam niliyoiona last week na Dar es salaam ambayo niliiona mwaka jana wakati serikali inatangaza uwepo wa corona ni Dar es salaam mbili tofauti! Ile mwaka jana nilifikia kwa Bro, na nilipofika pale home nilikuta kuna ndoo ya watu kunawa maji kwa sababu pale home watu ni wengi sana.

Mbali na ndoo ya maji, wapangaji waliwekeana zamu ya kununua zile sababu za maji! Lakini nilivyofika pale pale kwa Bro last week, nimekuta ndoo ile ile ambayo mwaka jana ilikuwa inatumika watu kunawa maji ili kujikinga na maambukizi, ndoo ile hivi sasa inatumiwa na shemeji yangu kwenye banda lake la chakula wakati pilipilika pale home zipo vile vile kama sio kuongezeka! Utawalaumu hawa watu?

Utawalaumu vipi wakati mara kwa mara Mheshimiwa rais anatangaza kutowepo kwa corona na kama ipo basi sio kwa kiwango wanachotutisha wazungu?!
 
Back
Top Bottom