Swali fikirishi: Maafa yakitokea tena, watanzania wataambiwaje ili wachange?

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Nov 25, 2010
6,135
17,800
God forbids! Lakini, yawezekana kukatokea kama yale ya tetemeko la Kagera au yanayofanana na yale. Kutaundwa tena Kamati ya Maafa. Kutafunguliwa tena akaunti ya kuchangia waathirika. Je, watanzania wataambiwaje ili wachangie tena kama kwa wanaKagera?

Iko wazi kuwa pesa zilizochangwa na walioguswa na maafa yale ya tetemeko zitaishia 'kukibeba' chama chetu cha CCM kisiasa. Ingawa inadaiwa kuwa 'Serikali' inajenga na kukarabati miundombinu yake, utakapofika uchaguzi (kwakuwa Serikali ni ya CCM), CCM itatamba kujenga!

Wachangiaji wa nje ya nchi nao wanajisikiaje ikiwa walivyoambiwa sivyo ilivyofanyika? Yaani, michango ilikuwa ya waathirika lakini imeishia kukarabati miundombinu ya Serikali. Bajeti za miundombinu zinazotengwa kila mwaka kwa ajili ya miundombinu zimechwa pembeni.

Imesemwa kuwa kila mtu abebe msalaba wake.Msalaba wa wanaKagera ni malazi, mavazi na chakula chao. Msalaba wa Serikali ndiyo michango ya waathirika? Naungana na Mzee Mwanakijiji kuwaambia waliochangia waathirika wa Kagera kuwa 'wakome'!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
 
Ili watu wachangie itabidi JPM asitie neno! Kuna maeneo mbalimbali watu wamepata maafa na wamesaidiwa kwa vifaa vya ujenzi na chakula chini ya uongozi wa mikoa na halmashauri, mfano wakazi wa kijiji kimoja cha halmashauri ya mji wa Sumbawanga ambao nyumba zao ziliezuliwa nakimbunga kilichoambatana na mvua kubwa!
 
God forbids! Lakini, yawezekana kukatokea kama yale ya tetemeko la Kagera au yanayofanana na yale. Kutaundwa tena Kamati ya Maafa. Kutafunguliwa tena akaunti ya kuchangia waathirika. Je, watanzania wataambiwaje ili wachangie tena kama kwa wanaKagera?

Iko wazi kuwa pesa zilizochangwa na walioguswa na maafa yale ya tetemeko zitaishia 'kukibeba' chama chetu cha CCM kisiasa. Ingawa inadaiwa kuwa 'Serikali' inajenga na kukarabati miundombinu yake, utakapofika uchaguzi (kwakuwa Serikali ni ya CCM), CCM itatamba kujenga!

Wachangiaji wa nje ya nchi nao wanajisikiaje ikiwa walivyoambiwa sivyo ilivyofanyika? Yaani, michango ilikuwa ya waathirika lakini imeishia kukarabati miundombinu ya Serikali. Bajeti za miundombinu zinazotengwa kila mwaka kwa ajili ya miundombinu zimechwa pembeni.

Imesemwa kuwa kila mtu abebe msalaba wake.Msalaba wa wanaKagera ni malazi, mavazi na chakula chao. Msalaba wa Serikali ndiyo michango ya waathirika? Naungana na Mzee Mwanakijiji kuwaambia waliochangia waathirika wa Kagera kuwa 'wakome'!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
Sichangii tena maafa Tanzania,tumechangia waathirika lakini tunaambiwa fedha zinajenga miundombinu,sisi hatukuchangia miundombinu?
 
Funzo nililopata kwa misaada ya kagera sijui kama nitakuja kuchangia tena maafa
hahaha nashukuru mi sidanganyiki kirahisi kwa kweli kwenye hii nchi tena likija suala la fedha.Bora niende mwenyewe huko kwa wana kagera hata nikawanunulie bati chache kulikon nitoe fedha yangu kwenye mifuko ya ...........
 
Binadamu ni watu wenye upendo daima, japo ni rahisi kukasirika ila ni wepesi kusamehe na wepesi kusahau ila sio kurudia makosa, hivyo hata maafa mengine yakitokea tena leo, watu bado tutachangia tuu ila this time ni lazima tuelezwe tunaombwa kuchangia nini kama ni wahanga au ni miundombinu.
Hivyo tutalazimisha kuwekwe matangazo ya michango miwili
1.Michango ya kuchangia wahanga wa tetemeko ambalo litaendena na picha za jinsi watu wanavyoteseka.
2. Michango ya kuchangia ukarabati wa miundo mbinu ya umma likiendana na picha za uharibifu wa miundombinu ya umma.

Hivyo kila mchangiaji atakuwa anajua kabla anachangia nini kama ni waathirika au miundombinu sio kuonyeshwa picha za wahanga jinsi watu wanavyoteseka hivyo watu kuhamasika kuchangia, lakini michango ilipopatikana kumbe ulikuwa ni ya kuchangia miundombinu ya umma na sio waathirika.

Paskali
 
Hiyo ya kuambiwa ni simple tu Recall Mkituchagua na baada ya miaka mitano ya kuwatendea UBAYA,DHULUMA NA HILA tukirudi kwenu kuomba tena mtuchague tunawaambiaje?then ==na tutakavyowaambia kwenye janga lijalo
 
Kuna taasisi na wazito ambao ni muhimu kuonekana vyema mbele ya jicho la serikali kwa maslahi ya shughuli (business) zao. Hao, bila shaka, watajitokeza. Lakini mtu binafsi wa kawaida kama mimi ambaye msukumo wangu ni nafsi yangu inayosukumwa na utu, inaweza kuwa taabu na isiwezekane kabisa pale nikijua hela hiyo haiendi moja kwa moja kwa yule mnyonge niliyemuona/msikia kwenye vyombo vya habari akanitia imani (huruma) sana.

Ni changamoto kwa kweli. Bado naamini (kwa mbaaali kiasi) kwamba rais keshafikiwa na somo hili na kwamba kuna marekebisho (some damage control) yatafanyika. Kuna misimamo yake mingi atajikuta akilazimika kubadilika. Dunia si rahisi kama anavyofikiri. Mwalimu Nyerere bila kutegemea, baada ya vita ya Kagera, alijikuta kabakiwa na option moja tu: kusaini mkataba na IMF manake hata rafiki zake wa Scandinavia hawakuweza kumsaidia bila kumwaga wino kwenye mkataba huo. Akaamua kuachia ngazi. I doubt if the great gentleman would even consider that as an option!
 
Binadamu ni watu wenye upendo daima, japo ni rahisi kukasirika ila ni wepesi kusamehe na wepesi kusahau ila sio kurudia makosa, hivyo hata maafa mengine yakitokea tena leo, watu bado tutachangia tuu ila this time ni lazima tuelezwe tunaombwa kuchangia nini kama ni wahanga au ni miundombinu.
Hivyo tutalazimisha kuwekwe matangazo ya michango miwili
1.Michango ya kuchangia wahanga wa tetemeko ambalo litaendena na picha za jinsi watu wanavyoteseka.
2. Michango ya kuchangia ukarabati wa miundo mbinu ya umma likiendana na picha za uharibifu wa miundombinu ya umma.

Hivyo kila mchangiaji atakuwa anajua kabla anachangia nini kama ni waathirika au miundombinu sio kuonyeshwa picha za wahanga jinsi watu wanavyoteseka hivyo watu kuhamasika kuchangia, lakini michango ilipopatikana kumbe ulikuwa ni ya kuchangia miundombinu ya umma na sio waathirika.

Paskali
Mkuu, siyo kwa haya yaliyotokea!
Likitokea tukio lingine linalohitaji mchango kutoka kwa wananchi then, serikali ikafungua akaunt maalum kwa michango hiyo hata kama itakuwa imeuaminisha umma kuwa itawapelekea wahanga hiyo michango, baada ya hiyo michango kutolewa ni rahisi sana kuelekezwa sehemu nyingine inayotaka maana tayari michango inakuwa tayari mikononi mwao!
Je nani ataweza kuishtaki au kuhoji?
Kagera, kwani si tuliambiwa ni michango ya wahanga lakini mbona imebatilishwa, sasa likitokea tukio lingine serikali itashindwaje kuwaambia wananchi kama ilivyowaambia kuhusu suala la Kagera..?
Na hata kama michango itapelekwa kweli serikali kwani haiwezi kupeleka kiwango tofauti na kile kilichotolewa kwa ajili ya wahanga?
...labda kama kutakuwa na mbadala wa uchangiaji lakini si kwa jinsi ilivyofanyika kwa Kagera!!
 
God forbids! Lakini, yawezekana kukatokea kama yale ya tetemeko la Kagera au yanayofanana na yale. Kutaundwa tena Kamati ya Maafa. Kutafunguliwa tena akaunti ya kuchangia waathirika. Je, watanzania wataambiwaje ili wachangie tena kama kwa wanaKagera?

Iko wazi kuwa pesa zilizochangwa na walioguswa na maafa yale ya tetemeko zitaishia 'kukibeba' chama chetu cha CCM kisiasa. Ingawa inadaiwa kuwa 'Serikali' inajenga na kukarabati miundombinu yake, utakapofika uchaguzi (kwakuwa Serikali ni ya CCM), CCM itatamba kujenga!

Wachangiaji wa nje ya nchi nao wanajisikiaje ikiwa walivyoambiwa sivyo ilivyofanyika? Yaani, michango ilikuwa ya waathirika lakini imeishia kukarabati miundombinu ya Serikali. Bajeti za miundombinu zinazotengwa kila mwaka kwa ajili ya miundombinu zimechwa pembeni.

Imesemwa kuwa kila mtu abebe msalaba wake.Msalaba wa wanaKagera ni malazi, mavazi na chakula chao. Msalaba wa Serikali ndiyo michango ya waathirika? Naungana na Mzee Mwanakijiji kuwaambia waliochangia waathirika wa Kagera kuwa 'wakome'!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam

Afu bado jamaa anakumbushia zile bil 4.5 za wale waliahidi.

Kama wakitoa watakua hawana akili sawa sawa.

Chama Cha Mapinduzi huwezi kukitenganisha na wizi na ujambazi
 
Kwanza hizo hela za kutoa kwa maafa mapya zitatoka wapi watu wamefulia?
 
God forbids! Lakini, yawezekana kukatokea kama yale ya tetemeko la Kagera au yanayofanana na yale. Kutaundwa tena Kamati ya Maafa. Kutafunguliwa tena akaunti ya kuchangia waathirika. Je, watanzania wataambiwaje ili wachangie tena kama kwa wanaKagera?

Iko wazi kuwa pesa zilizochangwa na walioguswa na maafa yale ya tetemeko zitaishia 'kukibeba' chama chetu cha CCM kisiasa. Ingawa inadaiwa kuwa 'Serikali' inajenga na kukarabati miundombinu yake, utakapofika uchaguzi (kwakuwa Serikali ni ya CCM), CCM itatamba kujenga!

Wachangiaji wa nje ya nchi nao wanajisikiaje ikiwa walivyoambiwa sivyo ilivyofanyika? Yaani, michango ilikuwa ya waathirika lakini imeishia kukarabati miundombinu ya Serikali. Bajeti za miundombinu zinazotengwa kila mwaka kwa ajili ya miundombinu zimechwa pembeni.

Imesemwa kuwa kila mtu abebe msalaba wake.Msalaba wa wanaKagera ni malazi, mavazi na chakula chao. Msalaba wa Serikali ndiyo michango ya waathirika? Naungana na Mzee Mwanakijiji kuwaambia waliochangia waathirika wa Kagera kuwa 'wakome'!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
Kwani zile shule na hospitali na vyote vinavyo karabatiwa vinatumiwa na kina nani?
Kama maafa yakitokea watachangia na wasio changia hawatoshitakiwa maana kuchangia si lazima.
 
11 Reactions
Reply
Back
Top Bottom