kkarumekenge
JF-Expert Member
- Aug 14, 2013
- 1,708
- 1,026
Juzi nikiwa Dodoma jamaa alimwaga umbeya. Alidai DC wa wilaya ya Butiama anaishi Kiabakari na amepanga kwenye nyumba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya DC huyo. Hivi kweli huyo DC atajengewa nyumba huko Butiama huku amepanga kwenye nyumba ya huyo ambaye ndiye angeagiza ujenzi ufanyike. Kweli inawezekana, Katibu Mkuu huyo aache pesa ya pango anayojilipa aruhusu ujenzi wa nyumba ya DC? Kama kuna kitu kimeadimika sana Tanzania, ni maadili ya uongozi.