Susuki carry

CHE GUEVARA-II

JF-Expert Member
Jun 17, 2010
571
156
Jamani, msinichoke,
Naanza kuwekeza rasmi (I am taking risk).
Naomba kujua hivi vi-pick ups vidogo vidogo sijui vinaitwa SUZUKI CARRY, HIJET n.k vinauzwa bei gani?
Showroom ni bei gani na ni showroom gani ina be nzuri? Kwa kuagiza ni bei gani jumla mpaka inatembea barabarani?
Na ni vya aina gani vizuri, maana nasikia sijui kuna Suzuki macho duara, macho mstatili, Zuzuki bichwa n.k

Nahitaji cha kubeba vyakula vya mizigo na kupeleka bidhaa mjini na kusaidia shughuli ndogondogo nyumbani.
 
Tata spare zake vp?
Maana nina MAZDA hapa spare zake zake zinanisumbua ile mbaya - natamani hata kuiuza kwa milioni 3 japokuwa ni nzima kabisa (Engine iko poa)
 
Nakushauri Suzuki Carry, hasa ukipata 4WD. Ukiagiza inacheza kwenye mil 7 mpaka kuitoa
 
Jamani, msinichoke,
Naanza kuwekeza rasmi (I am taking risk).
Naomba kujua hivi vi-pick ups vidogo vidogo sijui vinaitwa SUZUKI CARRY, HIJET n.k vinauzwa bei gani?
Showroom ni bei gani na ni showroom gani ina be nzuri? Kwa kuagiza ni bei gani jumla mpaka inatembea barabarani?
Na ni vya aina gani vizuri, maana nasikia sijui kuna Suzuki macho duara, macho mstatili, Zuzuki bichwa n.k

Nahitaji cha kubeba vyakula vya mizigo na kupeleka bidhaa mjini na kusaidia shughuli ndogondogo nyumbani.

Mkuu suzuki ndio yenyewe na kama huna shughuli nzito na njia nzuri chukua 2 wheel maana 4 wheel zinasumbua. Kuagiza inasimama 6.5 mpaka7ml.
 
Showroom ni sh. ngapi?
Nataka nilinganishe kati ya kununua showroom na kuagiza (cost vs benefit in terms of time, reliability, security, assurance etc).

Na kuagiza inachukua muda gani (minimum & maximum)?
Halafu kwenye mitandaosojawahi kuona Suzuki Carry (macho duara au mstatili ya zaidi ya mwaka 1998).
Nyingi zilizopo ktk late 90's ni Suzuki bichwa tu!
 
Nipe 6.3mil nikupe changu kimeingia September Mwaka huu.

Bima ni comprehensive!!

Ni aina gani ktk hizo nilizotaja hapo juu?
Tuma picha at least 5 tofauti za hicho ki-pick up hapa kwenye thread, PM, au ktk richkety@yahoo.co.uk
Toa data za mwaka kilipotengenezwa
Mileage ngapi?
Kwa nini unakiuza?
Then nitatuma Fundi wangu aje akikague.
 
Nimeshapata kwa 7.5M toka yard/ show room.
Ni bima gani bora ya magari (inayojali valid claims za wateja)?
Nataka nikate COMPREHENSIVE INSURANCE (ofisi zao zinapatikana wapi?)
Niko Dar.
 
Kuna show room iko SINZA mkono wa kushoto ukiwa unatoka Ubungo (kama mita 200 baada ya kuvuka ile njia panda inayoelekea/ inayotoka Sam Nujoma road kupitia makaburini.
 
Tumia AON watakukatia kwa Jubilee Insurance. Ndio wako juu kwa sasa
 
Call 0753432011 kwa huduma ya bima. Wanaitwa eagle insurance. Ofisi iko mikocheni ukitokea tmj/mayfair ni kabla tu ya kufika njia panda ya cocacola. AoN ni insurance kubwa na wasumbufu sana

Duh, asante kwa ushauri.
Mpaka sasa siamini cha AON (Jubilee Insurance) wala EAGLE INSURANCE.
Kwa nini?
By assuming that there are only, and only two Insurance companies, he probability of AON (Jubilee Insurance) being the right choice is 0.5 and Eagle Insurance is 0.5; the probability that EITHER AON (Jubilee Insurance) OR Eagle Insurance being the right choice is 1 (POSSIBILITY OF THIS EVENT OCCURRING IS VERY LIKELY - ABSOLUTELY POSSIBLE).
However, the probability of both AON (Jubilee Insurance) & Eagle Insurance being the right choice (which is this case) is dramatically reduced to 0.25 (POSSIBILITY OF THIS EVENT OCCURRING IS UNLIKELY)

Conclusion: Nahitaji (third + n) suggestion.
 
Back
Top Bottom