Suspected NBC massive fraud: SA investigators called in to verify

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,789
288,011
Suspected NBC massive fraud: SA investigators called in to verify

By ThisDay Reporter

23rd March 2010

A team of fraud experts from South Africa has been flown into the country to investigate allegations of corruption and theft of billions of shillings from the National Bank of Commerce.

It has been confirmed that the team of about ten experts from ABSA Group Limited, the NBC parent company, spent several days at the bank's headquarters in Dar es Salaam before leaving for home over the weekend.

ABSA Group owns 55 per cent of the shares in NBC, one of the country's biggest commercial banks.

Other shareholders are the (Tanzanian) government (30 per cent) and the International Finance Corporation (15 per cent).

The ABSA team from South Africa is understood to have investigated allegations of massive fraud at the bank, which has recently been hit by a series of internal thefts involving billions of shillings.

Well-informed banking sector sources told THISDAY: "The fraud experts went through the various NBC departments, particularly the credit section, as part of their mission."

"They stayed at the bank for four or five days, during which they perused dozens of files and bank transactions deemed suspicious."

It is understood that the team will now compile a report for the ABSA Group top hierarchy, which will probably include recommendations for personnel, institutional, and operational changes to be implemented within NBC in the wake of the scandal.

"They were working closely with local NBC staff members to try to establish how it all went down and who precisely were involved in the massive fraud," the sources said, adding that investigators from the Prevention and Combating of Corruption Bureau (PCCB) were also involved in the probe.

At least four junior staff members at NBC have already been removed from their posts as a result of the investigation. But officials say some of the more senior bank officials implicated in the fraud are still clinging to their jobs, hence raising fears that they may end up tampering with whatever evidence there is.

Said the source: "The lower-ranking officials already fired by the bank were just used as scapegoats in the whole scam. All the more senior officials have remained untouched so far."

According to PCCB officials, the Bureau is conducting its own major investigation into a fresh series of fraud incidents and financial crime within local banks and financial institutions, with NBC cited as one of the banks hardest hit by the wave.

According to THISDAY findings, some senior personnel in many of these banks and financial institutions are being probed on suspicion of conspiring with expert fraudsters to siphon away billions of shillings.

PCCB director general Dr Edward Hoseah has said preliminary investigations show the problem to be
 
Date::3/25/2010WIZI KWA NJIA YA MTANDAO: Gavana ayashukia mataifa ya Ulaya
Mwananchi
NDULU.jpg

Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Profesa Benno Ndulu ameyajia juu mataifa ya Ulaya akidai kuwa yamekuwa chanzo cha kukwamisha utekelezaji wa udhibitiwa wa fedha chafu.*ADAI YANAKWAMISHA UDHIBITI WA FEDHA CHAFU

Ramadhan Semtawa

GAVANA wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Profesa Benno Ndulu ameyalamu baadhi ya mataifa ya Ulaya kwamba, yanaficha siri za watu wanaoweka fedha zenye harufu ya uhalifu kwenye benki zilizoko katika nchi hizo.

Profesa Ndulu aliliambia gazeti hili jana kuwa tabia hiyo inapunguza kasi ya kukabiliana na matukio ya uhalifu kwenye sekta ya fedha nchini.

Kauli ya gavana Ndulu, inakuja kipindi ambacho kumekuwa na taarifa mbalimbali za uhalifu wa kutumia mtandao nchini ikiwemo kutorosha fedha katika maeneo mbalimbali ya ndani na baadhi ya watu kuweka fedha zao nje ya nchi bila kuingia kwenye rekodi za akiba ya fedha za kigeni BoT.

Wakati Profesa Ndulu akitoa kauli hiyo taarifa mpya zinaeleza kuwa kuna kigogo mmoja (jina tunalihifadhi)ameweka kiasi kinachodaiwa kuwa Sh9 bilioni kwenye benki moja nchini Uingereza.

Profesa Ndulu alipoulizwa kuhusu kiasi hicho kama kimo kwenye rekodi ya fedha za kigeni halali zilizomo kwenye rekodi ya BoT, alijibu: "Hapana, hilo sijalisikia popote, hiyo taarifa sina...lakini unajua kuna tatizo kwa wenzetu."

Lakini, vyanzo vya habari ndani na nje ya serikali, vinasema tayari fedha hizo zimeanza kustua mamlaka za ndani za Uingereza ambazo zimeanza kuomba taarifa za uhalali wake kutoka mamlaka za Serikali ya Tanzania.

Kuhamishwa kwa kiasi hicho kunakuja kipindi ambacho pia mabenki matatu makubwa nchini yakiwa yamekumbwa na wizi mkubwa wa fedha zinazoelezwa kufikia Sh300 bilioni ingawa vyombo vya usalama na BoT vimekuwa vikikana kuwepo tukio hilo kubwa.

Fedha za amana za mabenki yote nchini zilizopo ni Sh7.8 trilioni kiasi ambacho ni kikubwa na kinachodhihirisha uwezekano wa mabenki hayo matatu makubwa, kuweza kuibiwa kiasi hicho cha fedha bila athari zake kuonekana mapema na kwa urahisi.

Lakini, mkuu huyo wa taasisi ya fedha nchini pasipo kutaja jina la nchi yeyote, akizungumzia suala zima la kupambana na utoroshaji wa fedha nje ya nchi bila rekodi za benki hiyo, alisema: "Tatizo wenzetu hawa huwa hawatoi taarifa za kutosha kutuwezesha kufuatilia akaunti za watu kwenye benki zao kuona kama fedha zilizopo ni halali."

Alifafanua kwamba, yamekuwepo baadhi ya matukio, lakini kila yakifuatiliwa huwa vigumu mno kuweza kupata taarifa za siri za akaunti ya mteja kwenye benki zao kutokana na sheria na miiko yao.

"Wenyewe wanasema wana miiko na sheria zao, sasa ukiona mtu wanaanza kumfuatilia na kutoa taarifa zake labda atakuwa amehusika na uhalifu unaowahusu wao ndipo huanza kushirikiana," alisisitiza gavana Ndulu na kuongeza:

"Msione hivi, vyombo vyetu vinafanyakazi kubwa FIU (Financial Intelligency Unit) na sisi tunaweza kufuatilia kitu, lakini kuna ugumu wa kupata taarifa za kina na za kutosha kuhusu baadhi ya akaunti".

Profesa Ndulu alifafanua kuwa BoT ina mamlaka ya kuomba na kupatiwa taarifa za akaunti yoyote ndani ya nchi kama ina utata, lakini linapokuja suala la nje ya nchi hasa katika mataifa hayo ya Ulaya huwa ngumu kutokana na sheria zao.

Kwa mujibu wa Profesa Ndulu hiyo ndiyo sababu ya kuwapo shinikizo kubwa la asasi zisizo za kiserikali (NGOs) barani Afrika, kuomba mataifa ya Ulaya yasaidie kurejesha fedha zote za Afrika zilizoibwa na kufichwa kwenye benki zao.

Alidai kuwa mataifa hayo yamekuwa yakifurahia fedha zinazowekezwa kwenye benki zao ndiyo maana husita kutoa taarifa za kina na msingi kusaidia mbinu za kuchunguza uhalifu kwenye sekta ya fedha katika nchi za Afrika.

Alisema kama mataifa hayo hayatasaidia kutoa taarifa za msingi yanaweza kuweka ugumu wa kubana fedha zisizo halali zinazotoroshewa nje ya nchi.

Mataifa ya Ulaya ambayo yamekuwa yakipiga kelele za ufisadi yamekuwa yakilalamikiwa pia na wanaharakati barani Afrika kutokana na kuhifadhi mabilioni ya fedha zilizoibwa na viongozi au familia zao na wahalifu kisha kuwekwa kwenye benki zao na wanapogundua wanashindwa kuzirejesha.

Marais kama marehemu Jeneral Sanni Abacha wa Nigeria na Mobutu Seseseko, wanatuhumiwa kuweka kiasi kikubwa cha fedha kwenye benki za nchini Uswis na nyingine za Ulaya.

Abacha ambaye alifariki dunia mwaka 1998 akiwa madarakani alituhumiwa kuhifadhi dola za Marekani 1bilioni katika benki mbalimbali huko Uingereza, Marekani na Uswis. Kwa upande wa Mobutu, katika nchi ya Uswis alibainika kuwa na dola 3.4milioni huku akituhumiwa kuwa na mamilioni ya dola nyingine katika akaunti za siri nchini humo na baadhi ya nchi za Ulaya.
 
Wizi mkubwa sana umefanyika pale kwa njia za mikopo, na inasemekana huo mchezo tayari umeshaingia hadi CRDB Bank
 
Date::3/25/2010WIZI KWA NJIA YA MTANDAO: Gavana ayashukia mataifa ya Ulaya
Mwananchi
NDULU.jpg

Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Profesa Benno Ndulu ameyajia juu mataifa ya Ulaya akidai kuwa yamekuwa chanzo cha kukwamisha utekelezaji wa udhibitiwa wa fedha chafu.*ADAI YANAKWAMISHA UDHIBITI WA FEDHA CHAFU

Ramadhan Semtawa

GAVANA wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Profesa Benno Ndulu ameyalamu baadhi ya mataifa ya Ulaya kwamba, yanaficha siri za watu wanaoweka fedha zenye harufu ya uhalifu kwenye benki zilizoko katika nchi hizo.

Profesa Ndulu aliliambia gazeti hili jana kuwa tabia hiyo inapunguza kasi ya kukabiliana na matukio ya uhalifu kwenye sekta ya fedha nchini.

Kauli ya gavana Ndulu, inakuja kipindi ambacho kumekuwa na taarifa mbalimbali za uhalifu wa kutumia mtandao nchini ikiwemo kutorosha fedha katika maeneo mbalimbali ya ndani na baadhi ya watu kuweka fedha zao nje ya nchi bila kuingia kwenye rekodi za akiba ya fedha za kigeni BoT.

Wakati Profesa Ndulu akitoa kauli hiyo taarifa mpya zinaeleza kuwa kuna kigogo mmoja (jina tunalihifadhi)ameweka kiasi kinachodaiwa kuwa Sh9 bilioni kwenye benki moja nchini Uingereza.

Profesa Ndulu alipoulizwa kuhusu kiasi hicho kama kimo kwenye rekodi ya fedha za kigeni halali zilizomo kwenye rekodi ya BoT, alijibu: "Hapana, hilo sijalisikia popote, hiyo taarifa sina...lakini unajua kuna tatizo kwa wenzetu."

Lakini, vyanzo vya habari ndani na nje ya serikali, vinasema tayari fedha hizo zimeanza kustua mamlaka za ndani za Uingereza ambazo zimeanza kuomba taarifa za uhalali wake kutoka mamlaka za Serikali ya Tanzania.

Kuhamishwa kwa kiasi hicho kunakuja kipindi ambacho pia mabenki matatu makubwa nchini yakiwa yamekumbwa na wizi mkubwa wa fedha zinazoelezwa kufikia Sh300 bilioni ingawa vyombo vya usalama na BoT vimekuwa vikikana kuwepo tukio hilo kubwa.

Fedha za amana za mabenki yote nchini zilizopo ni Sh7.8 trilioni kiasi ambacho ni kikubwa na kinachodhihirisha uwezekano wa mabenki hayo matatu makubwa, kuweza kuibiwa kiasi hicho cha fedha bila athari zake kuonekana mapema na kwa urahisi.

Lakini, mkuu huyo wa taasisi ya fedha nchini pasipo kutaja jina la nchi yeyote, akizungumzia suala zima la kupambana na utoroshaji wa fedha nje ya nchi bila rekodi za benki hiyo, alisema: "Tatizo wenzetu hawa huwa hawatoi taarifa za kutosha kutuwezesha kufuatilia akaunti za watu kwenye benki zao kuona kama fedha zilizopo ni halali."

Alifafanua kwamba, yamekuwepo baadhi ya matukio, lakini kila yakifuatiliwa huwa vigumu mno kuweza kupata taarifa za siri za akaunti ya mteja kwenye benki zao kutokana na sheria na miiko yao.

"Wenyewe wanasema wana miiko na sheria zao, sasa ukiona mtu wanaanza kumfuatilia na kutoa taarifa zake labda atakuwa amehusika na uhalifu unaowahusu wao ndipo huanza kushirikiana," alisisitiza gavana Ndulu na kuongeza:

"Msione hivi, vyombo vyetu vinafanyakazi kubwa FIU (Financial Intelligency Unit) na sisi tunaweza kufuatilia kitu, lakini kuna ugumu wa kupata taarifa za kina na za kutosha kuhusu baadhi ya akaunti".

Profesa Ndulu alifafanua kuwa BoT ina mamlaka ya kuomba na kupatiwa taarifa za akaunti yoyote ndani ya nchi kama ina utata, lakini linapokuja suala la nje ya nchi hasa katika mataifa hayo ya Ulaya huwa ngumu kutokana na sheria zao.

Kwa mujibu wa Profesa Ndulu hiyo ndiyo sababu ya kuwapo shinikizo kubwa la asasi zisizo za kiserikali (NGOs) barani Afrika, kuomba mataifa ya Ulaya yasaidie kurejesha fedha zote za Afrika zilizoibwa na kufichwa kwenye benki zao.

Alidai kuwa mataifa hayo yamekuwa yakifurahia fedha zinazowekezwa kwenye benki zao ndiyo maana husita kutoa taarifa za kina na msingi kusaidia mbinu za kuchunguza uhalifu kwenye sekta ya fedha katika nchi za Afrika.

Alisema kama mataifa hayo hayatasaidia kutoa taarifa za msingi yanaweza kuweka ugumu wa kubana fedha zisizo halali zinazotoroshewa nje ya nchi.

Mataifa ya Ulaya ambayo yamekuwa yakipiga kelele za ufisadi yamekuwa yakilalamikiwa pia na wanaharakati barani Afrika kutokana na kuhifadhi mabilioni ya fedha zilizoibwa na viongozi au familia zao na wahalifu kisha kuwekwa kwenye benki zao na wanapogundua wanashindwa kuzirejesha.

Marais kama marehemu Jeneral Sanni Abacha wa Nigeria na Mobutu Seseseko, wanatuhumiwa kuweka kiasi kikubwa cha fedha kwenye benki za nchini Uswis na nyingine za Ulaya.

Abacha ambaye alifariki dunia mwaka 1998 akiwa madarakani alituhumiwa kuhifadhi dola za Marekani 1bilioni katika benki mbalimbali huko Uingereza, Marekani na Uswis. Kwa upande wa Mobutu, katika nchi ya Uswis alibainika kuwa na dola 3.4milioni huku akituhumiwa kuwa na mamilioni ya dola nyingine katika akaunti za siri nchini humo na baadhi ya nchi za Ulaya.



Huyu atalaumu Wazungu mpaka lini?
Kama anatumia billions of sh kukarabati nyumba ya BoT,atamlaumu mzungu?
Ndege ya rais,Meremeta,EPA,Mkapa deals,Richmond.etc

It is big joke.Azungumzie vijisent vya Dr Rashid na Chenge kwanza kuliko kuzungumzia geopolitics.
 
huyu naye Ndulu ana mtindio wa ubongo aiseee..
Governor mzima...anaongea kama mtu asiye na facts n figures his reasoning sounds like politics to me!..yani explaination yake ata mimi ningeweza toa...If the central bank thinks certain transfers are dirty any bank kwa mfano za UK wanaziflag ata Ku freeze aache kudanganya watu ( personally nili receive 10,000$ and had a call from my bank requesting further evidence..sasa imagine if my bank had a call from BOT over my account?? Inatia hasira watanzania tunafanywa wajinga sana na viongozi hawa)..tatizo BOT hata hiyo kazi ya ku contact mabenk hawajafanya too much siasa!
 
Governor mzima...anaongea kama mtu asiye na facts n figures his reasoning sounds like politics to me!..yani explaination yake ata mimi ningeweza toa...If the central bank thinks certain transfers are dirty any bank kwa mfano za UK wanaziflag ata Ku freeze aache kudanganya watu ( personally nili receive 10,000$ and had a call from my bank requesting further evidence..sasa imagine if my bank had a call from BOT over my account?? Inatia hasira watanzania tunafanywa wajinga sana na viongozi hawa)..tatizo BOT hata hiyo kazi ya ku contact mabenk hawajafanya too much siasa!
Umenifurahisha sana mkuu...huyu jamaa anasema mambo kama vile watu wa ulaya wanahamisha hizi hela bila kuwahusisha local banks. Kama hela zipo ndani ya nchi, kuwalaumu watu wa ulaya ni kuwaonea tu. Tungeanza kwanza wenyewe kuwa serious halafu ndio turukie huko ulaya.
Hii ni typical africans attitude. We always think the problem is not within our systems, but it is out there. Kwahiyo tumerelax kwasababu sisi hatuna matatizo.
 
halafu mbona kila ukikaribia uchaguzi kunakuwa na wizi mkubwa wa pesa za watu, mwaka 2005 just karibia na ucha, guzi watu waliiba sana pesa za umma, sasa wameona kule bot kwa sasa hakuna njia wahamia kwenye mabenki binafsi, kwanini jamani, Tanzania kuna matatizo gani, au yote haya ni kuandaa mazingira mazuri ya mzee kushinda uchaguzi kwa kishindo tena? hata mtoto acyejua logic mathematics au cross multiplication atajua tu kuna sababu ya msingi kabisa juu ya huu wizi and uchaguzi might be the main and core reason ya huu wizi. Mpaka itafika sasa watu tutakuwa hatuna imani na mabenki, make kama mzunguko wa pesa yangu uantumika kufanya uchafu ambao baadae utalingiza taifa kwenye maafa 100% i will be responsible, hata mbele za Mwenyezi Mungu nitakuwa na kesi ya kujibu

Achane uchafu huo jamani, kama tatizo ni ikulu si muombe kura tu kwa njia isiyo tumia pesa haramu
 
Back
Top Bottom