Sir M.D.Andrew
JF-Expert Member
- Jul 30, 2012
- 201
- 37
Ndugu wanaJF,binafsi nasikitishwa sana na uendeshwaji wa jeshi la polisi na maadili ya jeshi,kifo cha mkuu wa polisi wa mkoa,tena kifo cha namna hii ni aibu kubwa lakini pia kimefichua udhaifu mkubwa jeshi la polisi,kimaadili na kiutendaji,ndio maana wamekalia kudhibiti harakati za ndani na kuua watu kwa kisingizio cha majambazi au wavamizi wa hifadhi za taifa,,ni aibu kubwa kwa jeshi zaidi pale ambapo mkuu wao anakufa kifo kisichoeleweka sawasawa chanzo chake,maana kinahusishwa na ugoni! Lakini pia ukiachilia hayo kamanda yeye huwa halindwi?au kwa sababu alikuwa anafukuzia starehe za mwili akaamua walinzi wawe pembeni mathalani alikuwa na mke wa mtu? Kwa akili yangu,kwa kifo cha kizembe cha kamanda wa polisi mkoa wa mwanza iwe mwisho wa polisi tanzania,tuimarishe sungusungu inatosha,,haiwezekani kamanda wa mkoa afe kifo cha aibu namna hii....SUNGUSUNGU IIMARISHWE-TUMECHOKA NA POLISI