Sunday World: Jeshi la Afrika Kusini liliua zaidi ya wapiganaji 600 wa M23

Huihui2

JF-Expert Member
Jan 5, 2012
6,910
11,270
20250204_114310.jpg


Kwa mujibu wa gazeti la Sunday World la Afrika Kusini, Wanajeshi wa Afrika Kusini walipambana vikali na kuwaua waasi 600 wa M23 katika mapigano makali ya saa 24 mjini Sake, Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC). Waasi wa M23 walikusanya miili ya wenzao na kuitia moto ili kuficha ushahidi. Wanajeshi wa Afrika Kusini walifuata sheria za kimataifa kwa kuruhusu waasi kuchukua miili ya wenzao walipoinua bendera nyeupe. Katika mapigano hayo, wanajeshi 14 wa Afrika Kusini waliuawa. Rais Cyril Ramaphosa aliwasifu wanajeshi wake kama mashujaa waliokuwa na ujasiri mkubwa na kujitoa kwa dhati kutekeleza majukumu yao barani Afrika.
 
View attachment 3224846

Kwa mujibu wa gazeti la Sunday World la Afrika Kusini, Wanajeshi wa Afrika Kusini walipambana vikali na kuwaua waasi 600 wa M23 katika mapigano makali ya saa 24 mjini Sake, Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC). Waasi wa M23 walikusanya miili ya wenzao na kuitia moto ili kuficha ushahidi. Wanajeshi wa Afrika Kusini walifuata sheria za kimataifa kwa kuruhusu waasi kuchukua miili ya wenzao walipoinua bendera nyeupe. Katika mapigano hayo, wanajeshi 14 wa Afrika Kusini waliuawa. Rais Cyril Ramaphosa aliwasifu wanajeshi wake kama mashujaa waliokuwa na ujasiri mkubwa na kujitoa kwa dhati kutekeleza majukumu yao barani Afrika.
Hadi Sasa watu zaidi ya 900 Wameuwawa.

Sasa hao M23 ilikuaje wakapoteza wapiganaji wengi kiasi hicho?

Yaani wameiteka Goma Kwa gharama hiyo?

Pia kama ni kweli ilikuaje Wanajenga wa S.A na Tanzania,Burundi,Malawi nk wakashindwa kuzuia kutekwa Kwa Goma?

Kuna harufu ya propaganda hapa
 
Hadi Sasa watu zaidi ya 900 Wameuwawa.

Sasa hao M23 ilikuaje wakapoteza wapiganaji wengi kiasi hicho?

Yaani wameiteka Goma Kwa gharama hiyo?

Pia kama ni kweli ilikuaje Wanajenga wa S.A na Tanzania,Burundi,Malawi nk wakashindwa kuzuia kutekwa Kwa Goma?

Kuna harufu ya propaganda hapa
Thamani ya Huo mji kwa Ngongoti ni zaidi ya hiyo Idadi.
Japo PropaSauth Africa imetumika hapo
 
Hadi Sasa watu zaidi ya 900 Wameuwawa.

Sasa hao M23 ilikuaje wakapoteza wapiganaji wengi kiasi hicho?

Yaani wameiteka Goma Kwa gharama hiyo?

Pia kama ni kweli ilikuaje Wanajenga wa S.A na Tanzania,Burundi,Malawi nk wakashindwa kuzuia kutekwa Kwa Goma?

Kuna harufu ya propaganda hapa
Angalao gazeti la Sunday World limetufungua macho. Maana vyanzo vingine vya habari vinaipalilia M23 tu kuwa ndiyo wenye uwezo. Tuendelee kusubiri tutaujua ukweli
 
Vita vya Kongo friendly fire huwa inaua sana kuliko risasi za adui inasemekana hata hao South Africans 14 wameuwawa na mortar kutoka kwa Wazalendo na inasemekana ushahidi upo.

Vita vya Kongo huwa vinahusisha magrupu mengi mengi kweli kweli kwahiyo kujua nani ni nani kwenye uwanja wa mapambano inakuwa ni vigumu sana.
 
Kagame ni mchumba tu, hawezi kuwa baba lao. Silaha yake kubwa ni sympathy anayopata duniani kwa ile genocide ya 1994.

Nje ya hapo ni poyoyo kama kuku wa broiler
Wewe unasimuliwa kwenye kijiwe Cha kahawa chenu Mimi nipo uwanja wa mapambano naona kagame anavyowachakaza Hawa wachumba wa sandf,jw na WA burundi
 
Hahahaha hao jamaa wanachekesha kweli waasi 600 uwadondoshe kama kuku🤣🤣🤣 propaganda baada ya kuchezea vichapo🤣🤣🤣🤣🤣
 
Back
Top Bottom