MUSSA ALLAN
JF-Expert Member
- Oct 13, 2013
- 18,925
- 13,259
Wandugu!
Nimemsikia Waziri Mkuu wa Awamu ya tatu, Mh.Fredrick T Sumaye kupitia ITV habari akikemea Rushwa kwenye uchaguzi. Anafanya vyema sana. Ila alipoendelea kuongea niligundua kuna kasoro kubwa kwenye kauli zake. Mheshimiwa Sumaye aliwashauri wananchi wakipewa rushwa wapokee, ila kwenye kura wampe wamtakae!
Sasa nikajiuliza, sheria za Nchi zinasemaje kuhusu kutoa na kupokea Rushwa?
Ina maana huyu "Waziri Mkuu" hajui kuwa kutoa, kuomba na kupokea Rushwa ni kosa la jinai? Kwanini anawashauri wananchi wavunje sheria?
Sumaye chunga sana kauli zako!
Nimemsikia Waziri Mkuu wa Awamu ya tatu, Mh.Fredrick T Sumaye kupitia ITV habari akikemea Rushwa kwenye uchaguzi. Anafanya vyema sana. Ila alipoendelea kuongea niligundua kuna kasoro kubwa kwenye kauli zake. Mheshimiwa Sumaye aliwashauri wananchi wakipewa rushwa wapokee, ila kwenye kura wampe wamtakae!
Sasa nikajiuliza, sheria za Nchi zinasemaje kuhusu kutoa na kupokea Rushwa?
Ina maana huyu "Waziri Mkuu" hajui kuwa kutoa, kuomba na kupokea Rushwa ni kosa la jinai? Kwanini anawashauri wananchi wavunje sheria?
Sumaye chunga sana kauli zako!