Kakke
JF-Expert Member
- Dec 4, 2010
- 1,883
- 1,482
Waziri Mkuu Mstaafu, Frederick Sumaye
Kwa ufupi
Alisema nchi nyingi hupoteza amani na utulivu wao katika hatua hii ya mchakato wa kura na kukataa matokeo.
Arusha.Waziri Mkuu Mstaafu, Frederick Sumaye amesema Tume ya Uchaguzi isipotenda haki katika kutangaza matokeo, inaweza ikasababisha uvunjifu wa amani nchini.
Sumaye aliyasema hayo jana alipokuwa akifungua semina ya uhamasishaji ya vijana wa CCM iliyofanyika mkoani Arusha.
"Wakati wa uchaguzi ni lazima wahusika wote hasa Tume ya Uchaguzi lazima itende na ionekane inatenda haki sawa kwa kila mgombea wa kila chama.
"Upendeleo na uonevu wa aina yoyote iwe baina ya vyama au baina ya wagombea ni sumu kwa amani na utulivu wetu…Tume kutokuwa na uwazi wa kutosha katika shughuli zote zinazohusu uchaguzi hasa wakati wa kuhesabu kura na kutangaza matokeo.
"Hisia yoyote ya udanganyifu, upendeleo au wizi wa kura ni sumu ya amani na utulivu. Uchaguzi ndipo mahali ambapo raia hutumia haki yake ya kuchagua na kuchaguliwa na hiyo haki yake ya msingi," alisema Sumaye huku akishangiliwa.
Sumaye anayejinasibu kuwania urais, alisema jambo lolote linalotafsiriwa kupokonya haki hii haitavumiliwa na hujibiwa kwa mapambano.
Alisema nchi nyingi hupoteza amani na utulivu wao katika hatua hii ya mchakato wa kura na kukataa matokeo.
"Nchi nyingi zimejikuta katika uvunjivu wa amani na utulivu kunapokuwa na chama au upande moja unaokataa matokeo ya kura zilizopigwa. Mifano ya hali hii ni mingi katika nchi za Afrika na mara kadhaa Serikali zimeangushwa au kuishia katika mgawanyo wa madaraka jambo ambalo linawanyima raia haki ya kutetewa bungeni na upande wa upinzani ambao katika utaratibu huo nao huingia katika serikali ya mseto.
"Ni vyema pale udhalimu haukutumika katika uchaguzi, vyama vyetu vikajua kuwa asiyekubali kushindwa si mshindani na hakuna utaratibu ambao unawafanya washindani wote kuwa washindi," alisema.
Chanzo: Mwananchi