kipara kipya
JF-Expert Member
- May 2, 2016
- 13,344
- 14,817
Wengi tulijua kwa uwezo wa bwana Fredrick Sumaye kisiasa ni mdogo sana, umaarufu wake kisiasa ulikuja mwaka 95 alipobebwa na mbeleko ya Uwaziri Mkuu baada ya kuteuliwa na Rais Mkapa.
Ni imani kama angesimama yeye kama yeye alikuwa hatoboi, hata huko jimboni kwake Hanang alikuwa akipita kwa mavirigiza tu lakini si kwa uwezo wake kisiasa.
Hata ndani ya CCM alijulikana ndio maana alishindwa mara kadhaa katika kura za ndani ya CCM kama si kukatwa kabisa.
Haikushangaza 2015 ghafla alipojiunga na Chadema, na kujifanya ni mshauri na msindikizaji wa mgombea Urais kupitia bendera ya Ukawa Mzee Lowassa.
Ilijulikana wazi hapo ameamua kujivua nguo mwenyewe na kujionyesha udhaifu wake kisiasa na alijua kusafiria nyota ya Lowassa kama si mbeleko.
Hata Chadema walipompatia huo uwenyekiti kwa ushauri wa Lowassa kama ishara ya shukrani ya kujitolea. Wengi walijua kama kungekuw na uchaguzi wa kweli basi Sumaye asingetoboa.
Mbeleko ya Mzee Lowassa imedhihirika muda mfupi tu baada ya kusimama peke yake, asijitie visingizio kibao vya uwenyekiti wa Mbowe hii imejiweka wazi tu kama kwenye kanda, tena bila mgombea kashindwa.
Je huko taifa angesema maneno gani wakamuelewa?
Sumaye umeamua kujivua nguo kuonyesha uwezo wako mdogo kisiasa na mbeleko ya Mzee Lowassa imechakaa hivyo imekuangusha, lakini pia pongezi kwa wana Chadema kwa kugundua wewe si mwenzao siku zako zinahesabika.
Chukua maamuzi mapema kama wenzio walioona mbali Chadema msingi wake ulijengwa kwa jasho na damu, wewe ulitaka kujitwalia madaraka kirahisi bila kujua wenye Chadema kama wapo hai na wanakuangalia.
Ushauri, jitafakari jitathimini chukua maamuzi mapema mzee siasa ni mchezo mchafu. Ulizoea mbeleko sasa imekubwaga.
Ni imani kama angesimama yeye kama yeye alikuwa hatoboi, hata huko jimboni kwake Hanang alikuwa akipita kwa mavirigiza tu lakini si kwa uwezo wake kisiasa.
Hata ndani ya CCM alijulikana ndio maana alishindwa mara kadhaa katika kura za ndani ya CCM kama si kukatwa kabisa.
Haikushangaza 2015 ghafla alipojiunga na Chadema, na kujifanya ni mshauri na msindikizaji wa mgombea Urais kupitia bendera ya Ukawa Mzee Lowassa.
Ilijulikana wazi hapo ameamua kujivua nguo mwenyewe na kujionyesha udhaifu wake kisiasa na alijua kusafiria nyota ya Lowassa kama si mbeleko.
Hata Chadema walipompatia huo uwenyekiti kwa ushauri wa Lowassa kama ishara ya shukrani ya kujitolea. Wengi walijua kama kungekuw na uchaguzi wa kweli basi Sumaye asingetoboa.
Mbeleko ya Mzee Lowassa imedhihirika muda mfupi tu baada ya kusimama peke yake, asijitie visingizio kibao vya uwenyekiti wa Mbowe hii imejiweka wazi tu kama kwenye kanda, tena bila mgombea kashindwa.
Je huko taifa angesema maneno gani wakamuelewa?
Sumaye umeamua kujivua nguo kuonyesha uwezo wako mdogo kisiasa na mbeleko ya Mzee Lowassa imechakaa hivyo imekuangusha, lakini pia pongezi kwa wana Chadema kwa kugundua wewe si mwenzao siku zako zinahesabika.
Chukua maamuzi mapema kama wenzio walioona mbali Chadema msingi wake ulijengwa kwa jasho na damu, wewe ulitaka kujitwalia madaraka kirahisi bila kujua wenye Chadema kama wapo hai na wanakuangalia.
Ushauri, jitafakari jitathimini chukua maamuzi mapema mzee siasa ni mchezo mchafu. Ulizoea mbeleko sasa imekubwaga.