Sumaye na Lowassa hawakuwepo?

Kiokote

Member
Nov 9, 2010
86
42
Historia ni mwalimu mzuri, na kuna wakati ni vigumu kuikana.

Baada ya kusomwa taarifa mbili za Kamati za Makinikia pameibuka manabii na mashujaa wa nchi wakidai "..Rais Magufuli alikuwa wapi kipindi hicho chote" amekuwa Mbunge na Waziri kwa kipindi cha takribani miongo miwili na sasa Ndiye Rais. Kwanini hakuchukua hatua? Baadhi ya mashujaa hao walionukuliwa kirefu na vyombo vyetu vya habari ni Luwasa na Sumaye.

Najiuliza, kipindi hicho chote Sumaye na Lowasa walikuwa wapi? Je, hawakuwa Mawaziri na Je, hawakuwa wabunge? Bahati njema wote wawili wamepata kuwa Mawaziri wakuu huku Sumaye akihudumu kwa kipindi chote cha mpito huo na kuvunja rekodi ya kuwa Waziri Mkuu pekee tangu nchi hii ipate uhuru kuhudumu kwa miaka 10. Aliongoza kipindi cha mageuzi ya kiuchumi na ubinafsishaji wa migodi hii yote (1995-2005). Lowasa yeye amekuwapo kama Waziri Mkuu (2006-2008) lakini kabla ya hapo amekuwa Waziri kamili kwa zaidi ya miaka 20. Na amekuwa mbunge.

Wawili hawa mpaka kufikia Julai 2015 walikuwa wanachama watiifu wa CCM. Walikuwa sehemu ya yale majibu ya "Ndiooooooooo" kwa muda wote huo. Leo ushujaa wao ni upi?

Shukrani kwa Luwasa kung'amua kuwa mchakato mzima wa kufikia maamuzi ya kiserikali hauwezi kumwacha salama aliyekuwa Waziri mwenyedhamana (mtetezi mkuu wa hoja). Lakini pili, kwa dhana ya collective responsibility, hakuna namna yeyote aliyewahi kuwa Waziri au Mbunge kwa kipindi chote hicho (ukiondoa wale wa upinzani waliowahi kupinga) kukwepa wajibu.

Sumaye na Lowasa hawakuwepo?
 
Sio ndio maana walijiondoa? Hata jambazi akiokoka huwezi mlaumu kwa matendo ya zamani ambayo kesha yakana kuwa ni dhambi
 
Historia ni mwalimu mzuri, na kuna wakati ni vigumu kuikana.

Baada ya kusomwa taarifa mbili za Kamati za Makinikia pameibuka manabii na mashujaa wa nchi wakidai "..Rais Magufuli alikuwa wapi kipindi hicho chote" amekuwa Mbunge na Waziri kwa kipindi cha takribani miongo miwili na sasa Ndiye Rais. Kwanini hakuchukua hatua? Baadhi ya mashujaa hao walionukuliwa kirefu na vyombo vyetu vya habari ni Luwasa na Sumaye.
Pole sana! Ulitakiwa kujiuliza kwanini wanasema Magufuli alikuwepo na hatajwi mtu mwingine yeyote!!

Ukimsikia JPM akiongea mtu anaweza kudhani jamaa kadondoshwa kutoka sayari ya Mars ili kuja kuingoza Tanzania ambayo alikuwa haifahamu hata kidogo!!!

Hata mwananchi wa kawaida alikuwa anafahamu kwamba makampuni ya madini yanafanya wizi mkubwa sana! Hilo lipo wazi!

Lakini JPM ukimsikia anaongea utadhani haya mambo kayafahamu baada ya kuingia Ikulu wakati yupo serikalini kwa angalau miaka 20 sasa!!!!
 
Swali lako la Kipuuzi unajua tofauti ya Waziri na rais. Ukishajua hivyo utakuwa umejibu swali lako
 
Watu wawili katika kundi la walafi 100.wakisema hapana watasikika????
 
Historia ni mwalimu mzuri, na kuna wakati ni vigumu kuikana.

Baada ya kusomwa taarifa mbili za Kamati za Makinikia pameibuka manabii na mashujaa wa nchi wakidai "..Rais Magufuli alikuwa wapi kipindi hicho chote" amekuwa Mbunge na Waziri kwa kipindi cha takribani miongo miwili na sasa Ndiye Rais. Kwanini hakuchukua hatua?
........

Sumaye na Lowasa hawakuwepo?
Kwa hiyo kuwepo kwa Sumaye na Lowassa kunafuta kuwepo kwa JPM? Sijui nani ameturoga
 
Lowasa aliyajua na ndiyo maana katika kapeini alisema atapitia upya mikataba ya madini. Mbona hamkushangilia kipindi chote wakati upinzani wanapiga kelele, wakati mnamfukuza zito bungeni?
 
Unajua unaweza kuwepo katika bunge au uwaziri na ukashindwa kufanya lolote ikiwa kiongozi mkuu au taasisi ya juu yako yenye maamuzi juu yako, ikiwa inataka ufanye inachokitaka (unakubaliana nacho tu kulinda kazi yako).
Yesu majority walitaka asulubishwe lakini Pilato hakuona kosa la mtu huyo................. mnajua kilichotokea. (wengi wape)
Mifano ni mingi lakini JPM kajitolea kulifanya hili lililomshindwa JK tumuunge mkono, ndio maana najiuliza ilikuwaje JK picha ilikuwa haipandi na MKAPA kwa muda mrefu kumbe ni mambo haya ya mikataba.
Alichokishindwa JK kakiweza JPM.
 
Sio ndio maana walijiondoa? Hata jambazi akiokoka huwezi mlaumu kwa matendo ya zamani ambayo kesha yakana kuwa ni dhambi
ACHA KUPOTOSHA ,SISI SIO NYUMBU KAMA UNAVYOFIKIRI, UNATAKA KUSEMA WALIJIONDOA KWA HAYA. LABDA NIKUKUMBUSHE WALIJIONDOA ILI KWA UROHO WA MADARAKA, WALIJIONDOA BAADA YA KUKATWA. NYUMBU WEWE UENITIA HASIRA ASUBUHI YOTE HII!!!!
mwanahalisi-jpg.523400
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom