Sumaye kugombea urais kupitia chama cha upinzani ikiwa....

Akihojiwa leo asubuhi kupitia redio Clouds, Sumaye alisema: 'Mimi ni mwanaCCM damu lakini endapo nikichukua fomu ya kugombea urais halafu nikashindwa na mtu (Lowasa) kwa sababu ya kutumia fedha kuhonga na kugawa rushwa, basi mtanisamehe--nitagombea kupitia chama chochote cha upinzani', alisema.

Wakati huo huo, mwanasiasa mkongwe, babu Kingunge Ngombale Mwilu amewaunga mkono wale walioanza mapema mbio za urais kwa sababu kujitokeza mapema kutawafanya wananchi wawajue, wawajadili na kufanya uamuzi sahihi wakati wa uteuzi/uchaguzi utakapofika.

MY TAKE:
1. Sumaye anatanguliza mbele maslahi binafsi kuliko maslahi ya chama/umma; na hii ndiyo tabia ya wanaCCM wengi--wanajali matumbo yao zaidi ya maslahi na ustawi wa nchi. Ufisadi na ubadhilifu wa mali za umma miongmi mwa wanaCCM, ni matokeo ya ubinafsi na uchumia tumbo na utovu wa maadili

2. Huu mchuano wa URAIS, ambapo kila mtu huibuka na kusema la kwake, utaipasua CCM hata kabla ya 2015.

Ngoja tusubiri tuone huu mtanange utaishaje.

Kwanza ungetangaza maslahi ambayo umeyficha nyuma ya mada yako. Pili sio Clouds ni Radio Tumaini ya Kanisa Katoliki, ambayo maajabu yaliyotokea hata file la hayo mahojiano limepotea!!!!!

Jambo lingine ni kwamba hakusema atagombea wala atachukua fomu kwa chama kingine bali amesema chama kitagawanyika kama atapitishwa anayegawa fedha za rushwa kwani hata yeye hatompiga kampeni mla rushwa, na akasisitiza akipitishwa mtu msafi hata yeye atakipigia kampeni chama chake. Sasa hayo maslahi unayoyasema yako wapi? ndio maana umechanganya mada na ya Kingunge kumtetea Lowassa. Hujakatazwa kumtetea mtu lakini tujitahidi kutopindisha maneno kwa kulishwa maneno na kuyaweka humu. Kwa taarifa ni kwamba watu wamerekodi live majumbani mwao na audio ipo.

Ni kweli ndani ya CCM hakuna msafi asilimia mia moja hali kadhalika kwa sasa tumeshasikia ndani ya upinzani nako si safi kabisa na sasa wabunge wanajichotea mamilioni (wakiwamo wapinzani) na wanatetea hadi mapovu yanawatoka. Lakini jambo la msingi wanaokemea rushwa tusiwabeze huenda wakatubu na Lowassa asimame akemee rushwa na ufisadi ili tumuone naye ni msafi ama anaelekea kutubu.
 
CCM wanajisifu wao wakongwe wa democrasia cha ajabu

1. Lowasa anapigwa vita kwasababu ya wakaskazin, rejea kauli ya UVCCM kule pwana (Rais ajae hawezi toka kaskazin)

2. Samwel Sita anabaguliwa vibaya kwasababu sio wa pwani ni mnyamwezi wa Tabora, hata uspika alitoswa

3. Mwakyembe, Mwandosya pia wanabaguliwa kwasbabu ya wao sio wa pwani-watu wa mbeya hawatakiwi, kumbuka

-Afya ya mwandosya ipo matatani, ukitaka kufahamu kwanini ccm wanafaham nadhani kunaharufu ya kukoliba hivi

-Afya ya mwakyembe matatani, ccm wanafaham sababu ya hii makitu

-Na Mulugo katimuliwa uwaziri kawambwa kaachwa kwasababu ni mjomba wa Kikwete.

Sasa tunasubiri kuona huo umakini wa ccm kubaguwa watu wa magharibi, kaskazin na kusin kama ndiyo demokrasia

na kukivusha salama kwa manufaa ya watu wa mikowa ya pwani peke yao.

Duh!! Afya ya MWakyembe matatani, Lowassa mzima kabisa ila ni Mkaskazini!!! no comment
 
Acha dhana ya kibaguzi wewe kama huna hoja ya msingi bora ukae kimya. Wanaopiga kura sio watu wa pwani, pwani ni sehemu ndogo sana ya Tanzania na wajumbe wanaomteua mgombea wa uraisi wa CCm wanatoka nchi nzima. Inaonekana wewe mbaguzi ndio mnaoeneza propaganda eti chadema chama cha kikanda.


Nataka unijibu kitu kidogo tu.

1. Uvccm waliposema kiongozi/rais ajaye hatatoka kaskazin walimaanisha umoja au ubaguzi

2. Je ccm ilichukuwa jukumgani kuwawajibisha wale uvccm kama kweli hawakupata baraka za wakuu wa huko pwani

3. kama ccm ilichukuwa hatua stahiki kukemea kitendo kile nani alitoa kauli ya kulaan, wapi na lini?

Huo ndio ubaguzi ndani ya ccm. kama hufaham basi UVccm wanafaham na ndiyo sababu juzi wamendeleza waliyo yaasisi kule pwali kwa Edward Lowasa kupitia Makonda.

Tuendelee mpaka tuhitimishe tufaham nani hasa mbaguzi na kwanini...
 
Mi rais hata atoke chooni nini kaskazini? Nitampigia kura mradi awe na akili timamu sio kusema utaruhusu bangi na pombe gongo halafu nikuchague maviiii!
 
Mi rais hata atoke chooni nini kaskazini? Nitampigia kura mradi awe na akili timamu sio kusema utaruhusu bangi na pombe gongo halafu nikuchague maviiii!


Inamaana funza wa chooni na kinyesi kwako sio tatizo? lazima uwe wa ajabu.....
 
Akihojiwa leo asubuhi kupitia redio Clouds, Sumaye alisema: 'Mimi ni mwanaCCM damu lakini endapo nikichukua fomu ya kugombea urais halafu nikashindwa na mtu (Lowasa) kwa sababu ya kutumia fedha kuhonga na kugawa rushwa, basi mtanisamehe--nitagombea kupitia chama chochote cha upinzani', alisema.

Wakati huo huo, mwanasiasa mkongwe, babu Kingunge Ngombale Mwilu amewaunga mkono wale walioanza mapema mbio za urais kwa sababu kujitokeza mapema kutawafanya wananchi wawajue, wawajadili na kufanya uamuzi sahihi wakati wa uteuzi/uchaguzi utakapofika.

MY TAKE:
1. Sumaye anatanguliza mbele maslahi binafsi kuliko maslahi ya chama/umma; na hii ndiyo tabia ya wanaCCM wengi--wanajali matumbo yao zaidi ya maslahi na ustawi wa nchi. Ufisadi na ubadhilifu wa mali za umma miongmi mwa wanaCCM, ni matokeo ya ubinafsi na uchumia tumbo na utovu wa maadili

2. Huu mchuano wa URAIS, ambapo kila mtu huibuka na kusema la kwake, utaipasua CCM hata kabla ya 2015.

Ngoja tusubiri tuone huu mtanange utaishaje.

Palipokolezwa nyekundu pahusika:
Kwani mkuu ungetaka CCM iendelee kubaki hai kwa manufaa gani? si ilishakaribia kufa na kinachoelendea sasa ni majipu kupasuka tu...kumbukka kuwa majambazi, majangili, mafisadi, wateka nyara, wauza unga, wanajisi watoto, waiba kura..., ongezea sifa nyingine! ndio sifa chache tu kati ya sifa lukuki za hao jamaa! Kwa sifa kama hizo za kuzimu, ni chama hai kinachohitajika kuwepo duniani? kiongoze wananchi watanganyika wapole, maskini (wa kulazimishwa) na wasio na hatia kama wa nchi yetu? Genge hili litapasuka, kitakufa na wanaokishabikia na kujining'iniza nacho wanakwenda nacho...!
 
Hapana ! Huwezi kumlinganisha Pinda na Sumaye hata siku moja
Pinda yuko kwa vile ameteuliwa na raisi wake vinginevyo hawezi

Sumaye hajawahi kulia bungeni na wabunge walikuwa na nidhamu..

Sumaye serikali ilikuwa inatisha siyo kila waziri anasema apendavyo
 
tpaul hapo uliposema huu mchuano wa Urais ambapo kila mmoja anajitokeza ndani ya ccm na kusema lake hakika itawagharimu sana ccm na itawapasua vipande vipande na Mi binafsi ingekuwa hivyo ingependeza sana!

Na watapasuana wenyewe kwa wenyewe!
 
Last edited by a moderator:
tatizo la wanaCCM ni makundi yaliyojengwa na JK yapata miaka 10 iliyopita. na kingine ambacho kitawaumiza zaidi ni kutokuaminiana (refer kauli ya JK ya wanaCCM kutoachiana chupa ya maji).
 
Kwanini viongozi wa ccm wanamhanya lowassa hivyo? Mpaka sitta na yeye anasema hatampigia kampeni lowassa akipitishwa,sumaye na sitta akili zenu mbovu,lowassa anakubalika na watz akikosa kura zenu 2 atashinda tu
 
Arusha. Mpasuko ndani ya CCM unazidi kuongezeka baada ya viongozi wa chama hicho Mkoa wa Arusha na Wilaya ya Monduli kuibuka na kukemea ‘siasa za vitisho na hofu' dhidi ya Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa.

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Arusha, Onesmo Ole Nangole, akiambatana na Mwenyekiti wa Wilaya ya Monduli, Reuben Ole Kuney na Katibu Mwenezi wa CCM Mkoa wa Arusha, Isaack Joseph alieleza kuchoshwa na kauli za vitisho dhidi ya Lowassa zinazotolewa na baadhi ya viongozi wa chama hicho, wakati wanachama wote ni sawa na hakuna mwenye ukubwa mithili ya tembo wa kumtisha mwenzake.

Kauli ya kiongozi huyo, imekuja siku mbili baada ya Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete kukemea vitendo vya rushwa kwa watu wanaotaka kuwania urais na kuiagiza Kamati ya Maadili ya chama hicho inayoongozwa na Makamu Mwenyekiti wa CCM, Philip Mangula kuwashughulikia.

Akizungumza katika mkutano wa utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi katika Kata ya Monduli Mjini ambao pia ulienda sambamba na maadhimisho ya miaka 37 ya CCM, Nangole alisema wanachama wote wa CCM wana haki sawa na hakuna wa kuogopwa kama tembo, wala mdogo wa kunyanyaswa kama sisimizi, ili mradi hakuna ambaye anavunja sheria na taratibu za chama hicho.

"CCM ni yetu sote, hakuna mtu wa kuogopwa kama tembo wala sisimizi, mimi binafsi sijaona kosa alilofanya Lowassa hadi sasa. Kwa nini wanamfuatafuata na kumshambulia kupitia vyombo vya habari?" alihoji Nangole.

Alisema anawashangaa baadhi ya viongozi kuanza kutoa kauli za kumshambulia Lowassa na kumtishia kumpeleka katika Kamati ya Maadili ya chama hicho kwa tuhuma kuwa, ameanza kampeni za urais, jambo ambalo sio kweli, kwani tangu mwaka 1993 amekuwa akiendesha harambee mbalimbali na amekuwa akifanya sherehe kila mwaka nyumbani kwake.

"Nakumbuka Rais Jakaya Kikwete mwenyewe alihudhuria sherehe nyumbani kwa Lowassa mwaka 2006 na alimpongeza kwa sherehe hiyo kwa kuwaalika marafiki zake wengi na kupokea mwaka mpya, lakini nashangaa sasa sherehe yake kuwa nongwa," alisema Nangole.

Alisema anaamini kuna ajenda ya siri dhidi ya Lowassa, kwani hata makada wengine wa chama hicho wameonyesha nia ya kuwania urais, lakini hakuna ambaye anawasema.

"Kwani hatujuani? Tunajuana, wapo wanaopita wanasema hawajaoteshwa wanangoja kuoteshwa, wengine wanasema afya zao nzuri na wanaweza kuongoza miaka mitano, wengine wamesambaza kalenda nchi nzima na wengine wanapigiwa kampeni na viongozi wa juu wa chama, lakini hakuna anayesemwa zaidi ya Lowassa," alisema Nangole.

Nangole alisema wao wanajua taratibu za chama, hivyo hawawezi sasa kuanza kampeni kabla ya muda mwafaka.

Alisema Tanzania ni ya watu wote na waliongia CCM ni kutokana na kuwa na imani ya chama hicho, hivyo hakuna sababu za ubabe na baadhi kujiona bora zaidi ya wengine.

Alisema Lowassa tangu mwaka 1993/4 alipokuwa waziri katika Ofisi ya Waziri Mkuu, alianza utaratibu wa harambee kusaidia wazazi waliokuwa na watoto wanaokosa nafasi ya shule na kuanzisha mifuko na alikuwa akienda kanisani na misikitini, iweje leo iwe nongwa?

"Mungu amempa uwezo akisimama watu humfuata nyuma katika kusaidia wanyonge, yeye ana nguvu za Mungu, nadhani hiyo ndiyo inamletea taabu. Sasa mimi niulize kuna kamati za maadili sawa, tangu mwaka 1993 ameanza harambee leo wanasema ameanza kampeni?" alihoji Nangole.

Alisema Lowassa amekuwa akisaidia kila pembe ya nchi katika nyumba za ibada na hafanyi kampeni, kwani hao wanaosaidiwa siyo wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM.

Amshambulia Malecela

Alisema anamheshimu sana Makamu Mwenyekiti mstaafu wa chama hicho, John Malecela na alidhani angetumia busara zake kumsaidia Rais Kikwete ili kukabiliana na matatizo ya kijamii kuliko kuibua suala la fulana za kuashiria Lowassa ameanza kampeni.

"Tuna matatizo ya ajira, elimu, afya, ajali, rais anahangaika usiku na mchana, ningedhani huyu mzee mwenye umri mkubwa ameongoza nchi kama Makamu wa Rais, Waziri Mkuu na Makamu Mwenyekiti wa CCM, angemshauri Rais kwani tuna matatizo mengi kuliko fulana. Mimi nadhani busara zake zingesaidia taifa kuliko fulana ambazo hata wanamichezo wanapewa. Nimesikitika sana," alisema Nangole.

Nangole amekuwa mwenyekiti wa tatu wa CCM mkoa kujitokeza hadharani na kutoa matamshi ya kutetea kinachoelezwa kama mienendo ya Lowassa.

Wengine ni Khamis Mgeja wa Shinyanga na Mgana Msindai wa Singida wanaoungana na wabunge, John Komba wa Mbinga Magharibi na Beatrice Shellukindo wa Jimbo la Kilindi.

Lowassa asiwe na hofu

Kwa upande wake ole Kuney alisema anashangaa watu wanaomshambulia Lowassa bila sababu za msingi hasa kuhusiana na mbio za urais ambazo hata hajatangaza.

"Mbona watu wengi wanasema wanataka kugombea na wanajulikana, mbona hawasemwi. Tunamwomba Lowassa asiwe na hofu awapuuze hawa watu, wanatapatapa kama wafamaji," alisema Ole Kuney.

Alisema lazima ijulikane Lowassa ana watu, ana marafiki wa kila aina, kwa hiyo akizunguka na wajasiriamali hakuna tatizo.
 
kuibuka kwa sumaye kisiasa kumetokana na ombwe la uongozi lililopo ndani ya ccm na serikali yake kwa sasa hivi. ndiyo maana hata sumaye anajiona mwenye jongo miongoni mwa vipofu.
 
Mi rais hata atoke chooni nini kaskazini? Nitampigia kura mradi awe na akili timamu sio kusema utaruhusu bangi na pombe gongo halafu nikuchague maviiii!

Maelezo tu yanatufahamisha kuwa huyu ni gamba au la!mjipange mwaka kesho
 
Mi rais hata atoke chooni nini kaskazini? Nitampigia kura mradi awe na akili timamu sio kusema utaruhusu bangi na pombe gongo halafu nikuchague maviiii!

Hakika wewe ni mmoja wa wanaonufaika na hii sheria ya kijinga ya eti "kudhibiti gongo" na bila shaka ni Polisi wewe!
Gongo ni mradi wa kuwatajirisha polisi na watawala wa vitongoji ( wengi wao wakiwa maCCM) wanaopelekewa "mgawo" kila siku na wapika gongo. Unajua fika kwamba likihalalishwa watoto hawataenda choo.
Eti na wewe unataka tukuchukulie kama ni critical thinker! Ukweli ni kwamba yeyote mwenye akili timamu anayeweza kuufikirisha ubongo wake kiduchu tu hata kwa kiwango cha darasa la nne atagundua marufuku ya gongo ni mradi wa kuwanufaisha watawala wanaogawana tozo toka kwa watengenezaji kiila siku wengi wao wakiwa viongozi wa CCM, Mahakimu na Polisi wa ngazi zote wanaopelekewa mgawo na walio chini yao.
Hii inafafanua kwa nini maCCM yamelishikia bango tamko la Dr. Slaa kwamba endapo chama chake kitashika dola kitaukatilia mbali mrija huu.
Hatua hiyo haitakuwa ya ajabu kwani karibu nchi zote zinazotuzunguuka wameruhusu na wako sawa tu.
Uganda wanaiita waragi, Msumbiji Aguadenti Kenya chang'aa n.k.
Juu ya bange sijamsikia akisema ataihalalisha ingawa kwangu haitakuwa ajabu pia kwani hata Marekani na nchi kadhaa za ulaya wameamua kuihalisha kwa baadhi ya matumizi. Hivi wewe unaishi katika shimo gani kiasi cha kushindwa kuelewa hata mambo madogomdogo kama haya?
 
Kama naota ndoto leo ni tarehe 31/10/2015 pale uwanja wa UHURU kukiwa kumefurika watu, bendi ya Capt Komba ikitumbuiza, inaashiria mgombea wa thi thi emu ndio mshindi. Juu la jukwaa kuu kwa mbali (mimi niko mbali) namuona Raisi wa sasa anatabasamu na anapiga makofi na kucheza taratibu kulingana na mdundo wa muziki wenyewe. Kwa mbali zaidi kwenye lando kuu la kaskazini naona benzi leusi rangi iliyokolea kwa sababu iko tinted sikumuona aliyekua ndani, ila nafikiri ndio anayekwenda kuapishwa. Nikiwa naangalia kwa hamu niweze kumuona anayeshuka ghafla njozi ikakatika nikashtuka.Tuombe Mungu niote niangalie atakayeshuka kuapishwa
 
Hapana ! Huwezi kumlinganisha Pinda na Sumaye hata siku moja
Pinda yuko kwa vile ameteuliwa na raisi wake vinginevyo hawezi
kwani sumaye kafanya kitu gani au kwa kupambana na vyama vya upinzani na kuwahonga akina lamwai ili upinzani ufe.sumaye hana jipya bora mara 20 lowasa hata anayo mifano km mashule ya kata maji shinyanga na mto nile
 
Back
Top Bottom