Sumaye azungumza na waandishi; ajibu maswali masuala ya kitaifa

Ningekuwa mwandishi - haya ya akina Sumaye na akina mrema yasingepata nafasi kwenye magazeti yangu!

By the way - wangemuuliza Havard alisomeshwa na nani?- Serikali au yeye mwenyewe! You would be surprised!
 
Wachangiaji wengi humu naona hawasomi contents, isipokuwa wanajibu kwa kusoma headline tu.

Kwenye tangazo lake alitangaza mambo ambayo atayazungumzia, badala ya kuzungumzia hayo watu wanaanza kuguess, wakati ashasema atakachozungumza.

Ameanza kuchangia million tano, wengine muungeni mkono katika kuliwezesha jukwaa la wahariri au kitu kingine kitakachofanya waandishi wetu waive katika fani yao.
 
Hi ni swali muhimu la kumuuliza kiongozi yeyote( Sitta,Sumaye, JK etc)?: Aeleze uamuzi au ushauri wowote mbaya aliowai kuufanya au kuagiza utekelezwe.

Kama ni malaika:Atasema hajawai
 
Wachangiaji wengi humu naona hawasomi contents, isipokuwa wanajibu kwa kusoma headline tu.

Kwenye tangazo lake alitangaza mambo ambayo atayazungumzia, badala ya kuzungumzia hayo watu wanaanza kuguess, wakati ashasema atakachozungumza.


Ameanza kuchangia million tano, wengine muungeni mkono katika kuliwezesha jukwaa la wahariri au kitu kingine kitakachofanya waandishi wetu waive katika fani yao.

Tatizo hukuepo wakati mjadala ulipoanza ku-evolve. Lakini naelewa unachotaka kusema japo umekosea.
 
Sumaye as the longest serving PM...Has the right to call press conference..especially katika wakati tulio nao ..ni muhimu kwa watu wenye sauti kutoa nasaha zao mbali mbali...

Suala la kugombea urais ameshasema hagombei..tuache ku speculate sasa...

Kikwete anaendelea na urais kwa kipindi cha pili...hiyo compromise imeshafikiwa..ni wazi....la sivyo watu kama salim na sumaye wangeamua kugombea ukweli hali ya hewa ingechafuka ....sana.,ni wazi wamekubali amalizie muhula wake!
 
Simuelewi. Pale mwanzo alisema hatapokea maswali!

Hilo pembeni. Kwa nini anapoulizwa kuhusu akaunti zake na kutangaza mali zake anakimbilia kusema yeye sasa ni raia wa kawaida lakini yuko tayari kuzungumzia uchaguzi, rada nk? Raia gani "wa kawaida" anaitisha press conference?

Mimi kama Ngabu, sioni kwa nini alifanya waandishi wa habari wasiende ibada na misa za saa 4 wakasikilize maneno yake matupu
 
Mbona tunamwekea manaeno kinywani? Great thinker would not make such a baseless guess. Kwani URAISI si ni haki ya kila mmoja hapa kwa mujibu wa katiba?

Aliyoyaeleza nimeyafurahia kwa sababu, damage za wahariri kwa watu wasiokuwa na pa kusemea ni kubwa sana. Na ningefurahi sana kama wote tungeangalia contents za mkutano wake. Mfano: Kwanini huyo mhariri amedharau wito uliotolewa kwake kutoka kwenye chombo ambacho ni cha kwao waandishi wenyewe. Hivi kama wanadharau vyombo vyao wenyewe sisi tutashawishika vipi kwenda hapo tena?

Unaweza kuona namna mtu anavyoweza kutupa habari ya kukumaliza hewani kisha akakaidi kila kinachotakiwa, lakini yeye maisha yake yako sawa na wewe ndiyo kashakumaliza.

haya ndiyo muhimu kwenye press conference yake.
 
Kama PM aliyekuwa madarakani kwa muda mrefu alichukua jitihada au aliweka mazingira gani kwa hili tatizo la biased, corrupted journalism?. Na Taasisi ya Utangazaji Tanzania( TVT,RTD)iko chini ya ofisi ya PM
 
Huyo Billionea Sumaye hana Chochote zaidi ya kuwanunua waandishi wa HAbari,
swali ni kuwa kama lile gazeti la mwanzo lililomwandika kama ana Account nje mbona alilipeleka Mahakamani, lakini hili lingine mbona anaishia kwenye majukwaa tu.

anakuja mbele za watu kulialia ili aonekane rofa, kumbe ni tajiri wa kutupa, huyo Bwana ana boats za uvuvi na mpaka ndege yake mwenyewe katiak kiwanda chake cha samamki MAfia anamtumia mama mmoja wa kihindi,

na watu hawana habari, Buguruni karibu yote keshainunua kwa kutumia wanunuaji wake fake, muda si mrefu ataanza kujenga apartment zake hapo buguruni

hiyo ya Shamba na Kigoda ni la ukweli, kama anaonewa angeenda mahakamani
 
Thanks Frederick Sumaye, PM wetu ambaye alipomaliza muda wake alikuwa kidogo tu apigwe na wananchi kwa sababu tuhuma zilikuwa zimemuelemea.

Nafikiri sasa huu utakuwa mwanzo wa watu wengine waliotuhumiwa kwa tuhuma mbalimbali kuanza kujisafisha kwa kuja na ukweli.

Nafikiri wale waliotuhumiwa kwa UFISADI kuanzia Kagoda, EPA, Richiemond, Utapeli wa Elimu nk nao watatoka muda si mrefu hili tujue ukweli wa mambo.

Lakini pia naona mambo aliyoyasema mengine ni ya muda mrefu. Je alikuwa wapi asiweze kujisafisha wakati ule mpaka anatoka sasa? Ni ubize wa shule? Au ndio kuelekea uchaguzi mkuu?

 
Hivi alikuwa wapi siku zote hizo kuzungumza haya?why now?

Ni kwamba pamoja na kwamba mtandao ulimtumia magezeti kumchafua kwa ukweli na uwongo, JK kamuomba amuunge mkono na kumpigia debe. labda na yeye atapigiwa debe 2015.

Ndiyo sababu kaja muda huu.
 
Ni kwamba pamoja na kwamba mtandao ulimtumia magezeti kumchafua kwa ukweli na uwongo, JK kamuomba amuunge mkono na kumpigia debe. labda na yeye atapigiwa debe 2015.

Ndiyo sababu kaja muda huu.

Kwahiyo alivyodai kwamba kuzungumza kwake na waandishi leo hakuna uhusiano na uchaguzi mkuu wa mwaka huu ilikuwa ni dangaya toto?
 
Tunajua kachelewa kuongea lakini aloongea ni sensitive matter maranyingi waandishi wa habari wanakuza sana mambo na kuzua wakati mwingine huumiza watu.
 
Kwa Tanzania yetu hii, tunashukuru kuna vyombo vya habari kama JF vinavyoweza kutupatia habari kutoka source.

Zaidi ya hapo tungepata habari kutoka magazeti ya kesho ambayo hayataandika hata hiyo habari aliyosema Mh. Sumaye bali maswali na majibu aliyoulizwa, au alivaa nini etc. Wait & See!!!
 
Haya yanayotokea leo ya watu kuchafuana ni matokeo ya wao wenyewe kutumia vyombo vya habari kujijenga kisiasa kwa kuchafua wenzao. Waandishi wengi wa habari wapo tayari kufanya lolote la kishetani endapo fedha itatangulizwa. Wote tunakumbuka kuelekea uchaguzi wa 2005 watu walivyokuwa wananunua vyombo vya habari kuwachafua wenzao.

Huyu Sumaye alikuwa wapi katika miaka yake mingi ya uwaziri mkuu kukemea na kusisitiza maadili katika vyombo vya habari? Inafaa pia aombe radhi kwa makosa waliyotutendea watanzania, sio kutaka tumwonee huruma mwizi mkubwa.

Nadhani wamesign pact ya kusafishana na kupigiana debe na mchekeshaji mwenzake wa magogoni, shame!!
 
kwa sasa kutangaza sio raisi sana kwa sababu mwelekeo wa Mkulu bado haujajulikana na Mkwara wa UWT (Usalama wa Taifa), kupitia Sheikh Yahaya kwamba Damu lazima imwagike mtu akimpinga JK katika njia ya Magogoni,

kwa hiyo atakuwa na kauoga fulani, lakini nadhani 2015 lazima atajitosa

Mkuu,

umenivunja mbavu.ila mbinu ya mwaka huu kali,ukiona hali inaweza kuwa mbaya wewe mtumie tu sheikh yahya.Ati ikiwa hivi au vile 'utakuafa kifo cha ghafla'
 
Haya yanayotokea leo ya watu kuchafuana ni matokeo ya wao wenyewe kutumia vyombo vya habari kujijenga kisiasa kwa kuchafua wenzao. Waandishi wengi wa habari wapo tayari kufanya lolote la kishetani endapo fedha itatangulizwa. Wote tunakumbuka kuelekea uchaguzi wa 2005 watu walivyokuwa wananunua vyombo vya habari kuwachafua wenzao.

Huyu Sumaye alikuwa wapi katika miaka yake mingi ya uwaziri mkuu kukemea na kusisitiza maadili katika vyombo vya habari? !!

Kumbuka Sumaye ni muathirika mkubwa sana wa uchafuzi uliofanywa na vyombo vya habari dhidi yake kuelekea 2005, na endapo angepambana nao wakati ule akiwa PM dhidi ya tuhuma zilizokuwa zinaelekezwa kwake ingetafsiriwa kuwa ni ukandamizaji wa serikali dhidi ya vyombo vya habari.
 
Back
Top Bottom