SUMATRA kujiingiza kwenye mkumbo wa Kupiga marufuku Siasa nchini, ni aibu kwa nchi na Idara za Umma

Queen V

JF-Expert Member
Jan 19, 2012
776
1,330
Mwaka jana mwezi wa 7, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli alitoa Marufuku ya kufanyika kwa mikutano ya kisiasa nchini na kwamba siasa hadi 2020.

Kama hiyo haitoshi, mwezi Novemba, 2017 Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Majini na Nchi Kavu (SUMATRA) ilipiga Marufuku abiria kuzungumza siasa, dini, biashara ndani ya basi! ‬

SUMATRA ilisema kuwa atakayebainika kufanya vitendo hivyo hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.

Agizo hilo lilikuja baada ya kudaiwa kuwapo kwa mvutano wa kupinga kanuni mpya kati ya SUMATRA na Chama cha Wamiliki Mabasi yaendayo Mikoani (TABOA) na Umoja wa Wamiliki wa Vyombo vya Usafiri Dar es Salaam (UWAMADAR).

Bila kutaja ni sheria na kanuni ipi, Mkurugenzi wa SUMATRA amesema ufanyaji wa vitendo hivyo katika mabasi ni kinyume na kanuni za usafirishaji.

Wanasiasa wengine(maana wapo wanaofanya siasa hata kwenye mikutano isiyo ya chama) wamekatazwa kufanya siasa nchini maana mikutano na maandamano ya kisiasa ndio chachu ya ukuaji wa kisiasa.

Wananchi tumekatazwa kujadili siasa pia. Je Siasa zimemilikiwa na Chama/ Watu fulani?
 
Haya yote yanafanywa ili kutetea matumbo. Sasa hivi Wafanyakazi wa Serikali wanafanya kazi ili rais awaone. Ndo maana unaona watu wanatoa matamko yaliyo nje ya majukumu yao. Mfano Sumatra. Hawa jamaa ni Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Majini na Nchi Kavu lakini wanazungumzia Siasa ili wapate kiki. Huko kwenye Majini na Nchi Kavu hawasikiki.

Rais alipiga marufuku siasa. Nao wanapiga marufuku siasa ili rais aone wapo naye uelekeo mmoja. Wanajiaibisha na ni ujinga.
Inaelekea kuna ‘bundi’ anainyemelea nchi yetu taratibu na huenda watu wamechoka amani iliyopo. Ndo maana wanabana matundu yote ya kuongelea kuanzia Mitandaoni. Kuna kipindi walitaka nchi nzima iwe inaangalia habari tbc1 tu eti ndo uzalendo. Hivi Vitendo tumevichoka kwa kweli

Rais akiwa mkoani Singida alisema: “Wasije wakanijaribu, mimi ni tofauti sana na kama wapo watu wanawatumia wakawaeleze vizuri”. Bila kujua amechaguliwa. Kufanya siasa anasema ni kufanya fujo. “siyo mtu unatoka Hai kwenda Kahama kushawishi watu wafanye fujo”

Ndiyo maana Vyama vya Upinzani Vikaja na msamiati “dictatorial democracy” yaani demokrasia ya kidikteta au ya kiimla kwa lugha nyepesi. Kinachoendelea katika nchi yetu hii ya kidemokrasia ni sheria ya utawala badala ya utawala wa sheria. Yaani watawala ndo wanaamua sheria iweje sio sheria inaamua watawala watawaleje.

Kanuni ya kwanza ya mwendo ya Newton inasema: “kitu huendelea kuwa katika hali ya kupumzika au mwenendo endelevu isipokuwa kikilazimishwa kufanya vinginevyo na nguvu kutoka nje”.

Wazungu waliwanyanyasa na kuwatesa sana mababu zetu, lakini pamoja na kwamba wazungu walikuwa na Uwezo Mkubwa mwisho wa siku walibwaga manyanga.

Wahenga walisema Giza likzidi kunakuwa kunakaribia kupambazuka.
 
Kwakweli nmeshangaa sana. Ngoja kwanza nione mawazo ya hawa wakuu wanasemaje. Pale Ubungo kuna watu walikuwa wanapanda asubuhi wanaombea safari, nasikia na wao wamepigwa marufuku.

Mbaya zaidi, Konda na dereva ndo watakamatwa. Ndo Mamonita hahahaaa.... Jamaa nlisikia akise a, “Kuruhusu watu waanze siasa, mahubiri, mambo ya kwao, wanapiga kelele…. hapa ni dereva au kondakta wa lile basi ndio tutamchukulia hatua,” Jamani!.

Naomba Kuuna Mchango wa hawa wakuu kwenye huu Mjadala. Je ni sahihi? Nini kifanyike?

Hii aione mkuu lendila, Jitu jeusi, mjr95, Bonny, Concoction, Boniphace Kichonge, Pohamba, imhotep, MKWEPA KODI, lusungo, Job K, Terrible Teen, gemmanuel265, Earthmover, idawa, jogi, Annael, Elitwege, leonaldo, OKW BOBAN SUNZU, PakavuNateleza, Halaiser, na tajirijasiri
 
Hivi Siasa ni nin kutoka kwenye tafsiri ya @Pascal Mayalla kwenye uzi wa Nini maana ya siasa?
aliseme "Siasa ni utekelezaji wote wa mkataba kati ya watawala na watawaliwa ambao msingi wake ni katiba na demokrasia ambayo ni serikali ya watu, inayoongozwa na watu kwa manufaa ya watu, 'The people by the people and for the people'

Sasa unapokataza upande mmoja kuzungumzia utekelezaji wa huo mkataba unakuwa unavunja maana kamili ya siasa kwa ujumla wake.
Maisha ya watanzania tumechagua kutawaliwa na siasa kwa maana hata huyo aliekataza hilo swala amelizungumzia kwenye muktadha wa siasa na kumfurahisha alie juu yake.
Siamin kama kuna mabadiliko makubwa ambayo yamefanyika Sumatra kiasi cha kusababisha uongozi uliokuwepo kipind cha awamu iliyopita usiwepo tena sasa hv kwa maana ya uongozi mpya kuona sio haki kwa watawaliwa kuzungumzia utekelezwaji wa mikataba yao na watawala kwa mising ya katiba na demokrasia.

Sehemu ya tatu ya katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzani HAKI NA WAJIBU WA MAONI
18.-(1) Bila ya kuathiri sheria za nchi, kila mtu yuko huru kuwa na maoni yoyote na kutoa nje mawazo yake, na kutafuta,
kupokea na kutoa habari na dhana zozote kupitia chombo chochote bila ya kujali mipaka ya nchi, na pia ana uhuru wa
mawasiliano yake kutoingiliwa kati.

Kwa muktadha huo sasa naona kama sumatra wanavunja uhuru wa kuingilia mawasiliano yeti kati ya mtu mmoja na mwengne kwa maana inapanga cha kuzungumza kati ya mtu mmoja na mwengne
 
Nafikiri mleta HOJA hukuelewa wala hukufuatilia walichosema Sumatra hata kdg na anachofanya ni upotoshaji, walichosema Sumatra (kwani mie nilifuatilia sana hili) ni haya yafuatayo;
  1. Ni marufuku kwa watu wanaoingia ktk mabasi na kuanza kufanya siasa za vya vyama vyao (kuhubiri) na sio abiria kwa abiria kuongea yao.
  2. Wanaoingia ktk mabasi na kuanza kuhubiri imani zao za dini kwa abiri walio ndani ya mabasi
  3. wanaoingia na kuanza kunadi biashara zao kwa kuuza bidhaa ndani ya mabasi yawapo safarini.
Nafikiri kabla hatujaanza 'kupayuka' ni vyema tukasoma taarifa vzr na kufuatilia habari husika.
 
Hivi Siasa ni nin kutoka kwenye tafsiri ya @Pascal Mayalla kwenye uzi wa Nini maana ya siasa?
aliseme "Siasa ni utekelezaji wote wa mkataba kati ya watawala na watawaliwa ambao msingi wake ni katiba na demokrasia ambayo ni serikali ya watu, inayoongozwa na watu kwa manufaa ya watu, 'The people by the people and for the people'

Sasa unapokataza upande mmoja kuzungumzia utekelezaji wa huo mkataba unakuwa unavunja maana kamili ya siasa kwa ujumla wake.
Maisha ya watanzania tumechagua kutawaliwa na siasa kwa maana hata huyo aliekataza hilo swala amelizungumzia kwenye muktadha wa siasa na kumfurahisha alie juu yake.
Siamin kama kuna mabadiliko makubwa ambayo yamefanyika Sumatra kiasi cha kusababisha uongozi uliokuwepo kipind cha awamu iliyopita usiwepo tena sasa hv kwa maana ya uongozi mpya kuona sio haki kwa watawaliwa kuzungumzia utekelezwaji wa mikataba yao na watawala kwa mising ya katiba na demokrasia.

Sehemu ya tatu ya katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzani HAKI NA WAJIBU WA MAONI
18.-(1) Bila ya kuathiri sheria za nchi, kila mtu yuko huru kuwa na maoni yoyote na kutoa nje mawazo yake, na kutafuta,
kupokea na kutoa habari na dhana zozote kupitia chombo chochote bila ya kujali mipaka ya nchi, na pia ana uhuru wa
mawasiliano yake kutoingiliwa kati.

Kwa muktadha huo sasa naona kama sumatra wanavunja uhuru wa kuingilia mawasiliano yeti kati ya mtu mmoja na mwengne kwa maana inapanga cha kuzungumza kati ya mtu mmoja na mwengne

Mkuu, huu mstali umenibariki sana, Asante. Kumbe kuna mambo kwenye katiba mazuri tu.
Bila ya kuathiri sheria za nchi, kila mtu yuko huru kuwa na maoni yoyote na kutoa nje mawazo yake, na kutafuta,
kupokea na kutoa habari na dhana zozote kupitia chombo chochote bila ya kujali mipaka ya nchi, na pia ana uhuru wa
mawasiliano yake kutoingiliwa kati.
 
Nafikiri mleta HOJA hukuelewa wala hukufuatilia walichosema Sumatra hata kdg na anachofanya ni upotoshaji, walichosema Sumatra (kwani mie nilifuatilia sana hili) ni haya yafuatayo;
  1. Ni marufuku kwa watu wanaoingia ktk mabasi na kuanza kufanya siasa za vya vyama vyao (kuhubiri) na sio abiria kwa abiria kuongea yao.
  2. Wanaoingia ktk mabasi na kuanza kuhubiri imani zao za dini kwa abiri walio ndani ya mabasi
  3. wanaoingia na kuanza kunadi biashara zao kwa kuuza bidhaa ndani ya mabasi yawapo safarini.
Nafikiri kabla hatujaanza 'kupayuka' ni vyema tukasoma taarifa vzr na kufuatilia habari husika.
Basi labda huku mtaani inapotoshwa, Ndo maana nikaomba msaada kwa nyie wadau wa habari mtakuwa mnaujua Ukweli. Kumbe kuna watu walikuwa wanapanda kwenye daladala na kuanza kupiga Siasa. Mimi huwa naona wahubiri wanapanda pale Ubungo wanapiga neno la Mungu wakifika maeneo ya mbezi wanashuka. Ukifika chainze wanapanda Machinga wakifika mbele wanashuka.

Sijawahi kutana na mwanasiasa.
 
Sumatra wakomae na madereva wavuta bangi,ila watuache tusikilize kwaya na kaswida huku tukiongelea mambo ya taifa letu.
Hata mimi nilikuwa na hayo mawazo, kama yako. Kuna mambo mengi inabidi wapiganie sio hili la siasa tena kwenye mabasi ya watu binafsi. Au abiria waliwalalamikia?
 
Nafikiri mleta HOJA hukuelewa wala hukufuatilia walichosema Sumatra hata kdg na anachofanya ni upotoshaji, walichosema Sumatra (kwani mie nilifuatilia sana hili) ni haya yafuatayo;
  1. Ni marufuku kwa watu wanaoingia ktk mabasi na kuanza kufanya siasa za vya vyama vyao (kuhubiri) na sio abiria kwa abiria kuongea yao.
  2. Wanaoingia ktk mabasi na kuanza kuhubiri imani zao za dini kwa abiri walio ndani ya mabasi
  3. wanaoingia na kuanza kunadi biashara zao kwa kuuza bidhaa ndani ya mabasi yawapo safarini.
Nafikiri kabla hatujaanza 'kupayuka' ni vyema tukasoma taarifa vzr na kufuatilia habari husika.

Hebu soma hii taarifa ya chombo kimoja cha habari kuhusu suala hili; je wamepotosha?

""Bila kutaja ni sheria na kanuni ipi, Mkurugenzi huyo amesema ufanyaji wa vitendo hivyo katika mabasi ni kinyume na kanuni za usafirishaji.

"Tutaanza kuzuia wasafiri wa wapo ndani ya mabasi kuacha kuzungumza masuala ya siasa, dini na kufanya biashara. Tukibaini hilo hatua za kisheria zitachukuliwa kwa abiria na dereva ikibidi," amesema na kuongeza

‘Kwa madereva hasa wa kwenda mikoani, njiani wanapandisha wafanyabiashara na kufanya biashara ndani ya basi, hatua kali zitachukuliwa kwa dereva na huyo anayefanya biashara.’""
 
Hata mimi nilikuwa na hayo mawazo, kama yako. Kuna mambo mengi inabidi wapiganie sio hili la siasa tena kwenye mabasi ya watu binafsi. Au abiria waliwalalamikia?
Hakuna mtu anaweza kulalamika kuhubiriwa,kuongea ni utamaduni wetu sasa mtu atoke musoma mpaka dar huku amenyamaza tu.
 
Sumatra wakomae na madereva wavuta bangi,ila watuache tusikilize kwaya na kaswida huku tukiongelea mambo ya taifa letu.
Kwa upande wangu Hii inasaidia watu kutema nyongo. Mtu anapoongea anatoa uchafu. Hawa watu wa dini wanatoa elimu na kurekebisha mienendo ya watu kuwa na tabia njema. Kama kweli wamekatazwa hajafanya poa. Ngoja nitafute hilo tamko.
 
Hebu soma hii taarifa ya chombo kimoja cha habari kuhusu suala hili; je wamepotosha?

""Bila kutaja ni sheria na kanuni ipi, Mkurugenzi huyo amesema ufanyaji wa vitendo hivyo katika mabasi ni kinyume na kanuni za usafirishaji.

"Tutaanza kuzuia wasafiri wa wapo ndani ya mabasi kuacha kuzungumza masuala ya siasa, dini na kufanya biashara. Tukibaini hilo hatua za kisheria zitachukuliwa kwa abiria na dereva ikibidi," amesema na kuongeza

‘Kwa madereva hasa wa kwenda mikoani, njiani wanapandisha wafanyabiashara na kufanya biashara ndani ya basi, hatua kali zitachukuliwa kwa dereva na huyo anayefanya biashara.’""
Ila nadhani haina nguvu, hivi kuna mtu kashakamatwa. Ningepata msafiri anambie kama kweli wale machinga na wahubiri kama bado wanapanda. Ngoja wakina Jay One, sosoliso, Mhakiki, James Martin wakija online watanielezea hii imekaaje.
 
Sumatra pia wakomae na vitu kama unywaji wa pombe kwenye mabasi na majahazi.
Zamani wale madereva walikuwa wanaweka viroba kwenye chupa ya maji halafu anaiweka pale kwenye dashboard ukiona utajua maji. Sumatra wangesaidiana na Polisi kuwasaka walevi, lakini mazungumzo waache raia wajadili mambo kwa upana na kuongezeana ufahamu.
 
Back
Top Bottom