Suluhisho la mgogoro wa CUF: Prof. Lipumba na Maalim Seif wagombee Uenyekiti wa CUF Taifa

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Nov 25, 2010
6,135
17,802
Kila uchao, Prof. Ibrahim Haruna Lipumba na Maalim Seif Sharif Hamad wamekuwa 'wakipimana ubavu' ndani ya CUF. Imefikia hadi CUF kuonekana imegawanyika kati ya CUF Bara na CUF Zanzibar. Hadi sasa, hakuna aliyevuka bahari na kwenda kwa mwenzake kufanya ziara au mkutano.

Ni kama kila mmoja amemiliki kwake. Suluhisho lisilo na vitisho ni hili. Wawili hawa wanapaswa kugombea Uenyekiti wa CUF Taifa. Wanapaswa kuchukua fomu;kupiga kampeni na kupigiwa kura. 'Mbabe' ataibuka kidedea kwenye sanduku la kura. Hilo litamaliza mvutano usio na mfano kati yao.Au mnaonaje?

Nimekumbuka, Prof. Lipumba alishafukuzwa na kuvuliwa uanachama wa CUF! Awapishe wenye chama chao. Tunakaribia kumchoka!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
 
Profesa aombe kwanza kadi ya CUF, aombe kujiunga na CUF maana sasa si mwana cuf hana malaka yoyote ndani ya cuf, na kuomba kuna kukubalika na kukataliwa.
 
Kila uchao, Prof. Ibrahim Haruna Lipumba na Maalim Seif Sharif Hamad wamekuwa 'wakipimana ubavu' ndani ya CUF. Imefikia hadi CUF kuonekana imegawanyika kati ya CUF Bara na CUF Zanzibar. Hadi sasa, hakuna aliyevuka bahari na kwenda kwa mwenzake kufanya ziara au mkutano.
Si kweli,tokea kuadabishwa kwa Lipumba na chama cha CUF,Maalim Seif ameshavuka bahari mara kadhaa.Labda ungesema hajatia mguu Buguruni. Maalim hakuhitaji kwenda huko kwa vile jengo la ofisi limetekwa na"Scorpions"kwa msaada wa nguvu ya tatu , na hakubaliki mtu yeyote kuonekana huko zaidi ya hao na maofisa wa nguvu ya tatu.
Wawili hawa wanapaswa kugombea Uenyekiti wa CUF Taifa. Wanapaswa kuchukua fomu;kupiga kampeni na kupigiwa kura. 'Mbabe' ataibuka kidedea kwenye sanduku la kura
Moja ya sifa ya msingi ya mgombea wa taasisi yoyote ile awe ni mwanachama hai wa taasisi hiyo.Lipumba hana sifa hiyo. Pili Maalim Seif hajawahi hata kutamani kuwa Mwenyekiti sasa hoja hiyo inaweza kubaki maskani tu. Kwa vili kura itajumuisha mwanachama na asiekuwa mwanachama, nani atakuwa msimamizi ili uchaguzi uwe huru na haki? CCM mwenye uzoefu wa kunyonga demokrasia au Manokoa wake?
 
Kila uchao, Prof. Ibrahim Haruna Lipumba na Maalim Seif Sharif Hamad wamekuwa 'wakipimana ubavu' ndani ya CUF. Imefikia hadi CUF kuonekana imegawanyika kati ya CUF Bara na CUF Zanzibar. Hadi sasa, hakuna aliyevuka bahari na kwenda kwa mwenzake kufanya ziara au mkutano.

Ni kama kila mmoja amemiliki kwake. Suluhisho lisilo na vitisho ni hili. Wawili hawa wanapaswa kugombea Uenyekiti wa CUF Taifa. Wanapaswa kuchukua fomu;kupiga kampeni na kupigiwa kura. 'Mbabe' ataibuka kidedea kwenye sanduku la kura. Hilo litamaliza mvutano usio na mfano kati yao.Au mnaonaje?

Nimekumbuka, Prof. Lipumba alishafukuzwa na kuvuliwa uanachama wa CUF! Awapishe wenye chama chao. Tunakaribia kumchoka!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam

Mjomba,mbona mmempa adhabu kubwa sana huyo msomi wa uchumi?Hebu mwambieni imetosha amejidhalilisha vya kutosha,CUF haitakufa ipo sana tu
 
Kila uchao, Prof. Ibrahim Haruna Lipumba na Maalim Seif Sharif Hamad wamekuwa 'wakipimana ubavu' ndani ya CUF. Imefikia hadi CUF kuonekana imegawanyika kati ya CUF Bara na CUF Zanzibar. Hadi sasa, hakuna aliyevuka bahari na kwenda kwa mwenzake kufanya ziara au mkutano.

Ni kama kila mmoja amemiliki kwake. Suluhisho lisilo na vitisho ni hili. Wawili hawa wanapaswa kugombea Uenyekiti wa CUF Taifa. Wanapaswa kuchukua fomu;kupiga kampeni na kupigiwa kura. 'Mbabe' ataibuka kidedea kwenye sanduku la kura. Hilo litamaliza mvutano usio na mfano kati yao.Au mnaonaje?

Nimekumbuka, Prof. Lipumba alishafukuzwa na kuvuliwa uanachama wa CUF! Awapishe wenye chama chao. Tunakaribia kumchoka!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
Maalim anavyomgwaya Lipumba akifanya hivi nachukua kadi ya CUF siku hiyohiyo
 
Lipumba Alisha sema bila yeye CUF hakuna hata Kama atashindwa atarudishwa madarakani na Polisi.
 
Prof cha msingi aombe kazi tu Rais lazima atampatia maana kawaona wengi tu sasa hivi wanatumia V8. Huko kwenye KAFU hana chake, aliitariki kipindi ikimuhitaji zaidi sasa na yenyewe imemtariki rasmi.
 
Mtu ambaye ameshafukuzwa uanachama wa chama ataruhusiwa vipi kugombea uenyekiti wa chama ambacho yeye si mwanachama!

Kwanini mnataka kulazimisha huyu pandikizi wa MACCM arudishwe CUF!? Mambo ya Ngoswe mwachieni Ngoswe au mpeni uenyekiti kwenye
Chama chenu cha wahuni na mafisadi.

Kila uchao, Prof. Ibrahim Haruna Lipumba na Maalim Seif Sharif Hamad wamekuwa 'wakipimana ubavu' ndani ya CUF. Imefikia hadi CUF kuonekana imegawanyika kati ya CUF Bara na CUF Zanzibar. Hadi sasa, hakuna aliyevuka bahari na kwenda kwa mwenzake kufanya ziara au mkutano.

Ni kama kila mmoja amemiliki kwake. Suluhisho lisilo na vitisho ni hili. Wawili hawa wanapaswa kugombea Uenyekiti wa CUF Taifa. Wanapaswa kuchukua fomu;kupiga kampeni na kupigiwa kura. 'Mbabe' ataibuka kidedea kwenye sanduku la kura. Hilo litamaliza mvutano usio na mfano kati yao.Au mnaonaje?

Nimekumbuka, Prof. Lipumba alishafukuzwa na kuvuliwa uanachama wa CUF! Awapishe wenye chama chao. Tunakaribia kumchoka!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
 
Back
Top Bottom