Hakuna haja ya kuzunguka huku na huko. Nchi moja kuwa na serikali mbili au tatu ni urasimu na garama zisizokuwa lazima. NCHI MOJA SERIKALI MOJA. Basi.1. Watu wa Tanganyika wenye makazi ya kudumu Zanzibar na Wazanzibar wenye makazi ya kudumu Tanganyika, wapewe uhiari, haki na uraia wa kuendelea kuishi Zanzibar au Tanganyika mtawalia.
2. Endapo Tanganyika na Zanzibar zitaendelea kuwa na uraia wa nchi moja, basi nchi hizi mbili ziwe na makubaliano maalum ya uraia maalum wa nchi mbili (Duo Exclusive Treaty on Special Dual Citizenship) kwa Watanganyika na Wazanzibar ambao watahiari kuwa na uraia wa nchi mbili baina ya Tanganyika na Zanzibar pekee.
3. Tanganyika na Zanzibar ziwe madola huru kama ilivyokuwa kabla ya muungano na zijiunge katika jumuiya au taasisi mbalimbali za kikanda au kimataifa ikiwa pamoja na Umoja wa Mataifa (UN), FIFA, nk.
4. Pasiwepo viza ya kusafiria kati ya Tanganyika na Zanzibar isipokuwa vitambulisho vya uraia au hati za kusafiria (passports) zitumike kumtambua Mtanganyika au Mzanzibar.
5. Iundwe Tume ya Mahusiano na Ujirani Mwema baina ya Tanganyika na Zanzibar (Commission for Relations and Good Neighbourhood). Tume hii pamoja na mambo yatakayojitokeza, ifanye yafuatayo:
(a) Kuweka utaratibu wa kuimarisha uhusiano na ulinzi wa pamoja wa Majeshi ya Ulinzi ya Watu wa Zanzibar (Zanzibar People’s Defence Forces - ZPDF) na Majeshi ya Ulinzi ya Watu wa Tanganyika (Tanganyika People’s Defence Forces -TPDF). Wanajeshi wa Tanganyika na Zanzibar wataendelea kutumika kwa pamoja kulinda watu na mipaka ya Tanganyika na Zanzibar.
(b) Kugawanya madeni ya nje kulingana na uwiano halisi wa jinsi yalivyotumika kusaidia nchi mbili za Tanganyika na Zanzibar.
(c) Kuratibu balozi za nje ili ziendelee kutumiwa pamoja kiofisi (shared consulates) kwa Tanganyika na Zanzibar hadi wakati ambapo uwezo wa kila nchi utaruhusu kuwa na ubalozi wake.
(d) Kuratibu fedha na/au sarafu za aina moja ili ziendelee kutumika kihalali kati ya Tanganyika na Zanzibar ili kudumisha uhusiano na utambulisho wa kihistoria.
Hitimisho
Nikiwa mwanafunzi wa Mwalimu Nyerere nihitimishe kwa kusema alichokataza ni kufukuzana baina ya Watanganyika na Wazanzibar. Akaita dhambi kubwa sawa na kula nyama ya mtu. Hakukataza maelewano na makubaliano ya amani. Na sitegemei watu wanaokubaliana kwa amani watapigana. Wala si sahihi kulinganisha hilo na Sudan ambao walipigana miongo kadhaa wagawane nchi.
Wakati vita vya Uganda na Tanzania vikielekea ukingoni kabisa Mwalimu Nyerere alilaumiwa kuwa anataka kuimeza Uganda, wengine wakadiriki kusema kama alivyoimeza Zanzibar. Yeye alijibu kuwa lililo la msingi ni kudumisha amani na nchi jirani na kuwa na uhusiano mwema - si kuunganisha nchi. Tubakie majirani wema kama ilivyo kwa Zambia, Msumbiji, Rwanda, Kenya na kwingineko. Kuwa na mahusiano mema na jirani ni jambo la msingi na si lazima muunganishe nchi.
Kuna nchi nyingi tunahusiana nazo vizuri sana na kwa ukaribu japo haziko jirani, sembuse Zanzibar na Tanganyika! Undugu ni mahusiano mema si kuunganisha nchi. Na ujirani na udugu wa kihistoria upo kwa nchi zote tunazopakana nazo na si Tanganyika na Zanzibar pekee.
Muungano usilindwe kwa vitisho na kulazimishana, bali kujenga na kuimarisha mahusiano na ushirikiano mwema wa viongozi na wananchi wa hizi nchi mbili.
Kuna faida nyingi za kitaifa na kimataifa kwetu sisi Watanganyika kuwa nchi kamili, na vivyo hivyo kwa Zanzibar. Tusizibiane fursa na kuendelea kukerana au kulalamikiana!
Tupige kura ya maoni- waZanzibari na waTanganyika kwa pamoja wanataka muungaano, sawa, tuwe nchi moja yenye serikali moja. Upande mmoja hautaki, au pande zote mbili hazitaki, tuachane na huu muungano ambao mpaka sasa wananchi wa hizi nchi mbili hawajapata nafasi ya kuutolea maoni kwa njia ya kura.
Kufikia hapa tunachojua kwa uhakika ni wanasiasa wachache tuu wa ccm ndio wanautaka muungaano kwa maslahi yao binafsi. na ndio wanaapa kila siku kulinda muungano huu. Waulize faida za muungano huu, kwa ulinganisho wa mathalani, kutokuwepo muungano baina ya Tanganyika na Rwanda auZambis na Malawi kama wanazo.
Sababu zilizo pelekea muungano mwaka 1964 leo hazina mashiko kabisa, hatupaswi kuung'ang'ania. Tunatumia gharama kubwa bila faida yoyote, kama tulivyotumia gharama kubwa kuhamia Dodoma, kwa kufuata sababu za miaka ya 1970, na mawazo ya Nyerere, bila kuzingayia kuwa sasa tuko karne ya 21 yenye maendeleo makubwa ya teknolojia ambapo njia za mawasiliano na usafiri hazitulazimu mji mkuu kuwa katikati. Yale mawazo kwamba ni rahisi adui kupiga Dar es salaam kwa vile ni pembezoni na imepakana na bahari yamepitwa na wakati. Hatuna haja ya kuwa na maadui, na tukiwa nao wanaweza kutupiga hata kutokea bahari ya Atlantic.