Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,172
CHADEMA yaiponza CCM
na Christopher Nyenyembe, Mbeya
USHINDI mkubwa na wa kimbunga uliolikumba jimbo la Mbeya Mjini na kupoteza kiti cha ubunge na viti vingi vya udiwani vilivyokuwa vikikaliwa na Chama cha Mapinduzi (CCM) umezua makubwa katika uteuzi wa viti maalumu kwa walioteuliwa kutoka kwenye kata zilizopoteza ushindi.
Uchunguzi uliofanywa na Tanzania Daima umebaini kuna kasoro kubwa katika uteuzi wa majina ya madiwani wanne wa viti maalumu watakaoingia katika Halmashauri ya Jiji la Mbeya huku wakiwa wametoka kwenye kata zilizoangushwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) hali ambayo imezusha malalamiko makubwa kwa wale walioachwa wakati kata zao ziliibuka na ushindi.
Uchunguzi huo ulibainika kuwa Jumuiya ya Wanawake wa CCM (UWT) kutoka wilaya ya Mbeya mjini iliteua majina ya madiwani wa viti maalum 14 kutoka tarafa za Sisimba na Iyunga kwa kuwa viti vipatavyo 14 vimechukuliwa na upinzani, CHADEMA wakiwa wamejizolea viti 12 na NCCR-Mageuzi viti viwili huku CCM ikijikuta inaambulia viti saba maalumu vya udiwani.
Hali hiyo katika kutafuta ukweli wa migongano hiyo ya kugombania viti hivyo, baadhi ya madiwani wa viti maalum walioteuliwa na majina yao kutupwa kapuni walidai wameumizwa na zoezi hilo kwa kuwa wenzao walioteuliwa wametoka kwenye kata ambazo CCM imekosa ushindi, lakini wanashangaa kata hizo kutoa viti maalumu na kuacha zile zenye ushindi.
Madiwani waliotemwa walipohojiwa na Tanzania Daima walisema uteuzi huo sio wa haki hasa wakizingatia kuwa safu ya madiwani wa viti maalum waliopitishwa ni wenye uwezo wa kifedha, wakitilia mashaka kuwa upendeleo huo unaweza kusukumwa kwa nguvu ya pesa.
Alisema kuwa kati ya madiwani saba wa viti maalum walioteuliwa waliotoka kata za Sisimba, Ilemi, Iganzo, Nsalaga, Tembela, Mwasanga na Mwakibete hawakustahili kupewa viti hivyo kwa kuwa kata hizo zilizokuwa zikikaliwa na CCM zimepoteza viti na hazina ugomvi na madiwani waliotoka kata za Itiji, Uyole na Manga kuwa hao wametoka kwenye kata ambazo CCM imeshinda viti vya udiwani wa jimbo.
Katibu wa UWT wilaya ya Mbeya Mjini, Shadya Mtoro alipohojiwa alisema kuwa jumuiya hiyo imefanya uteuzi huo kwa kuzingatia sifa za wanachama wake ambao ni wasomi, waadilifu na walioweza kuitumikia jumuiya hiyo kwa zaidi ya miaka mitano na kwamba katiba yao haisemi mwenye sifa ya kuwa diwani wa viti maalumu lazima atoke kwenye kata iliyoshinda udiwani.
na Christopher Nyenyembe, Mbeya
USHINDI mkubwa na wa kimbunga uliolikumba jimbo la Mbeya Mjini na kupoteza kiti cha ubunge na viti vingi vya udiwani vilivyokuwa vikikaliwa na Chama cha Mapinduzi (CCM) umezua makubwa katika uteuzi wa viti maalumu kwa walioteuliwa kutoka kwenye kata zilizopoteza ushindi.
Uchunguzi uliofanywa na Tanzania Daima umebaini kuna kasoro kubwa katika uteuzi wa majina ya madiwani wanne wa viti maalumu watakaoingia katika Halmashauri ya Jiji la Mbeya huku wakiwa wametoka kwenye kata zilizoangushwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) hali ambayo imezusha malalamiko makubwa kwa wale walioachwa wakati kata zao ziliibuka na ushindi.
Uchunguzi huo ulibainika kuwa Jumuiya ya Wanawake wa CCM (UWT) kutoka wilaya ya Mbeya mjini iliteua majina ya madiwani wa viti maalum 14 kutoka tarafa za Sisimba na Iyunga kwa kuwa viti vipatavyo 14 vimechukuliwa na upinzani, CHADEMA wakiwa wamejizolea viti 12 na NCCR-Mageuzi viti viwili huku CCM ikijikuta inaambulia viti saba maalumu vya udiwani.
Hali hiyo katika kutafuta ukweli wa migongano hiyo ya kugombania viti hivyo, baadhi ya madiwani wa viti maalum walioteuliwa na majina yao kutupwa kapuni walidai wameumizwa na zoezi hilo kwa kuwa wenzao walioteuliwa wametoka kwenye kata ambazo CCM imekosa ushindi, lakini wanashangaa kata hizo kutoa viti maalumu na kuacha zile zenye ushindi.
Madiwani waliotemwa walipohojiwa na Tanzania Daima walisema uteuzi huo sio wa haki hasa wakizingatia kuwa safu ya madiwani wa viti maalum waliopitishwa ni wenye uwezo wa kifedha, wakitilia mashaka kuwa upendeleo huo unaweza kusukumwa kwa nguvu ya pesa.
Alisema kuwa kati ya madiwani saba wa viti maalum walioteuliwa waliotoka kata za Sisimba, Ilemi, Iganzo, Nsalaga, Tembela, Mwasanga na Mwakibete hawakustahili kupewa viti hivyo kwa kuwa kata hizo zilizokuwa zikikaliwa na CCM zimepoteza viti na hazina ugomvi na madiwani waliotoka kata za Itiji, Uyole na Manga kuwa hao wametoka kwenye kata ambazo CCM imeshinda viti vya udiwani wa jimbo.
Katibu wa UWT wilaya ya Mbeya Mjini, Shadya Mtoro alipohojiwa alisema kuwa jumuiya hiyo imefanya uteuzi huo kwa kuzingatia sifa za wanachama wake ambao ni wasomi, waadilifu na walioweza kuitumikia jumuiya hiyo kwa zaidi ya miaka mitano na kwamba katiba yao haisemi mwenye sifa ya kuwa diwani wa viti maalumu lazima atoke kwenye kata iliyoshinda udiwani.