Sultan Qaboos wa Oman afariki dunia. Sultan Haitham Bin Tariq Al Said achaguliwa kuwa mrithi wake

Si kweli, walio kuuza wazungu na babu zako, hao waliuondoa utumwa.

Wazungu mpaka leo hii wanawanunua na kuwauza, huelewi hilo?

Unaelewa meli ya kwanza kupeleka Waafrika America iliitwa Jesus, yes Yesu?
Unaelewa biashara ya utumwa ilianza mwaka gani? Sultan Said alikuwa kinara kwenda kuwachukua watumwa kigoma.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
January 13, 2020
Zanzibar, Tanzania

Khitma kwa ajili ya Sultan Qaboos yasomwa Zanzibar
Kufuatia kifo cha Sultan Qaboos bin Said wa Oman tarehe 10 Januari 2020, wakaazi wa Mji Mkongwe wa Zanzibar wamekusanyika kumuombea dua kiongozi huyo mashuhuri duniani.


Source: Weyani TV
 
January 13, 2020
Zanzibar, Tanzania
Makamu wa Kwanza mstaafu Maalim Seif awapa mkono wa pole WaOmani
Kufuatia kifo cha kiongozi wa Oman, Sultan Qaboos bin Said, kilichotokea juzi, Makamu wa Kwanza Mstaafu wa Rais wa Zanzibar ambaye pia ni Mshauri Mkuu wa chama cha ACT Wazalendo, Maalim Seif Sharif Hamad, amekwenda kwenye Ubalozi Mdogo wa Oman uliopo Mjini Unguja kwa kuwapa pole raia wa Oman kutokana na msiba huo.


Source: Weyani TV
 
Afu watu wanashindwa elewa wa Oman kwa East Africa wapo wengi tu zaidi ya Zanzibar/Mombasa na wengi wapo ‘hinterland’ kuliko sehemu hizo za pwani kwa idadi (japokuwa machotara wa ki Oman ndo wengi zaidi)

Nashangaa hata wa Oman wengi wanajua ukisema umetoka Africa wanachukulia ni Zanzibar tu

Njoo Tanga, Mtwara,Lindi, baadhi ya sehemu Morogoro na nyumbani kwao sasa Tabora/Shinyanga (Shelui, Igunga, Nzega, Choma, Tinde, Itobo, Bukene, Nata, Mwangohe, Isaka, Kagongwa,Didia, Urambo, Sikonge, Mabama, Kaliua Sangilwa , Maganzo,Malampaka,Shagihilu nk) kuna jamii kubwa ya wa Oman sehemu hizo achia mbali Karagwe mpaka Rwanda na Burundi

Kwahiyo kwa baadhi ya jamaa zetu leo ni msiba mzito kwao ni WaTanzania kweli lkn pia historia yao inafungamana na Oman na ndo maana hakuna nchi nje ya Afrika na duniani kwa mtanzania yoyote huwezi kupata shida ya lugha ya Kiswahili zaidi ya Oman (Nina ushahidi kwa hili na mpaka vijijini kabisa nimefika Oman) kati ya watu wanne hauwezi kosa mmoja anaejua kiswahili na kuna wengine wanajua Kiswahili hata hawajafika huku wamejulia nyumban sababu wazazi wao wanaongea kiswahili labda kizazi hiki kiishe ndo kiswahili kwao kitaanza kupotea

Mkuu:
Kigoma Ujiji kuna msikiti uliojengwa na hawa wa Oman mwaka 1840.
 
Ukweli ni kwamba Historia ya Oman ni sawa na ya Korea ya Kaskazini na Kusini.

Historia za Nchi hizo 3 zinafichwa na wala haziruhusiwi kuandikwa popote pale ndiyomana hazitoki nje ya Nchi isipokuwa zinabaki Ndani ya Vichwa vya Raia wao wanaozishuhidia tu.

Unajuwa sababu ni nini?

Raia yoyote wa Nchi hizo akitoa Historia au Jambo baya lolote la Nchi hizo basi anahukumia kifo kwa uhaini (Treason).

Hivi Unadhani Mapinduzi aliyoyafanya Qaboos dhidi ya babayake hayakumwaga damu?

Ukweli ambao hauruhusiwi kuzungumzwa na Raia yeyote wa Oman ni kuhusu Mapinduzi haya.

Mimi ni Mzanzibar na Nina Familia ambayo ni Raia wa Oman na Wanaishi Mascut Oman. Miongoni mwa wanayoyajua lakini hayawezi kuandikwa popote ni kuwa!

Qaboos baada ya kusoma Oman ni Waingereza ndiyo waliomuwezesha kumpindua babayake ili kuitoa Nchi katika Siasa za Mashariki (Communism) za Russia na China na kuingiza Oman katika siasa za Magharibi (Capitalism).

Bila ya Waingereza Qaboos hakuwa na uwezo wa Kumpindua babayake.

Na katika Harakati za Mapinduzi hayo Babayake Qaboos alijeruhiwa kwa kupigwa Risasi ya Mguu na Kukimbilia Uengereza ambako alitibiwa na Kufa kwa Jeraha.

Baada ya Kifo chake Historia ya Mapinduzi hayo ikawa Banned, Na kumbukumbu zote kuhusu Babayeke, Qaboos akazifuta na Raia wakawa forced kusahau Legacy ya Babayake Qaboos.

Hadi sasa hakuna historia ya Babayeke Qaboos iliyochapishwa.

Ni huyu Qaboos Mtoto ndiye aliyezuiwa kutajwa babayake na kuhakikisha anasahaulika kama aliishi Duniani.

Kwanini Hajaowa?
Baada ya Mapinduzi kabla ya Babayake Kufa alimtumia ujumbe Mwanawe na kumwambia "Kama Ulivyonipindua Mimi, na Wewe Atatokea Mtoto wako Akupindue".

Hapo ndipo akayachukua hayo Maneno kwa uzito na Kuachana na Habari za Kuowa au Kuzaa Mtoto wa Kwenye Ndoa kwa kuhofia kuja kupinduliwa na Mtoto wake.

Ndiyo hapo akawa anaishi kwa Kuletewa Wanawake anaowahitaji ndani ya Palace yake anagonga wanaishi kwa kipindi anachotaka yeye mwenyewe Qaboos then wanalipwa na kuondoka.

But nisawa na kutekwa na Wasiojuilikana yaani ukiingia kwenye Qasri ya Qaboos ukitoka katu hitosema ulichofanywa.

In Short Jamaa inawezekana anaowatoto ambao kawazaa illegally kwa Mila za Kiislam na hawahesabiki kuwa ni Wanae.

Hata Hivyo ukweli usiofichika ni kwamba Kafanya Mageuzi Makubwa ya Kiuchumi ndani ya Oman.

Mkuu:
Ahsante kwa ufafanuzi huu mzuri.
Hivi ni kweli kuna uhusiano wa kindugu kati ya Masultani walio tawala Zanzibar na hawa wa Sultanate of Oman?
 
Hata Trump alienda North Korea

Ki video kinachoonyesha Kikwete kaenda Oman hakifanyi Oman na Tanganyika kuwa na historical ties...

Zanzibar, Mombasa, regions along slave caravan routes across East Africa may care about Sultan Kwabuz.

Masses of Tanganyikans in the hinterland couldn't care less about an Oman sultan.
Upumbavu umekutawala kiasi icho kumbe :D
 
Mkuu:
Ahsante kwa ufafanuzi huu mzuri.
Hivi ni kweli kuna uhusiano wa kindugu kati ya Masultani walio tawala Zanzibar na hawa wa Sultanate of Oman?

Ni kweli Masultan wa Oman na Wazanzibar walikuwa ni Watu wa Ukoo mmoja ambapo wote ni Kizazi cha Mfalme wa Oman aliyekuwa akiishi Zanzibar Sayyid Saeed Bin Sultan.

Kumbuka kuwa Makao Makuu ya Serikali ya Oman yalikuwa Zanzibar na Mfalme wa Oman alikuwa akiishi Zanzibar.

Ila katika Watoto wake wakatofautiana wakaamua kugawana Mmoja akarudi Oman kuwa Mfalme wa Oman pekee, na Mwengine akabaki Zanzibar kuwa Mfalme wa Zanzibar pekee.

Lakini Baada ya Uengereza kuitawala Oman na Zanzibar ikawa chini ya Muengereza.

Kwahiyo Zanzibar mpaka inapata Uhuru ilikuwa chini ya Uengereza huku Mfalme wa Zanzibar akiwa ni Puppet wa Uengereza na wala si Oman kama Watu wanavyodanganywa na kuaminishwa.

Oman yenye ilikuwa ni Koloni la Muengereza, Sasa Koloni litawezaje kutawala Zanzibar.

Na ukisoma harakati za kudai Uhuru za Kina Karume zote utaziona kuwa Walikiwa wakienda Uengereza kuzidai na wala Hawakuwahi kwenda Oman kidai Uhuru.

Na December mwaka 1963 (tarehe nimeisahau lakini unaweza kigoogle) utakutia kuwa Zanzibar ilikabidhiwa Uhuru wake kamili kitoka kwa Uengereza na wala si Oman.

Na Waziri Mkuu aliyekabidhiwa alikuwa ni Mswahili Muhamedi Shamte (Hakuna Muarabu anaitwa Shamte).

Bali kitokana na Chuki tu za baadhi ya Watu wa Ndani na Nje ya Zanzibar ndiyo zikapangwa njama za Kuipindua Serikali iliyokabidhiwa Uhuru ambayo Wazanzibari waliwapindua Wazanzibari wenzao.

Hakuna Muarabu aliyepinduliwa kwani Serikali na Viongozi wake walikuwa ni Waswahili.
 
Ni kweli Masultan wa Oman na Wazanzibar walikuwa ni Watu wa Ukoo mmoja ambapo wote ni Kizazi cha Mfalme wa Oman aliyekuwa akiishi Zanzibar Sayyid Saeed Bin Sultan.

Kumbuka kuwa Makao Makuu ya Serikali ya Oman yalikuwa Zanzibar na Mfalme wa Oman alikuwa akiishi Zanzibar.

Ila katika Watoto wake wakatofautiana wakaamua kugawana Mmoja akarudi Oman kuwa Mfalme wa Oman pekee, na Mwengine akabaki Zanzibar kuwa Mfalme wa Zanzibar pekee.

Lakini Baada ya Uengereza kuitawala Oman na Zanzibar ikawa chini ya Muengereza.

Kwahiyo Zanzibar mpaka inapata Uhuru ilikuwa chini ya Uengereza huku Mfalme wa Zanzibar akiwa ni Puppet wa Uengereza na wala si Oman kama Watu wanavyodanganywa na kuaminishwa.

Oman yenye ilikuwa ni Koloni la Muengereza, Sasa Koloni litawezaje kutawala Zanzibar.

Na ukisoma harakati za kudai Uhuru za Kina Karume zote utaziona kuwa Walikiwa wakienda Uengereza kuzidai na wala Hawakuwahi kwenda Oman kidai Uhuru.

Na December mwaka 1963 (tarehe nimeisahau lakini unaweza kigoogle) utakutia kuwa Zanzibar ilikabidhiwa Uhuru wake kamili kitoka kwa Uengereza na wala si Oman.

Na Waziri Mkuu aliyekabidhiwa alikuwa ni Mswahili Muhamedi Shamte (Hakuna Muarabu anaitwa Shamte).

Bali kitokana na Chuki tu za baadhi ya Watu wa Ndani na Nje ya Zanzibar ndiyo zikapangwa njama za Kuipindua Serikali iliyokabidhiwa Uhuru ambayo Wazanzibari waliwapindua Wazanzibari wenzao.

Hakuna Muarabu aliyepinduliwa kwani Serikali na Viongozi wake walikuwa ni Waswahili.
Na Sultan aliekimbilia uingereza aliitwa nani? Au ndio Shamte

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom