Suleiman Kumchaya haijui historia ya TANU karudia maneno ya mzee Pius Msekwa kuhusu TAA

Mohamed Said

JF-Expert Member
Nov 2, 2008
20,912
30,253

1574459989894.png

Gazeti la Hoja (Ijumaa, 22- 26, Novembe 2019) kuna makala ya Suleiman Kumchaya kuhusu historia ya TAA na TANU ambayo ina makosa sawasawa na makosa katika makala ya Mzee Pius Msekwa iliyochapwa katika gazeti la TAZAMA kiasi cha majuma mawili yaliyopita.

Suleiman Kumchaya anasema kuwa Julius Nyerere alipokuwa Makerere alikuwa anawasiliana na wazee wa Dar es Salaam akiwataka waanzishe chama cha siasa.

Ukisoma makala hizi mbili utazania ni jibu la mtihani la wanafunzi wawili watukutu walioangaliana mtihani jambo amabalo mwalimu hodari ataligundua mara moja katika kusahihisha.

Suleiman Kumchaya karudia maneno ya Mzee Msekwa kuwa TAA kazi yake ilikuwa, ''kutetea maslahi ya wafanyakazi Waafrika,'' na Julius Nyerere ndiye aliyeibadilisha TAA kuwa, ''chama cha siasa cha kudai uhuru,'' kazi ambayo aliifanya kwa kushirikiana na ''wazee wa pwani.''

Maneno haya yote ya Kumchaya hayana ushahidi katika historia ya uhuru wa Tanganyika na nathubutu kusema kuwa Kumchaya haijui historia ya TANU na inashangaza sana katika historia ya TANU kwa kila aizungumzae atataja, ''wazee,' ambao hawana majina kama vile hakuna awajuae.

Nyerere kabla hajafika Dar es Salaam hakuwa anajuana na mzee yeyote katika wazee wa Dar es Salaam ambao walikuwa katika siasa kwa hiyo hakuwa anaandikiana barua na mzee yoyote kuwataka waunde chama cha siasa.

Nyerere alikuja kujuana na wazee wa Dar es Salaam baada ya yeye kujuana na Abdul Sykes mwaka wa 1952 na kugombea nafasi ya urais dhidi ya Abdul Sykes katika uchaguzi wa mwaka wa 1953 na kushinda.

Kuanzia mwaka huu wa 1953 ndiyo Abdul Sykes akamjulisha Nyerere kwa wazee wa Dar es Salaam kuanzia na Mufti Sheikh Hassan bin Ameir, Jumbe Tambaza, Mshume Kiyate, Sheikh Suleiman Takadir na Said Chamwenyewe kwa kuwataja wachache na hii kazi ya kumtambulisha Nyerere kwa wazee na masheikh maarufu wa Dar es Salaam ilifanywa vilevile na ndugu wawili, Iddi Faiz Mafungo na nduguye Iddi Tosiri kwa kumpeleka Nyerere Bagamoyo kumtambulisha kwa Sheikh Mohamed Ramiya ambae wao alikuwa binamu yao.

Kila anaejisikia kuwataja ''wazee,'' utasikia, ''wazee'' lakini majina yao hayatajwi.
Kwa nini iwe hivi?

Historia ya TANU nimeieleza mara nyingi hapa kiasi naona tabu kuirudia tena.

Katika uchaguzi wa mwaka wa 1953 Nyerere aliingia katika uongozi na timu ya vijana watupu kama Abdul Sykes, Ally Sykes Tewa Said Tewa, Dossa Aziz, Joseph Kasella Bantu, Dome Budohi kwa kuwataja vijana wachache na mzee katika timu hiyo alikuwa John Rupia.

Wazee wa mwisho katika uongozi awamu yao ilikwisha mwaka wa 1950 baada ya mapinduzi yaliyofanywa na Abdul Sykes na Hamza Mwapachu yaliyowatoa madarakani Thomas Plantan na Clement Mtamila na nafasi zao za urais na katibu kuchukuliwa na Dr. Vedasto Kyaruzi kama Rais na Abdul Sykes Katibu.

Inaelekea Kumchaya kama Mzee Msekwa haijui historia hii na ndiyo sababu ya haya makosa ambayo kwa hakika hayana sababu ya kufanywa.

Hawa wangejitahidi lau kufanya utafiti kidogo katika Maktaba ya CCM wangelikuta pale Dodoma kuna majalada ya Hamza Mwapachu, Abdul Sykes na ya wazalendo wengine ingawa ndani hakuna nyaraka majalada ni matupu.

Mimi katika utafiti wa kitabu cha Abdul Sykes nimefika hapo.

Wangeanzia hapo wangeweza lau kwa uchache kupata historia ya TANU na wagelijua kuwa historia ya TANU inaanza na historia ya African Association chama kilichoundwa na Kleist Sykes mwaka wa 1929 na katika uasisi wa TANU wanae wawili Abdul na Ally Sykes walishiriki na wana historia ndefu ya chama hicho kushinda Julius Nyerere.

Wangelijua pia kuwa Abdul alifanya mazungumzo na Chief David Kidaha Makwaia kuanzia 1951 wakijadiliana kuhusu kuasisi TANU mazungumzo ambayo Abdul alikuwanayo na Hamza Mwapachu kwa miaka mingi na ilikuwa Hamza ndiye aliyemleta Nyerere katika harakati za TAA Dar es Salaam kuishia na Nyerere kuchaguliwa kuwa kiongozi wa TANU mwaka wa 1954 na kukabidhiwa jukumu la kuongoza mapambano ya kudai uhuru.

Jambo la kuhuzunisha katika magazeti haya ni kuwa baada ya kuandika makosa na mtu akasahihisha na kuwapelekea makala wanakataa kuchapa makala hizo wakitaka wabakie na historia ile rasmi yenye makosa.

Hakika huu ni msiba mkubwa pasi na mfano katika historia ya nchi yetu.
 
SULEIMAN KUMCHAYA HAIJUI HISTORIA YA TANU KARUDIA MANENO YA MZEE PIUS MSEKWA KUHUSU TAA

yawn.jpg

Hizi ngano zako sasa zinachosha…! Najua wazee wa Dar es Salaam walikuwa wazee wako na ungependa sana uwainue. Najua unavyohangaika na ngano zile zile kila mara lakini utake usitake kwa ufupi sana ni hivi...

Ni uongo uliopitiliza kudai kwamba AA iliyoanzishwa mwaka 1929 na Gavana wa wakati huo Cameroun kama klabu ya starehe kwa wasomi weusi ilikuwa na malengo ya kudai uhuru.

Hilo la kwanza na pili ni ukweli kuwa wakati Nyerere anahudhuria mkutano mkuu wa AA akiwakilisha jimbo la Tabora wewe ulikuwa hujazaliwa. Na kwamba viongozi wa AA walikuwa hawamjui Mwalimu Nyerere kabla ya mwaka 1953 alipohamia Dar es Salaam pia ni uongo.

Mtu ambaye yawezekana hakumjua Mwalimu Nyerere labda ni Abdul Sykes peke yake kwa sababu nyakati hizo hakuwepo...tunaanza kumsikia tu pale alipoongoza uvamizi wa ofisi za AA kuwatoa wazee wake!

Mwalimu Nyerere tayari alikuwa kiongozi wa AA mwaka 1945 akiwa Tabora na mwaka huo huo alifika Dar es Salaam na kukutana na viongozi na wanachama wa AA mojawapo akiwa Dossa Aziz.

Sasa, kama Mwalimu Nyerere na Abdul hawakukutana ni wazi kumbe Abdul Sykes hakuwa kati ya vinara wa AA mjini Dar es Salaam...swali la kujiuliza ni je, Abdul alikuwa nani ndani ya AA kabla ya kuvamia ofisi za TAA mwaka 1948 kwa ngumi na mateke?

cc: Nguruvi3, Yericko Nyerere, JokaKuu
 
Watu wanaingelea TAA wewe unaongelea AA. Majanga!
Hivu huwa mnaeleqa mnachokisoma au mnafanya lusidi kupindiaha ukweli au ndiyo upunguani wa hali ya juu?
Hahaha na Nyerere alikisikia chama cha starehe ndio akaja kujiunga nacho! Kwa mantiki yako.
Rudia tena kusoma aliyoandika Mohamed Said, TAA haikuwepo mwaka 1929. IIliyoanzishwa mwaka huo ni AA ama pororjo zaendelea kutawala...pole sana.
 
Rudia tena kusoma aliyoandika Mohamed Said, TAA haikuwepo mwaka 1929. IIliyoanzishwa mwaka huo ni AA ama pororjo zaendelea kutawala...pole sana.
Acha kucheza na maneno. Huwa sikisii.

Wewe kuanzia mwanzo mpaka mwisho katika porojo yako juu hapo umeitaja AA, hata mwaka 1953 bado unaitaja AA.

Kamsome tena Allama Mohamed Said juu kidogo hapo, 1924 kaitaja AA kufikia alipoitaja1951 kaitaja TAA baada ya hapo kaitaja TANU.

Swali la msingi hujajibu.

Hahaha na Nyerere alikisikia chama cha starehe ndio akaja kujiunga nacho! Kwa mantiki yako.

Au kwa elimu yako swali mpaka uone alama ya kuuliza?

Kwa kukujuza tu, Nyerere na Jumbe walianzisha CCM. Sijui kama bado unakishabikia leo hii.
 
Mbona hujamjibu hoja zake


Mag 3,
Ninachokushindia ni kuwa mwenzangu ghadhabu zimekujaa sana katika historia hii ungependa sana tubaki na ile ''official history,'' iliyowafuta wazee wangu.

Hii ndiyo sababu ghadhabu zako unazielekeza kwangu kwa maneno makali ya ''ngano,'' ''uongo,'' na lugha za kejeli kama ''ngumi na ''mateke,'' nk.

Mimi sitakuita muongo kwa haya uliyosema kuhusu Nyerere.
Nachukulia kuwa historia ya Nyerere huijui kwa kuwa hujaitafiti kama nilivyofanya mimi.

Nyerere hakuwa kiongozi wa TAA Tabora 1945.

Tarehe 3 Machi, 1945 African Association mjini Tabora ilifungua ofisi yake ikiwa na na viongozi wafuatao: Hamisi Simbe (Rais), Ramadhani Nasibu (Makamu wa Rais), M. K. Hemed (Katibu), Chamng'anda Usingizi (Mwenyekiti), Fimbo Mtwana (Mweka Hazina) na Rashidi Mussa (Mkaguzi wa Hesabu).

Unaliona jina la Nyerere hapo?

Julius Nyerere, wakati huo akifundisha St. Mary's School, alishuhudia sherehe za uzinduzi wa African Association.

Mwaka 1946 wasomi wa Makerere ndipo walianza kujishughulisha na African Association pale Hamza Mwapachu na Julius Nyerere walipochaguliwa Katibu na Katibu Msaidizi.

Baada ya uhamisho wa Mwapachu kutoka Tabora, Nyerere akashika nafasi yake na kuwa Katibu.

Angalia rejea hizi: Barua ya M.K. Hemed kwa Secretary, African Association, Dar es Salaam, 11 th January 1945, TAA Tabora Party Archives File 741. Angalia Iliffe, A Modern History of Tanganyika, uk 430-431.

Angalia pia E. A. M. Mang'enya, Discipline and Tears, Dar es Salaam University Press, 1984, uk. 173.

Haya niliyokueleza na rejea hizi naamini zinatosha kukufahamisha kuwa historia hii mimi naijua vizuri sana wala sibahatishi kwa hiyo hayo mengine wala sina haja ya kuyasemea kwa kuwa hayana maana.

Nakuuliza kati yetu mimi na wewe nani mwandishi wa ngano na nani anaeandika kwa ushahidi?
 
Suala la kusema tu wazee wa Dar es Salam bila kuwataja majina si haki na haileti afya katika historia. Wenzetu Ulaya mbona huwa wanataja majina tena hadi ya karne ya 15.

Mzee Said Hapo tu unajitofautisha na wanaopinga uelezacho ambao wengi hawajabahatika kuona nyaraka halisi za wazee wa DSM
 
Suala la kusema tu wazee wa Dar es Salam bila kuwataja majina si haki na haileti afya katika historia. Wenzetu Ulaya mbona huwa wanataja majina tena hadi ya karne ya 15.

Mzee Said Hapo tu unajitofautisha na wanaopinga uelezacho ambao wengi hawajabahatika kuona nyaraka halisi za wazee wa DSM
Nemo...
Kuna hofu kubwa ya kutaja majina...
 
Historian ndio imesha haribiwa... Ni ngumu sana kuja kuiweka sawa jamii nzima waweze ifahamu, watu wa bara ndio hawataki kabisa kuisikia wanataka kubaki na hii wanayo someshwa madarasani...
Chilla,
Historia iliharibiwa na sasa imetengenezwa.

Wengi hii leo wanaijua historia ya kweli ya TANU na kudai uhuru baada ya kuandika kitabu cha maisha ya Abdul Sykes.

Mtu halazimishwi kuamini asichokitaka wanaweza kundi la watu fulani kuwa wakaidi kutambua ukweli lakini ndani ya nafsi zao ukweli wa historia ya TANU wanaujua.
 
Chilla,
Historia iliharibiwa na sasa imetengenezwa.

Wengi hii leo wanaijua historia ya kweli ya TANU na kudai uhuru baada ya kuandika kitabu cha maisha ya Abdul Sykes.

Mtu halazimishwi kuamini asichokitaka wanaweza kundi la watu fulani kuwa wakaidi kutambua ukweli lakini ndani ya nafsi zao ukweli wa historia ya TANU wanaujua.
Naweza pata vitabu hivyo? Vimeandikwa pia kwa lugha gani ya Kiswahili au kigeni? Na gharama ya vitabu hivyo ni shilling ngapi?
 
Naweza pata vitabu hivyo? Vime andikwa pia kwa lugha gani ya kiswahili au kigeni? Na gharama ya vitabu hivyo ni shilling ngapi?
Chilla,
Vitabu hivi utavipata Ibn Hazm Media Centre Msikiti wa Mtoro na Manyema na pia Msikiti wa Mtambani kuna vya Kiingereza na Kiswahili bei elfu kumi tu.
 
Kulikuwa na associatians nyingi kipindi cha ukoloni, kama Arabs Associations, European Associations, Indian Associations, hizi zote zilikuwa na lengo la kulinda maslahi ya wafanyakazi na raia wao, hata African Association lengo lake kuu lilikuwa kulinda maslahi ya wafanyakazi na raia waafrica, sidhani kama lengo lake lilikuwa kupigania uhuru, inawezekana Nyerere ndio alibadilisha lengo na kuwa chama cha kupigania uhuru.
 
Chilla,
Vitabu hivi utavipata Ibn Hazm Media Centre Msikiti wa Mtoro na Manyema na pia Msikiti wa Mtambani kuna vya Kiingereza na Kiswahili bei elfu kumi tu.
Shukrani nitafika hapo kupata hizi nakara kwa lugha zote...
 
kulikuwa na associatians nyingi kipindi cha ukoloni, kama Arabs Associations, European Associations, Indian Associations, hizi zote zilikuwa na lengo la kulinda maslahi ya wafanyakazi na raia wao, hata African Association lengo lake kuu lilikuwa kulinda maslahi ya wafanyakazi na raia waafrica, sidhani kama lengo lake lilikuwa kupigania uhuru, inawezekana Nyerere ndio alibadilisha lengo na kuwa chama cha kupigania uhuru.
Laki...
Maslahi ya wafanyakazi Waafrika yakishghulikiwa na Tanganyika African Government Servants Association (TAGSA)ambako katika 1950s President alikuwa Thomas Marealle na Secretary Ally Sykes.

Wanakamati walikuwa Steven Mhando, Dr. Wilbard Mwanjisi, Rashid Kawawa na Dr. Michael Lugazia na wote hawa walikuwa wanachama shupavu wa TAA.

TAA 1950 ilikuwa chini ya Dr. Vedasto Kyaruzi kama President na Abdul Sykes akiwa Katibu na ndani yake kulikuwa na PoliticalSubcommittee ambayo wajumbe wake walikuwa Mufti Sheikh Hassan bin Ameir, Hamza Mwapachu, Abdul Sykes, Sheikh Said Chaurembo, Steven Mhando na John Rupia.

Mnatabika sana na kusoma historia ya kweli ya uhuru wa Tanganyika kiasi mnamlazimisha Nyerere abebe hata mizigo isiyomuhusu.

Haya yote mimi nimeyasoma ndani ya Nyaraka za Sykes.
Wewe hizi taarifa zako umetoa wapi?

Jihadhari na kuifunga akili yako ikawa inachukua hata uongo kwa kuilazimisha.
 
Mmi binafsi najiuliza kwanini serikali inahofia kuwataja wazee hao kama tafiti zote zinawathibitisha kuwa walianza harakat za Uhuru hata kabla ya hayati baba wa taifa,,au kwani kutawagharim nni kuwatambua na kuwapa héshma yao?! Au kama serikali haijui au haizïamini kwéli hizi watumie vyombo vyake vinavyohusika kujirdhisha..ugumu uko wapi au sielewi mimi
 
Ni dhahiri yaonyesha unakerwa na baadhi ya mambo, ila hilo halimaanishi kwamba kile usemacho wewe ndicho kilicho sahihi kwa 100%.

Suleiman Kumchaya anasema kuwa Julius Nyerere alipokuwa Makerere alikuwa anawasiliana na wazee wa Dar es Salaam akiwataka waanzishe chama cha siasa.
Ni kweli hapo juu sio kwamba Mwalimu aliwasiliana na "Wazee wa Dar" waanzishe chama, ila ni kweli alipokuwa Makerere alikuwa na mawasiliano na Dar, na nijuavyo mimi Mwalimu alitaka kuanzisha Chama ila kwa kuwasiliana na walio Dar ndipo aliposhawishiwa kuachana na huo mpango na ajiunge na Chama/harakati zilizopo tayari Dar. kwa hiyo hapo upo sahihi usemapo hakukuwa na mawasiliano ya kwamba wao Wazee waanzishe chama.

Wangelijua pia kuwa Abdul alifanya mazungumzo na Chief David Kidaha Makwaia kuanzia 1951 wakijadiliana kuhusu kuasisi TANU
Nakubaliana na wewe kina Sykes ndio walibuni (jina)TANU, na jina hilo ndio lilipitishwa wakati wa kuiua TAA...ingawa naona unasisitiza sana KUASISI kuliko KU transform TAA.

Katika uchaguzi wa mwaka wa 1953 Nyerere aliingia katika uongozi na timu ya vijana watupu kama Abdul Sykes, Ally Sykes Tewa Said Tewa, Dossa Aziz, Joseph Kasella Bantu, Dome Budohi
Ni sahihi kabisa na hata Mwalimu anapowataja Wazee awahusishi akina Sykes kwani wao hawakuwa Wazee wakati huo, sioni ni kipi kinachanganya hapa, inaonyesha kana kwamba Mzee said hutaki kukubali kwamba walikuwepo Wazee wengine wengi tu kwenye harakati zile.

Kila anaejisikia kuwataja ''wazee,'' utasikia, ''wazee'' lakini majina yao hayatajwi.
Kwa nini iwe hivi?

Na hii ndio sababu ya kuwataja Wazee bila kujali majina maana yaweza kuwa ukawataja wachache na kuonekana hukuwajali wengine wengi tu

Nyerere kabla hajafika Dar es Salaam hakuwa anajuana na mzee yeyote katika wazee wa Dar es Salaam ambao walikuwa katika siasa kwa hiyo hakuwa anaandikiana barua na mzee yoyote kuwataka waunde chama cha siasa.
Huu ni urongo wa mchana, na ndio maana unapishana na wengine wengi mimi nikiwa mmoja wao. Mwalimu alikuwa na mawasiliano na baadhi ya Watu/Wanaharakati waliokuwepo Dar, na miongoni mwao aliitwa Mzee Mwangosi...ingawa ni kweli alitambulishwa kwa kina Sykes baada ya kufika Dar.

Historia zako Mzee Said zinapungukiwa baadhi ya mambo, umeegemea sana kwenye taarifa za kina Sykes na wengine wachache tu.
 
Back
Top Bottom