Sukari madukani hamna, tatizo ni nini wakati tayari kuna bei elekezi toka Serikalini?

The Humble Dreamer

JF-Expert Member
Oct 12, 2015
7,440
10,232
Wakuu Salaam;

Nimezunguka madukani kutafuta sukari ili nipate chai angalau nichangamke kipindi hiki cha mvua maana baridi ipo kweli huku duniani niliko, sasa kila duka naloingia naambiwa sukari hamna!

Nimejaribu kwenda hadi maeneo ya stendi lakini bado sukari najibiwa hamna.

Nimeamua ninywe chai na malimao tu maana yenyewe yataifanya hiyo chai hata iwe na ladha. Malimao yenyewe saivi kuyapata ni shughuli haswa mana watu wananunua wakachanganye kwenye mvukizo ili wajifukize.

Nimejaribu kuwauliza watu baadhi wanadai sukari hakuna kila sehemu na watu wameficha stock ila hawana uhakika kama kweli wameficha. Sasa tatizo ni nini wakati juzi limetoka tamko lenye bei elekezi ya sukari?

Kuna mmoja kanidokeza kua, wale waliokua na sukari kabla tamko la bei elekezi halijatoka, waliendelea kuuza kwa bei ile ile ya juu yani 3500. Sasa wakikutwa wanauza bei hiyo au mteja akisema kauziwa kwa bei hiyo, muuzaji anakamatwa.

Kwanini ifikie hali hii sukari iadimike ghafla? Au kweli sukari hamna?
Au wafanya biashara wanaficha sukari?

Kama vipi serikali ije na tathmini mpya juu ya hili swala.

Huko ulipo vipi sukari inapatikana kama kawaida au nako hamna kama maeneo ya huku?

Na vipi kuhusu bei ya sukari huko ulipo? Au unatumia malimao kama mimi?
 
Umenikumbusha mbali sana, wakati huo bei ya bidhaa ikiwa inadhibitiwa na Serikali. Wakati huo kulikuwa na msemo mmoja mzuri tu kuhusu hali hiyo. Nao ni "The controlled price, is a price at which a commodity is not available". Kama ilivyokuwa nyakati zile, ndivyo ilivyo hadi sasa.

Hakika Mkuu!

Inahitajika tathmini mpya juu ya hili swala la sivyo kutaendelea kua na bei elekezi lakini bidhaa haipatikan hali inayopelekea wananchi kupata tabu
 
Saivi ukinywa chai na sukari unaonekana ni illuminati,kasi ya maisha inaweza kuwa na speed kuliko speed of light.....leo hii sukari imekuwa kama dhaabu inavyotafutwa,huwezi amini nilitafuta sukari juzi mpk nasema mzee deportivo la curuna asije nipata bure.

Sent using Jamii Forums mobile app
Sukari imekua dili, nimezunguka sana leo kuitafuta. Nimeagizwa niende sehemu fuln kutafuta huko ila nauli ya kwenda na kurudi ni 2000, sukari 3500 jumla 5500, nimeamua nitumie limao tuuu
 
Kwa sisi WANYONGE hata ikifika 10,000/ kwa kg hakuna shida,tutanunua tu,anaeona sukari inauzwa bei kubwa,akalime miwa!
 
  • Thanks
Reactions: sab
Kwa sisi WANYONGE hata ikifika 10,000/ kwa kg hakuna shida,tutanunua tu,anaeona sukari inauzwa bei kubwa,akalime miwa!
Nyie 'wanyonge' ndiyo mnaopiganiwa na serikali, sisi 'wenye nguvu' ndy tunateseka kipindi hiki
 
Na wew bado una maswali ya kitoto kwani bei elekezi ndio miwa au kiwamda cha kutengeneza sukari? kama sukari haipo viwandani au store sasa bei elekezi itasaidia nin
Na wewe bado sijui upoje; juzi tumeambiwa sukari ipo ya kutosha nchini lakini saiv hamna madukani, hiyo bei elekezi inaleta uwiano wa bei maeneo yote bila ukandamizaji. Mnatakiwa mkubali bei elekez na muache kuficha sukar
 
Na wewe bado sijui upoje; juzi tumeambiwa sukari ipo ya kutosha nchini lakini saiv hamna madukani, hiyo bei elekezi inaleta uwiano wa bei maeneo yote bila ukandamizaji. Mnatakiwa mkubali bei elekez na muache kuficha sukar
Tatizo ni corona huko ngambo wala wasitafte mchawi
 
Wakuu Salaam;

Nimezunguka madukani kutafuta sukari ili nipate chai angalau nichangamke kipindi hiki cha mvua maana baridi ipo kweli huku duniani niliko, sasa kila duka naloingia naambiwa sukari hamna!

Nimejaribu kwenda hadi maeneo ya stendi lakini bado sukari najibiwa hamna.

Nimeamua ninywe chai na malimao tu maana yenyewe yataifanya hiyo chai hata iwe na ladha. Malimao yenyewe saivi kuyapata ni shughuli haswa mana watu wananunua wakachanganye kwenye mvukizo ili wajifukize.

Nimejaribu kuwauliza watu baadhi wanadai sukari hakuna kila sehemu na watu wameficha stock ila hawana uhakika kama kweli wameficha. Sasa tatizo ni nini wakati juzi limetoka tamko lenye bei elekezi ya sukari?

Kuna mmoja kanidokeza kua, wale waliokua na sukari kabla tamko la bei elekezi halijatoka, waliendelea kuuza kwa bei ile ile ya juu yani 3500. Sasa wakikutwa wanauza bei hiyo au mteja akisema kauziwa kwa bei hiyo, muuzaji anakamatwa.

Kwanini ifikie hali hii sukari iadimike ghafla? Au kweli sukari hamna?
Au wafanya biashara wanaficha sukari?

Kama vipi serikali ije na tathmini mpya juu ya hili swala.

Huko ulipo vipi sukari inapatikana kama kawaida au nako hamna kama maeneo ya huku?

Na vipi kuhusu bei ya sukari huko ulipo? Au unatumia malimao kama mimi?
Nilipo ipo ila bei ni ile ile 4000 - 4500 🤦‍♀️🤦‍♀️
 
Tatizo ni corona huko ngambo wala wasitafte mchawi
Mi nipo wilaya ya Hai. Baada ya mkuu wa wilaya kufuatilia suala la bei,wenye maduka wakaamua wote kuondoa sukari madukani mwao. Kisa wanadai walinunua bei ya juu hawawezi kuuza kwa bei ya chini.

Tatizo hapa ni sisi watanzania. Hatuna jema. Sukari ilipokuwa bei juu, ikawa inapatikana kwa wingi,tulilia kwamba hatutamudu. Tuakaitaka serekali iingilie kati. Serekali imeingilia kati tunaona wafanyabiashara wanaonewa.

Huku ukienda dukani unaambiwa sukari hakuna. Ila kama mnafahamiana na una 3500 unapata yakutosha

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom