SUGU umenunuliwa kwa shilingi ngapi? Vinega na Magenge wanauliza!

Kibanga Ampiga Mkoloni

JF-Expert Member
Aug 9, 2007
18,698
8,843
Kweli hakuna cha MWANADAMU kisicho na BEI!!!! (Naamini vya MUNGU havina BEI, Mfano KIFO, UHAI nk)

TAMKO LANGU KWA UMMA HILI HAPA :::pEEN LAWYER:::

February 22, 2012 in Uncategorized

::::SINA BUDI KUTOA TAMKO LANGU KWA UMMA::::
::::::::::::::::peen lawyer::::::::::::::::

SIJAKUBALIANA NA MAPATANO YA SUGU NA RUGE/NA KAMA KWELI HIZI NI HARAKATI BASI KINEGA BADO NTAZIENDELEZA.

Unajua nini..!iam swahili original,,,na ntaendelea kuwa mimi kama awali…!kazi za kufikisha ujumbe wa watu kupitia internet haswa wale ambao wananyimwa sehemu ya kusikilizwa kwenye jamii..!online ndio maisha yangu..!

so chocchote kilichotokea ilikuwa ni part ya maisha yangu na kazi ambayo nimejitolea kuifanya,,,nimekaa na sugu jana na alinielezea yote jinsi yalivyomtokea na kumbana mpaka akaamua kuamua aliyoamua,,,,nimpongeze kwa kile alichoamua ,,,,na pili naomba niiweke wazi kuwa misimamo yangu katika unyonyaji unaofanyaka katika tasnia ya muziki sidhani kama ndio kweli mwisho umefika,,kwahiyo siamini swala la sugu kushikana mkono na ruge kwani bado sijaona mabadiliko ya ruge na clouds nzima…!

tulikuwa tunapigana na unyonyaji uliyokuwa unafanyika kwenye tansia ya muziki huu wa kizazi kipya,,na ruge na clouds walikuwa ni moja kati ya wale ma top wanao fanya mambo hovyo,,,kuna wengine wengi tu ambao tunatakiwa kuwafanyia kazi,,,,lakini kwakuwa tulipata power kubwa sana ya kupigana kwa kutumia nguvu ya umma,,,yaani jamii ilitupokea kwa nguvu zote,

na tulikuwa tunaongea mengi kuhusu clouds,,tukiachana na yale ambayo clouds wamesema watayabadilisha,,,lakini still bado kunaonekana kuna jambo linajificha hapa,,kivipi?sugu alishasema yeye hawezi kukaa na ruge mmeza moja labda mpaka alipwe fidia ya ule mchongo wake wa maleria,,na jana ilivyotokea hii inshu,,,,,katika taarifa alizokuwa akikisambazo mkoloni,,,

nakukuu “anti virus iko pale pale akiwemo na sugu ndani na kama madam mchovu anaongea usenge kumamake ndio atajua kuwa sisi sio madaktari hatutishii,haya ni maisha na hakuna anachokijua **** tu akae kimya……..kifupi kuchanwa kuko pale pale sio ruge wala nani…..tafadhalini kumbukeni sugu alishawaambia idadi ya watu wa kuchanwa imeongezeka mlidhani anatania??? au lini alisema kitu halafu hakikuwa???

suala la mazungumzo na kukubaliana masuala ya msingi baina yao kuhusu mradi wa malaria lilikuwa likifanyika mara kwa mara tu, sisi vinega tumekaa kimya na amekuwa katika malumbano hayo na vikao vingi tu na hatimaye leo wamekubaliana kimsingi tena kwa maandishi juu ya suala lao huku rugay akikiri kuwa ndiye alikuwa anazingua…….kuhusu upande wa harakati za muziki ziko pale pale…….ushindi wa sugu dhidi ya mradi wa malaria ni mafanikio ya movement,sasa bado virusi vingi tu kwenye hili game na tunakomaa nao…….with no apology!!!! “mwisho wa kunukuu…….!

NA PIA nilipokuwa napigiwa simu na watu kuhusu hili swala ambalo lilinishtua kama ningekuwa mwanamke wenye mamba ningezaa au mamba kualibika siku hii,,nilijaribu kupiga simu kwa baadahi ya vinega nakutakakujua nini kimetokea,,na nilipoongea na kulwa wa mapacha alinijibu yeah,,mkoloni ameniambia kuwa ruge alikuwa anaenda kule bungeni na kuongelea swala la kuyamaliza kwa kumlipa sugu ule mradi wake wa malaria,na kukubali kufata masharti ya vinegar kuhusu studio na TFU,,nikamwambia lakini unaona huku online jinsi watu walivyo chafuka,,,?akasema ngoja niongee na mkoloni awape taarifa,na simu ikakatika,pia niliongea na kinega adili naeye alionekana kutokuwa nataarifa yoyote kuhusu picha na mapatano ya sugu na ruge.

sasa je katika taarifa nilizopewa mm kama kinega wa antivirus ,,,kuna yoyote ilisema kuwa vinega tumeshinda hata na ile ya malaria?na je kwanini haijaongelewa hata kwenye ma television ?mm nilimuuliza sugu jana tarehe 21,o2,2012…..!

je nigga vipi unakumbuka kuhusiana na inshu yako ya maleria?umekuwa unajinadi ukisema kuwa ipo siku tu ruge atakulipa fidia yako ya ule mradi wa maleria,,na je mbona sijaona neno lolote kuhusiana na huo mradi hapo kwenye karatasi ????na sugu alinijibu kuwa wakati anaenda kwenye huu mkutano wa kupatanishwa alienda na lawyer wake ambae ni mh tundulisu.!so tundulisu ndie atakayefatilia mahakamani inshu ya maleria na mpaka ipatikane haki yake,,,,

nilitikisa kichwa nikaona je,,,,?nikweli sugu nnayemfahamu mm anaweza kukubali lile swala kivile?na nikarudi tena so umekuali kwasababu umeongea na ruge kuwa atakulipa ama?akasema nimekubaliana na ruge kwasababu kila hoja ya msingi niliyoiweka mezani kwenye kamati ya bunge ameijibu kwa kusema inalekebishwa ikimemo na hiyo ya maleria..!akaniuliza sasa peen,,ebu niambie kama ungekuwa wewe ungefanya nn?ikiwa kama kamati ya bunge imekuomba madai yako,,na umewapa madai yako na ndio yale ambayo kamati ya bungeimesikiliza kwenye mixtape zote mbili,,,

so kamati ya bunge ikampa ruge hayo madai na ruge akasema yuko tayari kuyafanyia kazi,,sasa mm ningeinuka na kusema sitaki suluu??niambie peen?nikamwambia sugu umefanya jambo ambalo ni kubwa kweli kama lilivyokuwa kubwa wakubwa wa watanzania,,lakini hapo ni sawa sawa na kuuza misimamo ya baadhi ya vinega ambao wanaonekana mitaani kama wamedandia huu msafara wa kwenda kunywa maji ya uzima.kwani antivirus ni kitu kikubwa na kama kweli ungekuwa na maamuzi kama hayo basi ingekubidi utupe taarifa na wenzio ili tukupe mawazo na misimamo yetu pia kama ilivyokuwa hapo awali,,,sugu alisema kamati ya bunge hakumpa nafasi ya kujadili hayo na sisi,,kwani ugumu ungezidi kuwa mkubwa katika kutoa maamuzi ya mwisho,so mim kama peen lawyer swahili original,,namuheshimu sana sugu na hata niliwahi kusema mtoto wangu wa pili akizaliwa na kama hatakuwa wakiume basi ningemuita sugu yaani (joseph),,

pia nampa pongezi kwa uamuzi wake wa kuamua kusitisha beef ambayo ni moja kati ya zile amri kumi za mungu kwa sisi wa christu,,

lakini kwangu mimi kama peen,,vita dhidi ya clouds itakuwepo pale pale bila kushirikisha sugu na yoyote ambaye atakuwa anaona kuwa clouds ni safi sana,,kwani kuna mambo ambayo bado yanaendelea hata kwa mfano jana tarehe 21,02 2011,,nadhani kama mlisikiliza vipindi vya clouds mlisikia jinsi tulivyokuwa tunatukanwa sisi wengine wenye muonekano kama tumedandia hii safari ya maji ya uzima,,

NA SASA mimi nilijikuta nimejiunga kwenye hizi harakati toka mwaka 2011 mwanzoni wakati baadhi ya vinega wameanzakurecord antivirus mixtape vol 1,,ndio nilipoongea na kina mapacha,na kuwauliza kuwa je mnadahni hii mixtape itasambaa vipi?na wakanijibu mitaani tu kwa sehemu za wanazoburn cd na internet café,,nikawaambia kuwa mimi nna SWAHILI ORIGINAL Pia ni kwaajili ya mambo kama hayo….!nna website ambayo inaweza kuwasaidia kusambaza online,,na tukafanya hivyo kweli,,mixtape hiyo ya mwaka 2010 ilipoisha tu kulwa aliniita na akanipeleka sehemu tukaburn cd ile na akasema tafadhari peen naomba iweke kweli online.

Uwe unatupa update za jinsi inavyo samba kwa idadi ya kipi,,,nilifanya hivyo nakumbuka kwenye website yangu kulikuwa na tatizo la kuweka file kubwa la kudownload kama lile ya album nzima ila nilichokifanya nilienda kwenye website ya kuifadhia iitwayo WWW.SENDSPACE.COM na link yake ilikuwa Download ANTiVIRUS MIXTAPE VOL 1 2010.zip from Sendspace.com - send big files the easy way nah ii ni ile mixtape ya kwanza ambayo bado ipo mpaka sasa kwenye hiyo link,na pia kwenye website yangu ya Swahili SWAHILI ORIGINAL pia ipo ni ANTIVIRUS MIXTAPE VOL ONE.

Sasa nahii volume two tulifanya hivyo hivyo sema kilichobadilika ni kwamba niliongeza space kwenye website yangu so file hilo la album nzima ya antivirus imeingia kwenye website yangu na watu walianza kudownload humo.

Watu wengi wamedownload ni ma elfu ya watu,,na watu walielewa nini tunaongelea bila kujali kama sugu na ruge wanachuki zao binafsi wala nini,kuna diagram inaonesha jinsi umma ulivyokuwa unapitia kwenye website yangu na kudownlaod hizo mixtape hapo chini.

Hizi ni statics za downloading toka kwenye website yangu.hizi ni za Antivirus volume Two tu,,toka sept ilivyotoka mpaka feb hii.unaweza kuona.

Usage Statistics for swahilioriginaltzcom.fatcow.com
Summary Period: Last 12 Months
Generated 21-Feb-2012 14:56 EST

Nilijitoa kwa hali na mali kwenye hii movement na nimekuwa kama kimbelembele kama baadhi ya maadui zetu walivyopenda kuniita,,lakini mimi sikujali hilo,,nilichoona nikwamba nafight kwaniaba ya mtoto wangu ambaye bado hajazaliwa,kiukweli kwenye huu muziki wakizazi kipya unakila aina ya utilitimba ambao naweza kuufananisha na siasa za bongo,,lakini niliamini kwakutumia njia tulizokuwa tunatumia kama vinega tungefika mwisho wa harakati kwa kuona mabadiliko kama yalivyo kwenye mapinduzi yoyote ya harakati,,”no shake hands but can’t you see the changes”nilijitoa kufa na kupona kwenye hizi harakati ila sasa naamini nimepata cha kumuadisia mtoto wangu ambaye kwasasa bado yuko tumboni na anamiezi 5 tu.
Naamini Kweli hakuna harakati zisizo na mwisho lakini na ni kweli KWENYE HARAKATI KAMA HIZI KUNA VIFO NA MASHUJAA,,SASA KAMA KWELI HIZI HARAKATI NILIJITOA KUFA AU KUPONA BASI NAOMBA NITANGAZEE KUWA MM BADO NI MPIGANANI NA BADO NAPIGANA DHIDI YA UPUMBAVU UNAFANYIKA KATIKA TASNIA HII YA BONGO FLEVA.
Kama sugu alishake hands na RUGE ilikumaliza tofauti zao basi ni wao na tofauti zao.lakini kwangu mimi napigano bado nayaona ni marefu sana na sitapenda kuwaonesha wananchi kikomo cha misimamo yangu,ni kweli ruge amekubali kuanzia suala la studio ya rais kurudishwa kwa basata ili iwe ya wasanii wote,pia t.f.u ijikabidhi kwa chama halali cha wasanii yaani t.u.m.a kama ambavyo tulikuwa tunadai na mpaka issue za wasanii kunyanyaswa na kubaniwa na pia suala la malipo hafifu vyote vimejadiliwa na kukubaliwa kwa utekelezaji…
harakati huwa ni ni mabadiliko yanayoonekana na sio kupeana ahadi za maneno au maandishi.

nasema nashukuru sana kwa wachache wanao elewa ukweli wa jambo hili,,na pia nawashukuru pia wengi wanaotukana harakati za antivirus nakuona kama tulikuwatunafanya biashara na mauzo yamashapatikana,,,na mwisho napenda kumshukuru mh joseph mbilinyi kwa kuuza utu na misimamo yangu kwa umma,,,kwani pale tulipomuweka yeye kama icon yetu vinega haikuwa inamaana kwenda kufanya maamuzi bila kutushirikisha kama ilivyokuwa awali.kweli tanzania ni nchi yenye tabia ambazo hakuna popote dunia.

sasa wasanii ambao tulikuwa tunawaita miskule,masnitch na waoga,,sasa sijui watamuita sugu nani na vinega?tumepoteza heshima kwa umma,na hususani vijana wa tanzania.na hili kwangu bado sijalikubali heshima yangu na utu wangu upo pale pale.

kweli ile hali ya kuchukulia kila kitu poa,,naona sasa imezaa mpaka baharini,,kila kitu tu poa haya wacha iwe poa kwako kwangu balaa.
yote haya nimeongea na kuandika baada ya jana 21- 02- 2012 kufanya kikao na sugu na baadhi ya vinega,na nilipotoka hapo ndio nikapata pa kuanzia kuandika.

HISTORIA NA SHINA LA ANTIVIRUS KWA UFUPI:
Naitoa hii ili kuwaonesha wale wachache wanao dhani kuwa hizi harakari zilianzishwa na sugu baada ya kuzimwa ile dili ya malaria,au kuwa mbunge.haikuwa hivyo.

Harakati za ANTIVIRUS NA VINEGA ni mkombozi wa wasanii wa muziki hapa tanzania,Kana mengi yanaendelea kuhusiana na hizi harakati hapa nchini,,kuna mazuri na hata mabaya pia yapo ambapo kuna kasoro ndogo za jinsi wanaharakati hawa wa antivirus zinavyoendeshwa kwenye jamii.

harakari hizi zimesimamishwa na nguvu ya album ya mchanganyo wa wasanii ambao walikuwa msatri wa mbele katika kuongea ukweli ambao ndio tatizo la huu muziki hapa tanzania.album hiyo inafahamika kwa jina la ANTIVIRUS,,na album hii imeundwa na mpangilio wa matolea maalumu amabyo yanatoka kila mwaka,toka mwaka 2010-11.

album hiyo pia kwakuzingatia maadili ya muziki na lugha iliyotumika humo ndani,,wasanii hao waliona haikuwa ni vema kuiita album,kwasababu haikuwa inauzwa na wala haikuwa official kwa jamii nzima ila kwa watu wazima tu na wadau wa muziki tanzania.

ni wasanii wengi walianza hizi harakati na mwanzo kabisa idea au wazo hili lilianzishwa na MAPACHA yaani kulwa na doto wa (MAUJANJA SAPLAYAZ) na baadae kumshirikisha mkoloni na profesa ludigo. Muda ulipozidi kwenda wazo hilo lilizidikukuwa na wasanii wengi walilipenda na walipenda kushiriki katika hiyo mixtape inayoongelea ushenzi wa wadau wa muziki hapa tanzania hususani kwenye secta ya bongofleva.

mapacha wakiongozwa,mkoloni na baadhi ya wasanii wakiongozwa na prof ludigo akiwa kama producer wa hii antivirus walianza mchakato wa kurecord mixtape ya kwanza mnamo mwaka 2010 na baada ya track kadhaa kukufanywa ndipo sugu nae alikuja na kujiunga na kuweka michano yake.hapo ni kabla hata hajawa mbunge na wala hajaanza kugombania ubunge,na kufanya vizri kwa antivirus hii ni ushindi tosha pia kwa sugu kwani misimamo iliyokuwa ikioneshwa kwenye hii mixtape ilimsaidia hata kwenye kampeni zake za kugombania ubunge.so kwenye mixtape hiyo ya kwanza sugu alionekana kuongelea sana dili la malaria na kufanya jamii ijiulize na kutaka kujua haki ya sugu ilikuwa wapi,so watu walikuja kupata ukweli kuwa sugu ndio alikuwa ana haki zote za ule mchono wa malaria,sema ruge aliingilia ndani.so akawa kama mtu aliyetendewa ubaya na jamii siku zote inakuwa na yule aliyetendewa ubaya na ndio maana hata vinega tumekuwa tukipata support toka kwa umma kwani watu wameguswa na uonezu.

so the crew ambayo ilizalisha hili wazo ni MAPACHA,hii inshu yote ilikuwa ni magenge ya mwenge NA Producer wao Prof Ludigo,ambapo maujanja saplayaz walipata wazo hilo la kuanzisha antivirus kutokana na unyanyapaaji wa wasanii na unyonyaji uliokuwa unaonekana kwenye kituo hicho cha media,,yaani clouds,,na walianza kuonekana hawafahi kuonekana pale tangu pindi walipoenda kwenye interview na kuulizwa je nyinyi kama mapacha mtu akitaka kuwaita kwenye show mtadai shilingi ngapi?wakasema tunahitaji milioni 250 ,

na walikuwa na makusudi yao kufanya hivyo na kwanzia hapo walikuwa wanaonekana kama vichekesho kwa watu kwani walikuwa wakicholeshwa na baadhi ya hao watangazaji kuwa wanajifanya wako juu,,na hapo ndipo walikaa mtaani wakiendelea na kazi nyingine za kuprint tshirts na wakiunda wazo la kuanza kurecord nyimbo ambazo zinaongelea huu ukweli wa clouds na watu kama hao,na baadae wazo lao la kudai haki kwa kuanzisha hii antivirus ilikuwa ni nzuri kwa kila mtu.wasanii wengi walipenda kujiunga na wengine waliogopa kujiunga kwani waliogopa kuonekana wanawasema clouds na wakati still walikuwa wanapenda kuendelea kupokea japo kile kipato kidogo ambacho wanapokea toka kwao.

Hiyo ndio historia fupi ya jinsi antivirus ilivyozaliwa,na baadae mpaka watu kama sisi tukajikuta ndani na tukuwa na misimamo na mapenzi ya dhati ya antivirus mpaka kujitoa kufa au kupona kwa lolote lile. So kwenye hizi mixtape ambazo zilikuwa zinafanyika watu walitoa madai ya msingi na umma ilielewa,na tumefanya show za kikoa mitatu,ambazo tulifanya viziri hasi mkoani dare s salaam,na mimi nilishiriki kama msanii na pia I.T TECHNICIAN kwenye harakati hizi.

NASHINDWA KUKUBALI KWELI KATIKA BAADHI YA VINEGA WA ANTIVIRUS,,walikuwa ni watu ambao siku zote wamekuwa wabishi na wenye kutaka kujua kiundani zaidi baadhi ya vitu ambavyo huwa vinaonekana tofauti,,lakini vinega hao leo hii ndio wamekuwa watu wa kutushawishi na sisi wengine tusioelewa huu mchongo eti nasisi tujirudi?tujirudi vipi na je heshima yangu na imani yangu kwa umma atairudisha ruge au sugu?

mimi sijakubaliana na hiliswala la kupatana kwa sugu na ruge kwa sababu nyingi kama hizi:-

1.sugu hakutushirikisha vinega wenzake juu ya hii inshu mpaka anafikia kuchukua uamuzi.

2.sugu alishawahi kuapa kusema hawezi kukaa meza moja na ruge unless ruge amemlipa kwanza ule mradi wake wa malaria.sasa kama ameweza kukaanae meza moja na hata ameweza kushake hands nae?je atakuwa amelipwa milioni ngapi mpaka kutusahau sisi wengine huku na kutupa surprise ya kutukatisha maisha?

3.kama kweli sugu ameamua kupatana na ruge je?clouds tabia zao ambazo wamekili kuzibadilisha watabadilisha ikiwa kwanza siku ya mapatanisha hayo watangazaji wake walianza kwa kutukashifu na kutukebei vinega ambao tumeonekana kama wafata upepo tusio na maamuzi na wala mawazo tu juu ya swala la upatanisho wetu na wao?

4.je ruge alikuwa anatafuta suluhisho kwa vinega au kwa sugu kama sugu?kwani sijaskia vinega wanatajwa kama ni watu tunaotakiwa kusimamisha hizi mambo za kuwasema kwa mambo yao ya uclouds,unyanyapaaji wa wasanii,na mengine.kwani mimi binafsi ntaendelea kureport na kuelezea umma juu ya mambo ambayo nayajua kuhusu clouds na ruge,sasa yeye ataweza kumchana tena?na je kama hatoweza tutakuwa na kinega gani tena kundini?

5.je kabla hajaamua hayo maamuzi yake sugu,je ni kweli aliamua kutuchoresha wenzake kwa umma kwa kutoonekana hatuna any say wala mawazo kwenye hizi harakari za antivirus?je heshima ambayo imeshuka kwangu itarudi vipi?

6.siamini kama upatanishi wao ndio ushindi wa antivirus kwani kwa nchini yangu mimi nayajua sana mambo kama haya,,hakutakuwa na anychange na wala hakutakuwa na heshima ya antivirus tena,so kila kinega ataheshimika kwa misimamo na mawazo yake kwa jamii.

7.kwanini madai yote ambayo alikuwa yanaongelewa na antivirus mixtapes ambayo ruge kayakubali kuyafanyia kazi hayakuwekwa wazi kwa umma kama yalivyowekwa yale ya studio ya raisi na TFU kwenda TUMA?namaanisha mradi wake wa malaria,ulikuwa hatusu ila ulituhsu tangu pale tulipo uingiza kwenye malalamiko na madai ya antivirus na kuwaambia wananchi,so kama ndio ilikuwa sababu ya yeye kukubali kutusahau wenzake kwasababu amembiwa kulipwa ile inshu yake basi kwanini hajaiweka wazi?

hayo ndio kati ya yale mengi ambayo yananitoa imani na upatanisho wa sugu na ruge na kunifanya nionekama kuna mambo ambayo yamejificha nyuma ya kamera,,

Sasa kuna maswali nimekuwa napokea toka kwa waandishi wa habari ,wasani,mashabiki na wadau wa antivirus..,kiukweli bado sijajua nini cha kuwajibu kwani nadhani ni maswali ambayo hayaniusu mimi,,kwani mimi siye ambaye nimeonekana kushake hands na ruge,mimi niko zangu na wala nilikuwa sina hiyo taarifa,,sasa kama kweli haya maswali yanahitaji majibu basi ningeimba hayajibu mh joseph mbilinyi sugu,ambaye ndie aliekubaliana na ruge kuhusu zile hoja zote za msingi.
MASWALI:

“I WANA KNW A LITTLE THINGS ABOUT
OUR SLOGAN ”ANTIVIRUS WITH NO
APOLOGIZE” plz Vinega help me am nt
clear”

“ BDO NNAUHAKIKA MAKUBALIANO YA SUGU NA RAGAY HATA WADAU WA KARIBU WA SUGU(kama mkoloni,d,k,peen,adil, n.k) HAWAKUSHIRIKISHWA WALA HAWAJUI LOLOTE NDO MAANA KILA M1 ANASEMA LAKE …MKOLONI KAPOST HICHI, PEEN NDO KWANZA ANALALAMIKALAMIKA NA MAFUMBO KIBAO,D MAUJANJA KABAKI KU-LIKE STATUS ZA W2, NA SAHV ADILI NAE KAONGEA KINGINE
….SUGU SUGU SUGU UNATUCHANGANYA…”

“KAMA RUGE ALIWEKA KUWAIBA BAADHI YA VINEGA KAMA MANZESE CREW,GANGWE MOB?SASA ANGESHINDWA VIP KUMUIBA NA SUGU?”

“HIVI KWELI KUNA MTU ANAIMANI TENA NA SUGU AU KINEGA WA ANTIVIRUS KWAUJUMALA? “

“SUGU NDIO ALIKUWA ICON YAO,SASA KAMA YEYE KATOKA NANI ATAONGEA KITU NA TUMSIKILIZE?MAANA TULIKUWA NA IMANI KUWA YEYE NDIO ANAYACHUKUA YA MITAANI NA KUYAPELEKA MJENGONI?DAH NDIO MAANA HATA ZITTO NAE ALIKUWA HIVI NA AKATULIA”
“Magenge haya maswali yananisumbua kichwa sana;
1. Kwann mpaka sasa MAGENGE yalyopka ANTIVIRUS album yapo kmya? Hata yanayoongea, yana2mia mafumbo!

2. Hizi T_Shirt za ANTIVIRUS 2nazotisha nazo ktaani, 2endelee kuztnga? Au ndo 2zpeleke ktk majumba ya makumbusho?

3. Kama Mh. Mbunge amepatana kirahisi na Gay? Hawez kupatana kweli na CCM na akarudisha kadi ya chama che2?

4. Kwann Mashoga wa WAFU FM wawe wa kwanza ku2juza juu ya hii inshu? Na si Kiongozi we2?

5. Vp khs show za FIESTA, 2anze kutmba 2? Na kuhusu zile line za AIRTEL 2lzozvunja, 2kazili_new au?

6. Vp khs zle ngoma za ANTIVIRUS, 2endelee kuzcklza? Na WAFU FM vp, nayo 2itegee ckio?

7. Ile operation 2lyojuzwa jana ya “Ondoa Uclauzz, Ongeza Magenge!” itaendelea? Vp khs zile show za ANTIVIRUS ztaendelea mikoani?

8. Kipi kimemsukuma Mh. Mbunge a2saliti? Gay amefka dau? Au Mh. Mbunge alkuwa akipma kasi ya mto kwa kuingiza mguu?
MAGENGE naombeni mwongozo, mana mpaka sasa nipo dilema.
9.Vinega wenye kama peen,mapacha na wakina adili wenye wameonesha kupigwa na supriz,,na hili swali kivip?post zao limeonesha kuwa watatujuza baada ya muda kivipi?walikuwa hawana habari yakutupa wakati wanayakologa au?

10. SUGU na WAPAMBE WAKO kitaa kitawahukumu,watu wamejitoa kwa ajili yetu japokuwa hawanufaiki na chochote leo hii mnawasalit?

11. mnategemea mtesema nini tena na umma iwasikilize?

12.hivi kama vinega wa online kama adili mapacha walikuwa hawana habari je wasanii kama sister p na mabaga fresh je?na hivi bou nako atawaelewa kweli?ndo maana nimemuona na vatoloco pamoja?

13.soggy vip jamani mbona kama hayupo hivi…?hata suma?jamani vip?dah jamaa kawacholesha wenzake kwa maamuzi yake binafsi…!

HAYO NI BAADHI TU YA MASWALI NILIYOPOKEA TOKA KWENYE SIMU YANGU YA MKONONI NA ONLINE.
WAKO KATIKA HARAKATI ZA KWELI NA NTABAKI KAMA MFANO WA REAL KINEGA LABDA WANIUE
PEEN LAWYER – SWAHILI ORIGINAL
22/2,2012

NB: one Copy kwa kila kinega,Na one copy kwa umma, one Baba yangu mzazi, one copy ntaiweka kama history ya mwanangu ambaye anategemewa kuzaliwa,na copy moya ntakuwa nampa kila anayenitukana na kuniuliza maswal
 
Poleni. Mbona hii iko wazi mkuu; madai ya sugu ilikuwa ni kulalamikia mchongo wake wa malaria haikubaliki. Inaonekana amepewa kitu na ameridhika na kama kawaida amewatosa wenzake! Ka nchi haka bwana ukipiga kelele na hasa ukijifanya unanyamazishwa, yanaisha.

Kuna fungu katika Biblia linasema " nitampiga mchungaji na kondoo watatawanyika" Angalieni msije tawanyika baada ya kinara wenu kuwekwa mateka.
 
Poleni. Mbona hii iko wazi mkuu; madai ya sugu ilikuwa ni kulalamikia mchongo wake wa malaria haikubaliki. Inaonekana amepewa kitu na ameridhika na kama kawaida amewatosa wenzake! Ka nchi haka bwana ukipiga kelele na hasa ukijifanya kama kiongozi vile unanyamazishwa, yanaisha.

Kuna fungu katika Biblia linasema " nitampiga mchungaji na kondoo watatawanyika" Angalieni msije tawanyika baada ya kinara wenu kuwekwa mateka.
 
ruge kichwa sana yaani kambana huyo mbilinyi hadi amefail pa kurukia.
Uzuri wa mbeya mp akiletaga usaliti huwa hapati nafasi mara nyingne najua analijua hili vizuri. Keshapoteza mvuto kwa vijana.
 
siasa zimeingilia harakati ndo inakuwa matatizo yake sasa hapo...but ukweli utajulikana kama mechi imeuzwa au ni makubaliano yamefikiwa bila kitu kidogo kupitishwa hapo....
 
ukistaajabu ya Musa ..utayaona ya Firaun...
Ndio maana waswahili wanasema ni bora kukaa kimya kuliko kuongea maneno maana siku moja utalazimika kuyala mwenyeweee.. SUGU VIPI TENA KAKA? au ni huo Uheshimiwaaaaaaa,....
 
mimi toka mwanzo japo nilikuwa nikiwa support vinega, na japo sikupenda the ya approach waliotumia kuwasilisha matatizo yao via mziki lakini shaka yangu ilikuwa kwa sugu.
Nilikuwa na shaka kwamba sugu bifu lake kubwa na ruge ni suala la maria haikubariki na haya mengine yalikuwa so minor ila ilibidi ayape kipaumbele kupata support ya watu wengi
I ama afraid kama akipewa chake harakati zitapungua na waliobaki watatelekezwa jambo ambalo naomba lisitokee maana atakuwa katosa watu wengi.
 
Kwanza huyu jamaa akajifunze kuandika taarifa.Anaonyesha namna gani wasani wetu wanashinda kuvuta bangi na kusahau masuala ya muhimu kama elimu ya kawaida tu ya kuandika taarifa.Pili,huyu jamaa anaonekana ni mtu wakupenda shari tu,hataki kukubaliana na ukweli kuwa wakati mwingine tunapaswa kujifunza kutafuta suluhu kwenye mambo ya msingi.Nakubaliana na yeye kuwa yawezekana Sugu akufanya vyema kutafuta suluhu bila kuwataarifu,ila hii haitafuta ukweli kuwa suluhu ni jambo la muhimu kwa maisha hya.Tatu,wakubaliane na ukweli kuwa Sugu ndio alikuwa icon kama wao wanavyosema,na kama Sugu ataamua kuachana na hizo harakati wasitegemee tena support ya wananchi,na wananchi walikuwa wanamkubali SUGU zaidi ya wao hao vinega wengine.Nne,Sungu kashatoa tamko kwa kuweka msimamo kuwa movement ya vinega itaendelea mpaka wasafishe hii tasnia ya bongo fleva,sasa kama movement itaendelea kwanini wanakuwa na shaka juu ya Sugu?

Ushauri wangu kwa Clouds Fm,watangazaji wake wengi ndio wanaendeleza huu mgogoro,mimi sikuwasikia wakisema kuwa vinega wengne walidandia huu mgogoro,lakini nilihisi wangeweza sema hivyo,na hii inatokana na tabia ya hizi redio hasa zinazojihita za burudani kwa vijana.Zimejaa watangazaji wenye asili ya majungu,maneno yasiyo na tija na mizaha mizaha kwenye mambo ya msingi,na hizi redio ndio zitakuja kutuharibia amani ya hii nchi....nakubaliana na huyu kinega kuwa hizo kejeli ni sababu tosha kuona kuwa muafaka wa Sugu na Ruge hauna maana.Nadhani watangazaji wa CLOUDS hasa Kibonde na wengine wajifunze kuwa watu makini na kupunguza mizaha kwenye mambo ya msingi...

Nawasilisha!!
 
Sugu hajielewi bado kichwa kikubwa ubongo wa mtoto.....
Sugu kashakula hele za malaria na ndo alichotaka
 
Sugu kawatumia tu kufanikisha target zake ila akae ajue cku za mnafki znahesabika. One day yes jamii itatambua nani ni na nani hata hayo chadema wamejshusha sana kupatana na ruge ni sawa na kupatana na ccm wanantia mashaka sana hawa.
 

Similar Discussions

1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom