Sugu: RC akisema atawatoa akina Roma Jumapili, ni kazi gani amewapa ambayo anajua hadi siku hiyo

Francis12

JF-Expert Member
Sep 30, 2016
7,533
22,276
Waziri Kivuli wa Habari Utamaduni na michezo Mhe Joseph Mbilinyi anaongea na waandishi wa habari muda huu kuhusu kupotea kwa Msanii Roma. Baada ya kauli ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paulo Makonda kusema msanii pamoja na mwenzake wanaweza kupatikana kabla siku ya jumapili

[HASHTAG]#WaziriKivuliHabari[/HASHTAG]

Wananchi wanahoji Roma na wenzake wako wapi sababu hawajui, lakini mtu anayejua walipo amesema watapatikana Jumapili.
Jana alisema hadi Jumapili Roma na wenzake watakuwa wamepatikana, sisi tunamtaka awaachi leo warudi kwenye familia zao.
Akisema atawatoa Jumapili, ni kazi gani amewapa ambayo anajua hadi siku hiyo watakuwa wamemaliza, atueleze.
[HASHTAG]#WaziriKivuliHabari[/HASHTAG]

Badala ya Wizara ya Habari kuomba ushirikiano wa wananchi, wamchukue huyo anayejua walipo.Mtu asiogope kupoteza uwaziri
 
Kiukweli Kauli ya RC wa DSM inaukakasi sana.....ingekuwa watanzania ni werevu tungekuwa tumepata picha kamili juu ya kupotea kwa Roma. Jeshi la polis limesema lipo kwenye Upelelezi, RC anasema atamtoa Roma kabla ya Jumapili.

kwanini jeshi la Polis wasiombe Msaada kwa RC?
 
[HASHTAG]#WaziriKivuliHabari[/HASHTAG]

Hivyo, Nay wa Mitego, Roma na wasanii wengine hawajakosea lolote sababu wao ni wasanii, na kazi yao ni kuimba.
 
Ndio kazi ya majizi chadema siku hizi, kupindisha kauli na kulisha maneno watu
 
Computa wamechukua..aisee ivi ni sababu gani Ney alikua amekamatwa..na sababu gan aliachiwa
Walitaka kujenga mazingira kwamba hawana haja na wasanii kutoa mawazo yao hivo basis hata akipotea mwingine ni rahisi kusema wao hawahusiki maana waliisha onyesha kutokerwa na nyimbo za kukosoa.
 
[HASHTAG]#WaziriKivuliHabari[/HASHTAG]

Watu wanaogopa kuendesha magari ya kifahari sababu kuna mtu atawaambia analitaka, au wajumuishwe kwenye dawa za kulevya
hahahahahaaaaaaaaaa nani huyo anatamani magari ya wenzake????
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom