Chakaza
JF-Expert Member
- Mar 10, 2007
- 39,759
- 71,138
Katika hali inayoonyesha kuwa Wabunge walio kuwa upinzani waka 'unga mkono juhudi' na kuja kupitishwa kwa nguvu ya dola kuwa Wabunge tena hawakubaliki hata na wenzao wa CCM.
Imedhihirika baada ya mbunge Mwita wa Sengerema kuingilia ili kuchafua mchango wa Sugu kisha kuitwa yeye na wenzake mapoyoyo na Bunge bila kujali itikadi likalipuka kwa shangwe.
Imekuwa ni tabia ya Wabunge hao wapya wa CCM kutumika/kujituma kutoa taarifa au mwongozo wa spika kujionyesha wao ni CCM damu kuliko walio wakuta hivyo kupata dharau miongoni mwa walio wakuta.
Ni swala la muda tuu, dharau kwao itakuwa wazi hata ndani ya CCM.