SUGECO imefungua njia kwa vijana wajasiriamali katika Sekta ya Kilimo na Biashara

Aman Ng'oma

JF-Expert Member
Nov 8, 2011
954
510
Vijana wengi wa Tanzania tuna shida kubwa katika bongo zetu. Tumegeuka kuwa jamii ya kulaumu na kulalamika badala ya kuchukua hatua.Tunapenda urahisi. Tunasahau kuwa zama zimebadilika. Hatufikirishi vichwa vyetu kujaribu kutumia japo sehemu ndogo ya elimu tuliyoipata chuoni kutafuta fursa za kukamata.

Badala yake tumekaa tukibweteka tukiamini siku moja tutapata kazi ya ndoto zetu huku siku zikizidi kuyoyoma bila mafanikio. Tumekuwa mizigo kwa wazazi wetu badala ya kuwa msaada. Hakuna mawazo mapya tunayotoa. Zaidi tunatamani utanashati bila kuwa na pesa mfukoni. Kazi za kuchafuka hatuzitaki tena hata kama zinatengeneza pesa kiasi gani. Usomi wetu umetufanya tuchague kazi.

Kijana asiyeenda shule, unakuta ana uwezo mkubwa zaidi wa kutengeneza pesa, kuliko msomi aliyehitimu chuo kikuu. Kijana asiyefika chuo kikuu hachagui kazi na vilevile yuko tayari kumtumia msomi kuuliza kitu asichokijua, lakini msomi yeye kwa upande wake hayuko tayari kujifunza kutoka kwa kijana asiyebahatika kufika chuo kikuu.

Tuna tatizo kubwa sana. Vijana wengi tumekosa mawazo mapya ya Ujasiriamali. Bongo zetu zimelala. Hatuoni fursa mpya pamoja na kwamba fursa hizo zimejaa tele mtaani. Tunahitaji kufunguliwa vichwa vyetu na macho ili tuweza kuondolewa tongotongo zinazotufanya tushishindwe kuona fursa.

Changamoto ya kushindwa kuona fursa haiwakabili tu vijana wasomi waliyohitimu vyuo mbalimbali pekee yao bali hata wazee wetu waliyostaafu kutoka kwenye utumishi wa umma au sekta binafsi nao wanakabiliwa na tatizo hili.

Utastaajabu kumwona mstaafu namna anavyohangaika mtaani kuyakabili maisha yake mapya. Hawezi kufanya kazi nyingine zilizo nje ya fani yake. Matokeo yake baada ya kustaafu utumishi wake, anakuwa hana uwezo tena wa kuratibu na kusimamia mradi utakaompatia pesa na kumwezesha kuishi maisha yanayofanana na yale aliyokuwa akiyaishi alipokuwa kazini.

Mstaafu anaishi maisha ya ajabu kabisa pamoja na kwamba, alipatiwa mafao yake yote na mfuko wake wa hifadhi ya jamii. Amekosa elimu ya ujasiriamali. Pesa za mafao yake ya kustastaafu, anaingiza kwenye miradi mfu. Matokeo yake anapata anguko kubwa lisilo kuwa na mfano.

Lakini yote hii ni kwa sababu kulikuwa hakuna taasisi au watu waliyojitoa sawasawa kunoa bongo za watu wengine ili wawe na uwezo kujitegemea mara baada ya kustaafu au kumaliza viwango mbalimbali vya elimu.

Ushirika wa Wahitimu Wajasiriamali wa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUGECO), kwa upande wao waliliona hili na kuamua kwadhati kabisa kujitoa kuwasaidia wahitimu wa vyuo mbalimbali na vijana wasiyowahitimu ili waweze kujiajiri wao wenyewe katika sekta ya Kilimo Biashara.

Kupitia SUGECO, vijana wamekuwa wakifundishwa stadi mbalimbali za kilimo biashara ikiwemo mbinu bora za kuendesha kilimo cha kisasa, kilimo chenye tija, ufugaji bora, Uongezaji wa thamani wa mazao ya Kilimo na mifugo, Usindikaji wa bidhaa mbalimbali za kilimo, uendeshaji wa mafunzo ya kuwajengea uwezo na kuondoa tongotongo katika bongo za vijana, kuwawezesha vijana wahitimu wa vyuo kuwa na miradi yao binafsi na kupata fursa ya kusimamiwa kwa ukaribu na hatua kwa hatua hadi mradi utakaposimama.

Si hivyo tu bali pia SUGECO wanajishughulisha na utoaji wa ufadhili wa mashamba Kitalu au Greenhouse kama ilivyozoeleka na wengi kwa vijana ili kuwawezesha kuendesha shughuli za kilimo chenye udhibiti wa magonjwa. Kana kwamba haitoshi, SUGECO wanaendesha programu kabambe ya kuwapeleka vijana nchini Israel kushiriki mafunzo kwa vitendo katika sekta ya Kilimo. Kila mwaka kuna kundi la vijana wasiyopungua 30 wanapelekwa Israel.

Ukikaa na vijana waliyopata fursa ya kwenda nchini Israel na ukasikiliza shuhuda zao, utabaini wazi kuwa sisi watanzaia bado hatufanyi kazi kabisa. Tunapoteza muda wetu mwingi kizembezembe. Wenzetu kule wanachunga sana muda wao na kujali zaidi kazi. Kwao siku zote muda huwa huwatoshi kutekeleza majukumu yao, hivyo wanajitahidi kuitumia kila dakika inayopatikana kufanya kitu kinachoonekana. Muda kwao una thamani kubwa sana hivyo haupaswi kuchezewa hata kidogo.

Siku zote waisrael wanaamini kuwa hakuna mtu atakayekufa kwa kufanya kazi. Kwa hiyo ukiwa Israel masaa mengi utayatumia kwa ajili ya kufanya kazi. Siku ya mapumziko kwao ni siku moja tu katika wiki na ni siku ya jumamosi ambayo pia siku hiyo wanaitumia kwa ajili ya kukufanya Ibada.

Kuwa meneja Israel ni tofauti sana na kuwa meneja katika nchi zetu za afrika ambapo meneja anakuwa anaongoza kwa kula bata, kule ukiwa meneja hakuna kula bata, bali meneja unakuwa kama manamba mkuu, unaingia kazini wa kwanza na kutoka wa mwisho na ukiwa kazini hakuna ubosi wewe meneja ndiyo unaokuwa mstari wa mbele kufanya kazi mwanzo mwisho. Hayo ni maelezo kwa ufupi sana kutoka kwa vijana waliyobahatika kwenda huko kwa ajili ya mafunzo kwa vitendo. Mfumo huu wa Israel ndiyo unaotumiwa na SUGECO katika utoaji wa mafunzo ya kilimo kwa vitendo kwa vijana wetu wa Kitanzania.

Mapema mwezi wa kumi mwaka huu, SUGECO kwa kushirikiana na wizara ya kilimo kupitia iliyokuwa Mamlaka ya Uendelezaji wa Bonde la Mto Rufiji (RUBADA) walifanikiwa kuendesha mafunzo ya Mnyororo wa thamani wa Kuku na Sungura katika Kambi ya Vijana ya Kilimo kwa Vitendo katika Kijiji Cha Mkongo wilayani Rufiji. Vijana kutoka maeneo mbalimbali ya nchi yetu walikuja kambini hapo kuhudhuria mafunzo hayo ambayo huendeshwa kwa muda wa wiki mbili kwa kila darasa moja.

Kwa namna mafunzo hayo yalivyoratibiwa na kuendeshwa kwa ustadi mkubwa, kila anayepita kambini hapo bila kujali kiwango chake cha elimu na umri, amekuwa akinolewa vizuri na kumwezesha kutoka na elimu itakayomfanya aweze kujitegemea yeye wenyewe badala ya kusubiri kuajiriwa.

Hadi sasa ni awamu mbili tayari zimeshapita katika kambi hiyo ya vijana ya Mkongo Rufiji. Katika awamu ya pili ya mafunzo yaliyofanyika mwezi wa kumi, nami nilipata fursa ya kuwa mmoja wa wawezeshaji katika semina hiyo na kupitia mafunzo hayo niliweza kuwafundisha vijana mnyororo mzima wa thamani wa kuku pamoja na Sungura.

Katika mafunzo hayo, kwahakika nimejionea kwa macho yangu ni kwa namna gani programu hii ya SUGECO inavyowanufaisha Watanzania.
Kwakweli hizi ni aina ya programu ambazo kimsingi kama nchi tunapaswa kuziunga mkono ili Vijana wetu wapite katika kambi hizo ili waweze kujifunza kilimo kwa vitendo pamoja na stadi mbalimbali zinazotolewa katika kambi hiyo zenye lengo la kuwatengeza vijana wawe sababu ya kujiajiri wao wenyewe na kuajiri wengine.

Mfumo wetu wa elimu haumwezeshi moja kwa moja kijana kupata stadi zitakazomwezesha kujiajiri mwenyewe. Lazima vijana bila kujali kiwango chao cha elimu, wapatiwe aina hii ya mafunzo yanayotolewa na SUGECO ili kuwafanya vijana wetu watamani zaidi kujiajiri badala ya kusubiri ajira za Serikali au mashirika.

Nakumbuka katika mafunzo hayo mbali na kujifunza mnyoro wa thamani wa kuku na Sungura, masomo yaliyoendeshwa kwa nadharia na vitendo, pia washiriki waliweza kujifunza kilimo cha mbogamboga na utengenezaji wa bidhaa mbalimba kama vile dawa za chooni, sabuni, shampoo, mishumaa, mafuta ya kupakaa ya mgando pamoja na nguo aina ya batiki.

Lakini somo jingine lililofundishwa siku hiyo ni somo la kubadilisha mtazamo wa kijana kutoka kwenye kasumba ya kutaka kuajiriwa na kupewa mbinu mpya zitakazo msaidia kijana aweze kujiajiri wenyewe na kusimamia mradi wake kikamilifu.

Mkurugenzi wa SUGECO Bwana Revocatus Kimario wakati anatoa salamu zake za jioni kwa washiriki kabla ya kuwasilisha mada yake ya *Namna ya Kumuhudia Mteja,* alianza kwa nukuu ya mwalimu wa kubadilisha mtazamo wa vijana Mr Masimba *“a mindset changer”* iliyosema “Tusaidiane kuondoa kutu vichwwani kwetu.” Nukuu hii ukiitafakari vizuri utaona ni kwa namna gani ilivyojaa ukweli, vichwa vyetu vina kutu nyingi, tunahitaji kusaidiwa kuondolewa.

Bwana Kimario aliniendelea kuwatanabaisha vijana kwa kuwaambia kuwa “tukiwa hapa (kambini) degree zako zote tunaziweka pembeni kwasababu degree zako hazina maana sana kama hauna uwezo wa kutengeneza pesa.” Kimsingi Bwana Kimario alisisitiza sana ubunifu na kujiongeza. Katika hili alisema “aliyejaribu na akashindwa, anafaida kubwa kuliko asiyejaribu. Kufeli haina maana umeshindwa bali utatafuta namna nyingine ya kujaribu.” Bwana Kimario katika kuongezea uzito hili, alimnukuu Bwana Jeseph Chilton Pearce aliyeelezea thamani ya ubunifu aliyosema, to live a creative life we must lose our fear of being wrong.” Kwa taafsiri isiyo rasmi akimaanisha kwamba kuishi maisha ya ubunifu kunahitaji kuondoa hofu ya kukosea.

Baada ya utangulizo huo aliyoutoa kwa washiriki, Mkurugenzi aliendelea na somo lake la *Namna ya Kumuhudumia Mteja.* Somo lilikuwa nzuri na kila mshiriki alivutiwa nalo. Laiti nafasi ingeruhusu ningeweza kulidadavua somo hilo kwa upana wake kadiri ya mafundisho yalivyotolewa Mkurugenzi ndugu Kimario.

SUGECO imeundwa na vichwa vinavyojua kufikiria. Vinavyojua kiini cha tatizo la ajira kwa vijana na namna ya kuondoa tatizo hilo kupitia mafunzo ya kilimo Biashara. Kwahiyo wahenga walisema usione vyaelea, vimeundwa. Mambo yote mazuri yanayofanywa na SUGECO ni matokeo ya uratibu mzuri wa watu wafuatao: Kuna Dokta Anna Temu, ambaye ni Mwenyekiti wa Bodi na Dokta Flugence Mishili Makamu mwenyekiti. Kwenye kamati ya utalaam na ufundi kuna Dokta Daniel Ndyetabula, Dokta Betty Waized, na Dokta Felix Nandonde. Kwenye utawala utakutana na Bwana Revecatus Kimario, ambaye ni Mkurugenzi wa SUGECO, Bwana Joseph Masimba Mratibu wa Miradi, Bwana Ayubu E. Mundekesye meneja wa Mafunzo, Dickson Alex Mseko Meneja wa shamba na Prekseda Melkior kaimu meneja wa shamba.

Vichwa vyote hivyo kwa pamoja ndivyo vilivyotengeza wajasiriamali vijana wengi nchini katika sekta ya kilimo. Kila kona ya nchi ukipita utakutana na vijana wengi waliyonolewa na SUGECO wakishughulika na mafundo mbalimbali katika mnyororo wa thamani wa kilimo. Kuna wale wanaolima alizeti na kuchakata mafuta, kuna wanaozalisha asali, kuna wanaolima mbogamboga kupitia shamba kitalu, kuna wanaozalisha mbegu za viazi lishe na kulima viazi. Kuna waliyosaidiwa kuanzisha viwanda mbalimbali vya usindikaji. Kuna wanao jishughulisha na ufugaji wa kuku, Samaki na Mifugo mingine. Ukipita SUGECO kwahakika lazima utabadilika kifikra na kimtazomo.

Kwa ajili ya kuwafikia vijana wengi nchini ilifaa sana kama Wizara ya Kilimo na Ushirika, Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi pamoja na Wizara ya Vijana, kazi na ajira wangeangalia namna bora ya kushirikiana na SUGECO ili kuanzisha kambi mbalimbali za mafunzo ya kilimo kwa vitendo na kubadilisha fikra na mitazamo ya vijana. Kwa kufanya hivyo tutajenga taifa la kutenda badala ya kuwa taifa la kulalalamika. Na mwishowe matokeo chanya ya kiuchumi kwa vijana wetu na nchi kwa ujumla yangeonekana hasa katika kipindiki hiki ambacho nchi inaelekea kwenye uchumi wa viwanda.

Aman Ng'oma
Mkurugenzi Mtendaji
Kinasoru East Africa Tanzania Ltd
Info@kinasoruea.co.tz or amanngoma@gmail.com
0767989713 or 0715989713
Nduka Street, Chamwino Bonanza
Dodoma
*TANZANIA.*
 
Sawa..
Gharama/ada ya kuhudhuria kwenye kambi za mafunzo ni bei gani?
Naona kwny hizo kambi mnalenga zaidi vijana wadogo, je inakuwaje kwa wakubwa?
 
Vijana wengi wa Tanzania tuna shida kubwa katika bongo zetu. Tumegeuka kuwa jamii ya kulaumu na kulalamika badala ya kuchukua hatua.Tunapenda urahisi. Tunasahau kuwa zama zimebadilika. Hatufikirishi vichwa vyetu kujaribu kutumia japo sehemu ndogo ya elimu tuliyoipata chuoni kutafuta fursa za kukamata.

Badala yake tumekaa tukibweteka tukiamini siku moja tutapata kazi ya ndoto zetu huku siku zikizidi kuyoyoma bila mafanikio. Tumekuwa mizigo kwa wazazi wetu badala ya kuwa msaada. Hakuna mawazo mapya tunayotoa. Zaidi tunatamani utanashati bila kuwa na pesa mfukoni. Kazi za kuchafuka hatuzitaki tena hata kama zinatengeneza pesa kiasi gani. Usomi wetu umetufanya tuchague kazi.

Kijana asiyeenda shule, unakuta ana uwezo mkubwa zaidi wa kutengeneza pesa, kuliko msomi aliyehitimu chuo kikuu. Kijana asiyefika chuo kikuu hachagui kazi na vilevile yuko tayari kumtumia msomi kuuliza kitu asichokijua, lakini msomi yeye kwa upande wake hayuko tayari kujifunza kutoka kwa kijana asiyebahatika kufika chuo kikuu.

Tuna tatizo kubwa sana. Vijana wengi tumekosa mawazo mapya ya Ujasiriamali. Bongo zetu zimelala. Hatuoni fursa mpya pamoja na kwamba fursa hizo zimejaa tele mtaani. Tunahitaji kufunguliwa vichwa vyetu na macho ili tuweza kuondolewa tongotongo zinazotufanya tushishindwe kuona fursa.

Changamoto ya kushindwa kuona fursa haiwakabili tu vijana wasomi waliyohitimu vyuo mbalimbali pekee yao bali hata wazee wetu waliyostaafu kutoka kwenye utumishi wa umma au sekta binafsi nao wanakabiliwa na tatizo hili.

Utastaajabu kumwona mstaafu namna anavyohangaika mtaani kuyakabili maisha yake mapya. Hawezi kufanya kazi nyingine zilizo nje ya fani yake. Matokeo yake baada ya kustaafu utumishi wake, anakuwa hana uwezo tena wa kuratibu na kusimamia mradi utakaompatia pesa na kumwezesha kuishi maisha yanayofanana na yale aliyokuwa akiyaishi alipokuwa kazini.

Mstaafu anaishi maisha ya ajabu kabisa pamoja na kwamba, alipatiwa mafao yake yote na mfuko wake wa hifadhi ya jamii. Amekosa elimu ya ujasiriamali. Pesa za mafao yake ya kustastaafu, anaingiza kwenye miradi mfu. Matokeo yake anapata anguko kubwa lisilo kuwa na mfano.

Lakini yote hii ni kwa sababu kulikuwa hakuna taasisi au watu waliyojitoa sawasawa kunoa bongo za watu wengine ili wawe na uwezo kujitegemea mara baada ya kustaafu au kumaliza viwango mbalimbali vya elimu.

Ushirika wa Wahitimu Wajasiriamali wa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUGECO), kwa upande wao waliliona hili na kuamua kwadhati kabisa kujitoa kuwasaidia wahitimu wa vyuo mbalimbali na vijana wasiyowahitimu ili waweze kujiajiri wao wenyewe katika sekta ya Kilimo Biashara.

Kupitia SUGECO, vijana wamekuwa wakifundishwa stadi mbalimbali za kilimo biashara ikiwemo mbinu bora za kuendesha kilimo cha kisasa, kilimo chenye tija, ufugaji bora, Uongezaji wa thamani wa mazao ya Kilimo na mifugo, Usindikaji wa bidhaa mbalimbali za kilimo, uendeshaji wa mafunzo ya kuwajengea uwezo na kuondoa tongotongo katika bongo za vijana, kuwawezesha vijana wahitimu wa vyuo kuwa na miradi yao binafsi na kupata fursa ya kusimamiwa kwa ukaribu na hatua kwa hatua hadi mradi utakaposimama.

Si hivyo tu bali pia SUGECO wanajishughulisha na utoaji wa ufadhili wa mashamba Kitalu au Greenhouse kama ilivyozoeleka na wengi kwa vijana ili kuwawezesha kuendesha shughuli za kilimo chenye udhibiti wa magonjwa. Kana kwamba haitoshi, SUGECO wanaendesha programu kabambe ya kuwapeleka vijana nchini Israel kushiriki mafunzo kwa vitendo katika sekta ya Kilimo. Kila mwaka kuna kundi la vijana wasiyopungua 30 wanapelekwa Israel.

Ukikaa na vijana waliyopata fursa ya kwenda nchini Israel na ukasikiliza shuhuda zao, utabaini wazi kuwa sisi watanzaia bado hatufanyi kazi kabisa. Tunapoteza muda wetu mwingi kizembezembe. Wenzetu kule wanachunga sana muda wao na kujali zaidi kazi. Kwao siku zote muda huwa huwatoshi kutekeleza majukumu yao, hivyo wanajitahidi kuitumia kila dakika inayopatikana kufanya kitu kinachoonekana. Muda kwao una thamani kubwa sana hivyo haupaswi kuchezewa hata kidogo.

Siku zote waisrael wanaamini kuwa hakuna mtu atakayekufa kwa kufanya kazi. Kwa hiyo ukiwa Israel masaa mengi utayatumia kwa ajili ya kufanya kazi. Siku ya mapumziko kwao ni siku moja tu katika wiki na ni siku ya jumamosi ambayo pia siku hiyo wanaitumia kwa ajili ya kukufanya Ibada.

Kuwa meneja Israel ni tofauti sana na kuwa meneja katika nchi zetu za afrika ambapo meneja anakuwa anaongoza kwa kula bata, kule ukiwa meneja hakuna kula bata, bali meneja unakuwa kama manamba mkuu, unaingia kazini wa kwanza na kutoka wa mwisho na ukiwa kazini hakuna ubosi wewe meneja ndiyo unaokuwa mstari wa mbele kufanya kazi mwanzo mwisho. Hayo ni maelezo kwa ufupi sana kutoka kwa vijana waliyobahatika kwenda huko kwa ajili ya mafunzo kwa vitendo. Mfumo huu wa Israel ndiyo unaotumiwa na SUGECO katika utoaji wa mafunzo ya kilimo kwa vitendo kwa vijana wetu wa Kitanzania.

Mapema mwezi wa kumi mwaka huu, SUGECO kwa kushirikiana na wizara ya kilimo kupitia iliyokuwa Mamlaka ya Uendelezaji wa Bonde la Mto Rufiji (RUBADA) walifanikiwa kuendesha mafunzo ya Mnyororo wa thamani wa Kuku na Sungura katika Kambi ya Vijana ya Kilimo kwa Vitendo katika Kijiji Cha Mkongo wilayani Rufiji. Vijana kutoka maeneo mbalimbali ya nchi yetu walikuja kambini hapo kuhudhuria mafunzo hayo ambayo huendeshwa kwa muda wa wiki mbili kwa kila darasa moja.

Kwa namna mafunzo hayo yalivyoratibiwa na kuendeshwa kwa ustadi mkubwa, kila anayepita kambini hapo bila kujali kiwango chake cha elimu na umri, amekuwa akinolewa vizuri na kumwezesha kutoka na elimu itakayomfanya aweze kujitegemea yeye wenyewe badala ya kusubiri kuajiriwa.

Hadi sasa ni awamu mbili tayari zimeshapita katika kambi hiyo ya vijana ya Mkongo Rufiji. Katika awamu ya pili ya mafunzo yaliyofanyika mwezi wa kumi, nami nilipata fursa ya kuwa mmoja wa wawezeshaji katika semina hiyo na kupitia mafunzo hayo niliweza kuwafundisha vijana mnyororo mzima wa thamani wa kuku pamoja na Sungura.

Katika mafunzo hayo, kwahakika nimejionea kwa macho yangu ni kwa namna gani programu hii ya SUGECO inavyowanufaisha Watanzania.
Kwakweli hizi ni aina ya programu ambazo kimsingi kama nchi tunapaswa kuziunga mkono ili Vijana wetu wapite katika kambi hizo ili waweze kujifunza kilimo kwa vitendo pamoja na stadi mbalimbali zinazotolewa katika kambi hiyo zenye lengo la kuwatengeza vijana wawe sababu ya kujiajiri wao wenyewe na kuajiri wengine.

Mfumo wetu wa elimu haumwezeshi moja kwa moja kijana kupata stadi zitakazomwezesha kujiajiri mwenyewe. Lazima vijana bila kujali kiwango chao cha elimu, wapatiwe aina hii ya mafunzo yanayotolewa na SUGECO ili kuwafanya vijana wetu watamani zaidi kujiajiri badala ya kusubiri ajira za Serikali au mashirika.

Nakumbuka katika mafunzo hayo mbali na kujifunza mnyoro wa thamani wa kuku na Sungura, masomo yaliyoendeshwa kwa nadharia na vitendo, pia washiriki waliweza kujifunza kilimo cha mbogamboga na utengenezaji wa bidhaa mbalimba kama vile dawa za chooni, sabuni, shampoo, mishumaa, mafuta ya kupakaa ya mgando pamoja na nguo aina ya batiki.

Lakini somo jingine lililofundishwa siku hiyo ni somo la kubadilisha mtazamo wa kijana kutoka kwenye kasumba ya kutaka kuajiriwa na kupewa mbinu mpya zitakazo msaidia kijana aweze kujiajiri wenyewe na kusimamia mradi wake kikamilifu.

Mkurugenzi wa SUGECO Bwana Revocatus Kimario wakati anatoa salamu zake za jioni kwa washiriki kabla ya kuwasilisha mada yake ya *Namna ya Kumuhudia Mteja,* alianza kwa nukuu ya mwalimu wa kubadilisha mtazamo wa vijana Mr Masimba *“a mindset changer”* iliyosema “Tusaidiane kuondoa kutu vichwwani kwetu.” Nukuu hii ukiitafakari vizuri utaona ni kwa namna gani ilivyojaa ukweli, vichwa vyetu vina kutu nyingi, tunahitaji kusaidiwa kuondolewa.

Bwana Kimario aliniendelea kuwatanabaisha vijana kwa kuwaambia kuwa “tukiwa hapa (kambini) degree zako zote tunaziweka pembeni kwasababu degree zako hazina maana sana kama hauna uwezo wa kutengeneza pesa.” Kimsingi Bwana Kimario alisisitiza sana ubunifu na kujiongeza. Katika hili alisema “aliyejaribu na akashindwa, anafaida kubwa kuliko asiyejaribu. Kufeli haina maana umeshindwa bali utatafuta namna nyingine ya kujaribu.” Bwana Kimario katika kuongezea uzito hili, alimnukuu Bwana Jeseph Chilton Pearce aliyeelezea thamani ya ubunifu aliyosema, to live a creative life we must lose our fear of being wrong.” Kwa taafsiri isiyo rasmi akimaanisha kwamba kuishi maisha ya ubunifu kunahitaji kuondoa hofu ya kukosea.

Baada ya utangulizo huo aliyoutoa kwa washiriki, Mkurugenzi aliendelea na somo lake la *Namna ya Kumuhudumia Mteja.* Somo lilikuwa nzuri na kila mshiriki alivutiwa nalo. Laiti nafasi ingeruhusu ningeweza kulidadavua somo hilo kwa upana wake kadiri ya mafundisho yalivyotolewa Mkurugenzi ndugu Kimario.

SUGECO imeundwa na vichwa vinavyojua kufikiria. Vinavyojua kiini cha tatizo la ajira kwa vijana na namna ya kuondoa tatizo hilo kupitia mafunzo ya kilimo Biashara. Kwahiyo wahenga walisema usione vyaelea, vimeundwa. Mambo yote mazuri yanayofanywa na SUGECO ni matokeo ya uratibu mzuri wa watu wafuatao: Kuna Dokta Anna Temu, ambaye ni Mwenyekiti wa Bodi na Dokta Flugence Mishili Makamu mwenyekiti. Kwenye kamati ya utalaam na ufundi kuna Dokta Daniel Ndyetabula, Dokta Betty Waized, na Dokta Felix Nandonde. Kwenye utawala utakutana na Bwana Revecatus Kimario, ambaye ni Mkurugenzi wa SUGECO, Bwana Joseph Masimba Mratibu wa Miradi, Bwana Ayubu E. Mundekesye meneja wa Mafunzo, Dickson Alex Mseko Meneja wa shamba na Prekseda Melkior kaimu meneja wa shamba.

Vichwa vyote hivyo kwa pamoja ndivyo vilivyotengeza wajasiriamali vijana wengi nchini katika sekta ya kilimo. Kila kona ya nchi ukipita utakutana na vijana wengi waliyonolewa na SUGECO wakishughulika na mafundo mbalimbali katika mnyororo wa thamani wa kilimo. Kuna wale wanaolima alizeti na kuchakata mafuta, kuna wanaozalisha asali, kuna wanaolima mbogamboga kupitia shamba kitalu, kuna wanaozalisha mbegu za viazi lishe na kulima viazi. Kuna waliyosaidiwa kuanzisha viwanda mbalimbali vya usindikaji. Kuna wanao jishughulisha na ufugaji wa kuku, Samaki na Mifugo mingine. Ukipita SUGECO kwahakika lazima utabadilika kifikra na kimtazomo.

Kwa ajili ya kuwafikia vijana wengi nchini ilifaa sana kama Wizara ya Kilimo na Ushirika, Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi pamoja na Wizara ya Vijana, kazi na ajira wangeangalia namna bora ya kushirikiana na SUGECO ili kuanzisha kambi mbalimbali za mafunzo ya kilimo kwa vitendo na kubadilisha fikra na mitazamo ya vijana. Kwa kufanya hivyo tutajenga taifa la kutenda badala ya kuwa taifa la kulalalamika. Na mwishowe matokeo chanya ya kiuchumi kwa vijana wetu na nchi kwa ujumla yangeonekana hasa katika kipindiki hiki ambacho nchi inaelekea kwenye uchumi wa viwanda.

Aman Ng'oma
Mkurugenzi Mtendaji
Kinasoru East Africa Tanzania Ltd
Info@kinasoruea.co.tz or amanngoma@gmail.com
0767989713 or 0715989713
Nduka Street, Chamwino Bonanza
Dodoma
*TANZANIA.*
nilokuwa napitia kwa umakini nione kama kuna SEMBUCHE kwa kuwa sijaliona hilo jina, nitawatafuta.
 
Kuna tofauti gani na NAMAINGO? Kabla ya hii zisha tokea nyingine zaidi ya 4 za Malengo kama haya na zote zimepiga pesa zimepita hivi
 
Kuna tofauti gani na NAMAINGO? Kabla ya hii zisha tokea nyingine zaidi ya 4 za Malengo kama haya na zote zimepiga pesa zimepita hivi
chunguza kwa umakini kama Anna Temu & YZ wamo kweli basi ni mikono salama mkuu.
 
Vijana wengi wa Tanzania tuna shida kubwa katika bongo zetu. Tumegeuka kuwa jamii ya kulaumu na kulalamika badala ya kuchukua hatua.Tunapenda urahisi. Tunasahau kuwa zama zimebadilika. Hatufikirishi vichwa vyetu kujaribu kutumia japo sehemu ndogo ya elimu tuliyoipata chuoni kutafuta fursa za kukamata.

Badala yake tumekaa tukibweteka tukiamini siku moja tutapata kazi ya ndoto zetu huku siku zikizidi kuyoyoma bila mafanikio. Tumekuwa mizigo kwa wazazi wetu badala ya kuwa msaada. Hakuna mawazo mapya tunayotoa. Zaidi tunatamani utanashati bila kuwa na pesa mfukoni. Kazi za kuchafuka hatuzitaki tena hata kama zinatengeneza pesa kiasi gani. Usomi wetu umetufanya tuchague kazi.

Kijana asiyeenda shule, unakuta ana uwezo mkubwa zaidi wa kutengeneza pesa, kuliko msomi aliyehitimu chuo kikuu. Kijana asiyefika chuo kikuu hachagui kazi na vilevile yuko tayari kumtumia msomi kuuliza kitu asichokijua, lakini msomi yeye kwa upande wake hayuko tayari kujifunza kutoka kwa kijana asiyebahatika kufika chuo kikuu.

Tuna tatizo kubwa sana. Vijana wengi tumekosa mawazo mapya ya Ujasiriamali. Bongo zetu zimelala. Hatuoni fursa mpya pamoja na kwamba fursa hizo zimejaa tele mtaani. Tunahitaji kufunguliwa vichwa vyetu na macho ili tuweza kuondolewa tongotongo zinazotufanya tushishindwe kuona fursa.

Changamoto ya kushindwa kuona fursa haiwakabili tu vijana wasomi waliyohitimu vyuo mbalimbali pekee yao bali hata wazee wetu waliyostaafu kutoka kwenye utumishi wa umma au sekta binafsi nao wanakabiliwa na tatizo hili.

Utastaajabu kumwona mstaafu namna anavyohangaika mtaani kuyakabili maisha yake mapya. Hawezi kufanya kazi nyingine zilizo nje ya fani yake. Matokeo yake baada ya kustaafu utumishi wake, anakuwa hana uwezo tena wa kuratibu na kusimamia mradi utakaompatia pesa na kumwezesha kuishi maisha yanayofanana na yale aliyokuwa akiyaishi alipokuwa kazini.

Mstaafu anaishi maisha ya ajabu kabisa pamoja na kwamba, alipatiwa mafao yake yote na mfuko wake wa hifadhi ya jamii. Amekosa elimu ya ujasiriamali. Pesa za mafao yake ya kustastaafu, anaingiza kwenye miradi mfu. Matokeo yake anapata anguko kubwa lisilo kuwa na mfano.

Lakini yote hii ni kwa sababu kulikuwa hakuna taasisi au watu waliyojitoa sawasawa kunoa bongo za watu wengine ili wawe na uwezo kujitegemea mara baada ya kustaafu au kumaliza viwango mbalimbali vya elimu.

Ushirika wa Wahitimu Wajasiriamali wa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUGECO), kwa upande wao waliliona hili na kuamua kwadhati kabisa kujitoa kuwasaidia wahitimu wa vyuo mbalimbali na vijana wasiyowahitimu ili waweze kujiajiri wao wenyewe katika sekta ya Kilimo Biashara.

Kupitia SUGECO, vijana wamekuwa wakifundishwa stadi mbalimbali za kilimo biashara ikiwemo mbinu bora za kuendesha kilimo cha kisasa, kilimo chenye tija, ufugaji bora, Uongezaji wa thamani wa mazao ya Kilimo na mifugo, Usindikaji wa bidhaa mbalimbali za kilimo, uendeshaji wa mafunzo ya kuwajengea uwezo na kuondoa tongotongo katika bongo za vijana, kuwawezesha vijana wahitimu wa vyuo kuwa na miradi yao binafsi na kupata fursa ya kusimamiwa kwa ukaribu na hatua kwa hatua hadi mradi utakaposimama.

Si hivyo tu bali pia SUGECO wanajishughulisha na utoaji wa ufadhili wa mashamba Kitalu au Greenhouse kama ilivyozoeleka na wengi kwa vijana ili kuwawezesha kuendesha shughuli za kilimo chenye udhibiti wa magonjwa. Kana kwamba haitoshi, SUGECO wanaendesha programu kabambe ya kuwapeleka vijana nchini Israel kushiriki mafunzo kwa vitendo katika sekta ya Kilimo. Kila mwaka kuna kundi la vijana wasiyopungua 30 wanapelekwa Israel.

Ukikaa na vijana waliyopata fursa ya kwenda nchini Israel na ukasikiliza shuhuda zao, utabaini wazi kuwa sisi watanzaia bado hatufanyi kazi kabisa. Tunapoteza muda wetu mwingi kizembezembe. Wenzetu kule wanachunga sana muda wao na kujali zaidi kazi. Kwao siku zote muda huwa huwatoshi kutekeleza majukumu yao, hivyo wanajitahidi kuitumia kila dakika inayopatikana kufanya kitu kinachoonekana. Muda kwao una thamani kubwa sana hivyo haupaswi kuchezewa hata kidogo.

Siku zote waisrael wanaamini kuwa hakuna mtu atakayekufa kwa kufanya kazi. Kwa hiyo ukiwa Israel masaa mengi utayatumia kwa ajili ya kufanya kazi. Siku ya mapumziko kwao ni siku moja tu katika wiki na ni siku ya jumamosi ambayo pia siku hiyo wanaitumia kwa ajili ya kukufanya Ibada.

Kuwa meneja Israel ni tofauti sana na kuwa meneja katika nchi zetu za afrika ambapo meneja anakuwa anaongoza kwa kula bata, kule ukiwa meneja hakuna kula bata, bali meneja unakuwa kama manamba mkuu, unaingia kazini wa kwanza na kutoka wa mwisho na ukiwa kazini hakuna ubosi wewe meneja ndiyo unaokuwa mstari wa mbele kufanya kazi mwanzo mwisho. Hayo ni maelezo kwa ufupi sana kutoka kwa vijana waliyobahatika kwenda huko kwa ajili ya mafunzo kwa vitendo. Mfumo huu wa Israel ndiyo unaotumiwa na SUGECO katika utoaji wa mafunzo ya kilimo kwa vitendo kwa vijana wetu wa Kitanzania.

Mapema mwezi wa kumi mwaka huu, SUGECO kwa kushirikiana na wizara ya kilimo kupitia iliyokuwa Mamlaka ya Uendelezaji wa Bonde la Mto Rufiji (RUBADA) walifanikiwa kuendesha mafunzo ya Mnyororo wa thamani wa Kuku na Sungura katika Kambi ya Vijana ya Kilimo kwa Vitendo katika Kijiji Cha Mkongo wilayani Rufiji. Vijana kutoka maeneo mbalimbali ya nchi yetu walikuja kambini hapo kuhudhuria mafunzo hayo ambayo huendeshwa kwa muda wa wiki mbili kwa kila darasa moja.

Kwa namna mafunzo hayo yalivyoratibiwa na kuendeshwa kwa ustadi mkubwa, kila anayepita kambini hapo bila kujali kiwango chake cha elimu na umri, amekuwa akinolewa vizuri na kumwezesha kutoka na elimu itakayomfanya aweze kujitegemea yeye wenyewe badala ya kusubiri kuajiriwa.

Hadi sasa ni awamu mbili tayari zimeshapita katika kambi hiyo ya vijana ya Mkongo Rufiji. Katika awamu ya pili ya mafunzo yaliyofanyika mwezi wa kumi, nami nilipata fursa ya kuwa mmoja wa wawezeshaji katika semina hiyo na kupitia mafunzo hayo niliweza kuwafundisha vijana mnyororo mzima wa thamani wa kuku pamoja na Sungura.

Katika mafunzo hayo, kwahakika nimejionea kwa macho yangu ni kwa namna gani programu hii ya SUGECO inavyowanufaisha Watanzania.
Kwakweli hizi ni aina ya programu ambazo kimsingi kama nchi tunapaswa kuziunga mkono ili Vijana wetu wapite katika kambi hizo ili waweze kujifunza kilimo kwa vitendo pamoja na stadi mbalimbali zinazotolewa katika kambi hiyo zenye lengo la kuwatengeza vijana wawe sababu ya kujiajiri wao wenyewe na kuajiri wengine.

Mfumo wetu wa elimu haumwezeshi moja kwa moja kijana kupata stadi zitakazomwezesha kujiajiri mwenyewe. Lazima vijana bila kujali kiwango chao cha elimu, wapatiwe aina hii ya mafunzo yanayotolewa na SUGECO ili kuwafanya vijana wetu watamani zaidi kujiajiri badala ya kusubiri ajira za Serikali au mashirika.

Nakumbuka katika mafunzo hayo mbali na kujifunza mnyoro wa thamani wa kuku na Sungura, masomo yaliyoendeshwa kwa nadharia na vitendo, pia washiriki waliweza kujifunza kilimo cha mbogamboga na utengenezaji wa bidhaa mbalimba kama vile dawa za chooni, sabuni, shampoo, mishumaa, mafuta ya kupakaa ya mgando pamoja na nguo aina ya batiki.

Lakini somo jingine lililofundishwa siku hiyo ni somo la kubadilisha mtazamo wa kijana kutoka kwenye kasumba ya kutaka kuajiriwa na kupewa mbinu mpya zitakazo msaidia kijana aweze kujiajiri wenyewe na kusimamia mradi wake kikamilifu.

Mkurugenzi wa SUGECO Bwana Revocatus Kimario wakati anatoa salamu zake za jioni kwa washiriki kabla ya kuwasilisha mada yake ya *Namna ya Kumuhudia Mteja,* alianza kwa nukuu ya mwalimu wa kubadilisha mtazamo wa vijana Mr Masimba *“a mindset changer”* iliyosema “Tusaidiane kuondoa kutu vichwwani kwetu.” Nukuu hii ukiitafakari vizuri utaona ni kwa namna gani ilivyojaa ukweli, vichwa vyetu vina kutu nyingi, tunahitaji kusaidiwa kuondolewa.

Bwana Kimario aliniendelea kuwatanabaisha vijana kwa kuwaambia kuwa “tukiwa hapa (kambini) degree zako zote tunaziweka pembeni kwasababu degree zako hazina maana sana kama hauna uwezo wa kutengeneza pesa.” Kimsingi Bwana Kimario alisisitiza sana ubunifu na kujiongeza. Katika hili alisema “aliyejaribu na akashindwa, anafaida kubwa kuliko asiyejaribu. Kufeli haina maana umeshindwa bali utatafuta namna nyingine ya kujaribu.” Bwana Kimario katika kuongezea uzito hili, alimnukuu Bwana Jeseph Chilton Pearce aliyeelezea thamani ya ubunifu aliyosema, to live a creative life we must lose our fear of being wrong.” Kwa taafsiri isiyo rasmi akimaanisha kwamba kuishi maisha ya ubunifu kunahitaji kuondoa hofu ya kukosea.

Baada ya utangulizo huo aliyoutoa kwa washiriki, Mkurugenzi aliendelea na somo lake la *Namna ya Kumuhudumia Mteja.* Somo lilikuwa nzuri na kila mshiriki alivutiwa nalo. Laiti nafasi ingeruhusu ningeweza kulidadavua somo hilo kwa upana wake kadiri ya mafundisho yalivyotolewa Mkurugenzi ndugu Kimario.

SUGECO imeundwa na vichwa vinavyojua kufikiria. Vinavyojua kiini cha tatizo la ajira kwa vijana na namna ya kuondoa tatizo hilo kupitia mafunzo ya kilimo Biashara. Kwahiyo wahenga walisema usione vyaelea, vimeundwa. Mambo yote mazuri yanayofanywa na SUGECO ni matokeo ya uratibu mzuri wa watu wafuatao: Kuna Dokta Anna Temu, ambaye ni Mwenyekiti wa Bodi na Dokta Flugence Mishili Makamu mwenyekiti. Kwenye kamati ya utalaam na ufundi kuna Dokta Daniel Ndyetabula, Dokta Betty Waized, na Dokta Felix Nandonde. Kwenye utawala utakutana na Bwana Revecatus Kimario, ambaye ni Mkurugenzi wa SUGECO, Bwana Joseph Masimba Mratibu wa Miradi, Bwana Ayubu E. Mundekesye meneja wa Mafunzo, Dickson Alex Mseko Meneja wa shamba na Prekseda Melkior kaimu meneja wa shamba.

Vichwa vyote hivyo kwa pamoja ndivyo vilivyotengeza wajasiriamali vijana wengi nchini katika sekta ya kilimo. Kila kona ya nchi ukipita utakutana na vijana wengi waliyonolewa na SUGECO wakishughulika na mafundo mbalimbali katika mnyororo wa thamani wa kilimo. Kuna wale wanaolima alizeti na kuchakata mafuta, kuna wanaozalisha asali, kuna wanaolima mbogamboga kupitia shamba kitalu, kuna wanaozalisha mbegu za viazi lishe na kulima viazi. Kuna waliyosaidiwa kuanzisha viwanda mbalimbali vya usindikaji. Kuna wanao jishughulisha na ufugaji wa kuku, Samaki na Mifugo mingine. Ukipita SUGECO kwahakika lazima utabadilika kifikra na kimtazomo.

Kwa ajili ya kuwafikia vijana wengi nchini ilifaa sana kama Wizara ya Kilimo na Ushirika, Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi pamoja na Wizara ya Vijana, kazi na ajira wangeangalia namna bora ya kushirikiana na SUGECO ili kuanzisha kambi mbalimbali za mafunzo ya kilimo kwa vitendo na kubadilisha fikra na mitazamo ya vijana. Kwa kufanya hivyo tutajenga taifa la kutenda badala ya kuwa taifa la kulalalamika. Na mwishowe matokeo chanya ya kiuchumi kwa vijana wetu na nchi kwa ujumla yangeonekana hasa katika kipindiki hiki ambacho nchi inaelekea kwenye uchumi wa viwanda.

Aman Ng'oma
Mkurugenzi Mtendaji
Kinasoru East Africa Tanzania Ltd
Info@kinasoruea.co.tz or amanngoma@gmail.com
0767989713 or 0715989713
Nduka Street, Chamwino Bonanza
Dodoma
*TANZANIA.*
Post za hivi kwangu mimi ni zaidi ya zawadi yoyote kwa kuwa zinaniongezea hali ya kuendelea kutafiti ni kwa nini jamii yangu ipo kama ilivyo!
Ahsante sana mtoa uzi huu.
 
Watu kama hawa huwa siwaamini tz bado mkombozi wa kuwasaidia wanaojishugulisha na Kilimo bado kupatikana hao wanaojitokeza ni makanjanja.......
Bora mkulima upambane usimame mwenyewe tu

Ova
 
Ukiitwa kwenye fursa jua wewe ndio fursa.Nachoshangaa unakuta wanaoendesha semina hawawezi kuzalisha bidhaa za kulisha mtaa kwa Mwaka mzima.Ujanja ujanja tu
 
SOKO LA UHAKIKA LA VIAZI LISHE, CHANGAMKIA UPESI, LISIKUPITE!

Katika kuwajali wakulima wetu na kutambua mahangaiko yao kwenye masoko ya mazao wanayoyazalisha, kampuni ya kinasoru East Africa Tanzania Ltd imepata soko la uhakika la kuuza viazi lishe nje ya nchi kupitia wakala wao aliyepo hapa nchini. Wakati naitambulisha kwa mara ya kwanza fursa hii mpya katika mada yangu ya “Fursa Katika Kilimo cha Viazi Lishe, Tuchangamkieni Upesi”, watu wengi walikuwa na shauku kubwa ya kutaka kujua kwa undani juu ya kilimo hiki lakini vilevile walitilia shaka uwepo wa soko la uhakika la kuuzia aina hii ya viazi.

Kwa upande wangu, nilijitahidi sana kuwatoa shaka juu ya tatizo la soko na kuwahakikishia kuwa soko la viazi lishe lipo na tena ni la uhakika, kuanzi mbegu zenyewe zile za F1 na hata viazi vyake. Nilifafanua zaidi kwa kuwaambia kuwa viazi lishe licha ya faida nyingine nyingi zinazotoa, ni chakula kitamu na chenye kupendwa sana. Na pili mwonekano wa viazi hivyo umekuwa kivutio kikubwa kwa watu wengi na kufanya visiwe na upinzani sokoni.

Mathalani, ukivuna leo tani moja ya viazi lishe vyako na ukavipeleka sokoni Jijini Dodoma kwenye soko la Maisha Plus, soko la uuzaji wa Matunda, Mbogamboga, Samaki, Ndizi na Mazao mengine jamii ya mizizi, na ikatokea kule sokoni kuna wakulima wengine wamekutangulia wenye viazi vitamu vya kawaida, pamoja na kwamba wote mna viazi vitamu, lakini wewe mwenye viazi lishe utauza mapema zaidi na kuwaacha wakulima wenzako waliyokutangulia.

Kimsingi Viazi lishe ni chakula kizuri, kitamu na chenye Vitamin A kwa wingi ambayo ni muhimu sana kwa akinamama wajawazito, wanaonyonyesha, watoto na wazee katika kusaidia uonaji wa macho, uimarishaji wa kinga ya mwili, ukuaji na kufanya maendeleo bora ya mtoto.

Watu wengi wamekuwa wakiutumia unga wa viazi lishe kama moja ya malighafi au viwambajengwa kwa ajili ya kutengenezea unga lishe wenye virutubisho mbalimbali muhimu kwa ajili ya matumizi ya makundi tofauti tofauti ya watu kama ilivyoanisha hapo juu.

Umaarufu wa unga wa viazi lishe siku za hivi karibuni umeongezeka maradufu katika jamii yetu na kusababisha watu wenye maduka makubwa kama supermarket kuutafuta unga huo kwa udi na uvumba ili kuuza kwenye maduka yao. Ndiyo maana sasa hivi siyo ajabu tena kukuta unga huu ukiuzwa kwenye aina hiyo ya maduka. Umuhimu wa viazi lishe unaoneka zaidi kutokana na kuwa na matumizi mengi.

Unga wa viazi lishe unaweza kuutumia kama ambavyo unautumia unga wa ngano kwa ajili ya mapishi mbalimbali. Unaweza kutumia unga wa viazi lishe kwa kupikia keki, maandazi, ugali, chapati na Biskuti. Aidha, viazi vyake unaweza kutumia kwa ajili ya kutengenezea Krips, Chips ama kuchemshwa kawaida au kukaangwa na kuliwa kama vitafunwa asubuhi wakati wa kupata stafutahi.

Kwa jinsi viazi hivi vilivyo na matumizi mapana, hatunabudi kukiinua zaidi kilimo hiki ili kiwe dira na mkombozi kwa mkulima katika kuinua kipato chake binafsi, kaya na taifa kwa ujumla. Kupitia viazi lishe maisha ya mkulima yanaweza kuboreka sana.

Katika jitihada zetu za muda mefu, Kinasoru East Africa Tanzania Ltd, imefanikiwa kupata soko la uhakika la kuuzia viazi lishe. Soko hilo linahitaji tani 300 sawa kilo 300,000 kwa mwezi. Soko tulilopata ni soko endelevu na ni kubwa. Mkulima mmoja au kikundi cha wakulima wachache hawawezi kumudu kutoa kiasi cha viazi kinachotakiwa.

Kwahiyo, tunahitaji wakulima wengi zaidi ambao tutaingia nao mkataba kwa ajili ya kuzalisha viazi hivyo. Na kwamba mara baada ya viazi kukomaa, mkulima atapaswa kuvipeleka viazi hivyo Dar es salaam katika ghala maalum liloandaliwa kwa ajili ya kufanya ukusanyaji wa viazi hivyo. Kama itapatikana njia nyingine bora ya kukusanya viazi hivyo kutoka kwenye mashamba ya wakulima moja kwa moja ili kurahisisha usafirishaji, basi wakati utakapofika tutawajulisha njia hiyo.

Kwa kuzingatia mzigo mkubwa unahitajika, kinasoru East Africa Tanzania Ltd, imeshindwa kuingia mkataba wa jumla na mteja wetu anaohitaji viazi hivyo kutokana na kampuni yetu kushindwa kumudu kuzalisha kiasi cha viazi kinachohitajika. Lakini hata hivyo, hadi sasa bado hatuna wakulima wa uhakika tunaowafahamu wanajishughulisha na uzalishaji wa zao hilo na wenye uwezo wa kutoa tani 300 kwa mwezi.

Ikiwa ndivyo, tukaona si vyema tukaingia tamaa kwa kujifanya tunamudu kuzalisha viazi hivyo ilihali uwezo wetu ni mdogo, ndio maana tukaamua, kwa makusudi kabisa, fursa hii muhimu tuilete kwenu wakulima wenye utayari wa kufanya kazi hii ili tuweze kunufaika kwa pamoja kupitia soko hili muhimu.

Kwa upande wetu sisi kama Kinasoru East Africa Tanzania Ltd, tutabaki kwenye kusambaza mbegu bora za F1 zenye kumhakikishia mkulima mavuno mengi kwa ekari lakini vilevile tutahakikisha kuwa kila mkulima ambaye ataingia katika programu yetu hii anapata usaidizi wa kutosha wa kiufundi katika uendeshaji wa mradi wake wa kilimo ili kuhakikisha kuwa viazi vinavyozalishwa vinakidhi ubora unaotakiwa katika soko.

Mkulima anayehitaji kujiunga katika programu hii, atapaswa kulipia ada kwenye kampuni yetu ya Kinasoru East Africa Tanzania Ltd, kwa ajili ya kugharamia ushauri wa kiufundi pamoja na kuunganishwa kwenye soko. Ushauri wa kiufundi unalenga kuhakikisha kuwa mkulima wetu anazalisha viazi bora vyenye kukidhi viwango kwa soko la kimataifa.

Aina viazi lishe vinavyohitajika kwa sasa katika soko tulilonalo ni Kabode, Mataya, Ijumla na Jewery. Na kwa bahati nzuri sana mbegu zote hizi tunazo shambani kwa hivyo ni jukumu lako sasa wewe mkulima kuhakikisha kuwa unapata moja kati ya mbegu hizo ili uendane na mahitaji ya soko.

Aidha, kama wewe ni mkulima wa siku nyingi wa viazi lishe na katika miezi mitatu uliyopita uliweza kupanda aina moja wapo kati ya aina nilizotaja hapo juu na kwamba viazi vyako kwa sasa vimekomaa na viko tayari kwenda sokoni lakini kwa bahati mbaya sana, huna soko na una ekari kuanzia mbili na kuendelea, tafadhali usikae kimya, wasiliana nasi haraka ili tuweze kuunganisha kwenye soko letu.

Bei ya jumla ya kununulia viazi vilivyokomaa ni tsh 800 kwa kilo moja na kwa gunia lenye ujazo wa kilo 100 litachukuliwa kwa tsh elfu 80. Katika mradi huu mkulima hatakopwa. Mzigo utakapofikishwa katika kituo kikuu kilichoandaliwa cha ukusanyaji, utakaguliwa kuona kama uko sawa kiubora, utapimwa uzito wake na mwisho mkulima ataweza kulipwa kadiri ya kilo alizoleta.

Tunafahamu kuwa kuna maeneo ya nchi yetu kwasasa bado kuna mvua za masika zinaendelea kunyesha lakini kuna maeneo mengine mvua hizo zimeishia. Kwa watu wanaoishi katika maeneo ambayo bado mvua za masika zinaendelea kunyesha na kuna wale ambao wako katika maeneo ambayo mvua za masika zimeishia lakini wanamudu kuendesha kilimo kwa njia ya umwagiliaji, na wangependa kuingia katika programu hii, milango iko wazi. Kila mtu anakaribishwa kuweza kushiriki katika mradi huu wenye manufaa makubwa.

Kinasoru East Africa Tanzania Ltd inatamani kuona mkulima akinufaika kupitia kilimo chake. Kama utahitaji maelezo zaidi ya ufafanuzi tafadhali usisite kuwasiliana nasi kupita anuani zetu hapo chini. Hima hima wakulima! Twende pamoja, twende shambani tukalime.

Aman Ng’oma
Mkurugenzi Mtendaji
Kinasoru East Africa Tanzania Ltd
New office location: Msalato Bible
Te: +255767989713, +255715989713 & +255786989713
Email: amanngoma@gmail.com
Facebook Page: Kinasoru East Africa Tanzania Ltd
DODOMA, TANZANIA.
 
Back
Top Bottom