Sudani wanakitafuta kilichowapata walibya?

Peter Agostino

Senior Member
Sep 23, 2016
105
226
Kinachoendelea Sudani wengi wanaweza wakafikiria kwamba Jeshi linastahili lawama, ni kweli yaliyotokea yanahuzunisha, hayawezi kufumbiwa macho wala kutetewa lakini swali ni je, nani wa kulaumiwa kati ya Jeshi na Waandamanaji wanaotaka kupewa madaraka ya kusimamia nchi?

Itakumbukwa hata Libya ilikuwa ni hivyohivyo, waandamanaji walidai kutaka kuuondoa utawala wa kidikteta wa Muammar Gaddafi lakini nyuma ya pazia kumbe wananchi hao waandamanaji hawakuwa wamejiandaa wala kujipanga kuitawala nchi na isitoshe kumbe, katika msafara wa mamba kenge nao walikuwemo. Kulikuwa na watu wasioitakia mema kabisa Libya, watu wenye misimamo mikali wanaoendelea kuihangaisha Libya mpaka kesho.

Ikiwa Wanajeshi wa Sudani Walikubali kumuondoa bosi wao, Ommar Al Bashir, waandamanaji walitakiwa kuwa wavumilivu na kukubali kufanya kazi na jeshi mpaka pale hali itakapokuwa shwari na raia kukabidhiwa madaraka kwa amani. Ikiwa Jeshi lilikuwa na nia mbaya jinsi raia wanavyofikiri sidhani kama wangekubali bosi wao wa muda mrefu kupinduliwa.

Na Umoja wa Africa sidhani kama wanasoma alama za nyakati hata kidogo kwa kukimbilia kuiwekea vikwazo Sudani badala ya kushughulikia mzizi wa fitina. Libya walinyamaza hivyohivyo hadi Gadafi akauwawa kama paka kisha hadi leo hamna msaada wowote wa maana wananchi wa Libya wanaoupata zaidi ya kukumbuka maziwa na asali enzi za Gadafi. Waafrika tufike mahali matatizo yetu tuyatatue wenyewe kwa subira kama Rais wa Ethiopia anavyoonyesha mfano huko Sudani sasa, tusisubiri tena mpaka Marekani na Uingereza waje kufanya kama walivyofanya Libya.

Peter Augustino ni mwandishi katika Blog ya "JIFUNZEUJASIRIAMALI"
 
Peter kwani tatizo la kuacha wananchi wajitawale ni nini?

Mbona point ni ndogo sana hapa, kazi ya jeshi ni kulinda mipaka ya nchi kwa kupigana vita ikibidi na kazi ya wanasiasa ni kuongoza kisiasa, sasa kwanini kila mtu asifanye kazi yake mkuu. Shida ya majeshi ya afrika kwa kuwa yana silaha yanadhani yanaweza kufanya kila kitu. Katika karne hii kweli Peter unaona nchi inaongozwa na jeshi na unaona sawa?

Unaona sawa ikitokea vita wanasiasa wawakataze wanajeshi kwenda kupigana ili waende wao, itakuwa sawa?

Wanasiasa wamesomea na wamejiandaa kutawala wanajeshi wamesomea na wamejiandaa kulinda mipaka ya nchi kutoka kwa maadui wa nje fullstop!
 
Waandamanaji hawakujiandaa kutawala. Je, jeshi lilijiandaa kutawala!
Ukizingatia kuwa ni jeshi chini ya Albashiri ndilo lilikuwa madarakani muda wote, Wananchi hawa walipaswa kuwa na subira kidogo na kuwaona Majenerali wa jeshi waliokwishaonyesha nia njema kwao kwamba mwisho wa siku wangewakabidhi tu madaraka. Sidhani kama kitendo cha kuandamana "non stop" kama kilikuwa ni cha busara.
 
Peter kwani tatizo la kuacha wananchi wajitawale ni nini?

Mbona point ni ndogo sana hapa, kazi ya jeshi ni kulinda mipaka ya nchi kwa kupigana vita ikibidi na kazi ya wanasiasa ni kuongoza kisiasa, sasa kwanini kila mtu asifanye kazi yake mkuu. Shida ya majeshi ya afrika kwa kuwa yana silaha yanadhani yanaweza kufanya kila kitu. Katika karne hii kweli Peter unaona nchi inaongozwa na jeshi na unaona sawa?
Si sawa Kambaku, nakubaliana na wewe kuwa kila upande unapaswa kutekeleza majukumu yake, lakini ukumbuke pia kila jambo linahitaji mchakato fulani na muda wa kulitekeleza, haiwezekani tu from no where ukakabidhi madaraka kwa kundi la raia usiofahamu hata wamejipangaje. Ndio maana nikajaribu kuitumia Libya kama mfano. Sasa bora kipi? Libya ya Gadafi au Libya ya Magaidi wa IS? Tatizo sisi Waafrika tunadhani kwamba Uhuru hauna mipaka yeyote, ni sawa kama tulivyofikiri enzi za ukoloni kwamba mkoloni akitoka tu mwafrika matatizo yoote yangekwisha, matokeo yake hadi leo baadhi ya Waafrika bado tunalala kwenye nyumba za tembe karne ya 21!
 
Umeandika point tupu,Mungu akubariki,wewe na kizazi chako cha sita hadi kumi.Yaonyesha wewe ni msomi wa uhakika,kama una degree,basi umeipata kihalali kabisa.
Kinachoendelea Sudani wengi wanaweza wakafikiria kwamba Jeshi linastahili lawama, ni kweli yaliyotokea yanahuzunisha, hayawezi kufumbiwa macho wala kutetewa lakini swali ni je, nani wa kulaumiwa kati ya Jeshi na Waandamanaji wanaotaka kupewa madaraka ya kusimamia nchi?

Itakumbukwa hata Libya ilikuwa ni hivyohivyo, waandamanaji walidai kutaka kuuondoa utawala wa kidikteta wa Muammar Gaddafi lakini nyuma ya pazia kumbe wananchi hao waandamanaji hawakuwa wamejiandaa wala kujipanga kuitawala nchi na isitoshe kumbe, katika msafara wa mamba kenge nao walikuwemo. Kulikuwa na watu wasioitakia mema kabisa Libya, watu wenye misimamo mikali wanaoendelea kuihangaisha Libya mpaka kesho.

Ikiwa Wanajeshi wa Sudani Walikubali kumuondoa bosi wao, Ommar Al Bashir, waandamanaji walitakiwa kuwa wavumilivu na kukubali kufanya kazi na jeshi mpaka pale hali itakapokuwa shwari na raia kukabidhiwa madaraka kwa amani. Ikiwa Jeshi lilikuwa na nia mbaya jinsi raia wanavyofikiri sidhani kama wangekubali bosi wao wa muda mrefu kupinduliwa.

Na Umoja wa Africa sidhani kama wanasoma alama za nyakati hata kidogo kwa kukimbilia kuiwekea vikwazo Sudani badala ya kushughulikia mzizi wa fitina. Libya walinyamaza hivyohivyo hadi Gadafi akauwawa kama paka kisha hadi leo hamna msaada wowote wa maana wananchi wa Libya wanaoupata zaidi ya kukumbuka maziwa na asali enzi za Gadafi. Waafrika tufike mahali matatizo yetu tuyatatue wenyewe kwa subira kama Rais wa Ethiopia anavyoonyesha mfano huko Sudani sasa, tusisubiri tena mpaka Marekani na Uingereza waje kufanya kama walivyofanya Libya.

Peter Augustino ni mwandishi katika Blog ya "JIFUNZEUJASIRIAMALI"
 
Kuna watu humu duniani,Mungu amewapa kipaji cha hali ya juu,kama muandishi wa uzi huu,ukiusoma mwanzo hadi mwisho,unaona point za maana tupu.Huu ndio uzi wa mwaka,na ungefaa upewe tunzo ya kimataifa,ya uandishi bora.
 
Na hapa ndo panapoonesha ni kwa kiasi gani wanànchi wa Africa ni vichaa ama mazuzu .. Hamjui nn mnataka nn na lini , wanajidanganya kwa kujiangalia kwenye vioo eti wao ni sasa na Britain, US, Germany n.k. Mnaponzwa na tamaa za kupitiliza
 
Kinachoendelea Sudani wengi wanaweza wakafikiria kwamba Jeshi linastahili lawama, ni kweli yaliyotokea yanahuzunisha, hayawezi kufumbiwa macho wala kutetewa lakini swali ni je, nani wa kulaumiwa kati ya Jeshi na Waandamanaji wanaotaka kupewa madaraka ya kusimamia nchi?


Itakumbukwa hata Libya ilikuwa ni hivyohivyo, waandamanaji walidai kutaka kuuondoa utawala wa kidikteta wa Muammar Gaddafi lakini nyuma ya pazia kumbe wananchi hao waandamanaji hawakuwa wamejiandaa wala kujipanga kuitawala nchi na isitoshe kumbe, katika msafara wa mamba kenge nao walikuwemo. Kulikuwa na watu wasioitakia mema kabisa Libya, watu wenye misimamo mikali wanaoendelea kuihangaisha Libya mpaka kesho.


Ikiwa Wanajeshi wa Sudani Walikubali kumuondoa bosi wao, Ommar Al Bashir, waandamanaji walitakiwa kuwa wavumilivu na kukubali kufanya kazi na jeshi mpaka pale hali itakapokuwa shwari na raia kukabidhiwa madaraka kwa amani. Ikiwa Jeshi lilikuwa na nia mbaya jinsi raia wanavyofikiri sidhani kama wangekubali bosi wao wa muda mrefu kupinduliwa.


Na Umoja wa Africa sidhani kama wanasoma alama za nyakati hata kidogo kwa kukimbilia kuiwekea vikwazo Sudani badala ya kushughulikia mzizi wa fitina. Libya walinyamaza hivyohivyo hadi Gadafi akauwawa kama paka kisha hadi leo hamna msaada wowote wa maana wananchi wa Libya wanaoupata zaidi ya kukumbuka maziwa na asali enzi za Gadafi. Waafrika tufike mahali matatizo yetu tuyatatue wenyewe kwa subira kama Rais wa Ethiopia anavyoonyesha mfano huko Sudani sasa, tusisubiri tena mpaka Marekani na Uingereza waje kufanya kama walivyofanya Libya.


Peter Augustino ni mwandishi katika Blog ya "JIFUNZEUJASIRIAMALI"
Samaki hajui thamani ya maji mpaka akishatolewa majini ndiyo hujua.
 
Back
Top Bottom