Succession politics: JK to anoint a Zanzibari in 2015 (Kiswahili version)

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
219,470
911,173
Kuna mambo manne ambayo yananifanya nitofautiane na wengi ambao wamewatabiria akinamama wa bara Uraisi 2015 au hata mmbara mwingineyo yeyote yule. Kwa mtazamo wangu hili kamwe halitatokea. kwa maono yafuatayo.....

Matukio haya ndiyo yanayoniongoza kusema hivyo;-

a) Waziri wa Nchi Ofisi ya Raisi masuala ya Muungano, Mheshimiwa Seif Khatibu alikuwa wa kwanza kulipiga hili baragumu kuwa hii sasa ni zamu ya Mzanzibari kuwa Raisi baada ya Kikwete...............Khatibu ni mtu ambaye yupo karibu sana na JK na kwa hiyo ni rahisi sana kujua kauli hiyo ilitokea wapi...............Kwa maoni yangu Khatibu alitumiwa na JK kupima upepo wa kisiasa unavuma vipi.............

b) Maamuzi ya makusudi ya kupendelea makundi maalumu yaliyofanywa na Kamati Kuu ya CCM chini ya uongozi wa JK ndani ya CCM katika kipindi cha miaka mitano iliyopita..................Haya ni pamoja na kuwazibia wabara kugombea uenyekiti wa UVCCM na kumnufaisha mzenji....Masauni.ambaye hata hivyo alikwenda kuwadhalilisha kwa kukosa sifa za kuwa kijana wa miaka 35 au chini ya hapo na kuwa na vyeti vya kughushi vya umri wake wa kuzaliwa............................

Vile vile uteuzi wa wanawake watatu kugombea nafasi ya uspika na kuyaondoa majina yote ya wanaumme kwa visingizio vya gender-balance...........Matukio haya mawili yaashiria udikteta ndani ya CCM kuchukua sura ifuatayo mwaka 2015:-

Pamoja na kuwa CC ya CCM itaruhusu wagombea wote kutoka kila kona ya nchi kugombea Uraisi lakini majina yatakayorudi ni matatu tu kutoka visiwani kwa minajili ya kile ambacho JK atasema ni kuwaenzi wazanzibari..................na ya kuwa bila ya kuchukua hatua za makusudi hawatakuwa na nafasi za kutoa Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania....................

Usishangae kama nyuso mpya za visiwani zitaingizwa kwenye baraza la mawaziri litakalotangazwa hivi karibuni kwa minajili ya kuwajenga wazanzibari fulani fulani........kwa lengo la kuwaongezea sifa za kuukwaa uraisi.........na wengi wao watakuwa ni vijana ili huko mbele waseme tena hawa mbona ni vijana haswa na wengi tutakubali hizo ghiliba na kushangilia bila ya kujua malengo haswa nini............

Hivyo mkakati wa JK katika ni nani kumkabidhi nchi wabara andikeni mmeumia..................labda kura zisichakachuliwe na mmbara atatokea upinzani kuliongoza taifa hili..................

Lakini hilo nalo JK atahakikisha kamwe halitokei kwa sababu atakwamisha mabadiliko yoyote katika muundo wa NEC hadi baada ya uchaguzi wa 2015 ili kujenga mazingira ya mzanzibara aweze kutumia idara ya usalama wa taifa na NEC kutwaa madaraka isivyo halali na kinyume na sheria..............kama ambavyo yeye kajisimika madarakani bila ridhaa ya wapigakura na hivyo kuvunja katiba ya nchi hii.............

Habari njema ni kuwa CCM itagawanyika vipande vitatu vya kupinga maamuzi ya CC na upinzani utanufaika sana na wageni kutoka CCM.........na hapo kauli ya Baba wa taifa itakuwa imetimia ya kuwa ili CCM ishindwe kutwaa madaraka ni lazima ivunjike vipande vipande yenyewe.............................

Hivyo ukombozi wa kweli wa mtanzania unategemea sana JK afanye makosa haya comes 2015...................Eeeeeeeeeeeeeeehh mwenyezi Mungu mwongoze huko gizani nasi tupate unafuu wa kiuchumi na shida hizi zipungue za kudhulumiwa na mafisadi wa CCM......................

Haya ni maono yangu na ya kwako je..................waonaje mustakabali wa Taifa in 2015?
 
Back
Top Bottom