Salary Slip
JF-Expert Member
- Apr 3, 2012
- 47,013
- 144,371
Baada ya mkutano wa Mbowe na waandishi wa habari, kinachofuata ni wale vibaraka kuja na kauli za vitisho, kiburi, ubabe na majigambo katika kumjibu Mbowe.
Kauli ya Mbowe sasa ndio itakuwa mtaji wa watu kutafuta vyeo na uteuzi badala ya wao kutafakari na kukiri katika nafsi zao kuwa Boss wao ndio chanzo cha kumfanya Mbowe na wenzake waishiwe uvumilivu na kufikia kusema aliyoyasema leo hii.
Kitendo cha kuwafunga jela na kuwadhalilisha kama walivyolalamika,ndio kimewafanya wafikie ukomo wa uvumilivu na sasa wako desperate kufanya lolote kwa gharama yoyote na mimi sitowalaumu kwa lolote watalofanya na matokeo yake kwani ndio kilichokuwa kinatafutwa.
Hata hivyo, Corona ndio inaweza ikaepusha balaa hili japo kwa muda kwani wapinzani hawawezi kushinikiza mikutano na maandamano iwapo serikali itapiga marufuku mikusanyiko kwani hata wao wanaelewa watakosa support iwapo kutakuwa na mazingira kama hayo.
Pia, Mataifa ya nje yanayopinga huu ukandamizaji nayo yatatumia mwanya huu kutoa support kwa wapinzani hasa pale mabavu ya dola yatakapotumika bila busara.
Nimalizie kwa kusema: Mungu huwa na makusudi yake kwa kila jambo.
Kauli ya Mbowe sasa ndio itakuwa mtaji wa watu kutafuta vyeo na uteuzi badala ya wao kutafakari na kukiri katika nafsi zao kuwa Boss wao ndio chanzo cha kumfanya Mbowe na wenzake waishiwe uvumilivu na kufikia kusema aliyoyasema leo hii.
Kitendo cha kuwafunga jela na kuwadhalilisha kama walivyolalamika,ndio kimewafanya wafikie ukomo wa uvumilivu na sasa wako desperate kufanya lolote kwa gharama yoyote na mimi sitowalaumu kwa lolote watalofanya na matokeo yake kwani ndio kilichokuwa kinatafutwa.
Hata hivyo, Corona ndio inaweza ikaepusha balaa hili japo kwa muda kwani wapinzani hawawezi kushinikiza mikutano na maandamano iwapo serikali itapiga marufuku mikusanyiko kwani hata wao wanaelewa watakosa support iwapo kutakuwa na mazingira kama hayo.
Pia, Mataifa ya nje yanayopinga huu ukandamizaji nayo yatatumia mwanya huu kutoa support kwa wapinzani hasa pale mabavu ya dola yatakapotumika bila busara.
Nimalizie kwa kusema: Mungu huwa na makusudi yake kwa kila jambo.