Subaru mnatufilisi, Gari zinakunywa mafuta kama zinameza!

Kwaiyo uwezo wa forester cross sport ni uleule wa forester STI?
Maana haya matoleo matatu yananchanganya na sielewi ipi konki kati ya forester XT, forester cross sport na forester STI japo kwa bei hizo STI ziko juu sana kuliko hizo nyingine.
Forester STI nyingi manual transmission pia zinakuwa CC 2390 gear 6
 
Dah! ni swali kubwa sana coz ni magari mawili yanayofanana vitu vingi sana kwa upande wa engine kwenye body ndio kunatofauti...
mfano kwenye hayo magari yote kuna mabayo ni manual na Atomatic na pia kuna turbo..

labda tuu... cross sport zimeanzia 2005 hadi na 2008 kwa version ya SG
>>cross sport- ipo yenye turbo na non-turbo
Na xt zimeanza kuanzia 2002 na kuendelea na zina turbo zote ...

so kutokana na swali lako itategemea mapenzi yako yapo upande gani ingawa ikiwa nini nitachagua:-
Cross-sport ambayo ni SG9 STI-- Hapa utafurahia maisha

View attachment 1213648
Vipi kuhusu hii xt ya 2008 ambayo ni SH5
Screenshot_20190830-070952~2.jpeg
 
Vipi kuhusu hii xt ya 2008 ambayo ni SH5
View attachment 1213908
Matoleo haya ni luxury Sana ingawa yana body kubwa lakini ukubwa wa engine ni mmoja yote ni EJ20 na CC1990 pia hata turbocharger ni 2.liter.
Cha kushangaza Yale matoleo ya chini yake Yana uzito Mkubwa tofauti na haya mabox mara nyingi utakuta Yana kg 1400-1470 lakini matoleo ya nyuma uzito wake ni 1450-1500
 
Kwaiyo uwezo wa forester cross sport ni uleule wa forester STI?
Maana haya matoleo matatu yananchanganya na sielewi ipi konki kati ya forester XT, forester cross sport na forester STI japo kwa bei hizo STI ziko juu sana kuliko hizo nyingine.
STI ndio zipo vizuri kuliko zingine zote...
kuna tofauti kati ya forester ya kawaida xt na xt ambayo ni sti... unakuta sti kwenye performance ipo vizuri zaidi..
 
Vipi kuhusu hii xt ya 2008 ambayo ni SH5
View attachment 1213908
Ni gari nzuri kwa mtazamo ingawa bado mpya so kwangu mimi naona sijawa na uzoefu nazo sitaweza kuzungumzia sana..

Ila kwa maneno ya vijiweni(watu walio zitumia) wanasema sio nzuri kama haya matoleo ya nyuma yani... SF na SG, kwamba za 2000 -2008 mwanzoni ni imara zaidi na zinaimili mikiki mikiki ya subaru..
nadhani mwenyewe umeona hata hazifanani na matoleo ya nyuma, na naskia magari haya yametengenezwa hasa kwa kuzingatia masoko ya marekani na ulaya.
 
kiujumla SUBARU FORESTER ni magari mazuri sana kwa matumizi yote kinachowachanganya watu ni kwamba gari aina moja ila zipo katika magroup mengi..
forester :- sf 5,--unakuta ipo yenye turbo na non turbo(chips kavu),
>>>pia unakuta kuna STI,
>>>zipo 2.0 na 2.5
>>>zipo version za Japan na version za Kimarekani
forester :- x20-- hili toleo ni zile ambazo hazina turbo.
forester :- cross-sport--SG5-- hapa unakuta ipo yenye turbo na non turbo(chips kavu),
>>>pia unakuta kuna STI,
>>>zipo 2.0 na 2.5
>>>zipo version za Japan na version za Kimarekani
>>>Pia kuna SG9-hizi huwa ni manual na 6speed na ni STI +TURBO {HII NI GARI NZURI SANA KWENYE KUNDI HILI}
matoleo hayo ndio yaliotamba sana kutoka 2000-2008.
kuanzia 2008 ndio zikaanza hizi SH forester za tofauti ambazo mnaziona zinafanana na kama RAV 4 au matoleo a toyota...
 
Nimetumia subaru forester kwa zaidi ya miaka 12 sijawahi kuona ulaji huu something wrong with your fuel system
Mweleze, mwenyewe nimetumia subaru mwaka wa kumi huu cjaona ulaji huo. Mambo mawili yanaweza changia ulaji mbaya wa mafuta. Service hasa upande wa air cleaner element na uendeshaji mbaya (rough driving)
 
Matoleo haya ni luxury Sana ingawa yana body kubwa lakini ukubwa wa engine ni mmoja yote ni EJ20 na CC1990 pia hata turbocharger ni 2.liter.
Cha kushangaza Yale matoleo ya chini yake Yana uzito Mkubwa tofauti na haya mabox mara nyingi utakuta Yana kg 1400-1470 lakini matoleo ya nyuma uzito wake ni 1450-1500
Mzee wa Carina hii ina 1510kg
Ndio nataka nijilipue nalo
 
Aisee kile ki terious kid kina 650cc lakini naskia kina bugia hatari
Hivi ni tsh ngapi gari hii Daihatsu terios Kid, Mungu akinijaalia na mimi nataka nimiliki hako ka Daihatsu terios Kid
 
Hii ni 2013 kama sikosei. Niliangalia juzi mpaka hapa 28M inakuhusu
Kweli kabisa mi nimependa seat zake sio kama mabenchi ya Rav.4 CHAZA sasa XT nyingine haina pua mbinuko kwa bonnet ina maana hii turbo ipo au haipo, na inasemekana eti made in Singapore ndio bora kuliko made in Japan hebu msaada kidogo kabla ya kujilipuaView attachment 1209304View attachment 1209305View attachment 1209306View attachment 1209307View attachment 1209309View attachment 1209310View attachment 1209311View attachment 1209312View attachment 1209313
 
IST FWD 2003 CC 1290 nilitoka Dar hadi Shinyanga 990+ kilometres kwa lita 90 tu full AC safari nzima
 
Hivi ni tsh ngapi gari hii Daihatsu terios Kid, Mungu akinijaalia na mimi nataka nimiliki hako ka Daihatsu terios Kid
Ya mwaka 2002 kuanzia milioni 9 kamili unaikamata nje ya nyumba yako.
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom