Subaru Forester XT vs Kluger

Candela

JF-Expert Member
Aug 12, 2021
558
1,449
Wajuvi wa mambo,

Nipeni udambu juu ya hizo gari 2, okoeni ndoa yangu maana shemeji yenu akizimikiwa gari njiani atadai talaka. akikwama topeni ndio kabisa. kwa ufupi wife hapendi vigari sampuri ya ist, impreza nk, anasema anataka gari ya juu juu.

Nimeangalia angalia mitandaoni kulingana na bajeti yangu nimeona hizo akipata mojawapo atanizalia mtoto mwingine.

Nawasilisha.
 
Mkuu, mi sio mtaalamu wa mambo ya ndoa, lakini kwa ushahuri muulize yeye anachotaka, hafu mnunulie ilo ilo analotaka, otherwise utabaki kua na mtoto mmoja forever.

Tuje kwenye magari.

Sijui budget yako, lakini ningekua mimi kati ya hayo mawili ningeenda Klugger IV, ya 2.4L cylinder inline 4. Hiyo ni first gen, ila kama mfuko umenona nenda 2nd gen.

Mbadala wake ningejaribu Harrier 2nd gen.

Mwanamke anahitaji gari low profile. Subaru waachie hao wa mambio.
 
Wajuvi wa mambo, nipeni udambu juu ya hizo gari 2, okoeni ndoa yangu maana shemeji yenu akizimikiwa gari njiani atadai talaka. akikwama topeni ndio kabisa. kwa ufupi wife hapendi vigari sampuri ya ist, impreza nk, anasema anataka gari ya juu juu. nimeangalia angalia mitandaoni kulingana na bajeti yangu nimeona hizo akipata mojawapo atanizalia mtoto mwingine.
Nawasilisha.
Mkamatie Forester ya kijivu maana nimeona ikiendeshwa na demu inampendeza sana! Kuna mwanamama ana Forester mayai hizi XT namba DWF imekaza sana kila nikimuona natamani hata asimame nimuombe namba ila ndo hivyo yani nashindwa kumfikia.


Kluger nzuri ila kama utapata la 2nd au 3rd Generation lile ndio tamu zaidi kwa mwanamke. Ile first generation limekaa kiume sana
 
Wajuvi wa mambo, nipeni udambu juu ya hizo gari 2, okoeni ndoa yangu maana shemeji yenu akizimikiwa gari njiani atadai talaka. akikwama topeni ndio kabisa. kwa ufupi wife hapendi vigari sampuri ya ist, impreza nk, anasema anataka gari ya juu juu. nimeangalia angalia mitandaoni kulingana na bajeti yangu nimeona hizo akipata mojawapo atanizalia mtoto mwingine.
Nawasilisha.
Kazi unayo.
 
Sio yeye tu, anataka na sisi tumchagulie ili akisusa kumzalia aje kutulaumu huku :oops::oops:
Kwa hiyo anaetaka gari ni mtu A lakini anaechagua aina ya gari hiyo ni mtu C?

A na B wote hawana mamlaka wala uhuru wa kuchagua aina ya gari hiyo!

AAcA2h.jpg
 
Wajuvi wa mambo, nipeni udambu juu ya hizo gari 2, okoeni ndoa yangu maana shemeji yenu akizimikiwa gari njiani atadai talaka. akikwama topeni ndio kabisa. kwa ufupi wife hapendi vigari sampuri ya ist, impreza nk, anasema anataka gari ya juu juu. nimeangalia angalia mitandaoni kulingana na bajeti yangu nimeona hizo akipata mojawapo atanizalia mtoto mwingine.
Nawasilisha.
Asee ebu acha kulinganisha ujinga na forester asee.

Kwanza Forester iko economic way more ukilinganisha na kluger. Then ukija kwenye look (facial impression)..agh hata tusiongee forester takes it all. Perfomance sasa ndo sitaki kuweka neno maana inajulikana forester ni kinara.

Note! This is all about forester za kuanzia 2009). The only negative thing about forester ni spares though ukishafunga ndo mmemalizana hivo japo prices za spare zimechangamka kidogo.
 
Back
Top Bottom