Suala la sare za wanafunzi: Kwanini Serikali isitoe sare elekezi kwa wanafunzi wanaoanza kidato cha kwanza na Serikali ishone kwa kuchangia gharama?

Tafakari yetu

JF-Expert Member
Apr 19, 2021
1,502
4,408
Kuna suala la wanafunzi watakaoanza kidato cha kwanza ambao hawatakuwa na uwezo wa kununua sare waendelee na zile za shule ya msingi , kauli hiyo ilitolewa na aliyekuwa waziri wa Tamisemi.

Kiukweli nimeona mtazamo wa wengi juu ya suala ,kuna wengine wanasema kwamba sio mbaya waendelee nazo tu kwa sababu sare hazisomi ila ni wanafunzi.

Kuna wengine wanasema kwamba ni vema wakatafuta sare ili kutovunja utaratibu na wanapenda mbali zaidi wakisema sare zina mchango katika kujifunza kwa wanafunzi. Sijui kwa undani umuhimu wa sare na kujifunza kunakoelezewa ,hivyo wataalamu watudadavulie.

Wote, wana hoja za msingi ambao msingi mkuu ni kumpa mtoto fursa ya kupata elimu.

Ninatambua kwamba sasa kuna mabadiliko kwenye wizara ya TAMISEMI na kwamba waziri aliyetoa ushauri huo sasa hayupo kusema lakini tukumbuke tatizo la msingi la wanafunzi kukosa sare litaendelea kuwepo hivyo kama lisipopata muafaka yawezekana kweli wanafunzi wakakosa fursa ya elimu kwa sababu ya sare.

Tanzania ni nchi iliyobarikiwa ardhi kubwa yenye rutuba. Sare za wanafunzi zinatokana na moja ya mazao ya kilimo kama pamba na katani hivyo serikali ihamasishe kilimo cha mazao hayo .

Pia serikali itumie nguvukazi iliyo nayo katika kukuza kilimo cha mazao hayo. Watumike hata wafungwa pia katika kupunguza gharama.

Pia, serikali ije na sare elekezi kwa ajili ya wanafunzi wanaotarajiwa kujiunga na kidato cha kwanza. Kwa mfano, sare za rangi ya bluu na shati jeupo. Serikali kwa kutumia rasilimali ilizonazo kama viwanda watengeneze sare hizo na kuzisambaza mashuleni ambapo mwanafunzi atakayeanza kidato cha kwanza atanunua katika bei ndogo.

Hilo lisiishie hapo tu bali liende hadi kwenye vifaa vingine vya kujifunzia kama madaftari, kalamu na mabegi.

Huu ni muda muafaka kwa serikali kufanya uwekezaji mkubwa na kujenga viwanda vikubwa kwa kazi hii.
 
Swala ambalo hadi leo najiuliza kwa nini serikali hairuhusu watoto wa kike kusuka.

Pia kwa nini serikali bado inamtaka mwanafunzu kuvaa kiatu cheusi. Wakati kiatu ni kiatu na hakiathiri performance ya mtu
 
Swala ambalo hadi leo najiuliza kwa nini serikali hairuhusu watoto wa kike kusuka.

Pia kwa nini serikali bado inamtaka mwanafunzu kuvaa kiatu cheusi. Wakati kiatu ni kiatu na hakiathiri performance ya mtu
Wanaruhusiwa kusuka na ijumaa ni siku ya raba ,shuleni kwangu wanasuka kuanzia tano hadi saba
 
Nyerere na sera yake ya ujamaa alituharibu saana watanzania. Imefika mahali kila kitu kwa sasa tunataka tufanyiwe na serikali. Itatuchukua muda mrefu saana kutoka hapa tulipo.
 
Nyerere na sera yake ya ujamaa alituharibu saana watanzania. Imefika mahali kila kitu kwa sasa tunataka tufanyiwe na serikali. Itatuchukua muda mrefu saana kutoka hapa tulipo.
Kuna vitu tukubali tu bila serikali kufanya mambo hayaendi. Mambo yote yanayohusiana na miundombinu, afya na elimu ni mojawapo
 
Uniform ni uniformity ya wanafunzi, wanafunzi wanatokea mazingira tofauti tofauti, maskini na matajiri

Lengo la uniform ni kuziba gap Kati ya wanafunz wa level tofauti wakiwa mazingira ya shule,

Hivi wanafunzi wangeruhusiwa kuja na magari shuleni , vipi wanafunzi maskini wangejisikiaje?

Wanafunzi wakiruhusiwa kusuka watakavyo, vipi wale watakaosuka matano wakati wenzao wanasuka kwa 50,000

Mwanafunzi akiwa na sare za primary zimechakaa, wenzake za sekondari, huoni kama mwanafunzi aliyevaa sare za primary anajiona mnyonge na madhaifu?

Kama anayeingia sekondari avae za shule ya msingi, je anayeingia darasa la kwanza avae nguo za nyumbani ? au nursery?


KAMA UTAKAA CHINI NA KUWAZA VIZURI, UTAGUNDUA KUWA UNIFORM ZIPO KWA AJILI YA KUWAWEKA VUZURI KISAIKOLOJIA WANAFUNZI MASKINI, AMBAO WANGEFADHAIKA KWA KUONA WENZAO WANAVAA VITU VYA GHARAMA KUBWA NA WAO HAWANA
 
Back
Top Bottom