kasitile
Member
- Feb 22, 2011
- 32
- 0
Habari wa JF.
Katika kikao cha bunge kilichopita,suala la posho lilileta msuguano sana hasa kwa vyama vya CHADEMA (isipokuwa Shibuda) na CCM.Katika hilo,Mhe.Zitto Kabwe alikataa kuchukua posho ya vikao suala ambalo lilipelekea msuguano na Spika wa Bunge Bi.Anne Makinda.Baada ya hapo ikawa ni mijadala kwa upande wa wananchi.
Kilichonisukuma kuandika makala hii leo,ni safari ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe.Abbas Kandoro ya kwenda katika Halmashauri ya mojawapo katika mkoa huo.Hivi ni sahihi kwa waandishi wa Habari kupewa posho na Halmashauri kwa ajili ya kuripoti taarifa ambako wala hawakualikwa na Halmashauri?Waandishi waliolipwa ni Mtangazaji wa TBC1,Mwandishi wa gazeti la Mwananchi,Mwandishi wa gazeti la Habari leo na Mtangazaji wa ITV.Kuna Uhalali gani kwa Sekretariet ya Mkoa kupokea posho kwenye Halmashauri wakati wamepata posho kwenye taasisi yao?Wakati waandishi wa Habari walikuwa mstari wa Mbele sana kupinga posho wanazolipwa waheshimiwa wabunge,vipi kwa upande wao?
Jamani hii ni nchi yetu sote.Ifike sehemu kila mtu awajibike na kufanya kinachotakiwa.Kwa mwendo huu nchi yetu haiwezi kuendelea.Katika kipindi hiki nchi iko taabani sana kifedha,lakini wakati huo huo tunaendeleza malipo hewa ambayo hayawasaidii wananchi wetu,ambao kila kukicha maisha yanazidi kuwa magumu.Tuache unafiki,tuseme kile tunachokitenda.
Katika kikao cha bunge kilichopita,suala la posho lilileta msuguano sana hasa kwa vyama vya CHADEMA (isipokuwa Shibuda) na CCM.Katika hilo,Mhe.Zitto Kabwe alikataa kuchukua posho ya vikao suala ambalo lilipelekea msuguano na Spika wa Bunge Bi.Anne Makinda.Baada ya hapo ikawa ni mijadala kwa upande wa wananchi.
Kilichonisukuma kuandika makala hii leo,ni safari ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe.Abbas Kandoro ya kwenda katika Halmashauri ya mojawapo katika mkoa huo.Hivi ni sahihi kwa waandishi wa Habari kupewa posho na Halmashauri kwa ajili ya kuripoti taarifa ambako wala hawakualikwa na Halmashauri?Waandishi waliolipwa ni Mtangazaji wa TBC1,Mwandishi wa gazeti la Mwananchi,Mwandishi wa gazeti la Habari leo na Mtangazaji wa ITV.Kuna Uhalali gani kwa Sekretariet ya Mkoa kupokea posho kwenye Halmashauri wakati wamepata posho kwenye taasisi yao?Wakati waandishi wa Habari walikuwa mstari wa Mbele sana kupinga posho wanazolipwa waheshimiwa wabunge,vipi kwa upande wao?
Jamani hii ni nchi yetu sote.Ifike sehemu kila mtu awajibike na kufanya kinachotakiwa.Kwa mwendo huu nchi yetu haiwezi kuendelea.Katika kipindi hiki nchi iko taabani sana kifedha,lakini wakati huo huo tunaendeleza malipo hewa ambayo hayawasaidii wananchi wetu,ambao kila kukicha maisha yanazidi kuwa magumu.Tuache unafiki,tuseme kile tunachokitenda.