Return Of Undertaker
JF-Expert Member
- Jun 12, 2012
- 4,572
- 26,868
Kuna saa Akili inakataa kabisa kufanya kazi ya kutengeneza Logic. Huyu ni dreva- Tex ambaye anahusishwa na Tukio la kumteka MO.
Rais Magufuli aliwahi kusema watanzania sio wajinga. Ni kwa nini Rais Magufuli aseme kauli kama hii? Bila shaka anaona uzembe na watu kutokuwa Weledi katika eneo flan.
Nachanganyikiwa Surf tuliyoiona kwenye CCTV camera na hatimaye ikatelekezwa tukaikamata hatujajua bado mmiliki ni nani?
Mbona ukitaka kujua ilitengenezwa Lini na wapi, na nani wa kwanza kuinunua, akamuuzia nani mpaka mmiliki wa Mwisho utamjua?
Tupo imara kiasi gani katika maswala ya Kiuchunguzi? Motives ya watekaji ilikuwa ni nn? Si wamuulize mtekaji hao watekaji walikuwa wanataka nn kwake? Maana tukijua watekaji walikuwa wanataka nini watu wa uchunguzi wanaweza kutengeneza madhanio ya watekaji.
Hii Kesi ilikuwa imepoa kabisa na watu walishamsau Mo na maswahibu yake ya kutekwa. Kwa kifupi kesi hii ilikuwa imekumbwa na natural death, tumeenda kufufua maiti sasa inatuletea mainzi bila sababu.
Vyombo vyetu vya habari mpaka Leo havijawahi hata kufikiria kufanya mahojiano na MO katika swala nyeti kama hili la kutekana Nchini.
Akili inakataa kufanya connection kabisa.... Vyombo vyetu vya Ulinzi na Usalama visilale hadi Watekaji wote wakamatwe. Itatusaidia sana hasa kuondoa lawama ambazo Serikali imekuwa ikitupiwa kila kukicha.
Saidianeni na Interpol ikishindikana iteni hata CIA ili Ku clear hizi lawama. Duniani Tumezidiana hata Sisi waalimu sio kila kitu unaweza kufundisha mada nyingine ili zipate ufanisi tunatumia Mbinu ya kumwalika Mgeni.... Hata hapa ambapo watekaji wameanza kutuzidi maarifa tunapaswa kuwaita wengine wenye maarifa makubwa na vifaa vya kisasa zaidi.
Kuna faida kufanya hivyo, kwanza kutawaongezea vyombo vyetu vya uchunguzi Weledi kwa kuwa watakuwa wanajifunza pia kwa wenzao mbinu na watajua vifaa gani vinahitajika lakini pia tukiwapata watekaji tutakuwa tumeisaidia sana Serikali inayopakwa matope bila sababu.
Ole Mushi
0712702602