Chige

JF-Expert Member
Dec 20, 2008
13,497
29,832
Nafahamu kwamba watu wengi wameanzisha threads wakijaribu kuelezea suala la CAG Kisheria! Hata hivyo, wengi wao kama sio wote walichofanya ni kurundika vifungu vya kisheria bila kutoa ufafanuzi!

Mbaya zaidi, hawatoi ufafanuzi wa matumizi ya neno SHALL kwa mujibu wa sheria zetu! Nimelazimika kuanzisha uzi huu ili kuondoa mapungufu yote hayo.

Tuendelee.

Bila kujaza vifungu vingi, Katiba yetu Ibara ya 144 (1) inasema wazi kwamba:-
Controller and Auditor-General of the United Republic shall be obliged to vacate office upon attaining the age of sixty or any other age which shall be prescribed by a law enacted by Parliament.
Kwamba, CAG ATALAZIMIKA kuachia ofisi akifikisha miaka 60 au umri mwingine wowote utakaotajwa na sheria zilizotengenezwa na Bunge!

SWALI 1: Je, Profesa Mussa Assad amefikisha miaka 60?! Jibu HAPANA kwa sababu kumbukumbu zinaonesha amezaliwa Oktoba 06, 1961... kwa maana nyingine, atafikisha miaka 60 Oktoba 5, 2021.

SWALI 2: Je, Bunge limetaja huo UMRI MWINGINE WOWOTE?!

Jibu linapatikana kwenye Sheria ya Ukaguzi wa Hesabu za Umma, yaani Public Audit Act ya mwaka 2008, Ibara ya 6(2)(a) inayosema:-
Unless the question of removal becomes the subject of investigation in terms of Article 144(3) of the Constitution, the Controller and Auditor-General shall vacate office upon attaining the age of sixty five years;

Kumbe, Bunge likatunga sheria kwamba badala ya miaka 60, hatimae CAG ATALAZIMIKA kuachia ofisi akifikisha miaka 65. Tumeona Prof Assad ndo kwanza ana miaka 58.

SWALI 3: Nini hutokea CAG akimaliza miaka 5 ya kwanza?!

Hapa tena jibu linapatikana kutoka Public Audit Act 2008 Ibara ya 6 (1) inayosema:-
The Controller and Auditor-General shall hold office for the fixed term of five years and shall be eligible for renewal for one term only.
Hapo kwenye neno SHALL ndipo panapozua mgogoro!!

Watetezi wa uamuzi wa Rais wanasema neno SHALL sio shuruti! Kwa bahati mbaya sana, tafsiri yao wanaitoa kichwani na sio kwa mujibu wa sheria zetu!

Kwa mujibu wa sheria zetu, na kwa kuangalia Interpretation of Laws Act Ibara ya 53 (1&2) inasema kwamba:-
(1) Where in a written law the word "may" is used in conferring a power, such word shall be interpreted to imply that the power so conferred may be exercised or not, at discretion.

(2) Where in a written law the word
"shall" is used in conferring a function, such word shall be interpreted to mean that the function so conferred must be performed.
Kumbe, kwa mujibu wa sheria zetu, pasipo na SHURUTI hutumika neno MAY lakini linapotumika neno SHALL, hiyo ni SHURUTI!

Kwa maana nyingine, Public Audit Act inaposema "...and shall be eligible for renewal for one term only. Hapo suala la renewal ni SHURUTI kama ilivyosema Interpretation of Laws Act 53 (2).

Itakuwa sio SHURUTI either kama ameshafikisha miaka 65, au kama ambavyo 2008 Public Audit Act Ibara ya 6(2)(a) inavyosema kwamba:-
Unless the question of removal becomes the subject of investigation in terms of Article 144(3) of the Constitution, the Controller and Auditor-General shall vacate office upon attaining the age of sixty five years;
Kwa maana nyingine, kwavile Prof Assad hajafikisha miaka 65, hapo tafsiri yake ni kwamba AMETUMBULIWA na sio kwamba muda wake umeisha!!

Na CAG atatumbuliwa "...Unless the question of removal becomes the subject of investigation in terms of Article 144(3) of the Constitution."

Hiyo Ibara ya 144(3) ya Katiba yetu inasemaje? Jibu ni hili:-If the President considers that the question of the removal of the Controller and Auditor-General from office under the provisions of this Article needs to be investigated, then the procedure shall be as follows:
(a) the President shall appoint a Special Tribunal which shall consist of a Chairman and not less than two other members. The Chairman and at least half of the other members of that Special Tribunal shall be persons who are or have been Judges of the High Court or of the Court of Appeal in any country within the Commonwealth;
Kama tulivyoona hapo juu, CAG atalazimika kuachia ofisi endapo atakuwa amefikisha miaka 65, kinyume chake anaweza KUTUMBULIWA kabla ya huo umri ikiwa ametenda jambo linalohitaji investigation.

Hivyo basi, ni ama Rais atengue uamuzi wake wa awali wa kuteua CAG mwingine, au tuone akiunda Tume ya Kijaji ya Kumchunguza CAG kwa kosa analojua yeye na timu yake!!

CAG akiongezewa miaka mingine 5, ataimaliza akiwa na umri wa miaka 63... umri halali kwa mujibu wa Sheria ya Ukaguzi wa Hesabu za Umma ya mwaka 2008!![/QUOTE]


Aliyewahi kuwa Mkurugenzi wa FBI nchini Marekani, James Comey, ameandika katika kitabu chake A HIGHER LOYALTY maneno ya kuleta tafakuri kubwa. Amendika _“it is very hard to leave a group of people who are committed only to doing the right thing”_. Alikuwa anaeleza ugumu wanaopata watu waadilifu katika utumishi wa umma kutenda mambo kwa kufata sheria na taratibu. Mara nyingi hujikuta wapo peke yao. Athari ya wanayokutana nayo ni kuzidisha hofu kwa wengine wenye ujasiri na hatimaye kuendelea kuporomoka kwa maadili ya utendaji wa umma.

Katika hili la CAG, imeonyesha wazi kwamba wanasheria katika ngazi mbali mbali hawakutimiza wajibu wao.

Ibara ya 144 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano imeeleza wazi kama ifuatavyo:

*_"144 (1) bila ya kuathiri masharti mengine yaliyomo katika ibara hii, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Jamhuri ya Muungano atalazimika kuacha kazi yake atakapotimiza umri wa miaka siti au umri mwingine wowote utakaotajwa na Sheria iliyotungwa na Bunge”_*

*_“(2) Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu aweza tu kuondolewa katika madaraka ya kazi yake kwa sababu ya kushindwa kutekeleza kazi zake(ama kutokana na maradhi au sababu nyingine yoyote) au kwa sababu ya tabia mbaya, au kwa kuvunja masharti ya Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma, na hataweza kuondolewa kazini ila kwa mujibu wa masharti ya ibara ndogo ya [4] ya ibara hii”_*

Ibara hiyo ya Katiba inaeleza wazi kwamba umri wa kuacha kazi wa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu ni miaka 60. Hata hivyo Bunge limepewa uwezo wa kubadili umri na sio muda wa kazi wa Mdhibiti na Mkaguzi. Ni kanuni ya msingi ya kutafsiri sheria kwamba neno linapokuwa na maana mahsusi, haliwezi kutaftiwa tafsiri nyengine mbadala inayopingana na maana mahsusi ya neno hilo. Ibara ya
144 (1) ilikusudia kuweka umri wa kustaafu wa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu kama ulivyowekwa umri wa kustaafu wa Majaji chini ya ibara ya 110 ya Katiba ambao nao ni miaka 60.

Ibara ya 144 haitoi mwanya kwa Bunge kutunga Sheria ya kuweka muda wa kuendelea na kazi kwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu ambao utamfanya aondolewe kazini kabla ya muda uliowekwa na Katiba au kuongezwa na Sheria [miaka 65].
Hili linathibitishwa zaidi na ibara ya 144 (6) ya Katiba inayosema:

*_“ Mtu ambaye ni Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu au aliyepata kuwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu hawezi kuteuliwa kushika au kushikilia madaraka ya kazi nyingine yoyote katika utumishi wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano”_*

Kwa ibara hiyo, Profesa Musa Assad hawezi hata kukaimu nafasi yoyote katika utumishi wa umma, na hivyo atakuwa amestaafishwa katika utumishi wa umma kabla ya umri wa kustaafu. Hakuna kiumbe cha namna hiyo katika utumishi wa umma. Ikitokea hivyo, tafsiri sahihi ni kuwa mtu huyo amefukuzwa au kukatishwa utumishi wake. Na hilo, ni batili ya wazi kwa vile inakiuka masharti ya ibara ya 144(2) na (3) ya Katiba.

Sheria au tafsiri inayotoa mwanya kwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu kuondolewa kabla ya kufikisha umri wa kustaafu kisheria na kwa matakwa ya Rais bila ya kufuata masharti ya wazi ya utaratibu wa kumuondoa kabla ya kufikiksha umri wa kustaafu chini ya ibara ya 144(3) na (4), inavunja msingi wa kinga ya kikatiba [security of tenure].

Inasikitisha sana unapoona wanasheria katika mazingira kama haya, ambapo kuna mgongano baina ya Katiba na Sheria, wanaanza kutafsiri Sheria kuipindua Katiba na sio kutafisiri Katiba ili kuipindua Sheria inayopingana na Katiba kama inavyoelekezwa na ibara ya 64(5) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano.

Mwanasheria yeyote aliyemshauri Rais kumuondoa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa kutumia Sheria inayoweka masharti ya vipindi bila kuzingatia masharti ya wazi ya ibara ya 144(1) ya Katiba amemkosea sana Rais, amewakosea sana Watanzania na ameifedhehesha sana taaluma ya Sheria.

Fedheha kubwa zaidi kwa taaluma ya sheria ni pale wanasheria watapoanza kutofautiana katika kutafsiri masharti hayo ya wazi ya Katiba kwa itikadi au mirengo ya kisiasa au kwa baadhi kufanya hivyo kwa kupotosha ili kumfurahisha mteuzi.

Athari ya jambo hili haitokuwa kwa Profesa Mussa Assad. Athari kubwa ni katika mfumo wetu wa kikatiba, utawala wa sheria na matumizi ya mamlaka ya umma.


Zaidi soma:

 
Shall inayoongelea term limits mnaitafsiri vibaya.

Pia, likatiba lenyewe limejaa vituko linatakiwa kurekebishwa.

Ukiandika "shall be eligible for renewal" hapo ulazima unaongelewa kwenye eligibility. Eligibility ni potential ya kuwa CAG, si lazima aliye eligible kuwa CAG.

Mtu anaweza kuwa eligible voter, halafu akawa si voter.

Katiba inasema rais hawezi kuendelea kuwa rais baada ya vipindi vya urais viwili.

Je, hilo lina maana rais ni lazima awe rais kwa vipindi viwili vya urais?

Kama CAG anatakiwa kuwa CAG kwa miaka kumi, kwa nini mkataba wake ni wa miaka mitano?
 
Watanzania tuamke, Katiba ya mwak 1977 ina-limit mihula miwili ya miaka mitanomitano, ndiyo maana kabla ya hiyo katiba muda wao ulikuwa unabadilika.

Heb tupitie historia kidogo.
Screenshot_20191103-172215.png

Screenshot_20191103-172307.png

Yaani prof. Assad anavyochukiwa, hadi picha yake kwenye website (National Audit Office of Tanzania » The CAG) walishafuta kwenye orodha ya ma-CAG.

-Je, kafikisha miaka 60? (Mussa Juma ASSAD Born : 6 October 1961)
-Je, sheria ilibadilishwa lini kustaafishwa kabla ya miaka 60? (Mandatory retirement also known as enforced retirement or compulsory retirement)
-Je, anaumwa ama ametiwa hatiani na tume ya maadili?
-Je, Rais amefuata katiba inavyosema?

Screenshot_20191103-170758.png

Screenshot_20191103-131616.png
 
Watanzania tuamke,

-Je, kafikisha miaka 60? (Mussa Juma ASSAD Born : 6 October 1961)
-Je, sheria ilibadilishwa lini kustaafishwa kabla ya miaka 60? (Mandatory retirement also known as enforced retirement or compulsory retirement)
-Je, anaumwa ama ametiwa hatiani na tume ya maadili?
-Je, Rais amefuata katiba inavyosema?
View attachment 1252749
Unajua kuwa CAG ana kaa ofisi kwa vipindi visivyozidi viwili vya miaka mitano mitano?
IMG_20191103_133805.jpeg
 
Tumtakie CAG Mstaafu, Prof. Mussa Assad kustaafu kwema na amestaafu kwa heshima na kwa mujibu wa sheria na sio kwa hoja zozote za vitatange na vibirifitina, jina lake litaandikwa kwenye kile kitabu cha mashujaa wa kweli wa taifa wetu kwasababu ameacha Legacy.

Karibu CAG Mpya, Charles Kicheere, tunakutakia kazi njema.
Paskali
 
Watanzania tuamke,

-Je, kafikisha miaka 60? (Mussa Juma ASSAD Born : 6 October 1961)
-Je, sheria ilibadilishwa lini kustaafishwa kabla ya miaka 60? (Mandatory retirement also known as enforced retirement or compulsory retirement)
-Je, anaumwa ama ametiwa hatiani na tume ya maadili?
-Je, Rais amefuata katiba inavyosema?
View attachment 1252749
IMG-20191103-WA0003.jpg
 
Watanzania tuamke,

-Je, kafikisha miaka 60? (Mussa Juma ASSAD Born : 6 October 1961)
-Je, sheria ilibadilishwa lini kustaafishwa kabla ya miaka 60? (Mandatory retirement also known as enforced retirement or compulsory retirement)
-Je, anaumwa ama ametiwa hatiani na tume ya maadili?
-Je, Rais amefuata katiba inavyosema?
View attachment 1252749
Ndo keshaondoka sasa wengine waendelee.
 
Legacy ipi p naona unauma na kupuliza

State agent
Tumtakie CAG Mstaafu, Prof. Mussa Assad kustaafu kwema na amestaafu kwa heshima na kwa mujibu wa sheria na sio kwa hoja zozote za vitatange na vibirifitina, jina lake litaandikwa kwenye kile kitabu cha mashujaa wa kweli wa taifa wetu kwasababu ameacha Legacy.

Karibu CAG Mpya, Charles Kicheere, tunakutakia kazi njema.
Paskali
 
Hii comment yako Leo unaipaste kila kona kwenye uzi wa Prof Assad

Hutaki kujisumbua mkuu wala kuumiza kichwa au upo na John Mtembezi hapo aka John walker imepanda
Tumtakie CAG Mstaafu, Prof. Mussa Assad kustaafu kwema na amestaafu kwa heshima na kwa mujibu wa sheria na sio kwa hoja zozote za vitatange na vibirifitina, jina lake litaandikwa kwenye kile kitabu cha mashujaa wa kweli wa taifa wetu kwasababu ameacha Legacy.

Karibu CAG Mpya, Charles Kicheere, tunakutakia kazi njema.
Paskali
 
Pongezi kubwa kwa Prof. Assad kwa utumishi uliotukuka, ijapokuwa weledi na maadili yako ulikuwa mwiba kwa wengine. Kwa hakika historia yako imeandikwa kwa wino wa dhahabu, ambapo si ajabu ukaaminiwa na IMF ama WB na kukabidhiwa nafasi mpya unayostahili.

Aidha, pongezi pia kwa CAG mteule, mtangulize Mola mbele kwa nafasi hii mpya ulioaminiwa na kukabidhiwa kwa maslahi mapana ya uzalendo na taifa letu, hilo ni kama zigo la misumari endapo utaweka maadili na weledi kando ili upate kufuraisha watu fulani, haswa kwa yale yenye makandokando mengi.
 
Tumtakie CAG Mstaafu, Prof. Mussa Assad kustaafu kwema na amestaafu kwa heshima na kwa mujibu wa sheria na sio kwa hoja zozote za vitatange na vibirifitina, jina lake litaandikwa kwenye kile kitabu cha mashujaa wa kweli wa taifa wetu kwasababu ameacha Legacy.

Karibu CAG Mpya, Charles Kicheere, tunakutakia kazi njema.
Paskali
Huku nikuonyesha ukomavu. Safi P.
 
Back
Top Bottom