Lakini unamlinganishaje Prof. Assad kuendesha ist na Makonda aliyesema gari aina hiyo ni kuhongwa? Je, watu wamlaani Prof na kumfagilia makonda kuhusu mitazamo yao juu ya ist?Nmeshangazwa na haya mapambio dhidi ya CAG Prof Assad. Wengi wa wasiomfahamu wanamuona kwa yeye kuendesha IST ni mtu aliyejishusha sana na ni mwenzao.
Prof Assad anachofanya ni kucheza na akili za Watanzania. Mimi namfahamu akiwa anamiliki Benz pale UDSM na sijajua kama kwa sasa hana gari nyingine au ni maamuzi tu kutumia IST.
Kuna picha moja ashawahi kupiga Mo Dewji akiwa amepanda boda boda. Hii iliwapa sana faraja Watanzania. Lakini wanasahau Mo alipanda bodaboda wakati kuna Range Rove inamsubiri sehemu. Wewe unapanda bodaboda sababu ndiyo usafiri unaomudu.
Siku Mo Dewji akitembea kwa miguu toka anapoishi mpaka ofisini si sawa na wewe kutembea kwa miguu toka unapoishi mpaka ofisini. Yeye atakuwa anafanya mazoezi. Wewe utatembea sababu huna nauli.
Push-ups ukiamua upige mwenyewe hata 100 ni mazoezi. Push-ups hizo hizo ukiambiwa na mtu kwa kulazimishwa upige 50 ni adhabu.
Prof Assad kutumia IST si kwa sababu yeye ni maskini. Ni maamuzi tu but anaweza kuwa na gari za thamani zaidi. Anafahamu akili za Watanzania. Angeweza kwenda hata na bodaboda na wakashangilia sana kuwa huyu ni mwenzetu kabisa amejishusha.
Katika kujishusha pia kuna maana yake. Ni rahisi kwa mtu ambaye yupo juu kushuka chini na asifikiri ni shida, but kwa mtu aliye chini, siku zote hutamani kuwa juu. Je, aliye juu anaweza kujishusha chini na kuendelea kukaa chini?
Katika maisha kuna maigizo mengi. Tujiulize: Je, tunasoma na watoto wa Pro-Assad Nyanyembe Secondary Schools? Au Kitangoma Primary School? Je walisoma nasi Nyegehizi High School?
Je, huyu aliyejishusha anaishi nasi Buguruni kwa Mnyamani, au anaishi nasi Kigogo Mburahati? Tutofautishe maisha halisi na maigizo ndugu Watanzania.
Kwa taarifa yako hakuna mtanzania anayedhani eti Prof hawezi kuwa na "kipando" chenye hadhi zaidi ya Toyota ist.