Suala la Maji: Utawala corrupt unatuletea shida, Mchina akamatwa akichepusha maji mto Ruvu kumwagilia mboga

Missile of the Nation

JF-Expert Member
May 24, 2018
13,498
51,090
Ruvu-Mchina.jpg


Nataka niongee kwa hasira kali na leo Mod naomba mnivumilie lugha yangu. Hapa bongo kuna mambo ya kikhanithi yanaendelea sana na matokeo yake wananchi tunapata shida kwa sababu ya ukhanithi wa watu wachache.

Leo Nipashe wametoa taarifa kuwa kuna mchina amekamatwa anachepusha maji ya mto ruvu lita milioni moja kwa saa kumwagilia mbogamboga zake tu. Huu kama siyo ukhanithi ni kitu gani?

Huyu mtu haiwezekani anaingia nchini, anapewa vibali vyote halafu eti serikali isijue, Haiwezekani labda kama ni serikali ya mazuzu.

Leo kwa sababu kimenuka, maji hakuna wanajifanya kuja mbelembele kukamata bangusilo ili wammwagie lawama.

Tumeshasema mara kibao kuwa huu uhusiano wa kifala kati ya serikali yetu na wachina unatugharimu sana. Wachina wamekata miti sana nchi hii, Wao ndo wanconsume magogo ya miti kwa rate ya kutisha, halafu juzi serikali inajifanya kujikosha kwa kuzuia biashara ya magogo. Ilikuwa wapi siku zote?

Leo nilikuwa namsikiliza waziri wa zamani katika mtandao w clubhouse anaeleza kipindi alivyokuwa waziri wa mazingira alipojaribu kuwadhibiti wachina wasimalize misitu yetu. akapigiwa simu na wakubwa awaachie tu wachina waendelee!. Huu kama siyo uhujumu uchumi kwa nchi yetu ni nini?. Huu kama siyo Ukhanithi ni kitu gani?

Tunataka serikali yetu iache kuwaabudu Wachina, Tunataka serikali ilinde rasilimali za nchi hii. Hii tabia ya ubinafsi uliokithiri, upumbavu na kuuza nchi kukomeshwe mara moja.

Na wale wakubwa wanaouza nchi kwa vizawadi vidogo vya kufanyiwa massage huko Beijing waache mara moja tabia hizi za Kikhanithi
 
Huyo mchina ameanza lini kumwagilia mboga zake? na kina nani wanaohusika kumpa kibali cha kufanya hivyo? jibu ni hawa hawa viongozi wa CCM ambao leo wanatupigia kelele za kutunza mazingira.

Lakini pia, hayo maji ya mchina yakiachwa yakabaki mto Ruvu mwisho wa siku hizo lita zote zitaishia baharini kama hapatakuwepo na kiangazi kama kilichopo sasa.

Hivyo kama hao viongozi wakijitetea kwa kusema walitoa kibali kwa mchina wakati hali inaruhusu sijui mtawafanyaje hasa ikizingatiwa kila siku tunasisitizwa kilimo cha umwagiliaji ndio chenye tija, sasa iweje leo mwekezaji aonekane mbaya kwa kutumia fursa iliyopo?

Hapa sioni sababu ya kulia, kama pakiwepo na namna nzuri ya kutunza maji ya mvua wakati zikinyesha either kwa kujenga mabwawa au vinginevyo ndio njia nzuri ya kuepuka hili tatizo mbele ya safari, badala ya kumgeukia mwekezaji aonekane adui bila sababu yoyote, wakati adui yetu ni uzito wa kufikiri wa vichwa vya viongozi wetu.
 
Hiyo bodi ya maji ilipaswa wote wawe wameachishwa kazi baada ya kutangaza hii taarifa. Bodi ilikuwa likizo na sasa ndo wamerudi kazini baada ya madhara kuwa makubwa
Halafu cha ajabu mmoja wa wajumbe wa bodi ya maji ni CDF wa zamani Davis Mwamunyange halafu haya mambo ya kipuuzi yanaendelea nchini. Hii nchi inakwenda wapi?
 
Mala kumi mamlaka ya maji ifanye tathimini ya kiasi cha maji anacho tumia then alipe ili aendelee kulima mpaka atakavyo vuna mazao yaliopo shambani then akuna kutoa kibari Cha kulima baada ya kuvuna mazao yake kuliko kumzuia kumwagilia kwa sasa maana wote tutapata hasara
 
Mala kumi mamlaka ya maji ifanye tathimini ya kiasi cha maji anacho tumia then alipe ili aendelee kulima mpaka atakavyo vuna mazao yaliopo shambani then akuna kutoa kibari Cha kulima baada ya kuvuna mazao yake kuliko kumzuia kumwagilia kwa sasa maana wote tutapata hasara
Yaani umuachie mhalifu ambaye most likely kuna wakubwa aliowahonga ili afanye uharamia huo aendelee?
 
mboga mboga ndio zao hizo- usanii mtupu, vibali vyote serikali ya mboga mboga walimpa... sasa wanamkata wa nini ? au labda masharti yalikuwa achimbe kisima na sio kuvuna maji.. huko mbeleni lazima tuchapane tu kwa masuala haya haya ya maji.. ndio kitaeleweka...
Wanamkamata kujikosha tu ili ionekane chanzo cha ukosafu wa maji na umeme ni hao wachina na sio uzembe wa serikali katika kupanga vipaumbele vya nchi na hivyo kushindwa kutatua matatizo haya kwa miaka yote hii.

Mimi mtu anaeshabika chama cha MATAGA, namuona ana fake brain, na ubinadamu wake wa kujua mema na baya, pamoja na uwezo wake wa kufanyana reasoning, vyote ni questionable
 
Wanamkamata kujikosha tu ili ionekane chanzo cha ukosafu wa maji na umeme ni hao wachina na sio uzembe wa serikali katika kupanga vipaumbele vya nchi na hivyo kushindwa kutatua matatizo haya kwa miaka yote hii...
Yeyote anayeshabikia Mboga mboga ni Ndondocha tu.... ni kama vile wazazi wanapata watoto na wanaendelea kuwa watoto hadi siku zao za mwisho na bado hao hao wazazi wao wanawatunza tu kama yai, na huku wakiwaambia, mjitegemee, na wakati huo wanawabania watoto wao kujiendeleza .. ni ajabu sana hawa mboga mboga wamekuwa na monolopy ya akili za watanzania milion 60 na kuendea.
 
Back
Top Bottom