Suala la madini Tanzania; Kanuni ya 'Wagawanye ili uwatawale' inafanya kazi

urio f

JF-Expert Member
Mar 31, 2017
302
271
Kweli wazungu wana akili!.Wametuibia miaka mingi kwa kudanganya kuwa wanapeleka mchanga wa dhahabu kuchenjua huko Japan pengine na kwingineko.

Mtu mmoja mdadisi Siku zote alikuwa anatilia shaka.Anaamua aunde tume kuchunguza.

Anagundua wizi mkubwa.Wale wa upande wake waliohusika na wizi huo,anawachukulia hatua kali na kuanza kutafakari achukue hatua gani dhidi ya alioingia nao mkataba.

Cha ajabu,badala ya watz kuungana pamoja kumkemea mwizi,baadhi ya wataz,kwa mgongo wa demokrasia tuliyoletewa na wazungu,wanamtetea mwizi na kumlaani aliyegundua wizi.Anatishwa kuwa tutashitakiwa na mwizi na hivyo kulipa pesa nyingi.

Wengine wanasema chanzo ni mikataba mibovu hivyo ubovu wa mikataba hiyo anabebeshwa rais mwenye mwaka mmoja na nusu madarakani.Huyu hajawahi kuwa Waziri wa wizara hiyo.

Hata kama kuna uzembe upande wa serikali,kwa akili ya kawaida,nilitegemea walioibiwa waungane wamshughulikie mwizi.Wakishamaliza kumshughulikia mwizi,basi warejee na kusutana kwa uzembe!.Hapa ni kinyume chake!.

Ni sawa na kumfumania mtu akizini na mkeo,halafu badala ya jamaa zako kuungana nawe japo kumlaani mgoni wako,wao wanakubeza na kukuambia mgoni wako atakushitaki,na hivyo utamfidia fedha nyingi!.Woga huu unatoka wapi?.Ni heri nishitakiwe lakini mwizi wangu nimemjua.

Wengine wanapima uwezo wa Acacia dhidi ya TZ na kutetemeka.Kama watz ni waoga hivi bora kuishi Korea Kaskazini..Wengine wanasema tutafukuza wawekezaji.

Unaibiwa hivyo halafu bado unyamaze eti mwekezaji atakwenda!.Heri kukosa wawekezaji.Lakini kikubwa kinachotufikisha ktk mgawanyiko huu ni siasa.

Upinzani wanajua wakisifia hatua ya Rais itampa nguvu kisiasa na hivyo itakuwa vigumu kumshinda ktk chaguzi zijazo.

Kwa hiyo heri kumuunga mkono mwizi wetu wa madini kuliko rais aliyewagundua kuwa wanatuibia.Sikujua kuwa demokrasia ya vyama vingi ilikuja ili kutugawanya na kututawala!.

Moja ya vigezo Nyerere alivyotumia kuondoa mfumo wa vyama vingi ni kwa sababu unaondoa umoja.WATZ TUUNGANENI DHIDI YA WANYONYAJI WETU.
 
Kuna Mpinzani aliyekataa hilo au hukuwaelewa waliochangia Michango yao kwenye Sakaya zina?

Lissu amesema vyema nini tunatakiwa kufanya ili tushinde ulitaka tufanye je??

Tumpigie makofi aliyekuwako miaka 20 iliyopita ambaye ndiyo chanzo cha miswada mibovu ya sheria za madini??

Uliyaka tupongeze aliyechoma nyumba na sasa anarealise nyumba imechomwa.maana walipoambiwa na Wapinzani waliwatukana na kuwadhalilisha?

Uliwahi kumsupport Lissu alipowekwa jela kwa ajili ya kutetea Raslimali za Taifa??

Kama.hujaelewa ni bora kuuliza.

Lakini kumsifia na kumpongeza JPM ati kisa ametoa amri mchanga upimwe wakati yeye ni kati ya waliokuwa wanapiga makofi Kwenye hiyo misaada,duh kaka Tafadhali kuwa kidogo na ukweli.
 
Kweli wazungu wana akili!.Wametuibia miaka mingi kwa kudanganya kuwa wanapeleka mchanga wa dhahabu kuchenjua huko Japan pengine na kwingineko.Mtu mmoja mdadisi Siku zote alikuwa anatilia shaka.Anaamua aunde tume kuchunguza.Anagundua wizi mkubwa.Wale wa upande wake waliohusika na wizi huo,anawachukulia hatua kali na kuanza kutafakari achukue hatua gani dhidi ya alioingia nao mkataba.Cha ajabu,badala ya watz kuungana pamoja kumkemea mwizi,baadhi ya wataz,kwa mgongo wa demokrasia tuliyoletewa na wazungu,wanamtetea mwizi na kumlaani aliyegundua wizi.Anatishwa kuwa tutashitakiwa na mwizi na hivyo kulipa pesa nyingi.Wengine wanasema chanzo ni mikataba mibovu hivyo ubovu wa mikataba hiyo anabebeshwa rais mwenye mwaka mmoja na nusu madarakani.Huyu hajawahi kuwa Waziri wa wizara hiyo.Hata kama kuna uzembe upande wa serikali,kwa akili ya kawaida,nilitegemea walioibiwa waungane wamshughulikie mwizi.Wakishamaliza kumshughulikia mwizi,basi warejee na kusutana kwa uzembe!.Hapa ni kinyume chake!.Ni sawa na kumfumania mtu akizini na mkeo,halafu badala ya jamaa zako kuungana nawe japo kumlaani mgoni wako,wao wanakubeza na kukuambia mgoni wako atakushitaki,na hivyo utamfidia fedha nyingi!.Woga huu unatoka wapi?.Ni heri nishitakiwe lakini mwizi wangu nimemjua.Wengine wanapima uwezo wa Acacia dhidi ya TZ na kutetemeka.Kama watz ni waoga hivi bora kuishi Korea Kaskazini..Wengine wanasema tutafukuza wawekezaji.Unaibiwa hivyo halafu bado unyamaze eti mwekezaji atakwenda!.Heri kukosa wawekezaji.Lakini kikubwa kinachotufikisha ktk mgawanyiko huu ni siasa.Upinzani wanajua wakisifia hatua ya Rais itampa nguvu kisiasa na hivyo itakuwa vigumu kumshinda ktk chaguzi zijazo.Kwa hiyo heri kumuunga mkono mwizi wetu wa madini kuliko rais aliyewagundua kuwa wanatuibia.Sikujua kuwa demokrasia ya vyama vingi ilikuja ili kutugawanya na kututawala!.Moja ya vigezo Nyerere alivyotumia kuondoa mfumo wa vyama vingi ni kwa sababu unaondoa umoja.WATZ TUUNGANENI DHIDI YA WANYONYAJI WETU.
Wale tulio wapa dhamana ndiwo wametufikisha hapa Kwa kutengeneza mikataba ya siri wala siyo akili za hao wazungu.'ukosefu wa maadili'
 
Kuna Mpinzani aliyekataa hilo au hukuwaelewa waliochangia Michango yao kwenye Sakaya zina?

Lissu amesema vyema nini tunatakiwa kufanya ili tushinde ulitaka tufanye je??

Tumpigie makofi aliyekuwako miaka 20 iliyopita ambaye ndiyo chanzo cha miswada mibovu ya sheria za madini??

Uliyaka tupongeze aliyechoma nyumba na sasa anarealise nyumba imechomwa.maana walipoambiwa na Wapinzani waliwatukana na kuwadhalilisha?

Uliwahi kumsupport Lissu alipowekwa jela kwa ajili ya kutetea Raslimali za Taifa??

Kama.hujaelewa ni bora kuuliza.

Lakini kumsifia na kumpongeza JPM ati kisa ametoa amri mchanga upimwe wakati yeye ni kati ya waliokuwa wanapiga makofi Kwenye hiyo misaada,duh kaka Tafadhali kuwa kidogo na ukweli.
Suala hapa siyo upungufu wa sheria.Suala ni upungufu wa maadili kwa baadhi ya watz waliokabidhiwa jukumu la kusimamia(TMAA).Mwekezaji amerubuni baadhi ya watz wenzetu.Sasa rais hapo anakosa?Hatua anazowachukulia hazitoshi?
 
Wale tulio wapa dhamana ndiwo wametufikisha hapa Kwa kutengeneza mikataba ya siri wala siyo akili za hao wazungu
Suala hapa ni uadilifu wa watz wala siyo sheria.Madini yaliyopo kwenye makontena ni zaidi ya mara 10 ya ilivyokuwa imeelezwa kwenye makaratasi ya kusafirishia mchanga huo.Sheria hapo imechangia nini kwenye wizi huo?
 
Kuna Mpinzani aliyekataa hilo au hukuwaelewa waliochangia Michango yao kwenye Sakaya zina?

Lissu amesema vyema nini tunatakiwa kufanya ili tushinde ulitaka tufanye je??

Tumpigie makofi aliyekuwako miaka 20 iliyopita ambaye ndiyo chanzo cha miswada mibovu ya sheria za madini??

Uliyaka tupongeze aliyechoma nyumba na sasa anarealise nyumba imechomwa.maana walipoambiwa na Wapinzani waliwatukana na kuwadhalilisha?

Uliwahi kumsupport Lissu alipowekwa jela kwa ajili ya kutetea Raslimali za Taifa??

Kama.hujaelewa ni bora kuuliza.

Lakini kumsifia na kumpongeza JPM ati kisa ametoa amri mchanga upimwe wakati yeye ni kati ya waliokuwa wanapiga makofi Kwenye hiyo misaada,duh kaka Tafadhali kuwa kidogo na ukweli.
Tatizo kubwa ni CCM
 
Suala hapa siyo upungufu wa sheria.Suala ni upungufu wa maadili kwa baadhi ya watz waliokabidhiwa jukumu la kusimamia(TMAA).Mwekezaji amerubuni baadhi ya watz wenzetu.Sasa rais hapo anakosa?Hatua anazowachukulia hazitoshi?

Anachotakiwa kufanya huyo Rais asiye taka kusjauriwa ni kufuata ushauri wa wanasheria na siyo kukurupuka kama anaenda chooni.

Issue ni Umoja na ushirikiano lakini Umoja si wa upande mmoja tukiongea kuhusu umoja Nina maana ya Watanzania maana JPM Watanzania kwake ni wanaccm tu ndipo shida ilipo.
 
Suala hapa siyo upungufu wa sheria.Suala ni upungufu wa maadili kwa baadhi ya watz waliokabidhiwa jukumu la kusimamia(TMAA).Mwekezaji amerubuni baadhi ya watz wenzetu.Sasa rais hapo anakosa?Hatua anazowachukulia hazitoshi?

Anachotakiwa kufanya huyo Rais asiye taka kusjauriwa ni kufuata ushauri wa wanasheria na siyo kukurupuka kama anaenda chooni.

Issue ni Umoja na ushirikiano lakini Umoja si wa upande mmoja tukiongea kuhusu umoja Nina maana ya Watanzania maana JPM Watanzania kwake ni wanaccm tu ndipo shida ilipo.
 
Mlilalama hivyo kipindi tundulissu anawekwa ndani kwaajili ya hiyo migodi?
Sikuwahi kusikia Tundu Lissu aliwekwa ndani kwa kusema mchanga unaosafirishwa una dhahabu nyingi kuliko inavyoelezwa kwenye makaratasi ya kusafirishia.
 
Umeeleza vya kutosha, na mwizi akishagunduwa waliobiwa hawaungani basi atatumia mwanya huo huo kueneza propaganda zake kwa kila aina, subiri pesa zitagavyomwagika sehemu husika! Ila mwenye thread, nakuuliza swali, hivi kama ingekuwa ni sisi Watanzania tunwaibia UK wafikiri Waingereza wangegawanyika kwa hili?! Wale wahamiaji tu wanaipata fresh je wangekuwa wanachota zile dhahabu Bank of England(ambazo wengi wanadai hazijachimbwa UK) wafikiri ingekuwaje?! Hivi tunavyoongea si ajabu manowari za kivita zingeshatinga karibu na Tanzania! Fanya mchezo na wazungu, Falklands tu ilileta balaa pamoja na kwamba kile kisiwa ni cha Argentina! Mwingireza kakataa katu katu kukirudisha kisa mafuta! Acha kabisa...
 
Tatizo kubwa ni CCM

Tatizo siyo CCM, Tatizo ni Viongozi wa CCM wanaopandikiza Chuki,visasi na ubaguzi miongoni mwa Watanzania ili kwa pamoja tushinde kutetea raslimali zetu hao ni wakwanza.Wa pili ni wanaccm wanao fikiria chuki,Ubaguzi na visasi kwa Wapinzani ndiyo CCM italeta Maendeleo bila kujua hata Wapinzani ni Watanzania wenye haki sawa na wao.

Siku wanaccm hawa watakaporealise kwamba Wapinzani ni Watanzania wenye haki sawa na CCM ndipo Maendeleo yatakapokuja.

Maendeleo hayaji kwenye chuki na ubaguzi. Wanaccm walitakiwa wawachukie watawala waliojilimbikizia Mali na si Wapinzani lakini kwa sababu ya kukosa elimu wanaccm wamekuwa wakiaminishwa kwamba Wapinzani ni adui wa Maendeleo wakati adui wa Maendeleo ni wale tuliowapa dhamana ya kutuongoza.

Ni wakati umefika wa wanaccm kusema.basi kwenye Chuki na ubaguzi ili tupate Maendeleo
 
Anachotakiwa kufanya huyo Rais asiye taka kusjauriwa ni kufuata ushauri wa wanasheria na siyo kukurupuka kama anaenda chooni.

Issue ni Umoja na ushirikiano lakini Umoja si wa upande mmoja tukiongea kuhusu umoja Nina maana ya Watanzania maana JPM Watanzania kwake ni wanaccm tu ndipo shida ilipo.
Upo ushauri mzuri sana wa kisheria nimeuona wa mbunge wa Mtwara mini,Maftah Nachuma(CUF).Ni ushauri wa kizalendo na makini.Wengine wanatoa ushauri kwa kulaumu na kupotosha ili serikali izidi kuharibikiwa.Huu si ushauri wa kizalendo.Ni ushauri unaowanufaisha wezi.
 
Tatizo siyo CCM, Tatizo ni Viongozi wa CCM wanaopandikiza Chuki,visasi na ubaguzi miongoni mwa Watanzania ili kwa pamoja tushinde kutetea raslimali zetu hao ni wakwanza.Wa pili ni wanaccm wanao fikiria chuki,Ubaguzi na visasi kwa Wapinzani ndiyo CCM italeta Maendeleo bila kujua hata Wapinzani ni Watanzania wenye haki sawa na wao.

Siku wanaccm hawa watakaporealise kwamba Wapinzani ni Watanzania wenye haki sawa na CCM ndipo Maendeleo yatakapokuja.

Maendeleo hayaji kwenye chuki na ubaguzi. Wanaccm walitakiwa wawachukie watawala waliojilimbikizia Mali na si Wapinzani lakini kwa sababu ya kukosa elimu wanaccm wamekuwa wakiaminishwa kwamba Wapinzani ni adui wa Maendeleo wakati adui wa Maendeleo ni wale tuliowapa dhamana ya kutuongoza.

Ni wakati umefika wa wanaccm kusema.basi kwenye Chuki na ubaguzi ili tupate Maendeleo
CCM hii ya Bashite? hapa utasubiri sana.
 
Umeeleza vya kutosha, na mwizi akishagunduwa waliobiwa hawaungani basi atatumia mwanya huo huo kueneza propaganda zake kwa kila aina, subiri pesa zitagavyomwagika sehemu husika! Ila mwenye thread, nakuuliza swali, hivi kama ingekuwa ni sisi Watanzania tunwaibia UK wafikiri Waingereza wangegawanyika kwa hili?! Wale wahamiaji tu wanaipata fresh je wangekuwa wanachota zile dhahabu Bank of England(ambazo wengi wanadai hazijachimbwa UK) wafikiri ingekuwaje?! Hivi tunavyoongea si ajabu manowari za kivita zingeshatinga karibu na Tanzania! Fanya mchezo na wazungu, Falklands tu ilileta balaa pamoja na kwamba kile kisiwa ni cha Argentina! Mwingireza kakataa katu katu kukirudisha kisa mafuta! Acha kabisa...

Unadhani wanaotugawa ni wazungu au wawekezaji??

Hivi Lissu kwanini aliwekwa jela miezi mitatu kwa kosa la Uchochezi wakati anapiga nia Raslimali zetu!Hebu jiulize kuna mwanaccm hata mmoja aliyesimama na Lissu?Je kuna mwanaccm hata mmoja aliye ona na kuelewa hili akipiga kelele?

Wanaccm wengi walifika mahali wanasema ni bora Lissu anyongwe tu,wapo hata hapa JF wengine walidiriki kuandika,Leo kuna sababu ya kusifia JPM. Si ndiye Huyu aliyepaza sauti ya kuwadhalilisha Wapinzani kwamba hawajui lolote wapumbavu tu leo tinahitajika tusifie??

Si ndiye huyu leo kawaida Wapinzani mafudenge unategemea umoja utoke wapi??

Nani alimwambia CCM wanaadvocate kwa umoja wa Watanzania?? Ingekuwa kweli basi tusingesikia maeneo waliyoshika Wapinzani yana matatizo,tusingesikia wizi wa pesa za Halmashauri zinazoratibiwa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha na Waziri Simbachawene ukiendela na Rais amenyamaza,kwa sababu ni.Upinzani.

Umoja wetu utakuja tutakapopata Rais mwenye uchungu kweli na Taifa lake siyo huyu mwenye asili ya kitutsi!

Umoja wetu hatuwezi kujenga kwenye issue ya Mchanga, umoja wetu unatakiwa uwe nje ya Mchanga. Umoja wetu ndiyo Maendeleo yetu lakini wanaccm mko radhi Kwenye kuona Hata Wapinzani ni Watanzania??

Au Mara zote mmekuwa mkiwatukana na kuwa kebehi Wapinzani na kuwasifia wapiga madeal majambazi ya Raslimali zetu akianzia na Mkapa na JK.
 
10 Reactions
Reply
Back
Top Bottom