Suala la kujenga shule zaidi ya moja kwenye eneo moja lina faida gani? kwanini shule hiyo isiboreshewe miundo mbinu yake kuliko kuigawa?

The lost

JF-Expert Member
Jul 3, 2017
2,695
8,209
Ni moja ya suala la hovyo sana kwa mifumo yetu. Inawezekana vipi eneo lile lile ujenge shule mbili tena kaeneo kenyewe kagodo hakana kiwanja cha michezo, eneo la wazi la kutosha nk. Najiuliza hivi hawa wataalamu wetu wa masuala ya ardhi wanafanya nini huko chuoni?

Kwanini wasishauri ujenzi huu holela wa shule haufai. Unakuta shule inagawanywa kwa kigezo cha idadi ya wanafunzi halafu shule mpya inajengwa ndani ya eneo hilohilo. Mantiki ya kufanya hivyo huwa ni nini haswa?

Kwanini usiongeze miundombinu kwa shule hiyohiyo ili iweze kuwahudumia wanafunzi wote?
 
Back
Top Bottom