Kwanza tujiulize vigezo vinavyotumika kuwachagua wa kwenda jkt. Kama ulivosema si wahitimu wote huenda, nafasi ni chache, japo pia ndani ya walio chaguliwa wengine hukwepa kwenda. Nafasi za kazi nazo ni chache, hata hao wanao kuwa wameitwa jkt si wote wanao chukuliwa. Kwa kazi serikalini naunga mkono hoja, kuwachukua waliopitia jkt ni sahihi.Ni kawaida Kila mwaka JKT kuchukua wanafunzi wa kidato Cha sita na kuwapangia kambi za mafunzo ya JKT wanakotakiwa kuripoti.Lakini huwa hawachukui wote waliomaliza form six huchukua wachache na wengine kuachwa
Sasa linapokuja suala la ajira mtu hutakiwa awe na cheti Cha JKT Sasa huyo ambaye hakupewa hiyo nafasi inakuwaje ? Sababu si kuwa aligoma kwenda Bali hakupata nafasi .