Suala la dowans linanifanya nijiulize kama tunaowasomi ambao wako committed na maslahi ya taifa

Shayu

Platinum Member
May 24, 2011
608
1,653
Suala la kuwalipa tuzo dowans za mabillion ya shillingi linanipa mashaka mno na watu tuliowapa dhamana ya kuliongoza taifa hili, juu ya uzalendo wao na jinsi gani wanavyojitolea kwa manufaa ya taifa hili, linanipa mashaka na umakiini wao. Hivi hatuna wanasheria makini wenye uwezo wa juu katika masuala ya mikataba au ubinafsi na ufisadi umeshika hatamu miongoni mwetu? Wananchi wanabebeshwa mzigo wa kulipa hasara ambayo wao hawakuitenda, je ni hatua gani itachukuliwa kwa wote waliohusika? Nasikitishwa sana na taifa letu linakoelekea na watu wetu walivyokosa uzalendo kwa nchi yao wenyewe.
 
Mjomba/Shangazi suala hapa si wasomi wala wanasheria, kinachotakiwa ni wananchi wenyewe kuamua kuwa sasa basi. Wanachotakiwa ni kuwatoa viongozi hawa ambao hawana huruma na wanachi wanao watawala. Wao shida za wanaowatawala waziwapi taabu hata chembe, wanachofanya ni kuwaibia wananchi kwa mikataba mibovu kama hii ya dowans, mpaka wanananchi wanaoibiwa watakapo amua wao wenyewe kuwang'oa hawa mafisadi ndipo watakapo pona na kulipa hayo mabilioni ya dowans. Hata libya kwa sasa NTC hawahangaiki na kulipa mikataba kama hii ya dowans iliyo achwa na khadaffi.
 
Mjomba/Shangazi suala hapa si wasomi wala wanasheria, kinachotakiwa ni wananchi wenyewe kuamua kuwa sasa basi. Wanachotakiwa ni kuwatoa viongozi hawa ambao hawana huruma na wanachi wanao watawala. Wao shida za wanaowatawala waziwapi taabu hata chembe, wanachofanya ni kuwaibia wananchi kwa mikataba mibovu kama hii ya dowans, mpaka wanananchi wanaoibiwa watakapo amua wao wenyewe kuwang'oa hawa mafisadi ndipo watakapo pona na kulipa hayo mabilioni ya dowans. Hata libya kwa sasa NTC hawahangaiki na kulipa mikataba kama hii ya dowans iliyo achwa na khadaffi.
Kwahiyo tukiwaondoa tutakuwa na mabadiliko katika umakini wa uongozi?
 
Back
Top Bottom