Uchaguzi 2020 Suala la chama gani chaweza kutoa Rais 2020 limezikwa rasmi

BUBERWA D.

JF-Expert Member
Apr 22, 2011
2,293
1,170
Sasa ni dhahiri kuwa swala la chama gani chaweza kutoa rais wa JMT limezikwa rasmi na uhakika ni kuwa, CCM peke yake ndicho kitaendelea kutoa rais.

Ukifuatilia mijadala inayoendelea hasa ndani ya vyama vya upinzani na wapambe wao (wanaharakati) ni dhahiri kuwa wamebadili mashambulizi yao dhidi ya CCM na kuhamishia kwa mtu binafsi (JPM).

Tulizoea mara zote, kutokana na uasili na chimbuko la vyama pinzani na vyama vya kiharakati huwa ni kushambulia serikali na chama kilicho madrakani ili kuonesha kile wanachoita "ukosoaji."

Kwa Tanzania mambo yamebadilika; si wapinzani, wanaharakati, wala wale wanaowatuma na kuwafadhili wanashambulia CCM kama ilivyo, bali wamejikita katika kutafuta namna ya kushirikiana na makundi (kama yapo)ndani ya CCM ili kujaribu kutikisa utawala uliopo na hata ikiwezekana kuuondoa na kuingiza mtu ambaye ataendeleza utamaduni waliozoea wa kufyonza taifa. Hekaheka hizi zinasukumwa na mambo kadha wa kadha.

Kutokana na Tanzania tulipokuwa tumefikia, wanasiasa bila kujali vyama vyao, wanaharakati, wanahabari, viongozi wa serikali n.k kwa wingi wao japo si wote walitegemea kujinufaisha kwa kupora fedha za umma, kufyonza rasilimali za taifa n.k Wachache sana walikosa pesa za wizi, miradi ilikwama huku deni la taifa likikua, misafara isiyokoma kwenda ugaibuni wakilipana masurufu makubwa, n.k.

Hili kundi bila ya kujali itikadi ya vyama vyao, lilitengeneza kabila lao jipya la walaji. Kabila hili sasa limeungana kuhakikisha serikali iliyo madarakani, iliyojikita kuhakikisha inakata mirija ya minyoo ambayo imelifyonza taifa hili kwa miaka mingi inaondoshwa.

Kwa bahati mbaya, na mara zote ilivyo, huwa kuna kundi ambalo hutumika kufanikisha mipango ya kabila la walaji. Kundi hili lina sifa zifuatazo:-
  • Kuendeshwa na mihemko
  • Halina utamaduni wa kufikiri kwa udhati (critical thinking)
  • Huwa na tabia ya matumaini ya maisha mazuri bila kufuata njia sahihi
  • Ni kundi mara nyingi la umri wa kati
Kundi hili linajikuta kucha kutwa likishinda mitandaoni likitoa matusi mengi likitumaini kuwa maisha yatawanyookea kupitia kabila hili la walaji ambao wamekuwa madarakani miaka yote.

Aidha, kabila hili la walaji linaendesha vikao vya siri kila usiku kwa kushirikiana na baadhi ya watu waovu wa mataifa ya nje yenye uchu pia na mali za taifa letu kuhakikisha serikali hii inayowazibia inaondoka bila kujali ni chama gani ilimradi anayeingia atokane na kabila lao la walaji.

Kwahiyo, uchaguzi ujao ni kati ya kundi la wale wanaolitakia mema taifa hili liondokane na ufisadi na ubadhirifu uliokithiri na kufuata njia njema ya kimaendeleo na uadilifu dhidi ya kabila la walaji waliokatwa mirija yao iliyo lifyonza taifa hili. Uwanja wa mapambano waliochagua ni CCM. Hivyo ni kazi kwa kundi adilifu kucheza karata yake na kuwaondosha waovu (walaji) ndani ya chama kwa weledi mkubwa basi hapo itakuwa "..kazi iendelee.."

Tupo tayari kutokuchezewa na kabila ovu, uwezo tunao, sababu tunayo na nia tunayo.

Dunstan Buberwa Ntamilyango,
Mwananchi wa kawaida.
Biharamulo.
0759829015.
 
Sasa ni dhahiri kuwa swala la chama gani chaweza kutoa rais wa JMT limezikwa rasmi na uhakika ni kuwa, CCM peke yake ndicho kitaendelea kutoa rais.

Ukifuatilia mijadala inayoendelea hasa ndani ya vyama vya upinzani na wapambe wao (wanaharakati)ni dhahiri kuwa wamebadili mashambulizi yao dhidi ya CCM na kuhamishia kwa mtu binafsi (JPM).

Tulizoea mara zote, kutokana na uasili na chimbuko la vyama pinzani na vyama vya kiharakati huwa ni kushambulia serikali na cha kilicho madrakani ili kuomesha kile wanachoita "ukosoaji."

Kwa Tanzania mambo yamebadilika; si wapinzani, wanaharakati wala wale wanaowatuma na kuwafadhi wanashambulia CCM kama ilivyo, bali wamejikita katika kutafuta namna ya kushirikiana na makundi (kama yapo)ndani ya CCM ili kujaribu kutikisa utawala uliopo. Hekaheka hizi zinasukumwa na mambo kadha wa kadha.

Kutokana na Tanzania tulipokuwa tumefikia, wanasiasa bila kujali vyama vyao, wanaharakati, wanahabari, viongozi wa serikali n.k kwa wingi wao japo si wote walitegemea kujinufaisha kwa kupora fedha za umma, kufyonza rasilimali za taifa n.k Hakuna aliyekosa pesa za wizi, miradi ilikwama huku deni la taifa likikua, misafara isiyokoma kwenda ugaibuni wakilipana masurufu makubwa.

Hili kundi bila ya kujali itikadi ya vyama vyao, lilitengeneza kabila lao jipya la walaji. Kabila hili sasa limeungana kuhakikisha serikali iliyo madarakani iliyojikita kuhakikisha inakata mirija ya minyoo ambayo imelifyonza taifa hili kwa miaka mingi inaondoshwa.

Kundi hili linaendesha vikao vya siri kila usiku kwa kushirikiana na baadhi ya watu waovu wa mataifa ya nje yenye uchu pia na mali za taifa letu kuhakikisha serikali hii inayowazibia inaondoka bila kujali ni chama gani ilimradi anayeingia atokane na kabila lao la walaji.

Kwahiyo, uchaguzi ujao ni kati ya kundi la wale wanaolitakia mema taifa hili liondokane na ufisadi na ubadhirifu uliokithiri na kufuata njia njema ya kimaendeleo na uadilifu dhidi ya kabila la walaji waliokatwa mirija yao iliyo lifyonza taifa hili. Uwanja wa mapambano waliochagua ni CCM. Hivyo ni kazi kwa kundi adilifu kucheza karata yake na kuwaondosha waovu (walaji) ndani ya chama kwa weledi mkubwa basi hapo itakuwa "..kazi iendelee.."

Tupo tayari kutokuchezewa na kabila ovu, uwezo tunao, sababu tunayo na nia tunayo.

Dunstan Buberwa Ntamilyango,
Mwananchi wa kawaida.
Biharamulo.
0759829015.
1565765623295.png
 
Kabila bovu? what do you mean? CCM ni mbele kwa mbele, Ubaguzi wa Kikabila au Rangi na Dini hauna nafasi; Nchi moja Taifa Moja.
 
Sasa ni dhahiri kuwa swala la chama gani chaweza kutoa rais wa JMT limezikwa rasmi na uhakika ni kuwa, CCM peke yake ndicho kitaendelea kutoa rais.

Ukifuatilia mijadala inayoendelea hasa ndani ya vyama vya upinzani na wapambe wao (wanaharakati)ni dhahiri kuwa wamebadili mashambulizi yao dhidi ya CCM na kuhamishia kwa mtu binafsi (JPM).

Tulizoea mara zote, kutokana na uasili na chimbuko la vyama pinzani na vyama vya kiharakati huwa ni kushambulia serikali na chama kilicho madrakani ili kuonesha kile wanachoita "ukosoaji."

Kwa Tanzania mambo yamebadilika; si wapinzani, wanaharakati, wala wale wanaowatuma na kuwafadhi wanashambulia CCM kama ilivyo, bali wamejikita katika kutafuta namna ya kushirikiana na makundi (kama yapo)ndani ya CCM ili kujaribu kutikisa utawala uliopo na hata ikiwezekana kuuondoa na kuingiza mtu ambaye ataendeleza utamaduni waliozoea wa kufyonza taifa. Hekaheka hizi zinasukumwa na mambo kadha wa kadha.

Kutokana na Tanzania tulipokuwa tumefikia, wanasiasa bila kujali vyama vyao, wanaharakati, wanahabari, viongozi wa serikali n.k kwa wingi wao japo si wote walitegemea kujinufaisha kwa kupora fedha za umma, kufyonza rasilimali za taifa n.k Wachache sana walikosa pesa za wizi, miradi ilikwama huku deni la taifa likikua, misafara isiyokoma kwenda ugaibuni wakilipana masurufu makubwa, n.k.

Hili kundi bila ya kujali itikadi ya vyama vyao, lilitengeneza kabila lao jipya la walaji. Kabila hili sasa limeungana kuhakikisha serikali iliyo madarakani, iliyojikita kuhakikisha inakata mirija ya minyoo ambayo imelifyonza taifa hili kwa miaka mingi inaondoshwa.

Kwa bahati mbaya, na mara zote ilivyo, huwa kuna kundi ambalo hutumika kufanikisha mipango ya kabila la walaji. Kundi hili lina sifa zifuatazo:-
  • Kuendeshwa na mihemko
  • Halina utamaduni wa kufikiri kwa udhati (critical thinking)
  • Huwa na tabia ya matumaini ya maisha mazuri bila kufuata njia sahihi
  • Ni kundi mara nyingi la umri wa kati
Kundi hili linajikuta kucha kutwa likishinda mitandaoni likitoa matusi mengi likitumaini kuwa maisha yatawanyookea kupitia kabila hili la walaji ambao wamekuwa madarakani miaka yote.

Aidha, kabila hili la walaji linaendesha vikao vya siri kila usiku kwa kushirikiana na baadhi ya watu waovu wa mataifa ya nje yenye uchu pia na mali za taifa letu kuhakikisha serikali hii inayowazibia inaondoka bila kujali ni chama gani ilimradi anayeingia atokane na kabila lao la walaji.

Kwahiyo, uchaguzi ujao ni kati ya kundi la wale wanaolitakia mema taifa hili liondokane na ufisadi na ubadhirifu uliokithiri na kufuata njia njema ya kimaendeleo na uadilifu dhidi ya kabila la walaji waliokatwa mirija yao iliyo lifyonza taifa hili. Uwanja wa mapambano waliochagua ni CCM. Hivyo ni kazi kwa kundi adilifu kucheza karata yake na kuwaondosha waovu (walaji) ndani ya chama kwa weledi mkubwa basi hapo itakuwa "..kazi iendelee.."

Tupo tayari kutokuchezewa na kabila ovu, uwezo tunao, sababu tunayo na nia tunayo.

Dunstan Buberwa Ntamilyango,
Mwananchi wa kawaida.
Biharamulo.
0759829015.
Umetumia lugha nzuri kuwasilisha ujumbe wako inaonyesha wewe ni mtaalamu wa lugha na uwasilishaji wa jumbe hongera kwa uwezo huo lakin pia ulichokiandika hujawianisha walaji ni waliopita au waliopo? Lakin labda kama sijakuelewa vzr ila nahis nimeelewa kuwa walaji ni ambao hawako kwenye kigoda yaani ambao wanakitafuta kigoda ndani ya uwanja wa mapambano CCM kama ulivosema ila Nina uhakika hujafanya utafiti linganishi kujua yupi ni mlaji kati ya hawa wapambanaji wawili mim Nina uhakika pia kulingana na tafiti yangu ndogo kuwa inawezekana kabsa Mwenye kigoda ndio mlaji kuliko anaetaka kuchukua kigoda hivi karibun bwana machungwa maembe
Hii inatokana nanini emu jaribu kusikiliza mahojiano ya vyombo vya habari vya nje ya nchi na washirika wa Mwenye kigoda wasasa pia linganisha na mahojiano ya vyombo vya habari hvyo hvyo vya nje ya nchi na washirika wa Mwenye kigoda aliyepita bila shaka utaona tofauti kubwa Mwenye kigoda wa sasa anatuhumiwa sana kubana mambo meng lakin amesahau kuwa anabana hata mambo muhimu kwa wananch mfano Uhuru wa uzungumzaji, Uhuru wa vyombo vya kupikia na vyakutuletea habari za mapish pia amebana wenye pesa ambao wanatuletea masikini jeuri tonge sasa je tinge tutalipata wapi pia ametengeneza hofu kati kati ya washirika wa mwenye kigoda na wana wa i chini so can you guess what next wana wa I chin watahitaji kutafuta huo uhuru kama ambavo mwasisi wa i chini na washirika wenzake walitafuta Uhuru kwa wale wa British pound sijui kama utakuwa umenielewa lugha nliotumia lakin hata kama hujanielewa haina maana, utanielewa baadae ukifanya utafiti ni kina nani walaji kati ya hao wapamabanaji wawil asante nawasilisha
 
Umetumia lugha nzuri kuwasilisha ujumbe wako inaonyesha wewe ni mtaalamu wa lugha na uwasilishaji wa jumbe hongera kwa uwezo huo lakin pia ulichokiandika hujawianisha walaji ni waliopita au waliopo? Lakin labda kama sijakuelewa vzr ila nahis nimeelewa kuwa walaji ni ambao hawako kwenye kigoda yaani ambao wanakitafuta kigoda ndani ya uwanja wa mapambano CCM kama ulivosema ila Nina uhakika hujafanya utafiti linganishi kujua yupi ni mlaji kati ya hawa wapambanaji wawili mim Nina uhakika pia kulingana na tafiti yangu ndogo kuwa inawezekana kabsa Mwenye kigoda ndio mlaji kuliko anaetaka kuchukua kigoda hivi karibun bwana machungwa maembe
Hii inatokana nanini emu jaribu kusikiliza mahojiano ya vyombo vya habari vya nje ya nchi na washirika wa Mwenye kigoda wasasa pia linganisha na mahojiano ya vyombo vya habari hvyo hvyo vya nje ya nchi na washirika wa Mwenye kigoda aliyepita bila shaka utaona tofauti kubwa Mwenye kigoda wa sasa anatuhumiwa sana kubana mambo meng lakin amesahau kuwa anabana hata mambo muhimu kwa wananch mfano Uhuru wa uzungumzaji, Uhuru wa vyombo vya kupikia na vyakutuletea habari za mapish pia amebana wenye pesa ambao wanatuletea masikini jeuri tonge sasa je tinge tutalipata wapi pia ametengeneza hofu kati kati ya washirika wa mwenye kigoda na wana wa i chini so can you guess what next wana wa I chin watahitaji kutafuta huo uhuru kama ambavo mwasisi wa i chini na washirika wenzake walitafuta Uhuru kwa wale wa British pound sijui kama utakuwa umenielewa lugha nliotumia lakin hata kama hujanielewa haina maana, utanielewa baadae ukifanya utafiti ni kina nani walaji kati ya hao wapamabanaji wawil asante nawasilisha
Kwanza nikushukuru kwa uandishi wa kiungwana unaojikita kupanua mjadala. Mara nyingi napenda mjadala na watu waojikita katika hoja bila matusi na kejeli. Kwa njia hii, tnaweza jenga misingi yenye manufaa kwa jamii na taifa letu.

Kuhusu kabila la walaji wapo wapi; ni dhahiri kuwa kundi hili ni tabaka maalum lililojitengeneza na kama nilivyosema, halibagui itikadi ya chama wala rangi isipokuwa linaunganishwa na ile nia ovu ya kujinufaisha binafsi kupitia madalaka. Watu hawa wapo serikalini (watumishi), viongozi wa serikali, vyama, dini, michezo, viongozi wastaafu, n.k. Hivyo inawezekana hata kwa walio madarakani, madhari JPM habagui katika kuwabana basi wale wa kabila hilo ndani ya serikali wataunga mkono kabila lao japo kwa siri, na tunawajua baadhi tayari.

Kuhusu nani mlaji zaidi, na nieleweke kuwa mimi sitafanya mafumbo, kati ya JPM na Membe, si jambo ambalo ni absolute kutaja isipokuwa twaweza kufuatilia historia, malalamiko na upambe unao fanywa na kugundua kundi gani linapigania kurejesha ama kuimarisha mirija yao. Asilimia kubwa ya malengo ya kabila la walajiwanalalamikia yafuatayo:-
  • Kuvurugwa kwa chama; hapa hawazungumzii uvunjifu wa katiba yao bali kutokupewa kipaumbele katika utawala huu.
  • Lingine usilojua pengine, kunyang'anywa kwa mali za chama na kuzirejesha ndani ya chama,
  • Hofu ya ripoti ya Bashiru; hii imepangwa kushughulikiwa baada ya 2020. Hivyo kuna hekaheka zisizowekwa wazi kwa wapambe lakini lengo ni kuhakikisha JPM 2020 hayupo madarakani ili waepuke hicho kikombe.
  • Kuguswa kwa maslahi yao pahala pengi walipokuwa wakichuma.
  • Kutokupewa nafasi na vipaumbele katika nyadhifa watoto, ndugu na wapenzi wao
Hivyo membe ni taswira tuu lakini wenye kuwa nyuma ya membe na ku-push ajenda zao kujilinda ni wengi wenye sifa tajwa hapo juu. Hivyo ninacho weza kusema, kwa mujibu wa historia yao, wamekuwa madarakani watu wazima tunaona na mengi mazuri na mabaya wamefanya, je! kuna jipya wanataka kufanya zaidi ya walicho fanya? Au ni kuhitaji kurudi kwenye neeme zao?

Tukimrejea mzee Membe, ni miongoni mwa mawaziri wa mambo ya nje aliyedumu; katika wakati wake hakuna jambo ulilolitaka halijawahi kutokea akiwa kiongozi, mfano:-
  • Waandishi walitekwa na kuuwawa
  • Wataalamu walitekwa, kuumizwa na kuuwawa (ulimboka, kibanda, Mvungi, Mwaikusa, n.k)
  • Rasilimali za taifa zilichotwa na kupelekwa nje (vipusa, twiga hai, madini, n.k)
  • Pesa za serikali zilichotwa na kufichwa nje.
  • Mikataba mibovu iliingiwa na kuligharimu taifa letu.
  • Udini na mapigano ya kidini yaligubika taifa hili.
  • Magazeti yalifungiwa kama kawaida, n.k
Nini kipya twategemea kwa kundi hili kama si kuruka mkojo na kukanyaga mavi.

  1. Kwanini akili yetu imejikita kwa kundi hili kuwa mbadala wa JPM?
  2. Je hatuna kundi lililo jema zaidi kutufikisha kuliko akili yetu kujikita kwa walele?
  3. Je tumetafakari vema tunachofanya au tunachezeshwa kwata na walewale kwa kutumia mbinu ya kutupandikiza chuki wapate mradi wao?
  4. Uwezo wa fikra mbadala umeenda wapi, na kugeuka kuwa wapambe wa kundi tulilolituhumu miaka dahari?

Ndiyo maana nahitimisha kuwa, kwa sasa ni makundi mawili ndani ya CCM basi, vyama vingine vitaishia kushabikia kundi la walaji lililo nje na wachache waliojibanza serikalini basi, na hapo ujue wapinzani hao na wana harakati wana masilahi binafsi, la wangeendelea na agenda za msingi na sio kubaki kuwa wadaku wa makundi ndani ya chama tawala; kwakuwa malengo ya uanzishwaji wa multpartism sio hayo.
 
Maharagwe ni matamu sana,na huwa nayapenda...lakini yasipoiva vizuri...we!!!

Ndiyo matokeo ya nyuzi kama hizi.
 
Sasa ni dhahiri kuwa swala la chama gani chaweza kutoa rais wa JMT limezikwa rasmi na uhakika ni kuwa, CCM peke yake ndicho kitaendelea kutoa rais.

Ukifuatilia mijadala inayoendelea hasa ndani ya vyama vya upinzani na wapambe wao (wanaharakati) ni dhahiri kuwa wamebadili mashambulizi yao dhidi ya CCM na kuhamishia kwa mtu binafsi (JPM).

Tulizoea mara zote, kutokana na uasili na chimbuko la vyama pinzani na vyama vya kiharakati huwa ni kushambulia serikali na chama kilicho madrakani ili kuonesha kile wanachoita "ukosoaji."

Kwa Tanzania mambo yamebadilika; si wapinzani, wanaharakati, wala wale wanaowatuma na kuwafadhili wanashambulia CCM kama ilivyo, bali wamejikita katika kutafuta namna ya kushirikiana na makundi (kama yapo)ndani ya CCM ili kujaribu kutikisa utawala uliopo na hata ikiwezekana kuuondoa na kuingiza mtu ambaye ataendeleza utamaduni waliozoea wa kufyonza taifa. Hekaheka hizi zinasukumwa na mambo kadha wa kadha.

Kutokana na Tanzania tulipokuwa tumefikia, wanasiasa bila kujali vyama vyao, wanaharakati, wanahabari, viongozi wa serikali n.k kwa wingi wao japo si wote walitegemea kujinufaisha kwa kupora fedha za umma, kufyonza rasilimali za taifa n.k Wachache sana walikosa pesa za wizi, miradi ilikwama huku deni la taifa likikua, misafara isiyokoma kwenda ugaibuni wakilipana masurufu makubwa, n.k.

Hili kundi bila ya kujali itikadi ya vyama vyao, lilitengeneza kabila lao jipya la walaji. Kabila hili sasa limeungana kuhakikisha serikali iliyo madarakani, iliyojikita kuhakikisha inakata mirija ya minyoo ambayo imelifyonza taifa hili kwa miaka mingi inaondoshwa.

Kwa bahati mbaya, na mara zote ilivyo, huwa kuna kundi ambalo hutumika kufanikisha mipango ya kabila la walaji. Kundi hili lina sifa zifuatazo:-
  • Kuendeshwa na mihemko
  • Halina utamaduni wa kufikiri kwa udhati (critical thinking)
  • Huwa na tabia ya matumaini ya maisha mazuri bila kufuata njia sahihi
  • Ni kundi mara nyingi la umri wa kati
Kundi hili linajikuta kucha kutwa likishinda mitandaoni likitoa matusi mengi likitumaini kuwa maisha yatawanyookea kupitia kabila hili la walaji ambao wamekuwa madarakani miaka yote.

Aidha, kabila hili la walaji linaendesha vikao vya siri kila usiku kwa kushirikiana na baadhi ya watu waovu wa mataifa ya nje yenye uchu pia na mali za taifa letu kuhakikisha serikali hii inayowazibia inaondoka bila kujali ni chama gani ilimradi anayeingia atokane na kabila lao la walaji.

Kwahiyo, uchaguzi ujao ni kati ya kundi la wale wanaolitakia mema taifa hili liondokane na ufisadi na ubadhirifu uliokithiri na kufuata njia njema ya kimaendeleo na uadilifu dhidi ya kabila la walaji waliokatwa mirija yao iliyo lifyonza taifa hili. Uwanja wa mapambano waliochagua ni CCM. Hivyo ni kazi kwa kundi adilifu kucheza karata yake na kuwaondosha waovu (walaji) ndani ya chama kwa weledi mkubwa basi hapo itakuwa "..kazi iendelee.."

Tupo tayari kutokuchezewa na kabila ovu, uwezo tunao, sababu tunayo na nia tunayo.

Dunstan Buberwa Ntamilyango,
Mwananchi wa kawaida.
Biharamulo.
0759829015.
Nafikiri umebadili mawazo

Sent from my SM-A505F using JamiiForums mobile app
 
Uchaguzi huu CCM inakwenda kushinda kwa kishindo kwakua upinzani nidhaifu kuliko wakati wowote tangu kuanzishwa kwa vyama vingi.
 
Uchaguzi huu CCM inakwenda kushinda kwa kishindo kwakua upinzani nidhaifu kuliko wakati wowote tangu kuanzishwa kwa vyama vingi.
dalili za kushindwa ni pale MEKO anapokwama kuwafikia wananchi watakaompigia KURA mpaka sasa duru zinaonyesha kuwa mgombea wa CHADEMA #NIYEYE2020 TUNDU ANTIPAS MUNGWAI LISSU anaongoza kwa kuwafikia wananchi wengi na kuwaomba kura kwa style yake pendwa ya HAKI UHURU NA MAENDELEO YA WATU. Na pia anaonyesha mpaka sasa ameweza kuifikia mikoa zaidi ya 19 dhidi ya bwana MAGOFOOLY ambae anasuasua mpaka sasa ameshatembelea mikoa isiyozidi 13 na mikoa mingine anaonyesha kutoifikia kabisaa hivo kusababisha kukosa kuomba kura zao.
hii itamsaidia MH LISSU kuifikia mikoa yote 30 na kuzikusanya KURA nyingi zitazompatia nafasi na kumhakikishia USHINDI WA KISHINDO KIKUU.
hii imejidhihirisha pale mgombea wa ACT UBUNGE na kiongozi mkuu wa ACT ZITTO KABWE alipoutangazia UMMA kuwa KURA za URAIS apewe MH. TUNDU LISSU hii ni kutokana na mgombea wa URAIS ACT Bwana MEMBE kukubaliana na hili na hivo kumuachia LISSU aungurume nchi nzima.

kitendo cha MAGUFuly kukwepa kuzungukia mikoa mingine ilhali uwezo anao wa kuzungushwa nchi nzima kitasababisha kuzikosa KURA za wananchi hao.
#niyeye2020 TUNDU ANTIPAS MUNGWAI LISSU kwa manufaa yako wewe na wananchi wote.
#JITAMBUE
#HAKIUHURUMAENDELEOYAWATU
 
Back
Top Bottom