Suala la Ben Saanane lipelekwe MadhabahunI

BOB LUSE

JF-Expert Member
Jan 25, 2014
3,557
2,853
Nimesoma juhudi za kibinadamu zikigonga ukuta kuleta majibu mujarabu juu ya kupotea kwa mwanajanvi mwenze tu Ben wa Saanane.

Nashauri ndugu zake/jamaa waende kwa watumishi wa Mungu anayeona yaliyosirini afumbue hiki kiwingu.pale akili zetu zinapoishia ndio Mungu anapoingia kazini na kujitwalia utukufu wake.

Tuna watumishi wengi wa Mungu aliyehai,watoe wepesi kwa watanzania tusiojua kilichojiri.ili Mungu atukuzwe.

Barikiweni mjini na mashambani.
 
Mungu aliye hai atafumbuaa kitendawili hiki je kweli wamemuua. juzi nikisikia radio kwizera fm wanatangaza kuwa kuna mtu wamemkuta bwawa la kambi ya nyarugusu amefariki na hakutambulika. ghafla roho ililipuka nikahisi watu wanaopotea kwa mazingira ya kutayanisha labda aweza kuwa Saanane. je saanane aweza kuwa ametupwa maeneo ya kambini kama ilivyolipotiwa? je taarifa zimeenda vijiji vinavyozunguka kambi kujilizisha kuwa hakuwa mwaanakijiji mtz au mkimbizi? ni kizungumkuti lakini baba mwenye huruma anatufunua macho hivi karibuni.
 
Tatizo kuna watumishi wa Mungu(wachache ) na watumishi wa cccm(shockabsorbers) wengi.
Lakini haijalishi,cha msingi ndugu yetu apatikane akiwa salama wa afya ya mwili na akili.
 
Nimesoma juhudi za kibinadamu zikigonga ukuta kuleta majibu mujarabu juu ya kupotea kwa mwanajanvi mwenze tu Ben wa Saanane.

Nashauri ndugu zake/jamaa waende kwa watumishi wa Mungu anayeona yaliyosirini afumbue hiki kiwingu.pale akili zetu zinapoishia ndio Mungu anapoingia kazini na kujitwalia utukufu wake.

Tuna watumishi wengi wa Mungu aliyehai,watoe wepesi kwa watanzania tusiojua kilichojiri.ili Mungu atukuzwe.

Barikiweni mjini na mashambani.
kweli mpelekeeni hili swala Ngwajima au mzee wa upako.
 
Ishu ya Ben inachukuliwa Kisiasa badala ya Kibinadamu
kibaya kuna kunyoosheana vidole,kila mtu anajiona akili zake zinamwaminisha kilichosahihi.natamani wangefunguka akili waende kwa asiyeshindwa na jambo.
 
Ikitokea Ben kapatikana mzima na hana maelezo ya msingi alikuwa wapi, achukuliwe hatua gani? Hadi hivi sasa ni iwe kweli tu kapotea vinginevyo huu usumbufu sio wakuchekewa kabisa.
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom