Peter Stephano 809
Senior Member
- Feb 29, 2020
- 120
- 162
Na Peter Mwaihola
Sio ajabu kwa sasa kupita mtaa mmoja na kukuta Video Library zaidi ya 20 ambapo kila baada ya nyumba 3 unakuta library.
Hali hii inadhihirisha ni namna gani suala la ajira kwa Vijana limekosa ubunifu katika kutengeneza fursa za kipekee.
Kumekuwa na ombwe la Vijana wabunifu katika kutengeneza fursa hivyo kupelekea Vijana wengi kurundikana katika fursa moja au mbili zinazoonekana kuwa rahisi katika eneo husika.
Kwa sasa fursa Kama uendeshaji wa bodaboda na kufungua maktaba za Kanda za video yaani, video library ndizo zinaonekana kuwa na mrundikano wa wa Vijana wengi hususani waliohitimu elimu ya juu katika taaluma mbalimbali nchini.
Ubora wa elimu inayotolewa na vyuo nchini nayo inatiliwa mashaka kwakua imeshindwa kutoa Vijana wenye uwezo wa kubuni fursa mpya badala yake wanaishia kuzitumia tu zile zilizopo.
Aidha inaonekana Kuna kasumba ya wahitimu na Vijana wengi kuwa na kasumba ya kuchagua kazi fulani hususani za ofisini hivyo kushindwa kubuni kazi nyingine zikiwemo za kilimo.
Venance Makirika ambae ni mhadhiri wa uchumi kutoka chuo kikuu Cha kikatoliki Mbeya, CUCoM anasema kuwa vyuo vingi nchini haviwapiki Vijana kwenye ubora unaotakiwa ili wawe wabunifu pindi wanapohitimu elimu zao.
Pia Makirika anashauri kuwe na utaratibu wa kila chuo kufundisha masomo ya ziada yanayohusu ujasiriamali na ubunifu ili kukabiliana na tatizo la uhaba wa ajira kwa Vijana.
Makirika anawaasa Vijana kuondoa kasumba ya kusubiri kuajiriwa pamoja na kuchagua kazi Jambo ambalo Ni kikwazo Cha Vijana wengi kufikiri namna ya kujikwamua.
Sio ajabu kwa sasa kupita mtaa mmoja na kukuta Video Library zaidi ya 20 ambapo kila baada ya nyumba 3 unakuta library.
Hali hii inadhihirisha ni namna gani suala la ajira kwa Vijana limekosa ubunifu katika kutengeneza fursa za kipekee.
Kumekuwa na ombwe la Vijana wabunifu katika kutengeneza fursa hivyo kupelekea Vijana wengi kurundikana katika fursa moja au mbili zinazoonekana kuwa rahisi katika eneo husika.
Kwa sasa fursa Kama uendeshaji wa bodaboda na kufungua maktaba za Kanda za video yaani, video library ndizo zinaonekana kuwa na mrundikano wa wa Vijana wengi hususani waliohitimu elimu ya juu katika taaluma mbalimbali nchini.
Ubora wa elimu inayotolewa na vyuo nchini nayo inatiliwa mashaka kwakua imeshindwa kutoa Vijana wenye uwezo wa kubuni fursa mpya badala yake wanaishia kuzitumia tu zile zilizopo.
Aidha inaonekana Kuna kasumba ya wahitimu na Vijana wengi kuwa na kasumba ya kuchagua kazi fulani hususani za ofisini hivyo kushindwa kubuni kazi nyingine zikiwemo za kilimo.
Venance Makirika ambae ni mhadhiri wa uchumi kutoka chuo kikuu Cha kikatoliki Mbeya, CUCoM anasema kuwa vyuo vingi nchini haviwapiki Vijana kwenye ubora unaotakiwa ili wawe wabunifu pindi wanapohitimu elimu zao.
Pia Makirika anashauri kuwe na utaratibu wa kila chuo kufundisha masomo ya ziada yanayohusu ujasiriamali na ubunifu ili kukabiliana na tatizo la uhaba wa ajira kwa Vijana.
Makirika anawaasa Vijana kuondoa kasumba ya kusubiri kuajiriwa pamoja na kuchagua kazi Jambo ambalo Ni kikwazo Cha Vijana wengi kufikiri namna ya kujikwamua.